Mtambuzi huu ni kama tu mtego umeweka kwa sie akina mama/dada kutaka kuwaona wanachukuliaje usaliti. Mapenzi na mahusiano ya mapenzi huwa yanakuwa mara nyingi overrated or underrated na wahusika.
Siku zote mwanamke ama mwanaume ukitaka kuyaendesha mahusiano kwa mtindo wa kujifananisha na wanawake (kama wewe mwanamke) ama wanaume (kama wewe mwanaume) wenzio katika umuhimu wako katika maisha ya mpenzi wako inaweza leta shida sana kwa upande wa kujiamini; pengine hata kumuamini mpenzi wako juu ya penzi lenu.
1. Je utaichukuliaje kauli yake hiyo?
Mwanaume ni nadra kuwa atamwacha mwanamke ambae ANAMPENDA kweli eti tu sababu kafumaniwa (awe ni girlfriend, mke ama hawara); Atamuacha sababu alikuwa labda anamhitaji tu na ana umuhimu wowote or kama huyo ambae kafumaniwa nae atasimama kidete kutaka hayo mahusiano yasiwepo
Hivo akawa hana jinsi na kujikuta he has to let go.
2. Kama aliweza kumsaliti mpenzi wake aliyempenda sana, je hudhani kuwa hata wewe anaweza kukusaliti siku moja?
Kipimo cha mtu kukupenda ni nini Mtambuzi? How do you really know kuwa huyu ananipenda? How do you know kuwa anavyokupenda wewe ni chini ama juu ya mpenzi (wapenzi) waliopita hapo nyuma? Huu ni mtihani
Nadhani ni muhimu na busara kwa mtu kuangalia
Kama anapendwa (and feels kuwa s/he is loved) then yastahili kuridhika na kufurahia mapenzi as long as kuna heshima, amani na raha ndani ya penzi lenu. Kila mwanadamu hufanya makoso (iwe makusudi ama kwa kutereza); hivo kumjudge kwa makosa aliyofanya hapo nyuma IMO inakua kama unamuonea
For you never know ukute anaweza asikupende kama wa kale but wewe anakujali na kukuthamini na kafika to the extent hata wazo la kukusaliti halipo kabisa
Kuna kitu kingine watu inabidi tutambue
In most cases huyo mpenzi wako wewe sio mpenzi wake wa kwanza
Wapo waliopita na kwa sababu mbali mbali (kwa kupenda ama kutokupenda) hayo mahusiana yalikufa na ndio maana ukawa nae kwa maneno mengine sio ajabu kama na wewe pia mkaachana na akawa na mwingine tena
What matters is living the moment... What matters ni kuhakikisha kama huyo partner wako ni perfect fit basi nyote muwe dedicated kuhakikisha mnaenda sawa no matter the storm.. Ingawa wote huwa twaomba Mungu wewe uwe ni destination na sio an experience
Whether your wish itakuwa ama haitakuwa ni time pekee ambayo hutoa jibu.
3. Je utaamua kujiondoa mapema katika huo uhusiano au utaendelea na uhusiano huo kwa ile dhana kwamba yaliyopita si ndwele?
Take note mie nime observe.. Mwanaume akiseme nilimpenda sana yule mwanake (mara nyingi anakuwa bado anampenda) na hali mwanamke akisema the same thing (inakuwa ni kweli alimpenda but sio lazima kuwa bado ampenda). Katika hili la muhimu kutambua ni kua ni rahisi saana to make it work na mtu wako ulie nae sasa kuliko kuanza upya... Ukitaka kuachia ngazi kwa such a trival matter (tena lisilokuhusu) then utaachana na wangapi? Of coz lazima uoneshe hujapenda na kwamba hutapenda akufanyie hivo... Na pia mie personally nitataka kumujua huyo mwanake na kama wapo karibu sababu huyo anaweza kuwa hatari kwa afya ya penzi letu... Haya hivo hayo ndio mawazo yangu.