Eti Bongo kuna magari ya kike na ya kiume

Eti Bongo kuna magari ya kike na ya kiume

1686326765791.png

Kula chuma ya kiume hiyo🤣
 
Wabongo wana imani za ajabu sana, nakumbuka miaka ile bongo fleva inaanza kuchomoza kuna wajinga wakiona unasikiliza wabana pua wanakuambia ni mziki wa kike, wanasema mwanaume anasikiliza hip-hop
Hi tabia imehamia vyuoni, vijana wakishaingia chuo wanapiga chini nyimbo zote za kiswahili wanaanza kufagilia nyimbo za kizungu~Ukengeushi
 
Wala sio magari pekee, siku hizi wanasema ati mwanaume unatumiaje Simu ya Tecno 😂
 
magari ya kiume ni landcruiser v8, prado, discovery, fortuner na mfano wake
 
Ila kinachoumia hasa ni nyuchi zao mpaka kupata hayo magari mazuri.
Wanapitia mengi.
Sio wote man so usikariri, wengine wana run business zao wenyewe. Kama huyo nilieattarch picha yake hapo.
 
Kwa nijuavyo mm najua gari zipo za aina mbili tuu
1.. Manual hizi ni gari za kiume zaidi
2..Automatic hizi ni gari za kike

Halafu utamwona mwanaume anaendesha Automatic anajisifia gari linakimbia kweli kweli pale misigiri nilishuka na zote
unatuabisha wenye kuzivua na kuzivalisha
 
😀 sounds good kuona mwanaume anapush land lover discovery vogue Audi na land cruiser version yoyote tena manual.
Hivi vi auto auto vingi vya wadada😀😀
Unafikiri hizo gari ni sawa na map..umb..u kila mwanaume awe nayo
 
Bongo haiishiwii comedy, infact Bongo ni Bongo Movie.

Vijana wameisha brand magari kama Dualis, Murano, IST, RAV4, etc kama magari ya wanawake.

Pickup, harrier, vangaurd, x-trail, etc ndio za kiume.

Unakuta mtu anasema "sasa mwanaume ataendashaje IST au Dualis"

Alafu kuna mtu unakuta na yeye anababaika eti anunui gari ambayo ameipenda eti kisa watamsema kuwa anatembelea gari ya kike.

Kupambana na fikra za jamii duni ni ngumu sana, wataanza kuja na sababu mia nne kwa nini mwanaume asitembelee dualis wakati japan wanaume wanazitembelea kama wote.
Hata ukiwaza kwa kutumia makalio tu mkuu...Nadia ni gari ya kiume kweli!!?
 
Back
Top Bottom