Eti wanaume huwa hawaonji mara moja...!

Eti wanaume huwa hawaonji mara moja...!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,441
91331412.jpg


Upo msemo kuwa muonja asali haonji mara moja, na msemo huo hutumiwa sana kuwaelezea wanaume wanaowasaliti wenzi wao kwamba, hata wakifumaniwa, ipo siku watarudia tena.

Niliwahi kujadili jambo hilo humu wakati fulani, kama ungependa kujikumbusha unaweza kubofya hapa chini:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...waonji-mara-moja%85%85%85%85%85%85%85%85.html

Leo nina swali kwa dada zangu wa hapa JF:

Tuchukulie kwamba, unaye mpenzi ambaye mmependana sana, ni mwanaume wa ndoto zako, ana karibu sifa zote za mwanaume uliyekuwa unamuhitaji.

Inatokea siku moja katika mazungumzo yako na huyo mwenzi wako kuhusu mahusiano yake ya nyuma anakiri kwamba, wakati fulani aliwahi kuachana na mpenzi wake aliyempenda sana baada ya kumsaliti huyo mpenzi wake na mwanamke mwingine. Anazungumza hivyo bila kuonyesha hisia za kujutia kitendo chake hicho.

Hebu niambie,

1. Je utaichukuliaje kauli yake hiyo?

2. Kama aliweza kumsaliti mpenzi wake aliyempenda sana, je hudhani kuwa hata wewe anaweza kukusaliti siku moja?

3. Je utaamua kujiondoa mapema katika huo uhusiano au utaendelea na uhusiano huo kwa ile dhana kwamba yaliyopita si ndwele?

Hebu kina dada fungukeni hapa.............
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mtambuzi.

kuna aina mbili tu ya wanaume wataeweza kukwambia hayo:-
1.Mwanamme mjinga kuliko wote .
2.Mwanaume ambae anampago wa kukuacha (na anakupa misamiati hapo).

Kama mwanaume anakupenda kweli atafanya kila awezalo ndani ya uwezo wake
kukufanya uwe " comfortable" na kama atakwambia maisha yake hapo zamani za kale
Hayatakuwa na details nyingi sana. (kama ulivyoeleza hapo juu.)

kwa mwanaume wa hivyo
mi ntachukulia ananiambia mama funga virago kabla sijaku "exchange" mwehhh balaa sitaki.
 
mbona hiyo kauli nzuri sana nilishakutana nahuyu akaniambia hivi
1.nilishatembea na wanawake wasiopungua 100 na ushee ila katika wote hao nawapenda watano na katika hao watano jack na neema ndio naweza kuja kuwaoa alafu wewe uliyempenzi wake wa muda huo hajakutaja.
2 .unamwambia jamani mbona uko na mimi lakini bado unaendelea kuwasiliana na ma X -WAKO NA SIO MMJA AU WAWILI ANAKUAMBIA '',WANAMKE HAACHWI ILA ANAPUNGUZIWA MAWASILIANO TU''na kweli akienda popote anatembea na x-wake
3.Anakuwa na wanawake wengi kila kona inakuwa sio siri tena na wengine amezaa nao ni wengi kama kumi na wote anadili nao wazazi wanamkalisha nakumkanya anajibu''KHA SASA NIMEJITAHIDI SANA YAANI NIMEPUNGUZA IDADI YAO KUTOKA 20 SASA NIMEBAKI NA 12 TU AMBAO NAWAPENDA ''''' HAHAHAH
Mtambuzi najua umenielewa sana.
 
Hiyo ni kweli kabisa kaka Mtambuzi, Ndiyo maana mm huwa nakataa moja kwa moja, maana kuna wanaume wengine ukimuonjesha tu , lazima ataulizia tena, na ukimwambia hapana Anakwambia mbona siku ile ulinipa, na ukimwambia nilikupa mara moja tu anakwambia anataka tena , Sasa ubaya awe ndiyo boss wako, ameitaka tena na wewe umekataa utaona Rangi zote hapo ofisini, atakufanyia visa mpk utampa tena. Ndiyo maana mm huwa nakataa kabisa tangu mwanzo kama ni hapana ni hapana na sibadilishi mtizamo.

MM NILIOLEWA NA MWANAUME AMBAYE SIKUMTEGEMEA KUWA MUME WANGU , ALIDAI YEYE ANATAKA KUONJA TU,KUMBE ALIKUWA AMENIPENDA ANATAKA KUNIACHANISHA NA MCHUMBA WANGU, BASI ALIFANYA HILA MPK YULE MCHUMBA AKAJUA. NDIPO NIKAWA SINA PA KUSHIKA IKABIDI NIMKUBALI YEYE AWE MUME.
 
. Inatokea siku moja katika mazungumzo yako na huyo mwenzi wako kuhusu mahusiano yake ya nyuma anakiri kwamba said:
kuachana [/B]na mpenzi wake aliyempenda sana baada ya kumsaliti huyo mpenzi wake na mwanamke mwingine. Anazungumza hivyo bila kuonyesha hisia za kujutia kitendo chake hicho.

Hebu niambie,

1. Je utaichukuliaje kauli yake hiyo?

2. Kama aliweza kumsaliti mpenzi wake aliyempenda sana, je hudhani kuwa hata wewe anaweza kukusaliti siku moja?

3. Je utaamua kujiondoa mapema katika huo uhusiano au utaendelea na uhusiano huo kwa ile dhana kwamba yaliyopita si ndwele?

Hebu kina dada fungukeni hapa.............

Aliachana au aliachwa? Fafanua pls kwani hiyo ni muhimu sana; na inaweza kutupa picha kuwa alimpenda KWELI au aliFIKIRI anampenda.

Nina assume aliachwa na huyo mdada baada ya kusalitiwa.

haya anavyonisimulia hayo, na kutoonesha kutojuta ina maana 2 na naweza chagua nini cha kuamini inategemea ameuteka moyo wangu kiasi gani.
1. Hajutii mahusiano yake yote ya nyuma coz yuko na mimi and he is happy with me; na naweza chukulia cheating yake ilikuwa ni searching for something missing ambacho amekuja pata kwangu at last. AU
2. He is a self centered cheating bast.rd ambaye hajali feelings za wengine na hafai kuwa na mimi. (hii conclusion itakuwa supported na matendo yake na jinsi anavyonitreat na hata ile ya juu pia inakuwa supported and how he is now)
 
Mtambuzi huu ni kama tu mtego umeweka kwa sie akina mama/dada kutaka kuwaona wanachukuliaje usaliti. Mapenzi na mahusiano ya mapenzi huwa yanakuwa mara nyingi overrated or underrated na wahusika.

Siku zote mwanamke ama mwanaume ukitaka kuyaendesha mahusiano kwa mtindo wa kujifananisha na wanawake (kama wewe mwanamke) ama wanaume (kama wewe mwanaume) wenzio katika umuhimu wako katika maisha ya mpenzi wako inaweza leta shida sana kwa upande wa kujiamini; pengine hata kumuamini mpenzi wako juu ya penzi lenu.

1. Je utaichukuliaje kauli yake hiyo?

Mwanaume ni nadra kuwa atamwacha mwanamke ambae ANAMPENDA kweli eti tu sababu kafumaniwa (awe ni girlfriend, mke ama hawara); Atamuacha sababu alikuwa labda anamhitaji tu na ana umuhimu wowote or kama huyo ambae kafumaniwa nae atasimama kidete kutaka hayo mahusiano yasiwepo… Hivo akawa hana jinsi na kujikuta he has to let go.

2. Kama aliweza kumsaliti mpenzi wake aliyempenda sana, je hudhani kuwa hata wewe anaweza kukusaliti siku moja?

Kipimo cha mtu kukupenda ni nini Mtambuzi? How do you really know kuwa huyu ananipenda? How do you know kuwa anavyokupenda wewe ni chini ama juu ya mpenzi (wapenzi) waliopita hapo nyuma? Huu ni mtihani… Nadhani ni muhimu na busara kwa mtu kuangalia… Kama anapendwa (and feels kuwa s/he is loved) then yastahili kuridhika na kufurahia mapenzi as long as kuna heshima, amani na raha ndani ya penzi lenu. Kila mwanadamu hufanya makoso (iwe makusudi ama kwa kutereza); hivo kumjudge kwa makosa aliyofanya hapo nyuma IMO inakua kama unamuonea… For you never know ukute anaweza asikupende kama wa kale but wewe anakujali na kukuthamini na kafika to the extent hata wazo la kukusaliti halipo kabisa…

Kuna kitu kingine watu inabidi tutambue… In most cases huyo mpenzi wako wewe sio mpenzi wake wa kwanza… Wapo waliopita na kwa sababu mbali mbali (kwa kupenda ama kutokupenda) hayo mahusiana yalikufa na ndio maana ukawa nae – kwa maneno mengine sio ajabu kama na wewe pia mkaachana na akawa na mwingine tena… What matters is living the moment... What matters ni kuhakikisha kama huyo partner wako ni perfect fit basi nyote muwe dedicated kuhakikisha mnaenda sawa no matter the storm.. Ingawa wote huwa twaomba Mungu wewe uwe ni destination na sio an experience… Whether your wish itakuwa ama haitakuwa ni time pekee ambayo hutoa jibu.

3. Je utaamua kujiondoa mapema katika huo uhusiano au utaendelea na uhusiano huo kwa ile dhana kwamba yaliyopita si ndwele?

Take note mie nime observe.. Mwanaume akiseme nilimpenda sana yule mwanake (mara nyingi anakuwa bado anampenda) na hali mwanamke akisema the same thing (inakuwa ni kweli alimpenda but sio lazima kuwa bado ampenda). Katika hili la muhimu kutambua ni kua ni rahisi saana to make it work na mtu wako ulie nae sasa kuliko kuanza upya... Ukitaka kuachia ngazi kwa such a trival matter (tena lisilokuhusu) then utaachana na wangapi? Of coz lazima uoneshe hujapenda na kwamba hutapenda akufanyie hivo... Na pia mie personally nitataka kumujua huyo mwanake na kama wapo karibu sababu huyo anaweza kuwa hatari kwa afya ya penzi letu... Haya hivo hayo ndio mawazo yangu.
 
mbona hiyo kauli nzuri sana nilishakutana nahuyu akaniambia hivi
1.nilishatembea na wanawake wasiopungua 100 na ushee ila katika wote hao nawapenda watano na katika hao watano jack na neema ndio naweza kuja kuwaoa alafu wewe uliyempenzi wake wa muda huo hajakutaja.
2 .unamwambia jamani mbona uko na mimi lakini bado unaendelea kuwasiliana na ma X -WAKO NA SIO MMJA AU WAWILI ANAKUAMBIA '',WANAMKE HAACHWI ILA ANAPUNGUZIWA MAWASILIANO TU''
3.Anakuwa na wanawake wengi kila kona inakuwa sio siri tena na wengine amezaa nao ni wengi kama kumi na wote anadili nao wazazi wanamkalisha nakumkanya anajibu''KHA SASA NIMEJITAHIDI SANA YAANI NIMEPUNGUZA IDADI YAO KUTOKA 20 SASA NIMEBAKI NA 12 TU AMBAO NAWAPENDA ''''' HAHAHAH Mtambuzi najua umenielewa san
a.
 
Mambo gani haya mzee Mtambuzi kutukumbusha mambo ya ze past asubuhi asubuhi namna hii. Mzee mwenzangu tuwache tuchape kazi kwanza, hii mada ilitakiwa kujadiliwa siku za weekend!lol
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom