Fikra za Mwalimu: Hizi hapa.. mzikubali au mzipinge!

Naomba nitumie nafasi hii kuchambua aliyosema Mwalimu na kuonesha ni kwanini karibu wachangiaji wote wamekwepa alichosema na badala yake wameenda kwenye mambo ya luninga, kula yanga, n.k Najaribu kuongoza mjadala on an intellectual level ya kuangalia alichosema Nyerere na idea zake kuzichambua kwa kuziangalia idea hizo na si kingine. Philosophically, kujaribu kuona the validity of their assumptions and the plausability of their contents.

Natumaini tunavyoendelea mbeleni watu watazungumzia idea zenyewe na si kitu nje ya hizo kwani kufanya hivyo tutakuwa tunashikiri katika mjadala muhimu sana kuhusu mawazo na fikra za Mwalimu.

…. Throughout these speeches and writings, and through all the activities of the Governments which I have been privileged to lead and support, there is however one recurring practical theme. It is the theme of change. For Africa must change; change from an area where people (take?) out an existence and adapt themselves to their environment, to a continent which challenges the environment and adapts it to man’s need.

Afrika lazima ibadilike; kutoka bara ambalo linasubiri matukio nje yake yenye kusababisha mabadiliko kuelekea bara ambalo watu wake wanasimamia mabadiliko yao wao wenyewe. Ni nini kuarticulate ukweli kuwa lazima tuwe "a continent which challenges the environment and adapts it to man’s need." Hakuna aliyeonesha ubaya wa fikra hii.
Africa must change her institutions to make feasible her new aspirations;

Mwalimu anasema pasipo utata kuwa Africa must change her Institutions. Kwa maana ya kwamba vile vyombo ambavyo tulikuwa tumevizoea au ambavyo vilikuwa dhaifu havina budi kubadilishwa na kuboreshwa. Na ukiangalia utaona kuwa wazee wenzangu hapa ndicho wanachosema kwamba kuna vitu (institutions) ambazo hata leo hii vinahitaji kubadilika. Ni ubaya gani wa fikra hizi za Mwalimu kuwa "Africa must change her institutions to make feasible her new aspirations" What is wrong with this self-evident truth? Hakuna aliyeonesha hadi hivi sasa.

her people must change their attitudes and practices to accord with the objectives.

Mwalimu alisema vizuri tena kama prophetically ( I use the term rather liberally) kuwa Bara letu lazima libadili mitazamo na vitendo vyake. Ukiangalia hili ndilo ambalo wengi tunalijadili tunapoangalia mapungufu ya Mwalimu n.k tunasema tunataka tubadilike, tunasema tubadili attitudes zetu na matendo yetu. Ili tufikie malengo (objectives) ya kujenga taifa la kisasa na la watu wenye kufurahia Taifa lao. Tunasema tunataka tubadilike. Tunapozungumzia kuzingatia misingi ya utawala wa sheria, kuwa na maadili n.k tunachosema ni kuwa vitu hivyo havipo sasa na tunataka tubadilike. Hivyo tunakubaliana na Mwalimu kuwa we need to change our "attitudes and practices to accord with the objectives." Kuna ubaya gani katika ukweli huu mwingine kuwa kama kweli tunataka kufikia malengo yetu hatuna budi kubadilika? Hakuna aliyeonesha hadi hivi sasa.


And these changes must be positive,

Mwalimu anasema mabadiliko hayo hayana budi yawe mazuri. Kwa maana kubadilika kuelekea ubaya si mabadiliko tunayoyataka. Alichosema na ambacho kinashuhudiwa na wachangiaji wengi hapa ni kuwa tubadilike kuelekea upande chanya. Tunapoangalia historia yetu na kuona mapungufu ya viongozi waliotutangulia tunaona ipo haja ya kubadilika. Kubadilika huko siyo kurudia kanuni, na mifumo ambayo imeonekana imefeli au ilikuwa na kasoro kubwa lakini ni kubadilika kufuatia kitu kilichobora zaidi.

Na katika kufanya hivyo twaweza kujikuta tukirudia baadhi ya kanuni za msingi au fikra za msingi zilizotujenga sisi kama Taifa (kama tutakavyoona huko mbeleni). Kurudia ubovu au vitu hasi Mwalimu alikataa; kasema wazi mabadiliko tunayoyahitaji ni yale mazuri. Sasa kuna ubaya gani katika hoja hii ya Mwalimu kuwa "Changes must be positive"? Hadi hivi sasa hakuna aliyeonesha ubaya wa hoja hiyo ya Mwanafalsafa Mwalimu.

they must be initiated and shaped by Africa and not simply be a reaction to events which affect Africa.

Mwalimu hapa anaonesha wazi kuwa Afrika inaweza kuchagua watu wengine waamue mabadiliko ndani yake au yenyewe ibadilike yenyewe. Kwamba waafrika wenyewe waamue hatima ya maisha yao na kiasi cha mabadiliko wayatakayo. Leo hii tunapozungumzia mabadiliko wengi tutachukia na kukasirishwa wakija wazungu na kutuambia tufanye hivi au vile kwa vile wanaamini hivyo ni vitu vizuri kwetu.

Wengi tutaona tumetukanwa na kudharauliwa kama Wamarekani wakija na kusema "badilisheni Katiba yenu", fanyeni hivi au vile. Yawezekana wakawa wanasema kweli lakini yawezekana wengi tungependa kuona kuwa ni sisi wenyewe tunaamua nini tunachotaka. Sasa kwa Mwalimu kusema "Africa must initiate and shape" these changes kuna makosa gani hapo? Je tunataka wengine watubadilishe na sisi tuwe wajibuo yale yafanywayo na wengine? Hakuna aliyeonesha ubaya wazo hilo. Hakuna.

For a revolution has begun in Africa. It is a revolution which we hope to control and channel so that our lives are transformed. It is a revolution with a purpose, and that purpose is the extension to all African citizens of the requirements of human dignity.

Mwalimu hakuwa anazungumzia "Mapinduzi ya kijamaa" alikuwa anazungumzia "revolution" in terms of rapid change, yaani mabadiliko yaliyolazimishwa. Na mapinduzi hayo ya nchi za Afrika kujipatia uhuru na kuwa mataifa (kumbuka haya maandishi yalikuwa ni ya 1966) yalikuwa ni mapinduzi ambayo yasingeweza kuzuiwa.

Na anasema wazi kuwa mapinduzi hayo (mabadiliko hayo) yana lengo moja nalo ni "the extension of all African citizens of the requirements of human dignity". Je, haikuwa lengo la uhuru na utaifa wetu kuwa na sisi tuwe na utu na heshima kama ya wanadamu wengine? Je halikuwa lengo na limebakia lengo kuwa tuweze kujichagulia viongozi wetu na kuamua hatima ya maisha yetu? Sasa kuna ubaya gani kwa Mwalimu kusema kuwa mabadiliko haya lazima yatupeleke kwenye lengo moja nalo ni "extension of all Africans citizens of the requirements of human dignity"? Hakuna aliyeonesha wapi Mwalimu amekosea kwenye hilo. Hakuna.

The task before us is a big and complicate one.

Mwalimu hakuahidi luninga kwa kila mtu, hakuahidi maisha Rais, hakuahidi "maisha bora kwa kila Mtanzania" na wala hakuahidi kuwa njia ya kufikia maendeleo na mafanikio itakuwa ni nyepesi na isiyohitaji watu kuhangaika. Mwalimu hakuwa mtu wa kufikirika kuwa maneno matamu basi ndiyo huliwa. Alitambua kuwa kujenga Taifa siyo lele mama; Angeweza kutoa ahadi ya "maziwa na asali" kwenye hiyo nchi ya ahadi. Hakufanya hivyo. Alituambia mapema kabisa kuwa "the task is a big and complicated one".

Kujenga Taifa from scratch siyo lele mama. Na kama nilivyosema mahali pengine, ninafuraha na fahari kuzaliwa ndani ya Taifa lililojengwa na Mwalimu kuliko kuzaliwa katika Taifa la viongozi wasio kuwa na principles zenye kujenga Taifa. Leo hii wapo viongozi ambao wanafikiri tumeshajenga Taifa sasa tuanze kulila tu; wameacha kulijenga Taifa wamebakia kujenga mahekalu yao. Wanafikiri kazi ya kulijenga Taifa ilikuwa rahisi na imeshamalizika. Kumbe bado ni kibarua.

Sasa kuna ubaya gani kwa mwalimu kutuambia mapema kabisa kuwa "the task before is big and complicated one"?. Hakuna mtu aliyeonesha kuwa "the task should have small one and uncomplicated one". Hakuna.
In the process we shall have many decisions to make which involves clashes of principle –

Ni kiongozi ambaye huweza kuona matokeo ya maamuzi yake na kwa mbali anaweza kuyaona katika fikra. Mwalimu aliona ugumu wa maamuzi mengine na alituambia mapema kabisa kuwa yawezekana katika kujenga hili Taifa tutakutana na maamuzi ambayo yana "involve the clashes of principle". Huu ni ukweli. Leo hii tunashindwa kuchagua nini cha kufanya kwa sababu tumepoteza principles zenyewe na hatuna cha kushilikia au pa kuanzia. Kuna makosa gani katika kutambua kuwa katika kufanya maamuzi huko mbeleni tunaweza "kugonganisha kanuni" mbalimbali na maslahi mbalimbali? Hakuna aliyeonesha ubaya wa kauli hiyo ya Mwalimu; hakuna.

where we have to choose, let us say, between rapid development and individual freedom, or between efficiency and equality.

Ametoa mfano ambao kwa wengine naona umewapita kwa haraka. Katika kujenga Taifa na unakutana na migongano ya principle hauna budi kuchagua. Nitatoa mfano. Baada ya matukio ya Septemba 11 Marekani ilijikuta inagonganisha principles mbili ambazo zimelijenga Taifa hilo; Usalama wa nchi na Uhuru wa kila mtu (security and individual liberties). Sasa walipokuwa wanajaribu kuja na sheria ambayo ingeweza kuwasaidia baadaye (positive change) wakajikuta na jukumu "big and complicated one".

Matokeo yake ni kupitishwa kwa sheria ya "Patriotic Act" ambayo ilikuwa inajaribu kutafuta uwiano wa mambo haya mawili katika kujaribu kuja na sheria nzuri. Hadi leo hii karibu miaka nane baadaye bado wanahangaika kutafuta "balance" ya clashing principles.

Sasa, kuna makosa gani katika kauli ya Mwalimu kuwa tunaweza kujikuta tunagonganisha principles? Hakuna mtu aliyeonesha mapungufu ya kauli hiyo ya Mwalimu zaidi ya watu kuleta hadithi na stori za maisha yao. (If you have noticed I have not interjected my own experiences.. nimezaliwa, nimesoma, na kukulia katika Tanzania hiyo hiyo ya Mwalimu.. lakini sijengi hoja kupitia mwanga wa hisia, kumbukumbu na vionjo vyangu; najenga hoja kwa kutumia intellectual argument).

There is and will be no simple universal answer to such problems; the choice will have to be made in the light of historical circumstances and the conflicting needs of present and future.

If this is not "Bam!!" I don't know. Mwalimu anaeleza wazi kuwa hakuna jibu jepesi katika kuleta mabadiliko. Kuna watu wanazungumza humu kana kwamba Mwalimu angebonyeza hiki au kile na vitu vingekuwa hivi au vile; watu wanazungumza kana kwamba Mwalimu angeweza kuandika sheria hii basi mambo yote yangekuwa mswano.

Hapana; Mwalimu alijua na akaelezea wazi na mapema kuwa hakuna jibu jepesi katika kuleta mabadiliko ya kweli katika maisha ya Taifa hili. Alisema kuwa mabadiliko na maamuzi yoyote ya kuelekea mabadiliko hayo hayana budi kufanywa "in the light of historifcal circumstances and the conflicting needs of (the)present and future". Kuna ubaya gani katika kauli hiyo ya Mwalimu? Je mabadiliko hayaangalia "needs" za wakati uliopo au wa mbeleni au tunabadilika in a vacuum or empty space. Hakuna aliyeonesha mapungufu katika kauli hiyo ya Mwalimu zaidi ya kuzungumzia mambo elfu nje ya text tunayoiangalia. Hakuna.
The only certain thing is that if we forget any of our principles, even when we are ignoring or breaking them, then we shall have betrayed the purpose of our revolution and Africa will fail to make its proper contribution to the development of mankind.

Nobody could have said it better! Nani anapinga ukweli huo, ni nani haoni the majestic and glorious truth in such an eloquent utterance!? Hakuna ambaye amepinga zaidi ya kulaumu "KAMATA"!! Tulikulia kipindi hicho hicho, tunakumbuka mabasi ya RELWE (na mistari yake ya kahawia), nakumbuka kupita vilima vya Lukumburu siku chache baada ya askari wetu kuanguka tena nikiwa kwenye mabasi ya Kauru! Hivyo tukileta experience of "how life was so hard" nani alisema ilitakiwa iwe rahisi!? Yaani Marekani ya 1776 ilikuwa ni ile ile ya miaka hamsini baadaye na watu wangemlaumu George Washington na mababa wa US kwamba hawakuwa na Luninga na walikuwa na matatizo 1001 wakati wa kuanza kuijenga Marekani? Ndio maana watu leo wanafurahia ahadi za maneno matamu na ahadi za peponi lakini hawataki kuzifanyia kazi.

Watu wamesalimu amri mbele ya woga na kudai kuwa "haiwezekani"; wanachoshindwa kukiri ni kuwa "haiwezekani" kwa sababu hatuko tayari kujaribu na kufanya kazi kufanya iwezekane. Tunataka Mwalimu angetutengenezea njia nyeupe sisi tupite tu kama Watakatifu wanapoingia mji wa Yerusalemu! Hatutaki kushughulisha.

Nimeona hapa mara nyingi, mtu anakuja na kuuliza "jamani tuwekeeni Katiba" badala ya kuuliza "hiyo katiba iko wapi na mimi niisome"? Yaani watu wanataka mtu mwingine angewafanyia kazi zote, kusafisha shamba, kulima, kupanda, kupalilia, kuvuna na kuwawekea ghalani; wao wawe wanaenda kuchukua na kula tu! Na wangepata mtu wa kuwalisha wangeshukuru!


But the opportunity is before us provided we have to courage to seize it.

People are afraid to seive the opportunity. Ndio maana tunawaona wenzetu wa Zimbabwe wakitumia nafasi yao to seize this opportunity.

For the choice is not between change or no change; the choice for Africa is between changing or being changed – changing our lives under own direction, or being changed by impact of forces outside our control.

What a truth! Ni kweli tunaweza kukaa na kusubiri mabadiliko yatokee, au tunaweza kushiriki katika mabadiliko hayo. Mugabe ameshindwa kubadilika na sasa anabadilishwa na nguvu zilizo nje ya uwezo wake.

