Escrow: Stanbic Bank kuchafua hali ya hewa

Escrow: Stanbic Bank kuchafua hali ya hewa

Wakiweka hayo ya stanbic bank ccm inasambaratika karibia wagombea wao wanaotajwa wa urais woote wamo isipokuwa manywele tu
 
Tena wewe wa kwanza kabisa hahahahah mtafanya watu waogopane jamani. Akitokea mtu ana dawa ya kuficha majina lazima awe tajiri hapa chezea tz na imani za kishirikina

Si hata wewe unaona wanakemea watu wengine wasiue Albino lakini vidole vyao vya mikononi vimejaa mapete ya hao waganga wa jadi!
 
Wakiweka hayo ya stanbic bank ccm inasambaratika karibia wagombea wao wanaotajwa wa urais woote wamo isipokuwa manywele tu

Manywele yeye alishapata kikombe chake cha Richmond hana taabu! wapo waliogawana nyumba za serikali kama vile Nyerere aliwajengea wao! hawa watu ni waizi wakutupwa! na wala hawajali!
 
Nimepenyezewa taarifa na mnene mmoja wa Stanbic kuwa Viongozi waandamizi wa Stanbic Bank huko majuu wanakaribia kuchafua tena hewa ya nchi.Waandamizi hao wameagiza kuanikwa kwa majina ya waliochota malumbesa ya fedha za Escrow. Wamewaagiza wakuu wa hapa Tanzania kuhakikisha ifikapo Aprili mosi mwaka huu,majina hayo yawe public pamoja na mihamala yao ili kusafisha taswira ya Stanbic.

Ukisikia kusafisha hapa na kuchafua pale ndio huku.Siombi hilo litokee.Hawa wa Mkombozi Bank aka wa Rugemalira wametuhenyesha hivi.Wa Stanbic itakuwaje? Stanbic Bank,please and please, re-think and re-decide. Tumechoka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Kwenye uzi wangu wa kudai meli yetu Kagera......nilisema tutaitangaza Stanbic kuwa adui mkubwa wa Tanzania.
 
Wewe mburula hizo ni ndoto za mchana; hakuna benki ya kimataifa kama ilivyo Stambic inayotoa taarifa za wateja wake !!!! Ni hizi benki uchwara kama Mkombozi ndio zinaweza kulazimishwa kutoa siri hizo!!!
Tena usiombe ukaota ukiwa umeshiba.?
 
Stanbic ndio huko kina Mbowe inasemekana walichukulia mgao wao!?

sio kina mbowe tu hata familia ya mkuu wa kaya imo ndio mana wanaminya isitajwe hiyo mambo ya STANBIC hali ya hewa itachafuka.
 
Back
Top Bottom