Dada kwa hayo umejishushia thamani na unaonekana kabisa u radhi kufanya lolote lile ilemradi vitu ulivyopewa usirudishe.
Dada yangu hakuna kitu kizuri maishani kama kuwa na amani ya nafsi/roho. Na ili kuipata amani ya nafsi inatakiwa kuridhika na ulichonacho, uwe mtu wa kukubali kuachia baadhi ya mambo ambayo yanakukwaza maishani na kujipanga kivingine.
Kitendo cha kusema hutaki kumrejeshea kwa kuwa amekutumia ni kujidhalilisha wewe binafsi, kwani ulienda kwake na kuanzisha mahusiano kwa nia ya kupata faida nyingine ya mali tofauti na Love issues.? Ni kwa kauli kama hizi zinapelekea hata wavulana wadogo wawadharau wanawake na kuona wote ni walewale ya kuwa ni mal.aya.
Leo hii hutaki kumrudishia stahiki yake inayoonekana alikupatia, ila tambua sisi binadamu ni watu wa ajabu sana, kuna baadhi yetu wapo radhi kwa lolote kufanikisha alitakalo, siombei huyo awe mmoja wa hao. Kwani kukomaa kwako kutorudisha inaweza kuja kukucost usivyodhania sasa ama inaweza kuja kukunufaisha. Nakuacha na case study mbili ambazo si za muda mrefu.
1. Ufoo saro.
2. Mushi - Ilala.