Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Mbunge Ester Bulaya amesema “Mkataba wa ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere unaeleza mkandarasi akichelewa kukamilisha mradi anatakiwa kutozwa tozo, mradi ulitakiw akukamilika 2022 na taarifa zilizopi hautakamilika mwaka huu.
Amesema hayo Bungeni na kuhoji kwanini TANESCO hawajamtoza tozo Tsh. Bilioni 329 wakati Serikali ikichelewa kumlipa Mkandarasi inatozwa Tozo.
Aidha, amesema Mkandarasi alitakiwa kujenga miradi kwa ajili ya huduma za kijamii ya zaidi ya Tsh. Bilioni 200 lakini huduma hizo hazionekani, pia inadaiwa anajiandaa kufungua kesi Mahakamani dhidi ya Serikali akidai nyongeza.