Ephraim Mrema na Ufisadi TANROADS

TIARAEI ndiyo wapi? Au ina maana ya Ti Ar Ei? hihiiii Mie nilishachekwa kuwa sisi Watanzania tunaitamka vibaya R. Tunasema ARA badala ya AR... Sijui upi ni ukweli. Wakali wa lugha nijulisheni ili siku nyingine nijitete.
Huu ukabila mama naomba unisaidie. Mie najua tatizo lipo na inabidi liongelewe ila kuna wengine wanadai kuwa hiyo imesababishwa na HISTORIA ya nchi katika devide and rule..... Au mie nina KIHINDIHINDI nini? Maana Kizunguzungu Tanzania hakipo tena na sasa kwa mbali nahisi Kichagakichaga. Just asking.


Historia kwa kweli inachukua mkondo wake katika hii kitu, ila waliopata nafasi wakatake into advantage hasa kwa siku za karibuni ambapo wasomi wamekuwa wengi.
Na katika historia ya wachaga kuna mawili, moja ni kwamba walienda shule na hata ukiangalia hadi kufikia miaka ya mwanzo wa tisini, mkoa wa kilimanjaro ulikuwa ukiongoza kwa kuwa na shule nyingi za seko. Shycom ilikuwa ina idadi kubwa ya wachaga, sasa unategemea nini Bcom na na maexpert kwenye fani za fedha?

Pili, wachaga wanaweka mbele kujuana, na hivyo wenyewe hawamuweki mtu wao kwa memo tu, bali wanahakikisha ana vyeti vya kufaa. Tatizo linakuja kwamba kazi nyingi zilikuwa hazitangazwi, mzazi wako anamfuata baba yako waubatizo na kumwambia kuwa kijana kamaliza kusoma na anaupper second. Baba wa ubatizo au, shemeji, au jirani kule moshi, au mwanaukoo either kwa upande wa baba au mama anafanya mambo yeye mwenyewe au anaongea na jamaa zake hata kama sio wachaga kuhusu nafasi za kazi kwenye nafasi nzuri. Basi mwisho wa siku kijana anaambiwa aandike barua aombe position fulani anaisubmit na vitu kama hivyo. God knows better!

Huku kwetu tunaita tiaraei kumbe tunakosea eeh?
 
Ukabila
Kwa mara nyingine zile chuki dhidi ya wachagga zinaendelea kujitokeza kila jina la Kichagga linapotajwa. Tumefikia mahali wachagga wasiwe viongozi wa idara yoyote ile Tanzania na serikali itoe Memo kuelezea kuwa Wachagga hawastahili kushika nafasi yoyote ya juu, na kama wanashika wahakikishe kuwa akija mchagga "mwenzao" kuomba kazi asipewe nafasi hayo ili kusije kuonekana ukabila.

Na wachagga wote wenye kushika nafasi za juu serikalini wajiuzulu ili kupisha wananchi wa makabila mengine.

MMKjj
Asante kwa kulielezea hili vizuri. Lakini naona na wewe unakwenda kwenye MATAWI badala kwenda kwenye MIZIZI. Hapa tatizo si WACHAGA. Kwa wengine tunajua hili ila "ukiingia kichwani kwa watu wasioona mbali kwa mbele na kwa nyuma utaona kabisa wao tatizo ni Mchaga/Mhaya..." Tatizo ni kuwa kwa nini wengine WAMEBAKI NYUMA? Wamebaki nyuma kiasi kwamba hata ungelikuwa Chenge, ukitaka kuajiri na kutafuta hizo SIFA utaona kuwa waliokuzunguka ni Wachaga/Wahaya. Nilipokuwa JKT tulikuwa tunaandikisha na dini yako/Kanisa. Mhhh, asilimia 90 ya watu JKT walikuwa WAKATOLIKI. Pia hapa ukitaka kuajiri utaona kuwa WANAOSTAHILI ni hawa Wakatoliki. Sasa tatizo ni WAKATOLIKI WANAPENDELEANA??? Hapa tatizo ni kama alilosema Jokakuu na mimi kulielezea mapema kuwa ni HISTORIA imefanya hivi. Sasa tatizo si kuwa WACHAGA waache kazi au wasiajiriwe. Itakuwa yaleyale ya Uganda kufukuza Wahindi ingawa kuna wengine wanasema INAWASAIDIA SANA LEO. Sijui kama ni kweli au kwa sababu wana M7. Hili swala inabidi kwenda MORE DEEP na si kulichukulia juu juu. Kama ni hivyo, na mie napendekeza "Wakatoliki waache kazi na au wasiombe/wasipewe kama kwenye hicho kitengo juu yupo MKATOLIKI".
 
Mwanakijiji, something whiff aroud, naogopa sana kuproject this issue. Tunakoendea sijui as watu wameshakuwa sensitive na sijui kama kuna uwezekano wa hao watu kuondoka na kuwaachia makabila mengine. Kuna Wahaya na wanyakyusa wamedominate positions pia.

My take, ianzishwe directorate ya serikali na agency zake zote. Nafasi zote za kazi ziwe zinapelekwa kwenye hiyo directorate ambayo itazitangaza na kufanya usaili kwa kuhusisha experts from the appropriate unit inayotaka mfanyakazi.
 
hoja ya mbunge haijajitosheleza. hajamlinganisha bwana mrema na basic facts kwa hali yoyote.
si kielimu, kiujuzi, kimshahara na mengineyo.
atufafanulie hayo kwanza, ndio tumuite mtu fisadi.
kama CEO wote wanalipwa hivyo kwanini tumlalamikie yeye ( japo kuwa mie kwa nafsi yangu naona huo ni mshahara mkubwa sana kulinganishwa na mishahara mengine wanayolipwa watanzania)
 
hakuna haja ya kabila moja kuacha kazi au wasiombe kazi kisa wanaogopa ukabila! nafikiri mmeshindwa kumuelewa MKJJ...yeye katumia maneno yale kuonyesha ilivyokuwa surreal kumtegemea mtu asiombe kazi kwa kuwa tu wachaga wako wengi kwenye kazi fulani.
 
Mwanakijiji, something whiff aroud, naogopa sana kuproject this issue. Tunakoendea sijui as watu wameshakuwa sensitive na sijui kama kuna uwezekano wa hao watu kuondoka na kuwaachia makabila mengine. Kuna Wahaya na wanyakyusa wamedominate positions pia.

My take, ianzishwe directorate ya serikali na agency zake zote. Nafasi zote za kazi ziwe zinapelekwa kwenye hiyo directorate ambayo itazitangaza na kufanya usaili kwa kuhusisha experts from the appropriate unit inayotaka mfanyakazi.

Mama hata ikianzishwa hiyo directorate n.k itakuwaje kama Wachagga, Wanyakyusa na Wahaya wakizidi kujazana, they have had had an unfair advantage toka zamani. Kwanini tusiwazuie kuajiriwa angalau kwa miaka mitano?
 
Mama hata ikianzishwa hiyo directorate n.k itakuwaje kama Wachagga, Wanyakyusa na Wahaya wakizidi kujazana, they have had had an unfair advantage toka zamani. Kwanini tusiwazuie kuajiriwa angalau kwa miaka mitano?

ni kukiuka haki za binadamu. Kumbuka ambaye hata ajiriwa kwa ajili babake, mamake, au dadake alishaajiriwa kama mchaga atakuwa hatendewi haki. Its time to start afresh. Tuachane na ubaguzi and look on the sustainable way forward.
 
Mengi yanasemwa kuhusu Mrema. Ombi langu ni kama kuna mtu mwenye data za wachagaa wangapi wameajiriwa tangu Mrema azitoe.CV za wale waliokosa hiyo nafasi pia zitolewe ili sote tuweze kuzilinganisha na kuzichambua. Hivi Mghana alikuwa analipwa kiasi gani? Kuna ubaya wowote kwa Mtanzania kulipwa kiasi hicho au Tanzanians hawapaswi kulipwa kiasi hicho. We need to encourage Tanzanian walio nje kurudi kushika hizi nafasi badala ya kuachiwa wageni. Watanzania wanaofanya kazi kwenye company za kigeni wanalipwa zaidi za hizo za CEO wa Tanroads hili mbona hamlizungumzi?
 
maswali ya msingi hayajibiwi, ni hasira na chuki tu zinaendelea. Hadi mwisho wake hili swala litaonekana kama ni la umbea na chuki binafsi.
Pamoja na kwamba mbunge alionekana ana wivu (maybe wa maendeleo) na alishindwa kupanga hoja zake, labda kuna la maana la kuchunguza, labda kuna kosa la jinai, labda kuna kosa la kimaadili.
tutajauje? kama tukiendelea kuattack uikabila wake ambao hauna kosa, wak a hakuchagua.
1. je ana kosa?
2 waliomuweka wana makosa?
 
Watanzania bwana!

Tunalilia hatulipwi mishahara mizuri, halafu tunakimbilia kuingiza vimisheni tauni, kujiongezea.

Tumelewa UJAMAA uliosema kuwa kuwa Tajiri au kuwa na Kipato kikubwa ni dhambi, aliyekuwa na mshahara mkubwa tulimuita MNYONYAJI, BEPARI, BWANA na sisi kulea UNYONGE na UTWANA!

Nashangaa sana kuwa mpaka leo hakuna mipango mizuri iliyofanywa kuhakikisha kuwa mchakato wa Mishahara Tanzania unabadilishwa kwenda sambamba na mfumo wa Kiuchumi tulionao.

Kila siku Wafanyakazi wa Tanzania wanapunjwa mishahara kutokana na Serikali kujenga tabaka la watu tegemezi. Kila siku unasoma Serikali yetu iliyodai tumeindia UCHUMI HURIA inafanya mambo ya welfare, kusaidia jamii na wafanyakazi hasa Waalimu, Wauguzi, Askari, Polisi wajengewe nyumba na Serikali, lakini mishahara yao inabakia kuwa duni.

Kwa nini badala ya kuwajengea nyumba, wawalipe Watumishi wa Serikali na Mashirika mishahara mizuri na wawape mikopo ya kujengea hizo nyumba?

Hili la Mrema la watu kudai analipwa pesa nyingi sana na ni tatizo, halina nguvu. Kama mshahara uliotangazwa ulionyesha kuwa hicho ndicho kiwango, na Mrema alipoanza majadiliano ya kuingia mkataba wa kufanya kazi akaweza kushawishi kwa kutumia vigezo vya Utaalamu wake, na mshahara aliopewa Mghana, hakuna kesi kuwa eti yeye ni Fisadi.

La kujifunza kutoka hapa ni kutaka reform ya mishahara Tanzania! Tunataka Serikali iunde uchumi mzuri ambao utaruhusu kuongfezeka kwa mishahara na kupunguza makali ya Maisha.
 
Bonus Sh 122,000,000/= ?????? lol! imekua vodacom sasa hii.....halafu mtu kama huyu utakuta bado haridhiki na hapo..anafanya na ufisadi juu.!! Hii ndio TZ

Kweli kabisa..ktk bishara kipimo cha kupata bonus ni faida iliyopatikana etc! nilitegemea kwa TANROADS ingekuwa barabara zilizojengwa au kukarabatiwa lakini wapi??????
 
Tena ikiwezekana na Mrema aongezewe mshahara kuliko aliokuwa akuilipwa Mghana, ni kuwadhalilisha watanzania kusema kuwa Mrema analipwa fedha nyingi, kwani watanzania hawastahili hizo fedha nyingi?
Kama ajira yake ina mushkeli aulizwe Kikwete ambaye ndiye aliyesanction uteuzi wake, Mrema atasakamwa bure bila kosa kwani yeye hakujiingiza kwenye hiyo ajira. Lakini, kama alijiingiza katika manouvre fulani iliyosababisha akap[ata ajira hiyo, that is differemt sotry.
 
Mpita Njia.. tatizo siyo utendaji wake au performance ya TANROADS, ingekuwa hivyo Mpologomtsyi angesema..! Yeye tatizo lake ni binafsi.
 
Mrema ilipostiwa mahali ambako nadhani isingepata attention inayostahili. Je, hapa kuna ufisadi?[/B]
NASHUKURU HILO LA MREMA WA TANROADS LIMEKUJA MANAKE WATU WALINISHANGAA SANA NILIVYOANZISHA THREAD YA CV ZA MACEO WA SERIKALI. WENGI WAKAANZA KUNILAUMU. LAKINI MTAONA FAIDA YAKE JAMII FORUM KUWA YA KWANZA KUJUA MAMBO NA KWAMBA KUNA WATU WANAJUA MAMBO MENGI MAOVU. JAMANI NAOMBA KAMA TAKUKURU IKO SERIOUS IKAMCHUNGUZE NA KAMISHNA WA BIMA!!ANAUA BIMA TANZANIA,WANANCHI HAWAJUA CHOCHOTE KUHUSU BIMA NA PIA AMEWAPA WAKENYA NA WAHINDI WASIO NA ELIMU KAMA YEYE KUENDESHA KAMPUNI ZA BIMA NA AMEAJIRI WAHAYA WENGI KATIKA OFISI YA BIMA NA WENGINE HATA HAWAJULIKANI WAMEAJIRIWA KAMA MAOFISA AU LAAH. ANAONGOZA KWA KUSAFIRI NJE NA KUWEKA MAZINGIRA MAGUMU YA KAZI!
 
Watanzania bwana!

Tunalilia hatulipwi mishahara mizuri, halafu tunakimbilia kuingiza vimisheni tauni, kujiongezea.

Tumelewa UJAMAA uliosema kuwa kuwa Tajiri au kuwa na Kipato kikubwa ni dhambi, aliyekuwa na mshahara mkubwa tulimuita MNYONYAJI, BEPARI, BWANA na sisi kulea UNYONGE na UTWANA!

Nashangaa sana kuwa mpaka leo hakuna mipango mizuri iliyofanywa kuhakikisha kuwa mchakato wa Mishahara Tanzania unabadilishwa kwenda sambamba na mfumo wa Kiuchumi tulionao.

Kila siku Wafanyakazi wa Tanzania wanapunjwa mishahara kutokana na Serikali kujenga tabaka la watu tegemezi. Kila siku unasoma Serikali yetu iliyodai tumeindia UCHUMI HURIA inafanya mambo ya welfare, kusaidia jamii na wafanyakazi hasa Waalimu, Wauguzi, Askari, Polisi wajengewe nyumba na Serikali, lakini mishahara yao inabakia kuwa duni.

Kwa nini badala ya kuwajengea nyumba, wawalipe Watumishi wa Serikali na Mashirika mishahara mizuri na wawape mikopo ya kujengea hizo nyumba?

Hili la Mrema la watu kudai analipwa pesa nyingi sana na ni tatizo, halina nguvu. Kama mshahara uliotangazwa ulionyesha kuwa hicho ndicho kiwango, na Mrema alipoanza majadiliano ya kuingia mkataba wa kufanya kazi akaweza kushawishi kwa kutumia vigezo vya Utaalamu wake, na mshahara aliopewa Mghana, hakuna kesi kuwa eti yeye ni Fisadi.

La kujifunza kutoka hapa ni kutaka reform ya mishahara Tanzania! Tunataka Serikali iunde uchumi mzuri ambao utaruhusu kuongfezeka kwa mishahara na kupunguza makali ya Maisha.

Rev na wengine wengi mliochangia hili suala!

Kwanza kabisa naungana na wewe katika kushangaa hili la watu kubeza mshahara anaolipwa CEO wa Tanroads kwanza naomba kuainisha haya machache:
Kwanza, package ya malipo ya CEO wa tanroads inachangiwa na World Bank na Serikali ya TZ....uwiano kama sijakosea ni 70-80 kutoka World Bank na 20-30 kutoka Serikali ya TZ. Hii inaonyesha dhahiri kuwa serikali yetu haigharamii pesa nyingi kama Mh MB anavyotaka kuonyesha.

Pili, Hii package ni kwa CEO yeyote awe mTZ au foreignor....kwa wale wasiojua...CEO wa kwanza wa Tanroads alikuwa anatokea Norway na wa pili alikuwa anatokea Ghana na wote walikuwa wanakula the same package.....iweje leo anakula mTZ halafu wanamtolea macho na kumsimanga kama vile alikaa chumbani yeye na mkewe wakajiandalia hiyo package. Mbona wageni walivyokuwa wanalipwa hizo hela zote hakuna aliyenena kitu......viongozi wetu waache hii tabia...inayofanana na ukoloni mamboleo!

Tatu, linalotakiwa kuchunguzwa hapa na ajira ya Mrema ilivyopatikana sio malipo yake.....kwani inasemekana ni kweli hakuwa kwenye shortlisted candidates....hiyo list inasemekana ilikuwa ni ya wafanyakazi wa tanroads (maregional engineer 2 na madirector 2). Alikotokea Mrema na kuuchupalia uCEO wa tanroads ndiyo suala muhimu.....
 
Kigoma,

..actually i read somewhere kwamba Mrema alifukuzwa kazi toka Konoike. haikuelezwa vizuri alifukuzwa kazi kwasababu zipi. lakini hilo huwa ni doa kubwa proffesionally.

..hiyo "package" wanayopewa ma-CEO nadhani ni kubwa mno na haiendani na hali ya uchumi wetu. kuna umuhimu wa kuiangalia upya.
 
Suala la kuajiliwa kimtindo si kosa la Mrema bali mwajili. Vilevile Kumattack Mrema mojakwa moja kuwa kaajiriwa kupitia mlango wa nyuma ni kumkosea heshim,a na ni udhalilishaji, Mpologomi kumtaka radhi Mrema. Maswala mengine ya kuwafukuza wafanyakazi ni kitu ya msingi hilo linaweza kushughulikiwa kupitia vyombo husika.
 
Hii thread kila siku nilikuwa nairuka kumbe kuna ufisadi wa aina yake hapa?

Ballali mwingine huyu, mshahara zaidi ya dola 25,000 kwa mwezi lakini utendaji bado wa kusua sua.

Nchii yetu inaliwa na watu wengi mno, laiti haya mapesa yote tungeyaweka kwenye miradi ya uzalishaji, sasa vijana wetu wengi wangelikuwa na ajira badala ya kuendelea kuwa malofa kwenye nchi yao.

Pamoja na pesa zote hizo huenda bado jamaa anachota rushwa kama Chenge tu.
 
Back
Top Bottom