Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Hahahahaha. Sipati picha endapo walikugundua
 
Ihungo Ukimmiss demu wa Rugambwa uliyecheza naye disco unasimama kwenye vyoo vya shule unatazama madarasa yao roho inatulia.
 

ile shule uhuru wa manyani mpaka raha, wakijaga watoto wa kilimanjaro wanakimbiaga fasta, nakumbuka siku moja mwanafunzi alipigwa beto uwanjani baada ya kumaliza kiwanja cha mpira unapanda sasa kuingia shuleni, akakimbia huku anapiga kelele, dah kesho yake walifunga mabegi watoto wa kichaga ka 10 hivi. Sema mkuu wa shule alikua peace sana na wanafunzi, ila second nyodo nyodo nyingi sana
 

shule mnapewa na mikate kila jmosi na j2, nyama mara 3 kwa wiki, wali na ndizi, aahhh utake nini sasa.
 
We umbwe hawajawai kua na historia ya kupiga shule yoyote achilia mbali lyamungo
 
Nakumbuka nilichukua hela ya ada nikaenda kununua power no 1 ili niuze shule nipate cha juu loh sitaki kukumbuka

Unamuandikia boyfriend barua bila kuwa na kalamu nyekundu ya kuchorea kopa lenye mkuki katikati bado haijakamilika hahaha
 
 
Tabora Boys hiyooo.....Tuliita Berlin na mademu zetu wa Tabora Girls maarufu kama Warsaw
Enzi hizo za "Special Schools"...Vipaji maalumu!Shule ya jeshi,unapokelewa na afande Chacha kwenye geti la kwenda Ng'ambo.

Unaruka kichurachura getini mpaka Sina House,huku afande Chacha akiwa mgongoni.Master parade ni full gwaride,uwanja wa kati mnapiga kwata pamoja na Tabora Boys na Girls.Kutoroka kwenda Tukutuku kuonana na mademu wa Girls,mnapasua mabomba makusudi ili maji yakatike mpate nafasi ya kwenda kucheza na kuchota maji visima vya tukutuku na T/Girls.

Usiku kutoroka kwenda Ng'ambo kuangalia "pilau" kwa wananchi,mchakamchaka mpaka Kipalapala seminari kuu huku mnaimba nyimbo!!Nyangara,Unyuka,redo,mbarara na koi ndio misamiati ya Tabora School.Kila jumamosi mazoezi ya kwaya na Girls,mnaishia kutongozana tu na kubambiana siku ya disko.Wapi Mgulunde Cup?Student Centre na Milambo Boys
 
KUNUNUA KITUNGUU CHA KUCHANGANYA KWENYE MAHARAGE ILI YAWE NA RADHA NA INGINE KUPANDA DIRISHANI KUCHUNGULIA MSICHANA AKIPITA BARABARANI NA INGINE KUJIFANYA MGONJWA ILI ULE SOFT DIET YA WAGONJWA
 
I see!!!Class of 2008??!!Kumbe humu tupo na watoto wetu bila kujijua.
Kibosho Girls 2008....A school of my "Step-girl"....Humu tunajadiliana na watoto zetu kabisaaaa...
Hujambo mwanangu lakini?
 
1. kucheza chandimu kwa wale tunaokosa namba timu ya shule
2. kumwagiwa maji uende bundi
 
Daaa nakumbk ciku za wali nyama nilikuwa naingia na viatu kweny sefuria la wali ili nichukue wote alon.
 
Daaa nakumbk ciku za wali nyama nilikuwa naingia na viatu kweny sefuria la wali ili nichukue wote alon.
Haha we jamaa muongo asiee, yaani nao wanabaki wanakuangalia hivyo hivyo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…