Fikra kuhusu watu wakimya

Fikra kuhusu watu wakimya

Wana JF hivi ni kwanini watu wakimya (wasio waongeaji kitabia) jamii huwachukulia kama wanadharau....
"kwanza kuna tofauti kubwa kati ya upole na ukimya.., pili usione watu wanakuwa kimya mioyo imekuwa migumu mithiri ya jiwe kutokana na mambo wanayoona ama kufanyiwa na watu wanaishi nao, pia mtu mkimya na mpole akibadilika(tabiambaya) huwa anazidi mara 3 zaidi ya tabia anayoiga"
 
Mm ni mkimya hasa kwa watu wagen kwangu ila mkimya kias kidogo nyumbani. Ila megundua ukimya umenifanya baadhi ya watu siwez kuongea nao kabisa wala kuwa nao karibu. Sifa mojawapo ya watu wakimya hupenda kusikiliza kwa makin na kuzisoma tabia na hisia za wengine hivyo hujikuta wale ambao umewaona huendan nao ni vigumu sana kuwa nao karibu na huwa wakimya wengi wanajua mengi juu ya mawazo ya wengine
Dah we ndo kama mimi copyright kabisa
 
Mtu mpole flegmatic huwa wanaendewa kwa upole na utaratibu km akili zao inavyotaka. Ukimkasirisha atageuka kuwa kichaa au atakufanya adui yake milele
Mwenzako anaongelea MKIMYA, sio MPOLE, wewe unataka badili mada.
 
Watu huzaliwa na tabia za ndani (introvert) na wengi huwa na tabia za nje (extrovert).

Watu wenye tabia za ndani huwa mara nyingi hawana ujasiri wa kuzungumza hadharani kwa sababu hukosa kujiamini ingawa ukiwapa waandike hutaamini kwa jinsi wanavyofahamu mambo. Hawa huwa wanasoma sana lakini hawajiamini sana Shuleni utawakuta licha ya kupasua pepa lakini wakati wa masahihisho hawazungumzi wala kuchangia. Mwalimu usipowaelewa utadhani ni kiburi au dharau lakini hapana wako hivyo kwa asili. Watu hawa wakipitishwa kwenye mifumo ya kishule kama za seminari ndio huzidi kuwa wapole na wakimya sana

Wale wenye ujasiri sana wa kuzungumza huwa ni watu wenye kujaaliwa kujiamini halafu hawana aibu hata wakikosea jambo kwao huona poa tu ilimradi amejaribu na kwa ujasiri huo hujaribu jaribu na kwenye vingi hufanikiwa baadhi ambavyo humzidishia ujasiri.

Kwa hiyo si kweli kwamba watu wapoe/wakimya ni dharau au kiburi.
 
Mm ni mkimya hasa kwa watu wagen kwangu ila mkimya kias kidogo nyumbani. Ila megundua ukimya umenifanya baadhi ya watu siwez kuongea nao kabisa wala kuwa nao karibu. Sifa mojawapo ya watu wakimya hupenda kusikiliza kwa makin na kuzisoma tabia na hisia za wengine hivyo hujikuta wale ambao umewaona huendan nao ni vigumu sana kuwa nao karibu na huwa wakimya wengi wanajua mengi juu ya mawazo ya wengine
Yaani hii umenigusa Mimi kabisa.
 
Huwa mimi wakati mwingine naulizaga kwa ndugu wa karibu, hivi mimi wananichuliaje? Mkimya au mpole? Au nipo seriasi sana? Manake kazini mimi ni mkali sana lakini pia nina huruma sana. Napendaga sana kuwapa ushauri wenye matatizo. Ila mwisho wa siku nashindwa kujielewa why naogopwa na watu wazima,watoto na vijana wenzangu? I don't understand!
Same to me
 
Baadhi ya tabia tunafanana sana,

mimi ile seriousness ndio watu hinoogopa, lkn huwa sipendi kumtania tania mtu, natanianaga, lkn kwa umakini, huwa nafikiria kabla sijatokwa na neno mdomoni.

Nadhani upole ma ukimya ni sawa tu
Wewe upo Kama Mimi kabla ya kuongea kitu lazima nitafakari sana na kukichambua kabla ya kuongea.
Na mara nyingi nikichangia mada au nikitoa neno linatoa conclusion moja kwa moja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom