Fahamu mambo mbalimbali kuhusu Kilimo cha Korosho

Asante wadau. Nimeufuatilia uzi toka mwanzo una mawazo ya kujenga. Binafsi nilikuwa na wazo hili na mwaka huu nitaanza na hekari tano hadi kufikia lengo la hekari 20.
 
HABARI,
"Revolution,
Kweli mbole ya samadi sehemu nyingi ni adimu hata za viwandani zinafaa kutumika hizo husaidia kukuza haraka ila ki uhalisia hata ukipanda bila mbolea hii miti inaota na utavuna kama kawaida ila tofauti ya Kutumia mbolea husaidia kukua kwa haraka.

LUMUMBA
Ufafanuz murua mkuu.

Mimi Nina maswali kadhaa. Ushirika hukusanya korosho za wakulima,je.kuna malipo yoyote ya awali ambayo wakulima hulipwa? Au malipo pekee mpka mnada ufanyike ndo walipwe. Pia gharama za usafirishaj wa korosho ghafi kutoka kwa mkulima mpka sehemu za kuhifadhi hugharamiwa na mkulima?

Naomba ufafanuz wako mkuu
 
Asante sana mkubwa kwa jitihada zako za kutuelimisha na kuhamasisha ukulima huu wa korosho.

Samahani nina swali ambalo lipo nje kidogo na mada yako ya leo,ni hivi kuna taarifa kuwa sababu ya korosho yetu kuwa na soko ni kwa kuwa inatoka msimu ambao duniani kote hawavuni.

Je, ni habari za ukweli?ikiwa ni kweli vipi mikoa mingine ambayo ndo kwanza wanahamasishwa kulima?nao itatoka msimu mmoja na korosho za kusini?
 
Nashukuru sana mkuu Lumumba, nimepitia Uzi wote nauliza swali ambalo halijaulizwa, Je unaweza kumwagilia mikorosho labda kwa kutumia Sprinkler kila siku jioni kwaajili ya kuifanya ikue haraka haraka? Au unaweza shauri umwagiliaji kwa ratiba ipi? Case study ya shamba ambalo Lipo Lindi.


HABARI,
"Shark's Style,

Asante kwa kupitia uzi wote na kuelewa na Pia hongera kwa kuweka mkazo kwenye kilimo hiki cha korosho Ila napenda kushauri ni vema ukafika kwenye mashamba darasa na pia kwenye vituo vya utafiti kwa mafunzo zaidi.

Kwa umwagiliaji ni jambo zuri sana kama unachanzo kizuri cha maji ila kwa kutumia Sprinkler sishauri ufanye hivyo kwani utapoteza maji mengi kwakuwa miti iko mbalimbali tofauti na mahindi ni bora umwagilie kwa ndoo au mpira kwa shimo mojamoja kwani Mikorosho haitaji maji kilasiku ukuaji hautakuwa mzuri.

Kwa kipindi cha kiangazi umwagiliaji mzuri ni ndoo ya lita kumi kwa kila shimo kwa wiki moja inatosha sana,Ila kama utakuwa unamiche iliyofikia upana wa peni na ukapanda kipindi cha mvua na mche ukapata mvua kwa miezi 4-5 inatosha sana kuendelea kukua wenyewe na mikoa hiyo inamvua za kutosha sana.

Pia kama ni kipindi cha kiangazi unaweza kuzungushia mche na majani makavu kwa kuhifadhi unyevu.

LUMUMBA
 
Ufafanuz murua mkuu.
Mimi Nina maswali kadhaa. Ushirika hukusanya korosho za wakulima,je.kuna malipo yoyote ya awali ambayo wakulima hulipwa? Au malipo pekee mpka mnada ufanyike ndo walipwe.. Pia gharama za usafirishaj wa korosho ghafi kutoka kwa mkulima mpka sehemu za kuhifadhi hugharamiwa na mkulima?

