Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Ndugu uliyeanzisha uzi huu nataka nianze kutoa pongezi za dhati kwa uzi huu ulioanzisha ambao naamini utakuwa na manufaa makubwa kwa watu wengi.
Niko katika tafakari za kuanzisha michakato ya ujenzi, maswali yangu:-
1. Ni kiwanja chenye ukubwa gani kinafaa kwa ujenzi wa nyumba ya vyumba vitatu nyumba ya kawaida kabisa ya kitanzania.
2. Faida za ujenzi wa interlocking bricks (Dodoma).
Ninabaki nikiwa na moyo wa Shukrani nikisubiria majibu.
 
Minimum angalau kiwe na 400sqm ili ubakiwe na space ya kufanya vitu vingine.
Ndugu uliyeanzisha uzi huu nataka nianze kutoa pongezi za dhati kwa uzi huu ulioanzisha ambao naamini utakuwa na manufaa makubwa kwa watu wengi.
Niko katika tafakari za kuanzisha michakato ya ujenzi, maswali yangu:-
1. Ni kiwanja chenye ukubwa gani kinafaa kwa ujenzi wa nyumba ya vyumba vitatu nyumba ya kawaida kabisa ya kitanzania.
2. Faida za ujenzi wa interlocking bricks (Dodoma).
Ninabaki nikiwa na moyo wa Shukrani nikisubiria majibu.
Angalau kiwe na sqm 400 , ili ubakiwe na space ya kufanya mambo mengine.

Interlocking sijaona faida yake mpaka Leo. Nawashauri wateja wangu kutumia block.

Pia ujenzi wa Dodoma una gharama kulinganisha na Dsm
 
Minimum angalau kiwe na 400sqm ili ubakiwe na space ya kufanya vitu vingine.

Angalau kiwe na sqm 400 , ili ubakiwe na space ya kufanya mambo mengine.

Interlocking sijaona faida yake mpaka Leo. Nawashauri wateja wangu kutumia block.

Pia ujenzi wa Dodoma una gharama kulinganisha na Dsm
Watu wengi huwa wagumu kukubali mabadiliko, teknologia za ujenzi zimebadilika ila wengi bado tumebaki nyuma. Kuna ujenzi wa kutumia panels, interlocks bricks n.k

Faida za interlock bricks;
1. Matofari yanatumia kiasi kidogo cha saruji katika utengenezaji wake. Mfano mfuko 1 wa saruji unatoa tofari 75 hadi 90.
Pia katika kujenga inatumia kiasi kidogo cha saruji kutokana na mfumo wa kufungamana (locks) hivyo kusaidia kuokoa gharama za matumizi ya saruji na mchanga.

2. Ujenzi wa namna hii hauna ulazima wa kupiga plasta hivyo kuokoa gharama za saruji, mchanga, gharama ya fundi na gharama zinazohusiana na plasta kama skimming, white Cement, Gypsum powder, rangi n.k

3. Faida nyingine utapata nyumba yenye muonekano mzuri isiyokua na joto kali ndani.

Kwa ujumla ujenzi huu upunguza gharama za ujenzi kwa 30% hadi 40%.

bfe28f12d43098c73421b659b6b99727.jpeg
bca2a9bc43122a46ba9dad2d2d228478.jpeg
7e31b4df7247ff0700f62fee1b752f82.jpeg
447eb89001c0f5992f417c2736bd5f44.jpeg
 
Watu wengi huwa wagumu kukubali mabadiliko, teknologia za ujenzi zimebadilika ila wengi bado tumebaki nyuma. Kuna ujenzi wa kutumia panels, interlocks bricks n.k

Faida za interlock bricks;
1. Matofari yanatumia kiasi kidogo cha saruji katika utengenezaji wake. Mfano mfuko 1 wa saruji unatoa tofari 75 hadi 90.
Pia katika kujenga inatumia kiasi kidogo cha saruji kutokana na mfumo wa kufungamana (locks) hivyo kusaidia kuokoa gharama za matumizi ya saruji na mchanga.

2. Ujenzi wa namna hii hauna ulazima wa kupiga plasta hivyo kuokoa gharama za saruji, mchanga, gharama ya fundi na gharama zinazohusiana na plasta kama skimming, white Cement, Gypsum powder, rangi n.k

3. Faida nyingine utapata nyumba yenye muonekano mzuri isiyokua na joto kali ndani.

Kwa ujumla ujenzi huu upunguza gharama za ujenzi kwa 30% hadi 40%.

View attachment 1550510View attachment 1550515View attachment 1550517View attachment 1550518
Sitaki kuharibu biashara za watu lkn msimamo wangu kwa client ni kuwa ni bora kutumia block. Hata wewe najua unafahamu ni nini kinatokea baada ya mfupi kupita kwenye hayo majengo.
 
Hapa nitaelezea Sababu za msingi zinazosababisha majengo yanayofanana kujengwa kwa gharama tofauti.

Tuzungumzie mchoro wa nyumba ya vyumba vitatu vya Kulala kimoja kati ya hivyo ni master bedroom, sitting room, dining, kitchen ,public toilet na store.
Mchoro aliununua ndugu anaitwa Juma, baada ya Juma kununua Alitoa copy akawapa majirani zake wawili Hasani na John.