Mwalimu aliona mbali na aliona kuwa kuna mabadiliko yanakuja na yeye akaamua kuyawahi. Mzee Kitila amesema vizuri kabisa kuwa Kama Nyerere angeendelea kukaa madarakani yangeweza kumkuta ya Mugabe, siwezi kupinga; lakini kufikiri hivyo ni kwa mtu asiyemjua Nyerere. Nyerere asingeweza kuendelea kukaa madarakani kwa sababu intellectually he could see the upcoming change and he could not stop it. Ndio maana akaamua kukaa pembeni na kujaribu kuyaelekeza yaende vizuri. Leo hii tunazungumzia hali ya kisiasa nchini bila kukiri kuwa uamuzi wa Mwalimu kung'atuka ulikuwa ni uamuzi wa kijasiri sana na ulisaidia sana kulipeleka Taifa letu kwenye mabadiliko badala ya kusubiri nguvu za nje kutubadilisha kama yaliyomkuta Kibaki.


In Africa there is no stability in stagnation in this twentieth century; stability can only be achieved through maintaining balance during rapid change.

Tanzania has chosen to ride and try to harness the whirlwind which is sweeping through this continent. We know that some human dislocation is inevitable in this process, but we believe that much more would ultimately be involved in doing nothing. For we recognize that to try to maintain the status quo is to try to ignore the world.

Well said; tusingeweza kuendelea na "jinsi ilivyo" lazima tubadilike na ilibidi tubadilike. Lakini ni sisi wenye kusimamia mabadiliko hayo. Wakati mwingine mabadiliko yataudhi watu wachache au kusababisha usumbufu lakini kutofanya mabadiliko kwa kuogopa usumbufu ni woga.

Leo, US na nchi nyingi bado zinafanya mabadiliko na watu wanasumbuka kidogo lakini wanajifunza kuishi nayo. Kuna mabadiliko kadhaa ya sheria mbalimbali n.k na watu wanatakiwa kuadjust. Sisi tunaogopa kubadilika kwa sababu tuko kwenye comfort zones zetu.

Ndio maana hawa wakuu Butiama wamepatwa na woga na pale magogoni wanasitasita kufanya maamuzi kwa sababu wakibadilisha vitu basi tunaweza kusumbua watu kama kina Mkapa, Yona, na wengineo, na hivyo hawafanyi mabadiliko. Kwa wengine wetu hilo linaonekana ni jambo zuri.

Lakini utaona kuwa watu hapa wanataka mabadiliko katika Tanzania lakini hawatuambii ni usufumbufu na shida gani zinaweza kutokea kwa wananchi tukileta mabadiliko? Tukitunga sheria ambazo zitasababisha usumbufu kwa watu je tuzipitishe?

Kwa mfano, tukipitisha sheria inayosema kuanzia sasa hadi ndani ya miaka kumi ijayo, nyumba zote za Tanzania ni lazima ziwe aidha za matofali ya kuchoma au ya sementi na ziwe zimeezekwa mabadi au vigae. Lengo likiwa ni hatimaye kuondokana na nyumba za udongo na makuti na mitete! Je sheria kama hiyo ni nzuri au kwa vile itasababisha usumbufu basi tusifanye hivyo?

Vipi tukisema kuwa Jiji la Dar linahitaji mifereji mipya ya kupitisha maji yatuwamayo na kuyapeleka baharini. Katika kufanya hivyo kuna majengo na nyumba ambazo itabidi zivunjwa ili kulitengeneza jiji la kisasa; je tufanye hivyo licha ya usumbufu kwa wakati na wananchi wa Dar. Wanaoogopa usumbufu watasema "hapana" tusiwasumbue watu. Lakini leo hii hata Marekani wanafanya mambo hayo tena kwa sababu za kiuwekezaji kupitia sheria kama za "eminent domain" ambazo hata Tanzania tunazo na zimewekwa kwenye mikataba ukiwemo wa Barrick Gold kule Bulyanhulu na Buzwagi.

Sasa mwalimu kuelezea ukweli huo kuwa yaweza kusababisha usumbufu imekuwa ni ubaya? Je angesema mabadiliko yatakuwa kama kwaya ya mbinguni si watu wangepiga makofi? Leo watawala wetu wanashinda kufanya maamuzi magumu kama ya kusimamisha uchimbaji Mererani hadi utaratibu na miundo mbinu mizuri umewekwa italeta usumbufu.

Sasa kuna ubaya gani katika hoja ya Mwalimu kuwa
We know that some human dislocation is inevitable in this process, but we believe that much more would ultimately be involved in doing nothing. For we recognize that to try to maintain the status quo is to try to ignore the world.
Hakuna aliyeonesha ubaya wa hoja hiyo ya Mwalimu. Hakuna.

We prefer to participate in the shaping of our own destiny, and we believe that we have the resolution and the ability to overcome difficulties and build the kind of society we want.

Je hiki si ndicho mzee ES unakijenga hoja? Kuwa ni sisi wenyewe tuamua tunataka Taifa la namna gani na ni sisi wenyewe tushiriki katika kujenga Taifa hilo? Kwamba sisi ndio tuwe masters of "our own destiny and captains of souls"? Kuna ubaya gani katika maneno hayo ya Mwalimu kuwa "we have the resolution and the ability to overcome difficulties", kwani hatuna? Najua wengine hawawezi kwa sababu wanaogopa kubadilika au mabadiliko yatawasumbua; lakini ni watu wale wenye mawazo ya kuamini kuwa wanaweza kujenga Taifa walitakalo na wana resolve kufanya hivyo.

Kuna ubaya gani to state such a magnificent proposition kuwa tunaweza kushinda vikwazo vyote?

For those with courage to aspire, to believe, and to work, Tanzania is a challenging and exciting land. It is my privilege and my happiness to dedicate myself to its future.[/B]

What a dare! Kwa wale ambao hawana courage to aspire, or believe or work Tanzania kwao is not challenging and not exciting at all. Kwa sisi wengine ambao tunaamini change is necessary basi tunaona fahari kuhusishwa na mabadiliko hayo na tuko tayari kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo yanatokea.

Kwa kifupi:

Hadi hivi sasa hakuna aliyeonesha hata kwa karibu ubaya wa hoja ya Mwalimu kuhusu mabadiliko na kama alichosema hakikuwa sahihi. Ukiondoa malalamishi ya kukosa luninga, kula yanga n.k hakuna aliyeangalia kwa kina substance ya alichosema Mwalimu na kusema it was substantially untrue, illogical, beyond belief and inherently redundant. None whatsoever.

Kwa maneno mengine, fikra za Mwalimu kuhusu haja ya mabadiliko katika Afrika na katika Tanzania still stand today as it stood 42 years ago! My friends, we need to change for a change is necessary. The changes we need are the changes that we will be masters of. We can not wait for other people to come and change us or let other external forces to impact us so that we change. We have to take charge of of whatever idea we aspire to and work hard to bring it about.

This is the main idea in this piece. Do you agree?
 
Ngabu,
Norway ilikuwa moja kati ya nchi masikini sana kule Ulaya. Mwaka 1962 makampuni ya kimarekani yaliwafuta na kuwaambia kuwa wana mafuta katika eneo lao la bahari na wakataka(USA) wachimbe, ila Norway ilikataa. Si kwa sababu walikuwa hawataki kuchimba au walikuwa matajiri ila kwa kuwa hawakuwa na ujuzi wa aina yeyote kuhusu mafuta na mikataba,experience na zaidi fedha.Hawakutaka wamarekani pekeyao ndo wafanye uchimbaji huo na wao walipwe mrabaha tu. Kwa kushirikana na UIingereza waliamua kuchimba na kisha ndipo walialika Kampuni zingine za nje. Baada ya hapo Norway iliunda Kampuni ya mafuta iliyochini ya serikali ili ku-control shughuli zote za mafuta na serikali ikaamua kununua shea kutoka kampuni zingine za mafuta.
Kuwa na mali asili tele haina maana ukurupuke tu bila kuweka mikakati ni jinsi gani mali hizo zitaisaidia nchi. Nyerere sio kwamba hakutaka tufaidike na maliasili yetu ila aliona kuwa hatukuwa na uwezo wala uzoefu na wataalamu wa kutosha kusimamia mambo ya madini. Hakutaka yetukute yanayotukuta sasa, viongozi kama Mkapa kuruhusu uchimbaji bila mikakati yeyote ili mradi tu ahakikishe anafaidika katika kipindi chake cha uongozi.Madini yanakwisha bila Watanzania kufaidika.

Nchi za Scandinavia walichukua mambo waliyoona mazuri kutoka katika Ujamaa na baadhi kutoka katika Ubepari na kuyachanganya na ndo maana tunaona hapa walipo.
Nyerere alikuwa na filosofi nzuri sana ila zilitekelezwa vibaya. Alitaka kila mtu awe na maisha bora.Siku zote matajiri huishi kwa gharama watu fulani kuwa masikini.

Kwa hiyo mwaka 1962 na kurudi nyuma wa Norway wengi walikuwa wakiishi kwenye nyumba za udongo na kutembea pekupeku au kuvaa makatambuga?
 
Mwanakijiji....hizo unazodai fikra za Mwalimu si kwamba ni yeye pekee ndiye aliyekuwa akiwaza ama kufikiria hivyo! Ukiangalia kwa undani au hata kwa juu juu tu utaona kwamba mengi anayosema ni common sense na mara nyingi common sense ni relevant muda wote. Mimi sidhani kwa vile tu aliyaweka kwenye maandishi mawazo basi tuyafanye kuwa hayo ni mawazo aliyokuwa akiwaza Mwalimu na hakuna mwingine Afrika ama duniani aliyekuwa akifikiria kama hivyo. Nimesoma ulichochambua hapo juu na nimejikuta nasema...wait a minute...I sometimes think like that too and I agree....
 
Mkuu Ogah,

Heshima mbele mkuu, ninajua kuwa wewe ni kichwa, ila sikutegmea kuwa one day utakuja na hizo very low ideas, hapa tunamjadili Mwalimu, na the good he did kwa taifa letu, na what he did not na impact yake kwa wale tuliobaki,

They can go to hell, tutakula manyasi, na the rest of your story, exactly hizo kauli kama ni kweli zilisemwa ziliuwa wananchi wangapi? As opposed na wananchi waliohamishwa bila ridhaa zao na kuachwa maporini wakiliwa na simba I mean your response ni out of the ishu kabisa mkuu, ndio maana unahitaji kujibiwa out of the ishu pia!

Sikutegemea wewe kuja na kauli kama hizi za personal, knowing a lot of things Mwalimu did using Mkapa, pale Daily News ambavyo they did affect directly your personal life, may be unahitaji kuelimishwa who was on your side of interest against those attacks, kwa sababu I know the whole story bro, ila mnahitaji kuwa makini na hoja zenu hapa,

Ahsante Mkuu!

........kutofautiana kimawazo sijambo baya....ili mradi iwe katika kujenga na si kubomoa.........watu tunatofautiana pia ktk perceptions kulingana na wakati.....

Idea za Mwl JKN alizoweka Mwanakiji ndio kinachojadiliwa hapa and nothing less......kama uliona nimekuwa off (kwa mtizamo wako)....fine.......however hainizuii kuonyesha niliyoyaandika ya kwamba pamoja na kuwa ideas za JKN hazikufanikiwa.....haimaanishi kuwa zilikuwa mbaya......na baadhi ya watu wamejaribu kulinganisha na yanayotokea sasa na idea alizokuwa nazo JKN (they were out of ishu as well)......na ndio maana nikaweka ulichokisoma........

....other stories are out of context.......

tuendelee kujadili ideas za JKN

Asante Mkuu
 
Mwanakijiji: Katika yote hayo uliyoyanukuu, hebu tuambie ni yapi mwalimu aliyafanya alipokuwa madarakani? Kama alishindwa kuyafanya in his 23 years of leadership, is it fair to say that he was simply good at fantasising and rhetoric making?

It is too well known that Nyerere was superb at preaching about change, the importance of democracy and people's development as opposed to 'vitu's' development. Now how much change did he himself bring and how much democracy and 'people's' development did he leave us behind? Until his time of departure from office, higher education (which is a typical people's development phenomenon), for example, was only accessible to the previledged few making it extremely elitist.


the question is, should we really be obsessed with a history of rhetoric making?

There is no doubt that Nyerere was a great African statesman, but I believe we have always overstated his success as a leader.
 
........kutofautiana kimawazo sijambo baya....ili mradi iwe katika kujenga na si kubomoa.........watu tunatofautiana pia ktk perceptions kulingana na wakati.....

Idea za Mwl JKN alizoweka Mwanakiji ndio kinachojadiliwa hapa and nothing less......kama uliona nimekuwa off (kwa mtizamo wako)....fine.......however hainizuii kuonyesha niliyoyaandika ya kwamba pamoja na kuwa ideas za JKN hazikufanikiwa.....haimaanishi kuwa zilikuwa mbaya......na baadhi ya watu wamejaribu kulinganisha na yanayotokea sasa na idea alizokuwa nazo JKN (they were out of ishu as well)......na ndio maana nikaweka ulichokisoma........

....other stories are out of context.......

tuendelee kujadili ideas za JKN

Asante Mkuu

Mawazo yanayolenga katika kuendeleza jamii yanapofeli kufanikiwa basi hayo labda si mawazo mazuri na kuendelea kuyang'ang'ania ukitegemea mabadiliko ni ujinga mtupu!
 
Mwanakijiji: Katika yote hayo uliyoyanukuu, hebu tuambie ni yapi mwalimu aliyafanya alipokuwa madarakani? Kama alishindwa kuyafanya in his 23 years of leadership, is it fair to say that he was simply good at fantasising and rhetoric making?

It is too well known that Nyerere was superb at preaching about change, the importance of democracy and people's development as opposed to 'vitu's' development. Now how much change did he himself bring and how much democracy and 'people's' development did he leave us behind? Until his time of departure from office, higher education (which is a typical people's development phenomenon), for example, was only accessible to the previledged few making it extremely elitist.


the question is, should we really be obsessed with a history of rhetoric making?

There is no doubt that Nyerere was a great African statesman, but I believe we have always overstated his success as a leader.

Kitila,

Niliuliza hili swali kwenye ile thread nyingine ya kumpondea Nyerere. Hivi lile swala la kufundisha watu (hata wazima) kusoma na kuandika lilifanywa na nani na kwa nini?

Hivi lile swala la kulazimisha watu kwenda shule (ilikuwa ni kosa la kisheria kwa mzazi au mtoto kutokwenda shule) lilikuwa na madhumuni gani.

Kwa nini wakati wa Nyerere watoto na wazazi wao walilazimishwa kwenda shule?
 
Mwanakijiji: Katika yote hayo uliyoyanukuu, hebu tuambie ni yapi mwalimu aliyafanya alipokuwa madarakani? Kama alishindwa kuyafanya in his 23 years of leadership, is it fair to say that he was simply good at fantasising and rhetoric making?

It is too well known that Nyerere was superb at preaching about change, the importance of democracy and people's development as opposed to 'vitu's' development. Now how much change did he himself bring and how much democracy and 'people's' development did he leave us behind? Until his time of departure from office, higher education (which is a typical people's development phenomenon), for example, was only accessible to the previledged few making it extremely elitist.


the question is, should we really be obsessed with a history of rhetoric making?

There is no doubt that Nyerere was a great African statesman, but I believe we have always overstated his success as a leader.

Most of his impractical ideas were fairy tales as far as I'm concerned! Watu hawakuwa na muda wa kukaa chini kuchambua na kumsikiliza alichokuwa akisema kwa sababu rumba lilikuwa kali. Ukiwa na njaa ndugu unachofikiria wewe ni mlo tu. Haya ya mawazo mazuri na blah blah kibao wakati watu wanasota doesn't make doggone sense to me.
 
Mawazo yanayolenga katika kuendeleza jamii yanapofeli kufanikiwa basi hayo labda si mawazo mazuri na kuendelea kuyang'ang'ania ukitegemea mabadiliko ni ujinga mtupu!

Kwa kuongezea tu NN, Mimi binafsi kwa kweli katika kusoma kusoma kwangu biographies za viongozi wa kisiasa, sijaona mahala ambapo kiongozi amesifiwa sana kwa sababu ya kile alichokisema. Kote niliposoma nimeona viongozi wakisifiwa kwa yale waliyoyafanya. Ni Tanzania ambapo viongozi anaweza akaambiwa ni 'kiboko' kwa yale aliyoyatamka kwenye mkutano wa hadhara
 
Kitila,

Niliuliza hili swali kwenye ile thread nyingine ya kumpondea Nyerere. Hivi lile swala la kufundisha watu (hata wazima) kusoma na kuandika lilifanywa na nani na kwa nini?

Hivi lile swala la kulazimisha watu kwenda shule (ilikuwa ni kosa la kisheria kwa mzazi au mtoto kutokwenda shule) lilikuwa na madhumuni gani.

Kwa nini wakati wa Nyerere watoto na wazazi wao walilazimishwa kwenda shule?

Hivi ni kwa nini watu walazimishwe kwenda shule kama hawataki? Mtu kama hataki kwenda shule then poa tu...huo ni uamuzi wake. Haya mambo ya kulazimishana hayana nafasi....kwanza wewe ni nani kunilazimisha mimi nifanye kitu....ebo!!
 
Kwa kuongezea tu NN, Mimi binafsi kwa kweli katika kusoma kusoma kwangu biographies za viongozi wa kisiasa, sijaona mahala ambapo kiongozi amesifiwa sana kwa sababu ya kile alichokisema. Kote niliposoma nimeona viongozi wakisifiwa kwa yale waliyoyafanya. Ni Tanzania ambapo viongozi anaweza akaambiwa ni 'kiboko' kwa yale aliyoyatamka kwenye mkutano wa hadhara

Kitila,

Is it fair to say kwamba Nyerere hakufanya chochote kabisa katika kuleta maendeleo ya Tanzania?
 
Hivi ni kwa nini watu walazimishwe kwenda shule kama hawataki? Mtu kama hataki kwenda shule then poa tu...huo ni uamuzi wake. Haya mambo ya kulazimishana hayana nafasi....kwanza wewe ni nani kunilazimisha mimi nifanye kitu....ebo!!

Swali langu ni kuwa, Nyerere alifaidika nini binafsi kwa kulazimisha watu kwenda shule?
 
Mwanakijiji....hizo unazodai fikra za Mwalimu si kwamba ni yeye pekee ndiye aliyekuwa akiwaza ama kufikiria hivyo! Ukiangalia kwa undani au hata kwa juu juu tu utaona kwamba mengi anayosema ni common sense na mara nyingi common sense ni relevant muda wote. Mimi sidhani kwa vile tu aliyaweka kwenye maandishi mawazo basi tuyafanye kuwa hayo ni mawazo aliyokuwa akiwaza Mwalimu na hakuna mwingine Afrika ama duniani aliyekuwa akifikiria kama hivyo. Nimesoma ulichochambua hapo juu na nimejikuta nasema...wait a minute...I sometimes think like that too and I agree....


mzee, one can not take credit for something he never uttered or put into writing. Ukiwaza tu yanabakia mawazo, ukiyaweka chini yanakuwa ya kwako hata kama watu wengine wanayawaza. So unakubaliana na Nyerere kuhusu suala la change. Very good.
 
Mwanakijiji....hizo unazodai fikra za Mwalimu si kwamba ni yeye pekee ndiye aliyekuwa akiwaza ama kufikiria hivyo! Ukiangalia kwa undani au hata kwa juu juu tu utaona kwamba mengi anayosema ni common sense na mara nyingi common sense ni relevant muda wote. Mimi sidhani kwa vile tu aliyaweka kwenye maandishi mawazo basi tuyafanye kuwa hayo ni mawazo aliyokuwa akiwaza Mwalimu na hakuna mwingine Afrika ama duniani aliyekuwa akifikiria kama hivyo. Nimesoma ulichochambua hapo juu na nimejikuta nasema...wait a minute...I sometimes think like that too and I agree....


In fact kuna kitabu kilichoandikwa miaka 1950 ninacho (The Future of Socialism, kimebeba yote aliyokuwa anayahubiri Mwalimu ikiwamo the famous "tunahitaji vitu vinne ili tuendelee" (hii ni neno kwa neno-isipokuwa ni kwa kiingereza). Bahati mbaya sijawahi kuona mwandishi yeyote akikiri kwamba mwalimu aliazima hii idea kutoka hicho kitabu.

Na inabidi watu waelewa hapa kwamba we are not at all trying to downplay Mwalimu's performance as a leader. All we are saying is that his success has always been overstated !
 
Mwanakijiji....hizo unazodai fikra za Mwalimu si kwamba ni yeye pekee ndiye aliyekuwa akiwaza ama kufikiria hivyo! Ukiangalia kwa undani au hata kwa juu juu tu utaona kwamba mengi anayosema ni common sense na mara nyingi common sense ni relevant muda wote. Mimi sidhani kwa vile tu aliyaweka kwenye maandishi mawazo basi tuyafanye kuwa hayo ni mawazo aliyokuwa akiwaza Mwalimu na hakuna mwingine Afrika ama duniani aliyekuwa akifikiria kama hivyo. Nimesoma ulichochambua hapo juu na nimejikuta nasema...wait a minute...I sometimes think like that too and I agree....

....at least hapa ulionyesha kukubaliana na ideas........sasa kama hayo ni maneno yako mwenyewe sasa sijui ujinga uko wapi wakati wewe mwenywe una-qualify your statement............ they were common sense na ni relevant muda wote!!!!.....obsessed?
 
mzee, one can not take credit for something he never uttered or put into writing. Ukiwaza tu yanabakia mawazo, ukiyaweka chini yanakuwa ya kwako hata kama watu wengine wanayawaza. So unakubaliana na Nyerere kuhusu suala la change. Very good.

Oh yeah...kuhusu hilo suala la change nakubaliana naye! Anybody with an ounce of common sense would know and agree with it. I'm pretty sure you can also vouch for things that you've heard other people say and be like..yeah..I was thinking exactly the same. Kwa hiyo sidhani kama suala la change ni big deal hadi ummwagie misifa hiivyo....that's just common sense my friend.
 
In fact kuna kitabu kilichoandikwa miaka 1950 ninacho (The Future of Socialism, kimebeba yote aliyokuwa anayahubiri Mwalimu ikiwamo the famous "tunahitaji vitu vinne ili tuendelee" (hii ni neno kwa neno-isipokuwa ni kwa kiingereza). Bahati mbaya sijawahi kuona mwandishi yeyote akikiri kwamba mwalimu aliazima hii idea kutoka hicho kitabu.

Na inabidi watu waelewa hapa kwamba we are not at all trying to downplay Mwalimu's performance as a leader. All we are saying is that his success has always been overstated !

Overstated is the keyword here. Good job Kitila!
 
Mwanakijiji: Katika yote hayo uliyoyanukuu, hebu tuambie ni yapi mwalimu aliyafanya alipokuwa madarakani? Kama alishindwa kuyafanya in his 23 years of leadership, is it fair to say that he was simply good at fantasising and rhetoric making?


Narudi kwenye msingi, do you agree with the substance of the "need to change" jinsi Mwalimu alivyoweka. Wewe unamuangalia Nyerere kama kiongozi na mtawala, mimi katika hili naangalia falsafa ya Nyerere independent of his leadership or administration. Ninajaribu kujenga hoja ya kuangalia maandishi yake intellectually na kuona umaana wake suala la kufeli au kufanikiwa kwangu halipo kwa wakati huu.

Ukilielewa hilo ndugu yangu tutaenda mbele kwani bado kuna fikra nyingi tu ambazo bado hatujazifikia. Suala la kutekeleza au la ni jingine. Kama nilivyosema, Plato alipoandika kuhusu "The Republic" yeye hakuwa mfalme, na Adam Smith walipoandika kuhusu kanuni za Uchumi yeye hakuwa Mkuu wa kitendo cha Benki balia likuwa anaanisha mambo kifalsafa.

Hata mababa wa Marekani walipotangaza Azimio la Uhuru wa Marekani na kuandika Bill of Rights wao wenyewe walikuwa wana watumwa, wanawake walikuwa hawapigi kura, na wuesi walikuwa ni theluthi moja ya mtu! Lakini ukweli wa fikra zao zile ambazo kwani ni "rhetoric" unabakia pale pale.

So, do you agree on the rhetorical ideas of Mwalimu on change as articulated in the quoted text? Kama hukubali, naomba unioneshe wapi hukubali, it is very simple.

the question is, should we really be obsessed with a history of rhetoric making?

Nope, the question is do you agree on the content and substance of Mwalimu's principle on change and the need of Africa to change? That is the question.


There is no doubt that Nyerere was a great African statesman, but I believe we have always overstated his success as a leader.

I'm not talking about Nyerere's success, nazungumzia his philosophy. We have just started with one theme, the theme on change. And will try to explore this theme a little bit more today. Kama hukubaliani nayo sema tu hukubaliani nayo na kwanini. Can you do that?
 
Back
Top Bottom