Ewe msichana, kwanini uzae kabla ya kuolewa?

Ewe msichana, kwanini uzae kabla ya kuolewa?

Ni uamuzi tu kama ambavyo wewe mama wawili uliamua kuolewa.

Tena wengine unadhani hata wamekosa wa kuwaoa basiiiiii!!!

Tumekuwa watu wa kujudge sana, ila tuache kila mtu afanye anachoamini na kuona ni sahihi kwake, kuingia tu kwenye ndoa kisa tu fulani kaingia, au watanionaje,au mmemimbana nk nk ndio matokeo ya matetemeko ya ndoa nyingi za siku hizi hata Kuzifanya zikose maana.

Mie nimeamua kuolewa its okey, wewe haujaamua its okey pia.


[emoji106] [emoji122]


Sasa mtoto anawezaje kuzaliwa na mzazi mmoja? Ila namjua mmoja YESU and HE was great.


Tehe!, wewe bhana..
 
Msichana wa tatu ni yule anaepata mimba chini ya miaka 18 akiwa shule kutokana na kurubuniwa au kukosa elimu ya njia sahihi ya kuzuia ujauzito
 
nipo serias natafuta mwanaume wa kuzaa nae
akitokea mzuri muelewa mwenye utu nishajitoa muhanga
Does that all matter???

Spare us the Miss, unatafuta wa kuzaa nae na sio mume.... kwa iyo ingetosha tu yeye kua mzuri.

Hayo ya utu yatatuondoa kwenye kinyang'anyiro bila sababu bure. BTW nadhani nimekidhi vigezo kwa zaidi ya asilimia 94.
 
Nadhani una maanisha aliyeyelewa maana hamna mtoto anazaliwa na mzazi mmoja!!!

Ulichosema ni kweli madhara yapo makubwa... sema dada zetu hawaelewi
Yes kulelewa mkuu nilimaanisha.. hivyo..
 
kiukweli kabisa hakuna mwanamke asiyetaka kuolewa iyo nitaipinga kabisa ila sasa baadhi yao wanapokosa waowaji ndio utasikia habari za eti "SITAKI KUOLEWA NATAKA TU KUZAA" , Kwa hiyo ilo swala linategemea na uyo mwanamke labda hakuwahi kupata mtu aliye serious na maisha ndo sababu anaamua kuzaa bila kuolewa angalau mtoto kuwa faraja
 
Mimi naamini ni ubinafsi tu, unaamua kuzaa lakini hufikirii juu ya maisha ya mtoto bila baba. Nimekuwa na interaction na watu waliolelewa bila baba ndani, hawaipendi hali hiyo, kila mara wanalaumu sana kwa nini baba hakuwepo katika maisha yetu, laiti baba angenilea etc.

Mtu kufikiri kuzaa eti kwa vile ana uwezo wa kulea ni ubinafsi, huwazi kuhusu welfare ya watoto bali unajifikiria mwenyewe.
 
Mwache azae ulsiku hizi kuolewa sio hiari tena ni bahati, atakapotimiza miaka 50 hako katoto/ mtoto ndio faraja yake pekee
Mume han
Mtoto hana
Nyumba anayo
Uwezo anao

Sasa kwa nini asizae angalau ka kuja kurithi mali zake
 
Zaeni tu kwani tuko wengi tulozaliwa na masingo mama na maisha wanafurahia

Wanaume tumedhihirisha udhaifu wetu, zamani wanawake walikua wachache na waliweza kutumeneji wanaume,
Siku hizi wanaume wamekuwa wachache na wameshindwa kuwameneji wanawake
Wacha tu tutumike kama mbegu za maabara maana haina namna
 
Mimi naamini ni ubinafsi tu, unaamua kuzaa lakini hufikirii juu ya maisha ya mtoto bila baba. Nimekuwa na interaction na watu waliolelewa bila baba ndani, hawaipendi hali hiyo, kila mara wanalaumu sana kwa nini baba hakuwepo katika maisha yetu, laiti baba angenilea etc.

Mtu kufikiri kuzaa eti kwa vile ana uwezo wa kulea ni ubinafsi, huwazi kuhusu welfare ya watoto bali unajifikiria mwenyewe.
Kama vile ulikua mawazoni mwangu,

Wadada wanajifikiria wenyewe lakini hawamfikirii mtoto atakaelelewa bila baba,

Tena nishaona sana hasa wale waliozaa watoto wa kiume mbele wanakuja kushindwa kwenye malezi, maana mtoto anakua hamuheshimu mama ila baba akiwepo heshima inapatikana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom