Masaki
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 3,463
- 752
mmmmh.
Tall vipi mbona unaguna? Isije kuwa mkeo anaitwa Flora na mama yake alikuwa mwalimu wa shule ya msingi!!!!? Hahahahaha!
mmmmh.
Mkuu nazikumbuka sana hizo zama ila mie nilitesa na MOCCASSIN bana, ile kiatu ilikuwa BAB kubwa!!!!!!!! Moccassin yangu ilikuwa inajumuisha Moustache na kitai hapo mbele halafu ya brown, baba TOTOOOZ zilizimika sana tuu juu nna panki la kufa mtu kinyozi mwenyewe kwenye kioo cha kabati la chumbani. Kwenye timu ya BOLI nipo namba 8 ya shule full control wakati huo najiita Nii Lamptey wa GHANA, darasani napiga within top 5 Baba we acha tu maisha yalikuwa matamu Mnoooooooooooooooooooooooo
duh mzee ukumalizia kum-do kinguo nguo?Cecy alikua lanne b niko a,mtoto kanizimia kashindwa kusema akavumilia we wapi
Siku moja washkaji kama wanne hivi wananifata twende B kuna ishu kufika nakuta kundi la wanafunzi wamemzingira mtu....namwona binti wa watu kajiinamia analia wamemzunguka bado sijaelewa naskia "..ntakupa upige mpaka uchoke.." bado sijaelewa nashangaa...
Kumbe aliniandikia barua na hayo maneno ndani yake sasa wakati wa kuniletea ikibambwa wakaisoma
dah mtoto wa watu alikosa amani...
Sikujua kwamba nilikua HB mpaka baadaye kidogo
Tall vipi mbona unaguna? Isije kuwa mkeo anaitwa Flora na mama yake alikuwa mwalimu wa shule ya msingi!!!!? Hahahahaha!
.........Wanaume mna vituko kweli kweli, nimesoma maoni ya watu hapa hadi na mie nimekumbuka enzi hizo. Nakumbuka mwaka 1995 nilikuwa darasa la 4 basi mwenyewe ndio mtoto sijui lolote,kuna mkaka alikuwa anasoma darasa la 6, akaandika barua kwamba ananipenda na kumpa rafiki yake aniletee. Ndani ya hiyo barua alikuwa kaweka Tsh. 100 ya noti ya enzi hizo.........basi mimi nilisoma hiyo barua na kukuta mwenyewe kachora ua na kusema kwamba ananipenda. Ila mimi kwenye akili yangu wala sikuwa na uelewa nini haswa anamaanisha, basi baada ya kuisoma ile barua nikaamua kwenda kumpa mama yangu.
Mama akaanza kuniuliza ni nani kakupa hii barua? Nikamjibu kuna mtu nasoma naye ndiye aliyonipa hiyo barua kule shuleni...........basi kesho yake asubuhi mama akanipeleka shuleni hadi kwa mkuu wa shule na kumuita yule kijana aliyetumwa kunipa barua ili amtaje ni nani aliyompa barua ili aniletee. Yule kijana akamtaja jina huyo mkaka aliyekuwa darasa la 6 kwamba ndiyo aliyompa barua. Yule kijana alikuwa akiitwa Nelly alichapwa bakora 6 kutoka kwa mkuu wa shule.
Duh kumbe wewe bado ni kinda hivyo....
.........Nyani bana sasa toka mwaka 1995 hadi leo ni miaka mingapi imepita hadi uniite kinda........Mie sasa mtu mzima bana lol.
mnakumbuka raha za kuandikiana barua enzi za mwalimu? nani ana kumbukumbu hizo
unaambiwa kwa mara ya kwanza siku ile nilienda winga (kusimamisha) mpaka nilipofika home ikabidi nikae kidogo nje mpaka mashine ilipopoa (kama nusu saa hivi) ndio nikaingia home maana kikaptula chote kilikuwa kimepelekwa mbele
duh! hyo ilikuwa kali nimecheka mpaka basikuna jamaa mmoja alikuwa house boy wa nyumba ya jirani alitokea Musoma, sasa akapata demu akaimbisha na kukubaliwa kipindi hicho ndio UKIMWI umeingia bado mpya na kondomu ndio hata kutumia watu hawajui basi yule jamaa siku hiyo anaenda kuchenga ilibidi avae kondomu toka nyumbani kwao halafu ndio akaenda kwa demu jamaa njia nzima anatembea na mpira halafu kufika kule walipoaidiana demu hakutokea