Naomba ufafanuz wako mkuu


HABARI,
"BILGERT,
Unapokuwa kwenye ushirika huwa mara nyingi mpaka mnada ufanyike ndio mkulima analipwa ila mkulima ndio unatumia gharama zako kupeleka mazao yako kwenye ushirika,Ila kuna baadhi ya ushirika huwa wanakuwa na mkataba na mtu kusafirisha zao la washirika mnada ukifanyika mkulima anakatwa pesa ya usafiri kwa kilo au tani kutokana na ukubwa wa mavuno ya mkulima

LUMUMBA
 
Asante sana mkubwa kwa jitihada zako za kutuelimisha na kuhamasisha ukulima huu wa korosho,

Samahani nina swali ambalo lipo nje kidogo na mada yako ya leo,ni hivi kuna taarifa kuwa sababu ya korosho yetu kuwa na soko ni kwa kuwa inatoka msimu ambao duniani kote hawavuni...

Je ni habari za ukweli?ikiwa ni kweli vipi mikoa mingine ambayo ndo kwanza wanahamasishwa kulima?nao itatoka msimu mmoja na korosho za kusini?

HABARI,
"jombezi,

Asante nawe pia,Usijali hujatoka nje ya mada,Hizo habari ni za kweli ila sio duniani kote sisi msimu wetu tunavuna sawa na msumbiji ila kipindi hicho nchi kama India na Africa magharibi wanakuwa hawavuni hiyo ndio sababu kubwa inayofanya korosho yetu kuwa na bei kubwa na sio kuwa kubwa ila ni kuwa katika kipindi hicho kwenye soko la dunia korosho huwa bei iko juu kwani mahitaji ni makubwa Supply ni ndogo.

Sasa sisi ni Nchi ya 8 kwa duniani na ya 4 kwa Africa kwa uzalishaji wa korosho sasa Nchi kama India ambayo ni ya 3 Kwa uzalishai duniani na Nchi ya 1-3 kwa uzalishaji kwa africa Nigeria, Ivory coast, Guinea Bissau ambazo zinaongoza kwa africa zinakuwa nje ya msimu lazima korosho iwe bei juu kipindi hicho. Lingine Tanzania tuna mbegu za korosho ambazo zinasifika sana kwa ukubwa Nayo hiyo inachangia sana Korosho zetu kuwa na soko zuri. Hapo utakuwa umenipata kidogo Comrade.

LUMUMBA
 
Sawa. Hiyo namna ya "kubebesha" inaweza kutumika kwa mimea mingine pia, au ni kwa mikorosho pekee?
 
Shukrani sana Nimenunua ekari tano kwa kuanzia na sasa shamba Lipo kwenye kusafishwa maana nilinunua pori nimehamasika baada ya kutangazwa kuuzwa Elfu hamsini naishi Dar es salaam, sina utaalamu sana kuhusu msimu sahihi wa kupanda zao la korosho japo, pia nimefikiria kutumia miche iliyobebbeshwa ambayo naambiwa inapatikana Naliendele kwa bei ya sh 1000, Je kwa mwezi wa tatu ni msimu wa Kawaida kupanda zao Hilo?

Na Je kuja eneo Karibu Hapo lindi mjini naweza kupata mbegu zilizobebeshwa? Na pia Je naweza pata wapi shamba Darasa nikajifunze zaidi kwa maeneo Karibu na Dar au hata huko lindi? Na pia niepuke makosa gani kabla sijaanza utekelezaji wa mradi huu?

Shukrani sana kwa utayari wako mkuu PatriceLumumba
 
Sawa.. Hiyo namna ya "kubebesha" inaweza kutumika kwa mimea mingine pia, au ni kwa mikorosho pekee?

HABARI,
"antimatter,
Swali zuri,Hii njia ya kubebesha(GRAFTING)Inatumika kwenye mimea mingi sana sio mikorosho pekee Njii hii ilianza kutumia Enzi na Enzi (10-30 BC)Unajua jamii nyingi sana duniani zote zilizoendele kilimo ndio kimesaidia kwa asilimia zaidi ya 50 kwahiyo walikuwa na ujuzi mwingi sana.Na njia hii ilianza kwenye zabibu, Aple n.k

Kwa njia hi ya kubebesha mimea unaweza kufanya kwenye maembe,miti yote jamii ya michungwa,mapera,mafenesi,Mastafeli,parachichi kwa ujumla ni jamii kubwa ya miti siyo ya matunda pekee.

Nadhani hapo utakuwa umepata mwanga kidogo "antimatter,

LUMUMBA
 
Kwahiyo hii njia inasaidia kupunguza muda wa kusubiri mavuno bila shaka, kama ni hivo inamaana unaweza kuanza kupata korosho ndani ya mwaka mmoja?
 
HABARI,
"BILGERT,
Unapokuwa kwenye ushirika huwa mara nyingi mpaka mnada ufanyike ndio mkulima analipwa ila mkulima ndio unatumia gharama zako kupeleka mazao yako kwenye ushirika,Ila kuna baadhi ya ushirika huwa wanakuwa na mkataba na mtu kusafirisha zao la washirika mnada ukifanyika mkulima anakatwa pesa ya usafiri kwa kilo au tani kutokana na ukubwa wa mavuno ya mkulima

LUMUMBA
Samahan mkuu. Ni zao gani jingine la biashara tofaut na korosho. Ambalo lina soko zuri kimataifa
 
Kwahiyo hii njia inasaidia kupunguza muda wa kusubiri mavuno bila shaka, kama ni hivo inamaana unaweza kuanza kupata korosho ndani ya mwaka mmoja?

HABARI,
"mnyikungu,
Ndio hii njia inapunguza muda wa kuanza kuvuna ndani ya mwaka mmoja korosho zinatoka kwani unakwa ukpandikiza kikonyo kilichokuwa mwisho wa mti mama ambacho ni cha kutoa matunda ila sasa unashauriwa yale mau ya mwaka wa kwanza na wa pili uyatoe yasibebe matunda kwani mti unakuwa hauna nguvu bado na pia yanakuwa ni machache kwani mti unakuwa hauna matawi mengi ila unaweza kuanza kuvuna korosho chache kuanzia mwaka wa 3 ila muda unavyozidi kwenda ndio matawi yanaongezeka na mavuno yanaongezeka pia Tegemea kuanza mavuno baada ya miaka 3 ni muda mzuri.

Pia kuna mbegu za miaka 3 zipo pale Naliendele ila kwa hizi za kubebesha unakuwa na uhakia kwani mche utakuwa na tabia za ule mti mama uliotoa.

LUMUMBA
 
HABARI,
"mnyikungu,
Ndio hii njia inapunguza muda wa kuanza kuvuna Ndani ya mwaka mmoja korosho zinatoka kwani unakwa ukpandikiza kikonyo kilichokuwa mwisho wa mti mama ambacho ni cha kutoa matunda ila sasa unashauriwa yale mau ya mwaka wa kwanza na wa pili uyatoe yasibebe matunda kwani mti unakuwa hauna nguvu bado na pia yanakuwa ni machache kwani mti unakuwa hauna matawi mengi ila unaweza kuanza kuvuna korosho chache kuanzia mwaka wa 3 ila muda unavyozidi kwenda ndio matawi yanaongezeka na mavuno yanaongezeka pia Tegemea kuanza mavuno baada ya miaka 3 ni muda mzuri.
Pia kuna mbegu za miaka 3 zipo pale Naliendele ila kwa hizi za kubebesha unakuwa na uhakia kwani mche utakuwa na tabia za ule mti mama uliotoa.

LUMUMBA
Okey, hapo nimekuelewa. Sasa hivi wanahamasisha kilimo vha korosho huku Iringa ndo maana nataka nielewe vizuri ili nichangamkie fursa.
 
Shukrani sana Nimenunua ekari tano kwa kuanzia na sasa shamba Lipo kwenye kusafishwa maana nilinunua pori nimehamasika baada ya kutangazwa kuuzwa Elfu hamsini naishi Dar es salaam, sina utaalamu sana kuhusu msimu sahihi wa kupanda zao la korosho japo, pia nimefikiria kutumia miche iliyobebbeshwa ambayo naambiwa inapatikana Naliendele kwa bei ya sh 1000, Je kwa mwezi wa tatu ni msimu wa Kawaida kupanda zao Hilo? Na Je kuja eneo Karibu Hapo lindi mjini naweza kupata mbegu zilizobebeshwa? Na pia Je naweza pata wapi shamba Darasa nikajifunze zaidi kwa maeneo Karibu na Dar au hata huko lindi? Na pia niepuke makosa gani kabla sijaanza utekelezaji wa mradi huu? Shukrani sana kwa utayari wako mkuu PatriceLumumba

HABARI,
"Shark's Style,
Hongera sana kwa juhudi zako kwenye kilimo cha korosho nina uhakika utafanikiwa na ukiweza kufata ushauri mzuri unauhakika wa kuvuna tani 1 kila heka hilo nina uhakika nalo.Na tani moja ni zaidi ya milioni 3 kwa sasa.

Kuhusu msimu wa kupanda nikwambie tu korosho hazina msimu wa kupandwa ila inaitaji maji tu kama huna chanzo kizuri cha maji basi subiri msimu wa mvua ukianza unapanda.Kuhusu shamba darasa hapo jaribu kuwasiliana na Naliendele wanajua mashamba darasa yote Na ninauhakia maeneo ya pwani mkuranga lazima kutakuwa na shamba darasa maeneo hayo au nenda ofisi za mkoani pwani ukiulizia wanajua wapi shamba darasa lilipo.

LUMUMBA
 
Samahan mkuu. Ni zao gani jingine la biashara tofaut na korosho. Ambalo lina soko zuri kimataifa

HABARI,
"BILGERT,
Safi kwa swali zuri mazao yenye soko zuri kimataifa ni mengi sana,Muhogo,Parachichi,Tangawizi Nitatuma list yake kesho pamoja na masoko yake.Tatizo tulilokuwa nalo ni kwamba wengi wanaosafirisha kwenda nje sio wazawa wengi ni wahindi sasa wanakuwa na uchaguzi sana kwenye mazao yenye faida kubwa kama korosho.Ila kwa sasa soko la parachichi nalo limeanza kuwa kubwa hasa kwa Nchi za ulaya ujerumani,spain,wingereza,Uholanzi .nk.ndio maana kilimo chake kimeanza kuwa kikubwa sana iringa.

Kwa muhogo unga wake unahitajika sana China kwa wingi sana ila bado watu hawajaweka mkazo huko na shida bado hawana mtu wa kuwahakikishia soko nikimaanisha kununua. Tangawizi India na china pia wanahitai sana.

LUMUMBA
 
HABARI,
"BILGERT,
Safi kwa swali zuri mazao yenye soko zuri kimataifa ni mengi sana, Muhogo, Parachichi, Tangawizi nitatuma list yake kesho pamoja na masoko yake. Tatizo tulilokuwa nalo ni kwamba wengi wanaosafirisha kwenda nje sio wazawa wengi ni wahindi sasa wanakuwa na uchaguzi sana kwenye mazao yenye faidi kubwa kama korosho. Ila kwa sasa soko la parachichi nalo limeanza kuwa kubwa hasa kwa nchi za Ulaya Ujerumani, Spain, Uingereza, Uholanzi .nk.ndio maana kilimo chake kimeanza kuwa kikubwa sana Iringa.

Kwa muhogo unga wake unahitajika sana China kwa wingi sana ila bado watu hawajaweka mkazo huko na shida bado hawana mtu wa kuwahakikishia soko nikimaanisha kununua.
Tangawizi India na china pia wanahitai sana.

LUMUMBA
Shukrani mkuu.
 
Okey, hapo nimekuelewa. Sasa hivi wanahamasisha kilimo vha korosho huku Iringa ndo maana nataka nielewe vizuri ili nichangamkie fulsa

HABARI, "mnyikungu,

Sawa hongera sana Tena kwa Iringa mna fulsa nyingine ambayo maeneo mengi hakuna fulsa ya kilimo cha parachichi kwenye wilaya ya kilolo na mkoa wa Njombe nakutakia kila jema Comrade.

LUMUMBA
 
Back
Top Bottom