Foleni Dar es Salaam

Foleni Dar es Salaam

hivi hao mawaziri nao wanapita kwenye hii foleni?
tumeganda hapa mbezi lisaa sasa na magari hayaendi!!
_
_
 
hivi hao mawaziri nao wanapita kwenye hii foleni?
tumeganda hapa mbezi lisaa sasa na magari hayaendi!!
_
_

mawaziri wanakaa oysterbay,masaki,mbezi digital,mikocheni huko hawapiti na wakipita king'ora kinafagia barabara.
 
yaani ndo kwanza kibamba hapa,nasikia mizani gari hazipimi ili kupunguza foleni
_sijui mwanza tutafika saa ngapi
_
_
_
 
hii foleni ni balaa tangu saa 11.47 alfajiri niko ubungo Oilcom lakini muda wote huo hadi sa hivi 12.40 ndo nimefika ubungo plaza reporting time kazin ni saa moja na naelekea mjini lakin ndio kwanza niko hapa sijui nafika saa ngapi
huyu mwajiri atachoka kunielewa

mabasi yanayotoka stand kuu nayo yanaenda kupitia kule shekilango inazidi kuongeza msululu wa folen


nataman hata kupaa kwa kweli

Yaani leo ilikuwa hatari pale Ubungo,mimi nilikuwa nawahi ndege ya asubuhi saa 07h00 nimefika kwenye foleni ya Ubungo saa 05h10 nimetoka pale Ubungo saa 06h10.Yaani imagine eti nipo foleni pale tena kwa mbele kidogo ya kituo cha Rombo eti nakaa saa nzima na madakika.Yule trafiki wa leo asubuhi pale Ubungo ni ms.nge sana kazi zimemshinda mpaka kidogo nichelewe safari yangu.
 
tumetoka UBT saa 12 mpaka sasa hata kibaha hatujafika!
 
nimepita hapo naelekea mwanza na zuberi III .kwa hali niliyoiona ni heri ulale tu huko huko kazini weekend ndo urudi home.
_ni mtazamo tu
Mkuu, unamaanisha boarding? itabidi kuwe na mabweni na warden...
 
pole mamy yani mimi huo mda ndo kwanza sijui kama kunakuamka yani bado naota ... yani wengine tunawasili sa tatu lakini bado tunachelewa aiseee kazi kweli kweli
 
panaboa sana halaf utakuta asubuh ndo kuna magreda yanachimba
Sasa si ndio wakati wa kazi mkuu, vumilia tu haya yote yatakwisha ngoja strabag wamalize matengenezo. Mtafurahi nyinyi, huku mabasi yaendayo kwa kasi, kule fly over, huku barabara panaaa...Dah, itakua raha sana.
 
jana watu aliotoka ubungo saambili usiku walifika saanane usiku kuna roli lilianguka
 
Tafuta vichochoro mama

Mainroad itakuua

Nilishaikimbia zamani sana
 
pole...kama unaweza kupita chochoro nyingine hata kama ni mzunguko mrefu sana ni afadhali kuliko ubungo mataa coz pale nahisi kuna kaibilisi kadogo
 
it's crazy njia zote zimefunga huu ujenzi na ukamilike tu

Ukiwa unawahi usifuate njia kuu, chepuka! Kuna kipindi nilikaa kimara kwa mwezi mmoja, nilikuwa nachepuka, naingia Bahama mama mpaka UD, kisha sinza napita Tandale mpaka Morocco hotel Magomeni, nakatiza katikati mpaka naibukia Bondeni hotel ndiyo naingia barabara kuu jangwani mpaka town, nilikuwa nawahi vizuri tu.
 
Mi ndio natoka kibamba nakuja posta nipite wapi maana mnanitisha
 
Back
Top Bottom