Fao la kujitoa lafutwa rasmi

Fao la kujitoa lafutwa rasmi

Kwa hiyo wanataka tuchapike na maisha.. ila ikifikia tunataka tufe kwa maradhi wanatutibia kwa hela zetu za pensheni ili turudi tena kuchapika na maisha
 
Ni Kweli kaka, Katika Nchi hii mitaji ya biashara ni ngumu kupata na mikopo hakuna

Mkombozi wa Mtanzania Mnyonge ilikuwa FAO LA KUJITOA

Nchi kunyimwa misaada ni kiburi cha watawala....
Hii kitu alionywa lakin hakusikia.. akajitapa hii nchi ni tajir so misaada haitaji.
Ona sasa..
 
Mimi nilipanga nikalime na mazingira nimeandaa mtaji wangu ndio nnsf. Benki hawatoi mikopo kirahis. Sina kazi na kazi niliokuwa naifanya nilibahatisha kamkataba ka mwaka mmoja leo sina kazi na nimeamua kulima hata kama ni heka moja inatosha kuanzia leo sina nnsf imechukuliwa nianzie wapi mimi tena. Kweli mwenye kugombana na anayejiua wanafanana mana ni kuzidiwa kwa mateso
 
yani jamani tanzania tunaonewa sana, pesa zetu afu tunawekewa masharti.
 
Me nawaambia kila siku tume huru idaiwe mapema Tanzania ccm itoke vinginevyo watanzania mtapata tabu sana.
 
Wanatulazimishia magonjwa? Bima ya afya itamsaidiaje MTU kujikwamua kiuchumi baada ya ajira kukoma ?wasipougua je ?tuache uhuni.kwani walikuwa na mkataba wa fedha yao kugeuzwa bima ya afya ?
Unajua nimeshangaa sana... nani ni think tank wao? Anawapa mawazo ya kijinga kama haya.
Bima ya afya inamsaidiaje mtu akiwa hayupo kazin?
Watu wanataka kujiajiri, waweke mirad iwasaidie baada ya kustaafu alafu unabana hela yao ,unaweka bima ya afya, hiyo bima inawasaidiaje baada ya kustaafu au kuondolewa kazini?
 
TUCTA is time muoneshe msimamo wenu, no more uwoga , no more kujipendekeza kwa mheshimiwa. Hii inawahusu ninyi wafanyakaz ,why serikali iwabane iwawekee mazingira magum wakati nyie ndio moyo wa nchi hii?
 
Kuhusu fao la kujitoa wafanyakazi hatujui haki zetu,inakuwaje mtu contract yako iishe wakwambie usubiri miaka 55? Kama ni hivyo tunataka kwanza waje nasheria ambayo inasema unaajiliwa in terms of parmanent basis,Halafu viongozi wetu vichwa nazi hawajui athari za watu kutokuwa na ajira?


We ukinipa hela yangu nitaanzisha biashara au kilimo nitalipa kodi sasa nyie vichwa nazi nani amewaambia mninyime jasho langu?

Nyie vichwa Nazi mnaosema Tanzania ni yetu sote kama mimi ni sehemu ya Tanzania mbona mnataka kupola jasho langu ambalo limenivuja huku mkiomba niteketee na familia yangu? Mbona mmekuwa kama wakoloni.

Nyie vichwa nazi mnaoomba Tanzania yenye amani wakati mnataka kupola fao langu na familia yangu huku nyie baada ya miaka mitano au kumi mnalipatana mamilioni tena kwa kodi yangu ya PAYE na mnataka kupola fedha yangu kidogo.

Mheshimiwa Rais mimi si mwanasiasa kwa hili angalia nyuma, Wengine hatuna sehemu ya kusemea,Wengi ambao tunalia kuhusu hili fao la kujitoa ni wale watoto wa wakulima,usitegemee watoto wa akina Mbowe,Lowassa,Pinda,Membe,Maghembe,Mengi, Jenista Mhagama,Kabudi,Tundu Lissu,Ndugai na etc watakuja kulialia kama sisi,hawajui shida,Watoto wao hawajawahi kwenda shule bila viatu,hawajawahi kunywa uji wenye chunvi,hawajawahi kula ugali wenye wadudu kule bording,hawajawahi kusomea vibatari,hawajawhi kung'atwa na kunguni na kwenye ajira ni mwendo wa memo tu,

Hao watoto contract zao zikiisha tu kesho tu kalamba dume,Sisi watoto wa masikini kupata kazi nyingine inachukua muda na inawezekana usipate kabisa,Mheshimiwa Rais hizi ni sauti za wafanyakazi iliayo toka nyikani tafadhali hili usidharau, hao uliowapa madaraka hawana uchungu na sisi watoto wa masikini akina kayehura anisamehe kama nimekosea jina lake,Erio hawakukuchagua hawana cha kupoteza.

Baba mbona wamachinga uliwasikiliza sisi wa Sector binafsi unataka kutunyima fao letu? Angalia migodi inafungwa kwamba wanaingia hasara uzalishaji unapungua,Tanzanite one watu waliachishwa kazi wapo mtaani, Fastjet,Tigo kwa wahindi ndiyo maelfu,The Gurdian,TBL nakadhalika.

Serikali,Wabunge, Mahakama,Waajiri,Wafanyakazi na Wananchi hili suala linagusa masilahi ya mtu ambaye ni mfanyakazi,Wabunge ambao mnatuona wafanyakazi si lolote,Kwa sababu mnakopa kwenye mifuko yetu,mmegeuka wanyonyaji wa watanzania badala ya kuwasaidia eeh mungu tusaidie tuepshie mbali na hawa waliojaa shibe.

Mwisho mheshimwa Rais hata hao viongozi wetu ni walewale ambao wanapatikana kiujanjaujanja tu,hawapo kwa ajili yetu kwa ajili ya matumbo yao chaguzi zetu hazina tofauti na zile za vyama vya Siasa Rushwa tupu.
Hili fao la kujitoa linagusa vijana wengi ambao ndiyo nguvu kazi ya Taifa,Wazee haliwahusu kwa sababu wanauhakika baada ya miaka miwili mitatu wanachukua chao hata ukiangalia hao viongozi wetu ungewauliza nani ameajiliwa kwa mkataba hayupo hata mmoja ndiyo hawawezi kutusemea.

Njaa huleta wivu,husda,hasira na chuki katika Jamii,ehhee mungu tuokoe na dhulumama kwenye nchi yangu.
 
Hakuna shida, miaka minne ijayo tuna wa replace hawa baffoons na viongozi wangine. Fao letu litarudishwa tu
Jipe moyo tu, CCM mnaweza kuing'oa kwa Tume ya akina Jecha na Katiba hii?

Magu ameshatangaza kabisa Katiba mpya sio kipaumbele, bali kutunyoosha kwanza.

Vv
 
Sijakuelewa mkuu, unaposema Fao la kujitoa Withdraw Benefit imefutwa na badala yake ni Bima ya Afya. Naomba ufafanuzi kwani sioni kama fao la bima ya afya inaweza kukidhi mahitaji mengine kama ambavyo fao kujitoa lilivyo.

Dodoma. Serikali imesema fao la kujitoa halipo,badala yake imekuja na fao la bima ya afya.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bungena Vijana), Jenista Mhagama alisema hayo bungeni
jana kuwa suala la fao la kujitoa haliwezekani kwa sasa na badala yake imeanzisha mchakato wa fao la
bima ya afya ambalo itakuwa ni mbadala wa fao la kujitoa.

“Katiba ya Tanzania katika kifungu cha 11
kinaeleza namna ambavyo mifuko hiyo
(akimaanisha ya hifadhi ya jamii) inapaswa kuwa,
lakini hata juzi Mheshimiwa Rais aliagiza
utengenezwe utaratibu katika bima ya mfuko na
itakuwa ni mbadala wa watu wasiokuwa na ajira,”
alisema Mhagama.
Mapema bungeni jana, swali kuhusu malipo ya mafao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii liliwaibua wabunge wengi waliotaka kuuliza maswali ya nyongeza licha ya mawaziri kutoa majibu.

