Fedha...

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
PESA INA MAJINA MENGI KULINGANA NA MAHALI NA MATUMIZI
1.Kwenye ibada inaitwa Zaka/sadaka
2.Msibani inaitwa rambirambi
3.Shule inaitwa Ada au Karo
4.Kwenye vyombo vya usafiri inaitwa nauli
5.Ukiinunulia haki inaitwa rushwa
6.Kumdhamini mtu mahakamani inaitwa dhamana
7.Kwenye uchaguzi inaitwa takrima
8.Ukiwapa kina Preta snowhite inaitwa hongo

Mengine tukumbushane....
 
Kitaani inaitwa mpunga, mkwanja, kisu, mawe,........

Tukiwa na Majita Home tunaita FUBA.

Nyani Ngabu .. ongezea na hizi


Mpango, michuzi pesa (money), michuzi, + mikwanja, mapene, masimbi, chambi chambi, bingo, chapaa, dola, famba, faranga, fuba, goto, jiwe, mafweza, mapene, mavumba, mbumba, michuzi, mkwanja, mshiko, ngawila, ngudongudo, uchache, vumba;

Baba wa taifa, bluu, buku, buku teni, kifaru, kilo, kisu, majani, mkoba, nusu kilo, pochi, tenga, vifaru viwili, wekundu wa msimbazi;

Bati, dala, doma, fisi, gobole, gwala, hais, jero, jiti, karume, mbala, njoroge, nyanga, nyento, nyomi, paundi, pini.
 
Nyani Ngabu .. ongezea na hizi


Mpango, michuzi pesa (money), michuzi, + mikwanja, mapene, masimbi, chambi chambi, bingo, chapaa, dola, famba, faranga, fuba, goto, jiwe, mafweza, mapene, mavumba, mbumba, michuzi, mkwanja, mshiko, ngawila, ngudongudo, uchache, vumba;

Baba wa taifa, bluu, buku, buku teni, kifaru, kilo, kisu, majani, mkoba, nusu kilo, pochi, tenga, vifaru viwili, wekundu wa msimbazi;

Bati, dala, doma, fisi, gobole, gwala, hais, jero, jiti, karume, mbala, njoroge, nyanga, nyento, nyomi, paundi, pini.

Umemaliza kila kitu umesahau lakaki(buku tali aka buku 5)
 
ukiikusanya nyingi inaitwa utajiri

ukiikusanya kidogo inaitwa umaskini

ukiikusanya nyingi kwa njia mchanganyiko wa hongo na rushwa inaitwa ufisadi

Apeche alolo, arosto, waya, mabaga, majalala, ukapa, chacha, chalala, kalukwa, kauka, pigika, rosti, uawa kishenzi, ungua jua, waka;
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom