Ex boyfriend anataka nimlipe gharama zake

Ex boyfriend anataka nimlipe gharama zake

Mkuu una mshipa wa kiume hasa....mi leo sicomment nagonga like tu

Hata mimi namgongea like kubwa sana maana hawa dada zetu hawana maana kabisa nna mfano hai kabisa ya jamaa yangu mmoja nilikuwa nafanya nae kazi alimsomesha mchumba wake hadi chuo na alijinyima sana nusu ya mshahara wake anautuma kwa huyo mchumba wake chuoni sasa alikuwa anawasiliana na huyo mchumba wake ambaye alikuwa anatumia simu ya mtu ya kuazima kumbe yule aliekuwa anamuazima ile simu alikuwa bwana wa mchumba wa huyo rafiki yangu, at the end of the day yule msichana akampigia simu mchumba wake ambaye ni rafiki yangu kuwa anataka kuolewa na mtu mwingine sie yeye, jamaa alichanganyikiwa kabisa tukamshauri amwachie Mungu ni kweli aliolewa lkn the end of the day kumbe yule jamaa aliyemuoa hakuwa na mbele wala nyuma alikuwa tapeli tu wa town, ikabidi yule msichana aje kwetu mashemeji zake wa zamani kwa magoti ili tumuombee msamaha.
 
Mdada kweli umekosa majibu...moja mwambie akurudishie muda aliokupotezea...mbili mwambie kama alikukuta bikira akurudishie na kama hukuwa bikira mwambie ameitumia so imeongezeka airekebishe...tatu alete kwa maandishi kuwa yeye ndio alikukabidhi chochote....nne mwambie hukumuomba chochote...na mengine mengi
 
hapo sasa ndio aandae sanda kabisa...na mazishi atangaze akiwa hai....nyie mnampoteza mmasai wa watu...jamaa yuko njiani...shauri yenu.

Mdada kweli umekosa majibu...moja mwambie akurudishie muda aliokupotezea...mbili mwambie kama alikukuta bikira akurudishie na kama hukuwa bikira mwambie ameitumia so imeongezeka airekebishe...tatu alete kwa maandishi kuwa yeye ndio alikukabidhi chochote....nne mwambie hukumuomba chochote...na mengine mengi
 
ha ha ha ha ha! Umejibu kikauzu kama sio mdada vile!

Mtu akijifanya kauzu inabidi......huo upuuz niliwah bambana nao na alijuta.Mpk leo pete yake nnayo ipo tu.Juz kat analeta swaga za kutuma sms kuwa yupo ktk harus ya mtu wa kabila yangu na hajaniona,nkajua nye.ge zinamsumbua.....kwan kila mtu me ananihusu.
 
hapo sasa ndio aandae sanda kabisa...na mazishi atangaze akiwa hai....nyie mnampoteza mmasai wa watu...jamaa yuko njiani...shauri yenu.

Akileta ujinga minya pum.bu hizo asilete za kuleta.Kama anategemea akauze sasatel hiyo nyumban apate hela.....eboooooi!!!
 
Wee binti wee, kwanini umemwacha mwanaume kwa sababu nyepesi hivyo? Kwamba umegundua ana mke so what? Kwani kuna siku alishindwa kukufikisha wanakofikishwa wenzio au ni sababu tu ya kumwacha mwenzio? Akikuua utuletee mrejesho tujue mandhari ya peponi, na iwe fundisho kwa wenzio wenye tabia kama zako!
 
hilo ndo swali????lakini naogopa alichofanyiwa ufoo lakini swali linakuja yeye anataka pesa zake zote tangu ananijua hapo heaven on earh ingekuwa wewe ungefanyaje

Sasa we dada unakuwa kama huishi mjini! Unakubalije kumuacha wewe?! Ulishindwa nini kumzengua hadi akakuacha yeye? Au hujui style za kumzengua?
Muombe akununulie gari na nyumba akujengee... kwa kuwa hawezi atakataa... then unanuna mwanzo mwisho. Ugomvi kila siku, akitaka k unambania bania... hadi akasirike akuache mwenyewe. ..
Hapo hatakudai...
 
Ndugu wana mmu naomba msaada kwani nimejaribu kutafuta kwa njia ya kawaida nimekosa msaada,tatizo ni ex wangu yapata mwezi na kitu tangu tumeachana anataka nimrudishie gharama zake pamoja na baadhi ya vitu alivyoninunulia,kanitumia mesegi za vitisho ila kikubwa ni kwamba niligundua ana mke muda kidogo lakini kila nilipomwambia tuachane anasema nimrudishie kila kitu,tangu mwezi sasa nimefanya maamuzi magumu lakini ndo kama imekua mwiba kila saa sms na simu za kunitisha jana kaja kanigongea mlango nikakimbilia chooni maana taa ilikua inamulika hivyo hakuniona baadhi ya vitu alivyonipa kasoro kimoja ndo kina jina lake sasa nafanye kumbukeni kanitumia na kumbukeni ni mtu anaefahamiana na polisi sasa nafanyaje?

Ninavyojua mwanaume mstaarabu hadai chochote, anaweza kudai akiwa na hasira ila zikiisha anasahau, ushauri wangu siku nyingine acha kukimbilia kuachana tu hata kama kuna kosa, mapenzi yanaumiza sana, hakujiandaa na huwezi jua alikupenda kiasi gani, mimi naamini hakuna mapenzi yasiyo na mapungufu, huyo ndiyo ana mke ila kwingine utakakoenda utakutana na mengine, ulitakiwa muachane taratibu, mweleweshe wewe unahitaji mwanaume atakayekuwa mumeo yeye tayari ana mke, ni matumaini yangu mngeelewana naye angejiandaa kisaikolojia, kuibuka tu na kusema sikutaki ni hatari, ipo siku itakugharimu, ama muwe makini mnapoanzisha uhusiano.
 
hongera dada kwa maamuzi magumu
kama anamke anfuata kip[i kwako?
wanaume wengine ni vichwa maji sana
 
Jamaa yako mbona anakuwa muoga wa maisha inatakiwa asahau, hamna haja ya kurudishiana gharama

Kama alitoa kwa mapenzi na sasa mapenzi yamekwisha haihusiani na kurudishiana gharama
 
Kama wewe ndo umevunja Nkataba rudisaga fitu sake bana.nothing goes for nothing nanunua gari ili nilitumie kama siwezi kulitumia nauza nichukue changu.
 
Waswahli wanasema pesa hutaftwa ila sio uhai.kurport polis sio tatizo anaweza kukudhuru kwa njia yeyote midhali anakinyongo nawewe.sasa maamuzi yapo kwako.kama unaiman kua hutapata vitu vingine kamahivyo endelea kuvizui ila kama unajua mungu ndie mtoaji mpe uwe huru.angalia uhai wako na mali ulizoazimwa.

mkiva;
nakuunga mkono, kwanza hutakuwa na amani hata siku moja. Mwite tena kwa amani mchana peupe, kama una hofu kuwa anaweza kukudhuru, awepo mtu mwingine ka shahidi. Aingie ndani achukue kila kitu chake, kwani weye ulikuwa huna hata box la kulalia, achukue, apeleke atakako, usikubali hata kuvikomboa, Mungu atakupa vingine. Hukuzaliwa uje umchune.
Umegoma na hiyo papuchi yako, vyake vya nini?? Hutaki mwombe radhi uwe nyumba ndogo, usikubali ushauri wa kibabe. Siye twalala kwetu na wake zetu, weye ulipo lala chooni, siye ulituona hapo? Akili za kuambiwa....korogeamo na za kwako
 
Tafadhali Miss chagga,mangatara,Harufu,Tuko,Miss Strong kikao kimewateua muwe wafuatiliaji wa madeni kama majukumu yakiwazidi kuna reserve listi Osaba,Miss masai,Jeki

Kama na hizi ulipewa rudisaga ohooo ho!
beer_13838.jpg
 
Back
Top Bottom