Hawa wote walijengewa na fundi mmoja ambae ni mimi. Lkn Kila mtu kutumia gharama tofauti kusimamisha boma.

SABABU ZA MSINGI ZA KUFANYA GHARAMA ZA UJENZI ZITOFAUTIANE :

1. location
2. Uimara
3.land type. (slop au tambalale)
4.soil type
5.nyakati.

HAPA NITAZUNGUMZIA UIMARA
Msingi wa nyumba imara utajengwa Kama ifuatavyo.
. Utachimbwa kwenda chini urefu WA mita moja au zaidi.
. Utaanza na zege yenye ratio nzuri kabla ya kujenga tofali
.Utajengwa kwa tofali imara
.Utawekewa Beam yenye kusukwa nondo na ratio nzuri
.Utamwagiliwa maji ya kutosha.
ILI HAYA YOTE YAFANYIKE LAZIMA UMPATE FUNDI MZURI.

Juma aliomba nyumba yake nimjengee kwa viwango hivyo, ndio maana nilitumia tofali nyingi,cement nyingi, nondo nyingi, mchanga mwingi, kokoto nyingi, ring za kutosha, maji mengi nk. Ktk kujenga msingi.

John alisema uwezo wake mdogo , yeye alihitaji tuchimbe futi moja kwenda chini baada ya hapo tujenge tofali, hakuishia hapo pia alisema tusiweke Beam.

Kilichotekea ni utofauti wa Tshs zaidi ya million nne kati ya hiyo misingi miwili.

Kiufupi Juma alitumia 6mil
John Tshs 2.8mil
Hasani Tshs 4mil.

Kilichotofautisha ni uimara WA kujenga msingi. Hawa wote ni majirani.

Mpaka tunamaliza boma Juma alitumia 18m
John 7m
Hasani 12m.
Nyumba zote hizi zikipigwa rangi vizuri hutoweza kujua madhaifu ya awali mpaka pale utakapoanza kuona nyufa (expansion joint)

Hoja yangu hapa ni kwamba unapotokea mjadala wa gharama za ujenzi LAZIMA tuzingatie vitu mhimu vinavyosababisha gharama kuwa kubwa au ndogo.

Ushauri.
1.Tusipende kukimbilia kununua nyumba wakati hujui ilijengwa kwa viwango vipi.
2.Jenga nyumba imara ogopa vya Bei cheee
3.Nyumba kuijenga si lelemama, ili kumudu anza mdogomdogo. Ukiwa na 5m anza hata msingi.

Ukihitaji fundi, usisite kunitafuta, nafanya kazi mikoa yote tanzania
0655173113


UPDATES
tuendelee na mjadala wetu. Hapo awali tulijadili jinsi namna gani uimara wa nyumba unavyoathiri gharama za ujenzi. Leo tujadili namna location inavyoathiri gharama za ujenzi.

NAMNA LOCATION INAVYOSABABISHA GHARAMA ZA UJENZI KUWA TOFAUTI.

Mungu aliumba ardhi ktk mionekano tofauti. Kuna tambalale, milima na mabonde.
Ujenzi ktk Eneo tambalale unagharama nafuu kulinganisha na Eneo lenye slope . Lakini pia ujenzi wa Eneo tambalale lililoko Chanika mkoni DSM Unaweza kuwa na gharama tofauti na ujenzi wa Eneo tambalale lililoko msasani mkoani DSM. Hivyo hivyo ujenzi wa DSM unagharama kubwa kuliko ujenzi wa Mbeya.

SABABU ZA KUTOFAUTISHA GHARAMA KATI YA ENEO TAMBALALE NA LENYE SLOP.

sanasana hapa kimbembe huwa ktk kujenga msingi wa nyumba.

Msingi uliotumia tofali 1500 katika eneo tambalale, msingi huohuo ukitaka kuujenga ktk eneo lenye slope unaweza kutumia tofali 2300 au zaidi kulingana na ukali wa slope.
Tukumbuke kwamba Kwa kadri tofali zinavyoongezeka ndivyo na material mengine yanavyozidi kuongezeka kitu ambacho hupelekea kuongezeka kwa gharama za fundi. Si ajabu kumalizia 10mil ktk msingi wa nyumba ya Vyumba vitatu ktk Eneo LA slope.

Hivyo basi kama hutaki kutumia gharama kubwa kwenye ujenzi epuka kununua viwanja vilivyo na slope.

Jambo lingine linaloathiri ktk location ni upatikanaji wa material.
Mfano mtu anaejenga mbezi beach atanunua tani 18 Za mchanga zaidi ya 450.000 Tshs wakati mtu wa Chanika atanunua Kwa 220,000tshs.

Pia boma utakalojenga kwa 8mil Mbeya, DSM utalijenga Kwa zaidi ya 15mil. Sababu Mbeya tofali ni cheap, labour ni cheap nk.

JE, WAJUA KWAMBA KUNA MFUMO MPYA WA MAJI TAKA AMBAO HAUJAZI MASHIMO YA VYOO! USIHANGAIKE NA MFUMO WA ZAMANI. PATA MFUMO MPYA UACHANE NA GHARAMA ZA KUITA GARI ZA KUNYONYA UCHAFU.

Kwa ujenzi imara na wakisasa tutafutane 0655173113
Mungu akubariki. Ni mwl mwema!
 
Back
Top Bottom