Akijibu swali la wafanyakazi waliopatikana na vyeti feki kama wanaweza kulipwa mafao yao Waziri wa Utumishi Angella Kairuki ali hatuwezi
kutoa taarifa kwa sasa kwani bado
wanashughulikia jambo hilo ili kuona namna bora ya kufanya na wakifikia hatua nzuri watatoa majibu ya kuaminika na kuomba wapewe muda kwa sasa
Mapema mbunge wa Viti Maalumu,
Amina Mollel alitaka kujua kwa nini wafanyakazi waliopatikana na vyeti feki wasilipwe mafao yao.

Naibu wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera, Uratibu na Bunge), Anthony Mavunde alisema kuanzishwa kwa mifuko ya jamii kumefikia hatua mbalimbali ikiwamo kukamilika kwa tathimini ya mifuko ya hifadhi ya jamii
(actuarial evaluation) ambayo imetoa mapendekezo kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatia katika kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii.

“Mpaka sasa Serikali haijafanya uamuzi rasmi wa idadi ya mifuko itakayobaki baada ya kulinganisha mifuko iliyopo hivi sasa,” alisema Mavunde.


Chanzo..Mwananchi
 
Katika awamu hii kila tamko kuhusu utumishi wa umma ni la kumuumiza tu mfanyakazi.Kila siku ya jana yanakuwa nafuu.
 
Dodoma. Serikali imesema fao la kujitoa halipo,badala yake imekuja na fao la bima ya afya.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bungena Vijana), Jenista Mhagama alisema hayo bungeni
jana kuwa suala la fao la kujitoa haliwezekani kwa sasa na badala yake imeanzisha mchakato wa fao la
bima ya afya ambalo itakuwa ni mbadala wa fao la kujitoa.

“Katiba ya Tanzania katika kifungu cha 11
kinaeleza namna ambavyo mifuko hiyo
(akimaanisha ya hifadhi ya jamii) inapaswa kuwa,
lakini hata juzi Mheshimiwa Rais aliagiza
utengenezwe utaratibu katika bima ya mfuko na
itakuwa ni mbadala wa watu wasiokuwa na ajira,”
alisema Mhagama.
Mapema bungeni jana, swali kuhusu malipo ya mafao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii liliwaibua wabunge wengi waliotaka kuuliza maswali ya nyongeza licha ya mawaziri kutoa majibu.

Akijibu swali la wafanyakazi waliopatikana na vyeti feki kama wanaweza kulipwa mafao yao Waziri wa Utumishi Angella Kairuki ali hatuwezi
kutoa taarifa kwa sasa kwani bado
wanashughulikia jambo hilo ili kuona namna bora ya kufanya na wakifikia hatua nzuri watatoa majibu ya kuaminika na kuomba wapewe muda kwa sasa
Mapema mbunge wa Viti Maalumu,
Amina Mollel alitaka kujua kwa nini wafanyakazi waliopatikana na vyeti feki wasilipwe mafao yao.

Naibu wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera, Uratibu na Bunge), Anthony Mavunde alisema kuanzishwa kwa mifuko ya jamii kumefikia hatua mbalimbali ikiwamo kukamilika kwa tathimini ya mifuko ya hifadhi ya jamii
(actuarial evaluation) ambayo imetoa mapendekezo kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatia katika kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii.

“Mpaka sasa Serikali haijafanya uamuzi rasmi wa idadi ya mifuko itakayobaki baada ya kulinganisha mifuko iliyopo hivi sasa,” alisema Mavunde.


Chanzo..Mwananchi
 
Kuhusu fao la kujitoa wafanyakazi hatujui haki zetu,inakuwaje mtu contract yako iishe wakwambie usubiri miaka 55? Kama ni hivyo tunataka kwanza waje nasheria ambayo inasema unaajiliwa in terms of parmanent basis,Halafu viongozi wetu vichwa nazi hawajui athari za watu kutokuwa na ajira?


We ukinipa hela yangu nitaanzisha biashara au kilimo nitalipa kodi sasa nyie vichwa nazi nani amewaambia mninyime jasho langu?

Nyie vichwa Nazi mnaosema Tanzania ni yetu sote kama mimi ni sehemu ya Tanzania mbona mnataka kupola jasho langu ambalo limenivuja huku mkiomba niteketee na familia yangu? Mbona mmekuwa kama wakoloni.

Nyie vichwa nazi mnaoomba Tanzania yenye amani wakati mnataka kupola fao langu na familia yangu huku nyie baada ya miaka mitano au kumi mnalipatana mamilioni tena kwa kodi yangu ya PAYE na mnataka kupola fedha yangu kidogo.

Mheshimiwa Rais mimi si mwanasiasa kwa hili angalia nyuma, Wengine hatuna sehemu ya kusemea,Wengi ambao tunalia kuhusu hili fao la kujitoa ni wale watoto wa wakulima,usitegemee watoto wa akina Mbowe,Lowassa,Pinda,Membe,Maghembe,Mengi, Jenista Mhagama,Kabudi,Tundu Lissu,Ndugai na etc watakuja kulialia kama sisi,hawajui shida,Watoto wao hawajawahi kwenda shule bila viatu,hawajawahi kunywa uji wenye chunvi,hawajawahi kula ugali wenye wadudu kule bording,hawajawahi kusomea vibatari,hawajawhi kung'atwa na kunguni na kwenye ajira ni mwendo wa memo tu,

Hao watoto contract zao zikiisha tu kesho tu kalamba dume,Sisi watoto wa masikini kupata kazi nyingine inachukua muda na inawezekana usipate kabisa,Mheshimiwa Rais hizi ni sauti za wafanyakazi iliayo toka nyikani tafadhali hili usidharau, hao uliowapa madaraka hawana uchungu na sisi watoto wa masikini akina kayehura anisamehe kama nimekosea jina lake,Erio hawakukuchagua hawana cha kupoteza.

Baba mbona wamachinga uliwasikiliza sisi wa Sector binafsi unataka kutunyima fao letu? Angalia migodi inafungwa kwamba wanaingia hasara uzalishaji unapungua,Tanzanite one watu waliachishwa kazi wapo mtaani, Fastjet,Tigo kwa wahindi ndiyo maelfu,The Gurdian,TBL nakadhalika.

Serikali,Wabunge, Mahakama,Waajiri,Wafanyakazi na Wananchi hili suala linagusa masilahi ya mtu ambaye ni mfanyakazi,Wabunge ambao mnatuona wafanyakazi si lolote,Kwa sababu mnakopa kwenye mifuko yetu,mmegeuka wanyonyaji wa watanzania badala ya kuwasaidia eeh mungu tusaidie tuepshie mbali na hawa waliojaa shibe.

Mwisho mheshimwa Rais hata hao viongozi wetu ni walewale ambao wanapatikana kiujanjaujanja tu,hawapo kwa ajili yetu kwa ajili ya matumbo yao chaguzi zetu hazina tofauti na zile za vyama vya Siasa Rushwa tupu.
Hili fao la kujitoa linagusa vijana wengi ambao ndiyo nguvu kazi ya Taifa,Wazee haliwahusu kwa sababu wanauhakika baada ya miaka miwili mitatu wanachukua chao hata ukiangalia hao viongozi wetu ungewauliza nani ameajiliwa kwa mkataba hayupo hata mmoja ndiyo hawawezi kutusemea.

Njaa huleta wivu,husda,hasira na chuki katika Jamii,ehhee mungu tuokoe na dhulumama kwenye nchi yangu.
Naomba ujumbee huu uwafikie wahusika wenye mamlaka, labda wanaweza kulitazama upya hili suala
 
Ntaendelea kukomaa hadi dakika ya mwisho hapa mgundini kwangu lakini siyo nikaajiliwe na mtu.
 
Watetezi wa haki za binadamu kwani haki ya mtu ni kuishi tu?ninapopolwa haki yangu mbona mko kimya?
 
Ingeleta maana endapo mafao yetu yangetunzwa ktk dollar na sio tshs. Maana kama leo nimeachishwa kazi na kahelakangu waliko nako kwamfano ni 20m miaka 20 ijayo haitakua na thamani tena kulingana na hali yamaisha itakavyo kua
 
Hizi kadi za bima ya Afya ndio zitazonunua sukari,mchele pamoja na kulipia ada za watoto wetu? I xo piced off !
 
Back
Top Bottom