FiFA wafuta red card baada ya Simu ya Trump

FiFA wafuta red card baada ya Simu ya Trump

Labani og

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2020
Posts
23,010
Reaction score
32,905
Katika hali ya kushangaza, Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) limempa ruhusa mshambuliaji Folarin Balogun kucheza mechi dhidi ya Ubelgiji. Licha ya kadi nyekundu aliyopewa awali, FIFA imetumia mamlaka yake chini ya Kifungu cha 27 kubadilisha adhabu hiyo kuwa “kifungo cha nje” (suspended ban), hatua inayomfanya kuwa huru kuingia dimbani.

Uamuzi huo umepokelewa kwa shangwe na Rais wa Marekani, Donald Trump, aliyetoa shukrani zake akisema: “Asante FIFA kwa kufanya kile kilicho sahihi, na kurekebisha dhuluma kubwa!” Hatua hii inafanana na ile iliyowahi kumsaidia Cristiano Ronaldo kabla ya mashindano kuanza.

Ingawa awali Shirikisho la Soka la Marekani (US Soccer) halikukata rufaa na Balogun mwenyewe akiwa Seattle alikuwa ameshakubali kukosa mchezo huo, sasa mshambuliaji huyo hatari atakuwepo kikosini. Kadi nyekundu itasalia kwenye rekodi yake, lakini hatokosa mechi yoyote, jambo linaloipa Marekani nguvu mpya kuelekea mtanange wao dhidi ya Ubelgiji.

Hii ndo maana ya world super power,😂😂
 

Attachments

  • 1783293942695.jpg
    1783293942695.jpg
    85.8 KB · Views: 12
FIFA inaendeshwa kisiasa kama ilivyo kwa TFF ya Wallace Karia. Imagine waliifungia Urusi kushiriki mashindano ya shirikisho lao kwa sababu tu iliivamia Ukraine. Israel nayo ilipoivamia Gaza na kuua hovyo maelfu ya wananchi, imeufyata! Ina siasa na double standards nyingi sana.
 
FIFA inaendeshwa kisiasa kama ilivyo kwa TFF ya Wallace Karia. Imagine waliifungia Urusi kushiriki mashindano ya shirikisho lao kwa sababu tu iliivamia Ukraine. Israel nayo ilipoivamia Gaza na kuua hovyo maelfu ya wananchi, imeufyata! Ina siasa na double standards nyingi sana.
Ndo hivyo mkuu....haiunaga democracy 100%
 
FIFA inaendeshwa kisiasa kama ilivyo kwa TFF ya Wallace Karia. Imagine waliifungia Urusi kushiriki mashindano ya shirikisho lao kwa sababu tu iliivamia Ukraine. Israel nayo ilipoivamia Gaza na kuua hovyo maelfu ya wananchi, imeufyata! Ina siasa na double standards nyingi sana.
Naomba marekani atolewe na ubelgili. Hii rushwa ya wazi kabisa
 
Back
Top Bottom