Quemu
JF-Expert Member
- Jun 27, 2007
- 984
- 128
Huwa ninapenda kuangalia movie za kibongo.
Ingawaje tunajitahidi kwenda na wakati, lakini naona kuna makosa kibao ya wazi tunayafanya ambayo yangeweza kuepukika.
Editing
Kosa kubwa la kwanza ambalo tunafanya ni kukosa Editors ambao wako serious na kazi zao. Unategemea Editor ndio ambaye angefanya kazi mzuri ya kureview movie , yet bado kuna makosa madogo madogo kibao ambayo yananakera sana kuyaona.
Mfano Movie ya Oprah (Steve Kanumba, Vincent Kigosi, na Irene Uwoya)
1)Sauti - sauti ya hii movie inatoka kama sauti ya mwangwi (echo). Ni kama vile walikuwa wana record kwenye chumba cha mwangwi, halafu baada ya kuchukua sauti za waigizaji wenyewe, wakachukua sauti za ule mwangwi wenyewe. Yaani sauti inatoka kama ya mtu unayeongea naye kwenye simu ambaye amejifungia chumbani au kwenye kopo.
2)English subtitles - Hapa ndio kuna vituko kweli. Yaani unasoma hizo tafsiri ya English kwenye hii movie mpaka unabaki kushangaa. Ndio najua wengi tunachemsha kwenye English, lakini kama film industry ya Bongo inataka kuwa serious (kujiingiza kwenye soko la nje), basi haitakiwi kuruhusu makosa kama yale. Kuna part moja ndio iliniacha hoi kabisa. Steve na Irene walikuwa restaurant, Zanzibar. Basi Steve akawa anamwambia Irene tafuna tafuna tafuna, akimsisitizia kuwa atafune chakula anamchomlisha. Sasa kwenye subtitles tafsiri yake ikawa cat cat .cat. I was like enhe! Mwanzo sikujua walikuwa wanajaribu kuandika nini, lakini nikaja kugundua kuwa dhamira yao ilikuwa kuandika cut cut cut, neno ambalo bado sio tafsiri sahihi ya tafuna.
Sasa makosa mawili kama haya yalitakiwa yashughulikiwe na editor. Hapa ndipo editor anapo onyesha umahili wake katika fani hii. Udhaifu wa makosa kama haya unaonyesha jinsi gani editors wa kibongo wasivyo serious na kazi zao.
Wardrobes
Ukweli ni kwamba waigizaji wana overdress mno. Sasa sijui wanajaribu kuonyesha kuwa wanajua kuvaa sana au vipi? Lakini mara nyingi wanavaa loud clothes mno kulingana na scenes/story za movies.
Mfano - Movie ya Oprah (Steve Kanumba, Vincent Kigosi, na Irene Uwoya)
Vincent - anavaa very loud suits just kwenda kazini tu. Tena ana match na fancy shoes na hat kabisa. Unakuta kakupigia all white, kuanzia viatu, suruali, koti, kofi, na kakupigia shati moja kali jeusi . Halafu anaishia kwenda kazini mchana kweupe. I mean, watu upiga hayo mavazi wakiwa wanakwenda kwenye mtoko jioni.
Steve huyu yeye anakuvalia jacket moja zito la nguvu kwenye 100 degrees condition. Pia anakupigia miwani moja kubwa sana Anavaa hivyo vyote only kwenda chuo.
Miss Uwoya - Huyu ndio alikuwa anafunga kazi kabisa. Well, lazima nikubali kwanza, kuvaa tu anajua. Maana baadhi ya mavazi yake yalikuwa yananifanya niweweseke ile mbaya lol. Anyway, bibie huyu alikuwa anavaa pamba kali kama zile tulizozizoea kuwaona dada zetu wanugu wakivaa clubs (huku waki drop-it-like-its-hot). Yaani anakupigia capri ya nguvu, huku akimachisha na sleeveless top na fancy cowgirl hat (or whatever its called) mchana kweupe ..halafu huyo anaelekea sokoni kwenda kununua nyanya.
Scenes
Hawazingatii umuhimu wa mazingira wanayofanyia baadhi ya settings.
Mfano - Movie ya Oprah (Steve Kanumba, Vincent Kigosi, na Irene Uwoya)
Vincent supposedly ana ofisi pale kwenye jengo la Millenuim Tower. Sasa unakuta kila anapoenda kupaki pale juu, hakuna hata gari jingine kwenye ile parking. Well, inavyoonekana ile sehemu ya scene walitengeneza either jumamosi or jumapili. Lakini katika hali ya kuongeza ufanisi wa utengenezaji wa fialmu, ningetegemea pengine wangetengeneza scene ya ile sehemu angalu kwa siku mbili tofauti. Yaani, kwa sababu wameazima ofisi ya mtu kutengeneza filamu, basi wangefanya shooting ndani ya hiyo ofisi siku ambayo hakuna wenyeji (jumamosi au jumapili). Halafu wakafanya shooting ya kwenye parking siku ya weekday ambayo kuna magari yamepaki. Hiyo ingeipa movie ufanisi wa reality. I mean, hutegemei parking ya jengo kama lile kuwa empty siku ya kazi.
All in all, kwa mtazamo wangu, hili hawa wasanii wetu wa filamu waweze kuendelea na kutengeneza filamu zenye angalau standard quality, basi inabidi kuwe na panel ya critics. Ukosoajia utakaotoka kwa panel hii utawasaidia sana wasanii hawa kuzingatia kanuni za uigizaji. Ningependekeza baraza la wasanii Tanzania (kama lipo) liunde hii panel. Njia nyingine ni wadau kuunda a private panel of critics.
Ingawaje tunajitahidi kwenda na wakati, lakini naona kuna makosa kibao ya wazi tunayafanya ambayo yangeweza kuepukika.
Editing
Kosa kubwa la kwanza ambalo tunafanya ni kukosa Editors ambao wako serious na kazi zao. Unategemea Editor ndio ambaye angefanya kazi mzuri ya kureview movie , yet bado kuna makosa madogo madogo kibao ambayo yananakera sana kuyaona.
Mfano Movie ya Oprah (Steve Kanumba, Vincent Kigosi, na Irene Uwoya)
1)Sauti - sauti ya hii movie inatoka kama sauti ya mwangwi (echo). Ni kama vile walikuwa wana record kwenye chumba cha mwangwi, halafu baada ya kuchukua sauti za waigizaji wenyewe, wakachukua sauti za ule mwangwi wenyewe. Yaani sauti inatoka kama ya mtu unayeongea naye kwenye simu ambaye amejifungia chumbani au kwenye kopo.
2)English subtitles - Hapa ndio kuna vituko kweli. Yaani unasoma hizo tafsiri ya English kwenye hii movie mpaka unabaki kushangaa. Ndio najua wengi tunachemsha kwenye English, lakini kama film industry ya Bongo inataka kuwa serious (kujiingiza kwenye soko la nje), basi haitakiwi kuruhusu makosa kama yale. Kuna part moja ndio iliniacha hoi kabisa. Steve na Irene walikuwa restaurant, Zanzibar. Basi Steve akawa anamwambia Irene tafuna tafuna tafuna, akimsisitizia kuwa atafune chakula anamchomlisha. Sasa kwenye subtitles tafsiri yake ikawa cat cat .cat. I was like enhe! Mwanzo sikujua walikuwa wanajaribu kuandika nini, lakini nikaja kugundua kuwa dhamira yao ilikuwa kuandika cut cut cut, neno ambalo bado sio tafsiri sahihi ya tafuna.
Sasa makosa mawili kama haya yalitakiwa yashughulikiwe na editor. Hapa ndipo editor anapo onyesha umahili wake katika fani hii. Udhaifu wa makosa kama haya unaonyesha jinsi gani editors wa kibongo wasivyo serious na kazi zao.
Wardrobes
Ukweli ni kwamba waigizaji wana overdress mno. Sasa sijui wanajaribu kuonyesha kuwa wanajua kuvaa sana au vipi? Lakini mara nyingi wanavaa loud clothes mno kulingana na scenes/story za movies.
Mfano - Movie ya Oprah (Steve Kanumba, Vincent Kigosi, na Irene Uwoya)
Vincent - anavaa very loud suits just kwenda kazini tu. Tena ana match na fancy shoes na hat kabisa. Unakuta kakupigia all white, kuanzia viatu, suruali, koti, kofi, na kakupigia shati moja kali jeusi . Halafu anaishia kwenda kazini mchana kweupe. I mean, watu upiga hayo mavazi wakiwa wanakwenda kwenye mtoko jioni.
Steve huyu yeye anakuvalia jacket moja zito la nguvu kwenye 100 degrees condition. Pia anakupigia miwani moja kubwa sana Anavaa hivyo vyote only kwenda chuo.
Miss Uwoya - Huyu ndio alikuwa anafunga kazi kabisa. Well, lazima nikubali kwanza, kuvaa tu anajua. Maana baadhi ya mavazi yake yalikuwa yananifanya niweweseke ile mbaya lol. Anyway, bibie huyu alikuwa anavaa pamba kali kama zile tulizozizoea kuwaona dada zetu wanugu wakivaa clubs (huku waki drop-it-like-its-hot). Yaani anakupigia capri ya nguvu, huku akimachisha na sleeveless top na fancy cowgirl hat (or whatever its called) mchana kweupe ..halafu huyo anaelekea sokoni kwenda kununua nyanya.
Scenes
Hawazingatii umuhimu wa mazingira wanayofanyia baadhi ya settings.
Mfano - Movie ya Oprah (Steve Kanumba, Vincent Kigosi, na Irene Uwoya)
Vincent supposedly ana ofisi pale kwenye jengo la Millenuim Tower. Sasa unakuta kila anapoenda kupaki pale juu, hakuna hata gari jingine kwenye ile parking. Well, inavyoonekana ile sehemu ya scene walitengeneza either jumamosi or jumapili. Lakini katika hali ya kuongeza ufanisi wa utengenezaji wa fialmu, ningetegemea pengine wangetengeneza scene ya ile sehemu angalu kwa siku mbili tofauti. Yaani, kwa sababu wameazima ofisi ya mtu kutengeneza filamu, basi wangefanya shooting ndani ya hiyo ofisi siku ambayo hakuna wenyeji (jumamosi au jumapili). Halafu wakafanya shooting ya kwenye parking siku ya weekday ambayo kuna magari yamepaki. Hiyo ingeipa movie ufanisi wa reality. I mean, hutegemei parking ya jengo kama lile kuwa empty siku ya kazi.
All in all, kwa mtazamo wangu, hili hawa wasanii wetu wa filamu waweze kuendelea na kutengeneza filamu zenye angalau standard quality, basi inabidi kuwe na panel ya critics. Ukosoajia utakaotoka kwa panel hii utawasaidia sana wasanii hawa kuzingatia kanuni za uigizaji. Ningependekeza baraza la wasanii Tanzania (kama lipo) liunde hii panel. Njia nyingine ni wadau kuunda a private panel of critics.