Exclusive: TANESCO's Audited Report from PPRA

Nilikuwa sijajua kwanini b2men hawakai offisini. Ninahisi maneno yanawachoma kinoma hata wanatamani ardhi ipasuke. Majengo meupe yale hajawafariji tena. Mwalimu aliwaonya, huko si mahala pa mchezo mchezo tu....Ni mzigo mkuubwa!! Sasa wanajifanya kuzurura huku na kule kuhutubia mikutano na kusafiri kutwa ili wachoke na kusinzia vizuri bila mawazo. Kwao miziki mnayorusha ukumbini si charanga wala bongoflavor, ni ya maombolezo na haichezeki!

MDjs endeleeni kuturushia miziki, nasi tunairusha vijiweni kwa maskini wanaonyonywa jasho lao mchana kweupe!
 
Invisible,
tunashukuru sana kwa document hio, kwani mwaka huu tutajua mengi sana kutoka kwa wakubwa.
 
mwaka huu ni mwaka wa matukio ya kusisimua, mwaka huu nnazani ndio mwaka ambao huenda kikwete asiusahau maishani mwake.

hata hivyo zote ni changamoto ambazo zinamkabili kumpima ni mtu firm kama alivyotuahidi au maji moto
 
Jamani wale wenye nia ya kurekodi huu muziki waendelee maana soon kuna albums mpya zinakuja

Tunasubiri kwa hamu, mwafrika wa kike

leteni bandugu, ikiwa sebene, tokomile au lizombe leteni hizo album washereshaji tupo kuzipromote tena bureeeeeeee...........
 
Jamani wale wenye nia ya kurekodi huu muziki waendelee maana soon kuna albums mpya zinakuja

Kuna mengine hata kuyaweka mtu unajiuliza mara mbilimbili... Ngoja hali iwe shwari kwanza.

Kwa wale mnaojisajili tunaomba muwe na subira ili tuwape access ya kuweza kuchangia ama kupakua (to download attachments). Kuna spammers wengi na lazima tuwazuie ili mijadala iende sawa bin sawia.

Karibu
 
Jamani PCCB wanaweza kutuambia ule upuuzi wao wa kuisafisha RDC waliupata wapi? Sasa hii si aibu kubwa sana kwa huyu bwana Hosea na timu yake? Kweli hii nchi kazi bado ipo! Kila mahali pameoza. I wish kama kunauwezekano Invicible tupatie na hiyo ripoti ya PCCB pia tuione.

Si hao peke yao, hata JK alisema mkataba wa Richmond safi!!
 
dah! mimi naona kizunguzungu na sasa ndiyo naelewa kwa nini JK kasema wapinzani wataleta vita,hivi mnadhani huu mziki ukifika kwa wananchi kitimutimu chake kitakuwaje? Miye yangu macho!
 
hivi mnadhani huu mziki ukifika kwa wananchi kitimutimu chake kitakuwaje?

Kuna moja kila nikifikiria kuiweka naona maluweluwe... Naona kama zimezidi. Bora niendelee kubana nayo hadi next week ili niwaache watu waburudike na w/end (waweke shida chini na kurusha mikono juu)

W/end njema kwa wote
 
Invisible,

Weka hiyo kitu ingine mwanangu huu ndio wakati sasa wiki imeshapita
 
Shukran kwa hii report inayotuweka karibu na yanayojiri huko kwa jirani. Comparative analyses zinawezatusaidia sana kujenga hoja zetu sisi wakosoaji waviongozi wetu.

Kwa kweli ripoti inadhibitisha wazi kwamba ameyokuwa akiyasema Mchungaji Mtanzania Faustin Munishi ni ya kweli:

 
Last edited by a moderator:
Jamani Jamani,
'Political influence forced TANESCO to waiver from principles of the contract''
Who are these political influences???

"no performance bond attached with the contract" WTF??????
Jamani hata kama ni kula, kuleni kwa akili. Mkataba bila ya kuwa na njia ya ku CHECK perfomance ni sawa na kumkopesha mtu hela alafu umwambie "nilipe utakapojisikia"... WTF!!


''The contract between TANESCO (Tanzania Electric Supply Company) and Richmond Development Company was signed in strange circumstances at night and at the Ministry of Minerals and Energy, with some contractual issues protecting the client having been ignored,''
" Eeeeeh subiri kwanza, kuna wapiga chabo wengi. Infact, njoo usiku pale ofisini kwangu, watu wote wakishaondoka tutayamaliza. Usiwe na wasiwasi, nobody will know. usimwambie mtu." WTF???

Jamani hizi taarifa zina kopi ya Kiswahili?? maana ningependa kuona zikiwa kwenye magazeti ya udaku uone kama moto usingewaka.
 
Naungana na wenzangu katika kutoa shukurani zangu zisizokadirika kwa kazi hii nzito na nzuri pia.
 
Tunaomba santuri za Richmond na BOT. miziki hii inatamba kwenye chati, tunahitaji santuri zake kwa ajili ya playback.
 
alafu tunaambiwa njia pekee ya kuokoa shirika ni kuongeza gharama kwa mlaji, hivi hawa EWURA hawakuyaona haya yaliyopo kwenye hii ripoti? kumbe hata EWURA nao ni mafisadi kama waliamua kutupandishia gharama za maisha badala ya kuishinikiza Tanesco ijifanyi overhaul, hatari tupu.
 
alafu tunaambiwa njia pekee ya kuokoa shirika ni kuongeza gharama kwa mlaji, hivi hawa EWURA hawakuyaona haya yaliyopo kwenye hii ripoti? kumbe hata EWURA nao ni mafisadi kama waliamua kutupandishia gharama za maisha badala ya kuishinikiza Tanesco ijifanyi overhaul, hatari tupu.
Aaaah namuyamba wee, waswahili wanasema "ukishangaa ya musa utayaona ya firauni". hao wote ni watoto na wajukuu wa ufisadi aliotuwachia mkuu nyerere. Katuwacha hohe hahe, ki-uchumi, ki-elimu, ki-maadili. Kwa hiyo usishangae, ccm ilianzishwa na huyo mzee na ndio mpaka leo hiyo hiyo na watu ndio haohao. jee ulishaona maendleo toka wakati wa nyerere mpaka leo? mimi sijayaona. Elimu duni, Maji mpaka leo huwezi kunywa ya bombani, umeme asilimia kumi ya watanzania (kwa hesabu zao) kwa zangu nadhani ni asilimia tano tuu. Au system huijuwi ni nini?
 
Back
Top Bottom