ENZI ZILE (Tukumbushane)

ENZI ZILE (Tukumbushane)

...nakumbuka form one nilikuw bonge la domo zege,,,, sasa waskaji zangu kina "lusekelo" wakanituma nikakatokee kabinti kamoja hivi.... (sikakumbuk i jina)... wakanipa maneno kabisa ya kumwambia kwamba nanukuu "" MWAMBIE HIVI MIMI NIMETOKEA KUKUPENDA SANA ... TANGU MDA MREFU NILITAKA KUKUAMBIA LAKINI NILITAKA NIKUCHUNGUZE KWANZA TABIA YAKO... NIMEONA TABIA YAKO NZURI NA NINATAKA UWE MCHUMBA WANGU" nikagoma kwenda... wakanicheka sanaaaa... kuondoa noma nikasema acha niende nikakomae kwani kitugani bwana.... kufika pale maneno yakanitoka.... si nikaanza kumwuliza habari za mwalimu wa agriculture kama aliingia class.... baada ya hapo nikarudi kwa masela huku natabasamu wakajua yess jamaa kakubaliwa...wakaniuliza amesemaje... nikasema amekubali ila anasema nisubiri anifikirie kwanza.... wakaamini...

si wakaanza kumuitayule demu shemeji.... demu akamindi akaenda kwa ticha tukapewa adhabyu ya kufukia mashimo barabarani....
 
enzi hizo kondom hatujui ni nin.nakumbuka 1992,tuliokota condoms kibao nyuma ya gest moja tulikuwa tunakata majan ya mbuz,tuligawana kila m1 2,mi nikaenda nazo home huku napuliza kama puto na majan yangu kichwani bbilimkuta maza na ding wamekaa nje na mgen, mama alinifuata na kuanza hunipa kibano,ila hakunieleza ni nibi
 
1993 nikiwa stnd2 tulikuwa tunaenda kula zambarao kila tukitoka shule mchana, mti huo ulikuwa karbu na ofis ya tra wlya rombo,palikuwa na choo ambacho hakitumiki,siku1 tukakuta kuna kondom zimetumika na nyingine zimebak,dogo m1ja alikuwa anaitwa pius alikuwa anazifaham na anajua matumiz yake akachukua moja akaivaa akaanza kutuelekeza,sasa kwa kuwa alikuwa ndogo na haimtoshi dogo aliifunga kwa kamba a
 
Kitu kingine nimekumbuka....mnakumbuka zamani kulikuwaga na malori yanapita mitaani yakiuza magunia ya mkaa? Basi wale wauza mkaa walikuwaga wanakaa nyuma kwenye magunia kule...basi hawa jamaa walikuwa kila wakipita mtaani lazima tuwazomee na kuwatania sana. Basi walikuwa hawapendi.....siku moja lori la mkaa likapita mtaani bana...basi mimi kujifanya mjanja si nikaanza kuwatania. Heheheheee siku hiyo wakaamua kunitolea uvivu bana...jamaa mmoja akanishukia akaanza kunikimbiza. Ebana nilitoka mkuku kaa nini unaambiwa huku nikipiga mayowe...baaaaba...baaaaba.....dah...yaaani nikikumbuka nacheka sana. Lakini uzuri hakunipata wala nini...nilimtimulia vumbi tu jamaa
tunawaita "maji yamekatikaa" kisha wanatoa matusi ya hatar
 
Nakumbuka kwenye miaka ya 94 au 93 hivi kuna njemba lilinituma condom dukani yy alikua anaona noma kwenda, kwenda pale mwenye duka akagoma kunipa akataka nimuoneshe aliyenituma, ile kwenda na muuza duka kwenye ule uchochoro nilipomuacha yule jamaa, alitoka mbio za ajabu
 
Wakati nipo vidudu miaka ya 91 nakumbuka nilienda dukani kunywa soda,kipindi hicho kulikua na bahati nasibu kwenye pepsi, ile kupekua kizibo nikaona imechorwa picha ya baiskeli, kuna jamaa mmoja akaniomba tubadilishane kile kizibo anipe gari la mchanga, nikamuona nimempaaata
 
Dah enzi hizo noma,mi nakumbuka tulikuwa watoto kadhaa wa mtaa tunajisaidia haja kubwa then tunachamba kwa kujiburuza kwenye kichuguu,msala mda wa kuogeshwa!!!!
 
Enzi hizo za 99,kuna anko angu alikuwa kicheche mbaya,sa alikua akiwa anataka kumuita demu wake atoke nje,anajiita jina lake yake(uncle),"johniii",basi demu anatoka,wanakuja kwa bibi,mi nawekwa kuangalia ka kuna mtu anakuja niwatonye,ha ha haa!
 
Nakumbuka mwaka 1989 niko Uwanjani shule ya msingi(sasa inaitwa Kawawa),tukiwa mapumziko ikaja gari ndani yake kuna wazungu watatu na waafrika wawili wote wamevaa nguo nyeupe,ilipopaki tu nje ya ofisi ya walimu nikajikuta nimeropoka 'WANYONYA DAMU' wengine wakanipokea,watu tukatawanyika walimu wanastuka shule haina mtu,wakapiga kengele mpaka wakachoka. Kumbe walikuwa wamekuja kutuchoma ndui ila zoezi liliahirishwa mpaka kesho yake. Sikwenda shule wiki nzima na ndui sikuchomwa.
 
Yeah, I can Imagine! Ukizingatia siku hizo underwear chache, ukibahatika unavaa zile VIP.....kazi kweli kweli!

heheheee usinikumbushe chupi za enzi zile, wanaume VIP na zingine zilikuwa 007 james bond!! wanawake kuna aina fulani zilikuwa zimechorwa moyo na mkuki unachoma katikti zimeandikwa 'express mid night' hizo rangi zake sasa, nyekundu, kijani dark blue n.k tena hizo kwa wacheche waliobahatika wengine walikuwa wanapiga utupu tu hasa wanaume chupi wamezijulia ukubwani walio wengi
 
Napita tu,hizo enzi za chachacha,solo na utanikoma saa sita!

dum kampini nakumbuka tulikuwa tunaziita 'robot shoes' (naona ck hzi vimerudi kwa jina la kibajaji), watu tulikuwa tunavaa robot shoes, halafu tunacheza brake dance, nakumbuka enzi za kwenda majumba ya sinema za mchana saa 8 tulipoona sinema za michael jackson wacha tuwe tunaiga kucheza nakumbuka kakangu alivunjika mkono ktk harakati za kucheza nakumbuka baba alimpeleka hosp akafungwa pop aka mhogo halafu aliporudi home akapata kichapo cha nguvu! nakumbuka enzi hizo uncle wangu walikuwa wanaviatu vikiitwa 'rise on' virefuu vya brown vilikuwa vinauzwa BORA enzi hizo sh 99. kasheshe ilikuwa namna ya kuzipata hz sh 99! baade tukawa tunaziita 'teremka tuzoze' au 'mfaume waniliza' mmh tumetoka mbaali jamani
 
Kumbe wote ni vijana? Nilifikiri tumecheza wote "Embakasi" ya Les Mangelepa?

hee embakassy umenikumbusha mbaali enzi hizo uncles ndio walizicheza hizi na kulikuwa na kibao kingine murua 'nyako konya' kilifunika mbaya enzi hizo
 
kulikuwa na suruali 'pekos' za kitambaa cha krimplin na shati za kubanaaa 'slim fit' chini mtu katinga 'rise on' kachana afro la nguvu aka kibanda akiogea rexona ndio kidume cha nguvu madem wanamkimbilia . huwa naangalia picha ya uncle wangu alipiga studio moja arusha amevaa vivazi hivyo halafu kapigia kwenye stand imewekwa maua juu imeandikwa 'forget me not' huku kaweka alama ya vidole viwili juu eti piece.. oh those good days hazitarudi tena
 
Hahahaa!Mh, umenikumbusha vijarida vya dr love pimbi, enzi hizo tunavisoma darasani! Kumbe vilikuwa vya ukweli eeh!

halafu nakumbuka..........makala za harakati za pimbi.............................na kwenye gazeti la baraza la kenya lililokuwa likitoka kila Alhamisi..panapofuka moshi panaficha moto...........

mpaka leo huwa ninajiuliza kwa nini mzee kifimbo hakulipiga marufuku gazeti hilo la baraza maana lilikuwa limejaa vituko vya ngono kibao.........
 
Aaah mimi nilikuwa mtu wa ndaba zile za kuchumpa. Mnazikumbuka Avia, Hi-Tech, LA Gear? Ila kuna ndaba zilikuwa zinaitwa Troop....hizi zilikuwa bab kubwa enzi hizo. Mimi nilikuwa nazo pair mbili...nilitesa nazo sana aisee. Nakumbuka nilipata mademu kwa kutumia hizi ndaba. Halafu wakati wa likizo nilikuwaga lazima ninyoe panki...si unajua shuleni mapanki yalikuwa yanakatazwa....basi mimi nilikuwaga nasubiri mwezi wa sita na wa kumi na mbili....

Cheki Troop hiyo...

Troop-Is-Back-In-Town-5.jpg

brings back fond memories as a young boy!
 
Back
Top Bottom