Facts The Economist Got Them Wrong on Magufuli

Facts The Economist Got Them Wrong on Magufuli

Status
Not open for further replies.
Mkuu Ngokongosha, asante kwa bandiko hili. Hiki kinachofanywa na mwandishi huyu, ndicho kitu kilipaswa kufanywa siku nyingi na media zetu.

Paskali
Mkuu Ngokongosha, asante kwa bandiko hili. Hiki kinachofanywa na mwandishi huyu, ndicho kitu kilipaswa kufanywa siku nyingi na media zetu-NA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI HASA
 
By Dr. Herman Louise Verhofstadt...

It needs courage-but above all vendetta backed type of journalism to be bold enough to undermine and under write positive transformations happening in Tanzania under Mr. Magufuli in support and in favour of isolated incidents which are peculiar to the nature of politics in Tanzania and other neighbouring geo-politics.

The author is a Belgian health expert working with an international NGO in EAC countries who is currently ending his tenure in Tanzania. He has worked with poor communities for four years now.

Tusidanganyane, hii ni lugha ya Lumumba...halafu kwa ujinga wao wakamuita Mr. Magufuli, si Dr. Magufuli, makusudi ili kuwadanganya wafuasi wao wasioweza kuona zaidi ya pua zao.
 
Spoiler alert!!!!!Mzungu keshakula hela ya CCM...

Tunaelewa..hahahhaaa....kalipwa madafu mbwa mmoja wa kizungu nae abweke...

Eti "has worked with Poor Communities for four years now" ,halafu una audacity ya kutuletea huu upupu?

GTFOHMF!
Mkuu acha kujibu kimbea kama umevaa kanga, weka facts zako na wewe. Mathalani, jamaa kaandika yule mtumishi wa umma aliyesahau data za bajeti hakufukuzwa kwenye mkutano wa hadhara. Kama una fact ya kupinga hilo weka hapa.
 
Na makala ya kwanza ya The Economist ilidhaminiwa na UKAWA?
Umelogwa ila usiyoyataka yemesema tena kwa usahihi zaidi kuliko yale unayoyataka. aidha afadhali ya huyu mzungu ila yule wa kwanza kwa ubovu wa kiingereza kile atakuwa siyo mzungu bali mnyaturu mmoja anayejifanya mzungu
 
..makala ina makosa mengi madogo-madogo ya kiuandishi.

..siamini kama aliyeandika ni msomi wa kiwango cha PhD.
Ni makosa (solecisms) gani hayo? Tafadhali yataje kama yapo.
 
Waione Wasioitakia mema Tanzania. Asante mwandishi ingawa sijasoma yote, ila introduction inaonyesha kitu cha muhimu katika kueleza ukweli.
 
Sawa kabisa. Wale "noveau riche" waliokuwa wanatesa kwa matanuzi ya pesa za pombe bar na nyumba na magari ya bei mbaya mitaani sasa wapo chali na wamekuwa vitu adimu siku hizi. Magufuli is doing a great job. Everybody is toeing the line aka kuisoma namba

Mimi najiita mzalendo na naipenda nchi yangu TANZANIA; yote mambo anayofanya MAGUFULI hapa nchini kuleta maendeleo nayakubali na namsifu kwamfano vita dhidi ya rushwa , ujenzi wa miundo mbinu na pia ujenzi wa viwanda [ ingawa sikubaliani nae kujenga viwanda bila kuweka mkazo vile vile wa kuendeleza kilimo]. Mahala ninapotofautiana nae ni pale anapokuwa inconsistent katika maamuzi yake; huwezi kuamua kuwa sehemu za kanda ya ziwa wasivunjiwe nyumba zao hata kama wamekiuka sheria ili mradi eti walimpigia kura wa yeye kuwa RAIS at the same time watu wa mikoa mingine waliokiuka sheria zile zile wao nyumba zao zibomolewe!! Maamuzi kama haya huharibu umoja wa nchi kwa kuwatenganisha watu kutokana na kule wanakotoka.

Katika mambo ya uwekezaji ,napata shida sana kwa mfano pale anapoamua kununua ndege na kulipa hela zote kwa mkupuo mmoja[ cash]!! Angeweza kutumia fedha hizo hizo kununua ndege na pia kujenga shule na hospitali hapa nchini kama angefanya utaratibu wa kuwalipa watengenezaji Kidogo kidogo kwa makubaliano wakati ndege hizo zingekuwa zinafanya kazi!! Duniani kote hakuna nchi inayonunua ndege cash!! Katika miradi yetu ya miundo mbinu inaelekea tunaweka mkazo wa kumaliza hiyo miradi kwa muda mfupi bila kuangalia viwango vya utendaji; mifano ni barabara tunazojenga ambazo kila mara zinaharibiwa na mvua wakati wa masika hivyo kutumia tena fedha nyingi kurudia kuzitenegeneza. Angalia mabweni ya wanafunzi wa chuo kikuu, nia ya kuyajenga ilikuwa nzuri lakini papara ya kuyajenga ndio sababu ya nyumba hizo kuanza kupata nyufa baada ya muda mfupi!!


Magufuli kweli ana nia njema na nchi yake lakini je haya lote anayotekeleza yasingeweza kufanywa bila kukandamiza haki za msingi za wananchi? Je isingewezekana kupata haya mafanikio bila kuwakandamiza vyama vya upinzani, kupiga marufuku magazeti yanayokosoa sera zake , kuwateka na wananchi kupotea? Tukumbuke kuwa tunapozungumzia maendeleo ya nchi hatuzungumzii idadi ya barabara na magari yanayotembea barabarani bali inabidi tuzungumzie hali na ustawi wa wananchi kwa ujumla wake!!
 
Mimi najiita mzalendo na naipenda nchi yangu TANZANIA; yote mambo anayofanya MAGUFULI hapa nchini kuleta maendeleo nayakubali na namsifu kwamfano vita dhidi ya rushwa , ujenzi wa miundo mbinu na pia ujenzi wa viwanda [ ingawa sikubaliani nae kujenga viwanda bila kuweka mkazo vile vile wa kuendeleza kilimo]. Mahala ninapotofautiana nae ni pale anapokuwa inconsistent katika maamuzi yake; huwezi kuamua kuwa sehemu za kanda ya ziwa wasivunjiwe nyumba zao hata kama wamekiuka sheria ili mradi eti walimpigia kura wa yeye kuwa RAIS at the same time watu wa mikoa mingine waliokiuka sheria zile zile wao nyumba zao zibomolewe!! Maamuzi kama haya huharibu umoja wa nchi kwa kuwatenganisha watu kutokana na kule wanakotoka.

Katika mambo ya uwekezaji ,napata shida sana kwa mfano pale anapoamua kununua ndege na kulipa hela zote kwa mkupuo mmoja[ cash]!! Angeweza kutumia fedha hizo hizo kununua ndege na pia kujenga shule na hospitali hapa nchini kama angefanya utaratibu wa kuwalipa watengenezaji Kidogo kidogo kwa makubaliano wakati ndege hizo zingekuwa zinafanya kazi!! Duniani kote hakuna nchi inayonunua ndege cash!! Katika miradi yetu ya miundo mbinu inaelekea tunaweka mkazo wa kumaliza hiyo miradi kwa muda mfupi bila kuangalia viwango vya utendaji; mifano ni barabara tunazojenga ambazo kila mara zinaharibiwa na mvua wakati wa masika hivyo kutumia tena fedha nyingi kurudia kuzitenegeneza.

Magufuli kweli ana nia njema na nchi yake lakini je haya lote anayotekeleza yasingeweza kufanywa bila kukandamiza haki za msingi za wananchi? Je isingwezekana kupata haya mafanikio bila kuwakandamiza vyama vya upinzani, kupiga marufuku magazeti yanayokosoa sera zake , kuwateka na wananchi kupotea? Tukumbuke kuwa tunapozungumzia maendeleo ya nchi hatuzungmzii idadi ya Barbara na magari yanayotembea barabarani bali inabidi tuzungumzie hali na ustawi wa wananchi kwa ujumla wake!!
Jaribu kufuatilia ukweli wa anayoyafanya na kusema achana na propaganda zilizowahi kusemwa au kuandikwa kama reference yako
 
Jaribu kufuatilia ukweli wa anayoyafanya na kusema achana na propaganda zilizowahi kusemwa au kuandikwa kama reference yako

Itakuwa ni busara kama ungeandika kama mimi nilivyoandika yale unayodhani nikweli na yale unayodhani ni propaganda kwa mtazamo wako!! Usilazimishe niandike unavyotaka wewe.
 
Mange Kimbambi is behind all this...nimenfuatilia sana pale kwenye page yake na hivyo vilivyoandikwa hapo havina tofauti hata kidogo.. Opposition wanajikuta wako smart sana
Anatumika tuu, hana lolote, kuna watu fulani nyuma ya pazia wanatumia hizo taarifa na yeye kuzimwaga mitandaoni. Ndio hao hao wanao waandikia dondoo zote hizi magazeti Economist na mengine ya nje.
 
Hivi ndo vitu ambavyo akina Msigwa na wenzake wa Lumumba inabidi wafanye. Facts zipingwe kwa facts. Siyo hawa vijana wa Lumumba wanashinda JF wakiachia povu na kutukana. Povu na ulalamishi kamwe haviwezi ku-challenge andiko kama la Economist.

Mfano sijaona magazeti ya nje yanapo-acknowledge uthubutu wa JPM kujenga reli, na miradi mingine mikubwa! Hata re-negotiations za mikataba ya madini...I mean siyo kwamba JPM hana mabaya..Lakini na mazuri yake yasemwe! Tumkome nyani giladi!

Next time mkiona gazeti la kimataifa liwe the economist, Bloomberg nk wameandika habari negative kuhusu nchi/serikali yetu..inabidi wahusika waingie front kujibu kwa kuweka records straight. siyo kukimbilia JF na kuanza kulialia kwamba JPM anachukiwa na haya magazeti/jarida. Dunia haina huruma na yeyote.
Minimum expectetion ya mzazi kutoka kwa mwanaye ni heshima, mzazi hawezi kumsifia mtoto kisa mtoto anamheshimu, na minimum expectation pia ya wapiga kura na wengine kutoka kwa rais wao ni maendeleo ya miundombinu na mengine, tulichokitegemea kutoka kwa rais ni kuleta maendeleo, sasa kwanini umsifia kwa kufanya yale mnayoyatarajia kutoka kwake, yaani gazeti la Economist limsifie Magufuli kisa kajenga reli? Come on!! huyo mleta mada kaja kumsifia Magufuli na wala hakuna cha fact wala nini, kupishanisha madai yake na ya Economist ndo fact? au umesifia lugha..hata kama Economist isingeandika ilichokiandika bado ukweli ungebaki kuwa huu utawala ni wa magumashi.
 
Kumbe jamaa mwenyewe ni mgeni, anatoa ushuhuda wa kitu ambacho hakiishi, yaani suala la dada zetu kuzuiliwa kwenda shule anaita ni mkwara wa kuwafanya watoto wasifanye ngono na wakati kuna dada zetu hawaendi shule kwa kutii hilo agizo, halafu unaita facts, huyu mwandishi atakuwa katumwa.
 
bila shaka kaka Mayalla unasifia jaribio la Mwandishi la kujaribu kujibu hoja ila siyo fact zake alizotoa ambazo zinaonekana ni za kuponda gazeti la Economist na kutufanya watanzania kwamba hatuna akili.
Mkuu Ngokongosha, asante kwa bandiko hili. Hiki kinachofanywa na mwandishi huyu, ndicho kitu kilipaswa kufanywa siku nyingi na media zetu.

Paskali
 
Anatumika tuu, hana lolote, kuna watu fulani nyuma ya pazia wanatumia hizo taarifa na yeye kuzimwaga mitandaoni. Ndio hao hao wanao waandikia dondoo zote hizi magazeti Economist na mengine ya nje.
Nalifaham Sana hili Mkuu, Anajikuta Genius kinoma kumbe Zero IQ..

Ile miskule yake kwenye page yake inanifurahisha sana[emoji23][emoji23] wakitukanwa wanasapoti, wakiambiwa chochote wanasapoti
 
Nalifaham Sana hili Mkuu, Anajikuta Genius kinoma kumbe Zero IQ..

Ile miskule yake kwenye page yake inanifurahisha sana[emoji23][emoji23] wakitukanwa wanasapoti, wakiambiwa chochote wanasapoti
Eti hao ndio taifa letu la kesho, kweli inabidi tuipitie upya mitaala yetu ya elimu.
 
hana lolote huyu mzungu koko... anatafuta tenda ya kifisadi kwa Ba-SHIT-e !!

Usimtukane mwandishi, pamoja na MAPUNGUFU YA mtazamo wako, huyu bwana amejaribu kuelezea mazuri ambayo yamefanywa na JPM.
 
Kumbe jamaa mwenyewe ni mgeni, anatoa ushuhuda wa kitu ambacho hakiishi, yaani suala la dada zetu kuzuiliwa kwenda shule anaita ni mkwara wa kuwafanya watoto wasifanye ngono na wakati kuna dada zetu hawaendi shule kwa kutii hilo agizo, halafu unaita facts, huyu mwandishi atakuwa katumwa.
Soma tena ili uelewe
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom