Facts The Economist Got Them Wrong on Magufuli

Facts The Economist Got Them Wrong on Magufuli

Status
Not open for further replies.
Hawa economist nilipitia jarida leo nikajua ni upuuzi, kuna economist & Bloomberg , kwa mbali na BBC ,wanatumika sana kutoa makala ya kuichafua nchi yetu, kuna mtangazaji mmoja wa BBC nimesikia eti anasema maandamano yazidi kupamba moto Tanzania ,jamaa kakomaa na sauti yake kama kala makande kuongea vitu ambavyo havipo, yaani sisi watanazania/waafrica sijui tuna matatizo gani kichwani. Clinton alishindwa uchaguzi, mbona hatuoni rally za kila siku zikiendelea mji mmoja kwend mwingine? sana sana utamuona kwenye fund raising to mara moja , tujikite kwenye udhalishaji na tufanye siasa tukifuata sheria na taratibu,mazungumzo, tukipenda kusikia wazungu wa nje basi nchi yetu hii tutaipasua.

Mtalia sana.

Wanamshambulia uchwara kwa lipi labda?

Makinikia?Puliiiiizz

Acacia walishinda kitamboo sana.Hawana haja ya kuomba msaada Economics eti kupambana.

Acacia walishamshinda vibaya sana mahakamani,vibaya mno...

Semeni kuna fundamental problem na serikali ndio maana wanaongea,kungekua na mazuri wangesema...

Sababu ya makinikia sio yenyewe tu,kuna shida na hii serikali..Hilo mpo na denial nalo....

Sasa serikali nzima inapambana na mtu mdogo kama sisimizi anaitwa Nondo,mtoto mdogo,resources za nchi nzima zimewekwa kwake,ukiulizia why all these?Unashangaa majibu hakuna...Kuna tatizo kubwa very fundamental mnalo..Haya ya The Economics ni symptoms tu.
 
Huyu mwizi anadai jamaa hafukuzi watumishi live kwenye luninga?! Vyombo vyetu vya ndani viliripoti vipi huu ya tukio lile? Aliwafukuza akiwa wapi? Na ni nani aliyeuliza hadharani kule Kigamboni kuwa ''niwatumbue au nisiwatumbue?'' Uchumi wa nchi hii uko vizuri?! Kwa wananchi wa eneo lipi la Tanzania?!
Nina wasiwasi huyo mbeligiji kuna sehemu alikosea wakam-blackmail kuwa asipowatetea 'watarara naye mbere'
 
Huyu mwizi anadai jamaa hafukuzi watumishi live kwenye luninga?! Vyombo vyetu vya ndani viliripoti vipi huu ya tukio lile? Aliwafukuza akiwa wapi? Na ni nani aliyeuliza hadharani kule Kigamboni kuwa ''niwatumbue au nisiwatumbue?'' Uchumi wa nchi hii uko vizuri?! Kwa wananchi wa eneo lipi la Tanzania?!
Nina wasiwasi huyo mbeligiji kuna sehemu alikosea wakam-blackmail kuwa asipowatetea 'watarara naye mbere'


Mkuu

Huyu mzungu ni msanii wa hapa Dar walimpanga amekula hela za jamaa wa Kijani..

Hakuna authenticity wa hii makala.

Anaongea uongo wa wazi kabisa!

Sijui kwanini makala ya The Economics zinafanya serikali inapaniki namna hii...?I wonder...

Walichojibu kina uongo pia wa kutosha..Inaonesha na wao serikali si wakweli pia...
 
Huyo mtu mwenye jina hilo hayupo. Mtunzi ni wa kutunga. Hii ni barua iliyoandikwa na ccm wenyewe


Mkuu

Umestukia eee?Wameiandika wao wao wakaweka jina la mzungu kama rubber stamp tu.

Hawa CCM ni vituko..ndio kwanza season one tupo..More to come!

Watching....
 
Mkuu,
Nimeshatukia. Nimetumia tool kugundua majina na hilo jina halitokei popote.

Haiwezekani mtu mpaka awe Dr tena aende kuishi nchi za watu kusiwe na trace yake kwenye mitandao yote.

Hii barua imeandikwa na Lumumba na huenda mzee Mwanakijiji ndiye kaandika.
Mkuu

Umestukia eee?Wameiandika wao wao wakaweka jina la mzungu kama rubber stamp tu.

Hawa CCM ni vituko..ndio kwanza season one tupo..More to come!

Watching....
 
Huyo mtu mwenye jina hilo hayupo. Mtunzi ni wa kutunga. Hii ni barua iliyoandikwa na ccm wenyewe
Kama Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Idara ya Habari Maelezo, Wizara ya Hasbro, hawana uwezo wa kukanusha tuhuma kama zile, hao CCM, wakanushe kwa uwezo gani?!.

CCM wangekuwa na uwezo wa kukanusha hata nusu tuu, wangeishaitisha press conference!.

Unaweza kukuta Ikulu yetu ime subscribe Daily News, Uhuru na Habari Leo pekee, hilo The Economics kwa lugha ile, alisome nani?.

P
 
Hongera Sana JPM kwa kuanza kufanya mambo Kama PK...PK huwa anaajiri kampuni za nje zenye wataalam kumsaidia kujibu mashambulizi ya magazeti ya huko Ulaya. Naona jpm anaenda na beat za mentor wake
 
Spoiler alert!!!!!Mzungu keshakula hela ya CCM...

Tunaelewa..hahahhaaa....kalipwa madafu mbwa mmoja wa kizungu nae abweke...

Eti "has worked with Poor Communities for four years now" ,halafu una audacity ya kutuletea huu upupu?

GTFOHMF!
Jibu hoja kwa facts kama mwandishi alivyotoa facts!! Acha kubwabwaja!!
 
Kama Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Idara ya Habari Maelezo, Wizara ya Hasbro, hawana uwezo wa kukanusha tuhuma kama zile, hao CCM, wakanushe kwa uwezo gani?!.

CCM wangekuwa na uwezo wa kukanusha hata nusu tuu, wangeishaitisha press conference!.

Unaweza kukuta Ikulu yetu ime subscribe Daily News, Uhuru na Habari Leo pekee, hilo The Economics kwa lugha ile, alisome nani?.

P
Hahahahaa!! Yaani hata polex2 ana kigugumizi?
 
..Acacia wameiba usd 190 billion.

..halafu tumekubaliana nao NJE YA MAHAKAMA watulipe usd 300 million.

..kilichotokea hapo ni dhuluma juu ya wizi.
uliyaelewa hayo makubaliano?
 
wale waandishi wa kibongo wanaopeleka makala zao The economist wakajibu hii hoja sasa
 
Mkuu Ngokongosha, asante kwa bandiko hili. Hiki kinachofanywa na mwandishi huyu, ndicho kitu kilipaswa kufanywa siku nyingi na media zetu.

Paskali
Ni kweli mkuu pascal, hili swala ulilipigia kelele kwa nyuzi zako nyingi nilizowahi kuzisoma humu..
 
Wametafuta mchumia tumbo mmoja ili awajibu The Economist? Haha
Kichwa cha habari tu kimewaumbua...eti Facts The Economist Got Them Wrong on Magufuli! Hii ni lugha ya wapi kwa sababu hata kwangu ambapo Kizungu ni lugha ya tatu siwezi kuandika kitu kama hicho. Article nzima imejaa makosa ya grammar ambayo hayawezi kufanywa na mtu mwenye exposure kubwa kama inavyodaiwa kwa huyo daktari feki.

Pili, ukipitia article hii kwa umakini kuna kitu utagundua mara moja, inaonekana awali iliandikwa kwa Kiswahili halafu ikatafsiriwa kwa lugha ya Malkia na kubandikiwa jina bandia kwani mtu huyo anayedaiwa kuiandika hayupo. Aina hii ya usanii kwa sasa umeshika kasi katika juhudi wa kuutetea utawala ambao kwa kiwango kikubwa umekosa dira.

Ni yale yaleeee...Trump ampongeza Magufuli, Magufuli atunukiwa nishani kwa uongozi bora, Tanzania yashika nafasi ya kwanza/pili kwa ukuaji wa uchumi barani Afrika na mengineyo. Hii serikali yetu kwa kweli inahangaika halafu watu wenyewe wanaoanzisha hizi porojo ni wale walee [B]Ngokongosha[/B] na jamii ile ile ya wakwetu! Kalaghabaho!
 
Kichwa cha habari tu kimewaumbua...eti Facts The Economist Got Them Wrong on Magufuli! Hii ni lugha ya wapi kwa sababu hata kwangu ambapo Kizungu ni lugha ya tatu siwezi kuandika kitu kama hicho. Article nzima imejaa makosa ya grammar ambayo hayawezi kufanywa na mtu mwenye exposure kubwa kama inavyodaiwa kwa huyo daktari feki.

Pili, ukipitia article hii kwa umakini kuna kitu utagundua mara moja, inaonekana awali iliandikwa kwa Kiswahili halafu ikatafsiriwa kwa lugha ya Malkia na kubandikiwa jina bandia kwani mtu huyo anayedaiwa kuiandika hayupo. Aina hii ya usanii kwa sasa umeshika kasi katika juhudi wa kuutetea utawala ambao kwa kiwango kikubwa umekosa dira.

Ni yale yaleeee...Trump ampongeza Magufuli, Magufuli atunukiwa nishani kwa uongozi bora, Tanzania yashika nafasi ya kwanza/pili kwa ukuaji wa uchumi barani Afrika na mengineyo. Hii serikali yetu kwa kweli inahangaika halafu watu wenyewe wanaoanzisha hizi porojo ni wale walee [B]Ngokongosha[/B] na jamii ile ile ya wakwetu! Kalaghabaho!
Ina maana hujaelewa hoja zilizopo kwenye article au unajidai ni mtaalamu wa grammer
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom