Enzi zetu za utoto..........

Wengi wetu humu wakati tukiwa watoto tumekuwa katika mfumo tofauti kabisa wa maisha tofauti na yalivyo sasa kwa mfano mi nikiwa mtoto karibu kila sikukuu tulikuwa lazima tule pilau haijalishi ni xmas au eid na ikiwezekana na nguo mpya. Cine Clubndio yalikuwa maeneo yetu ya kutembelea na mashindano ya kudance nyimbo kama OPP, Ice Ice baby, Nzawisa na kadhalika.

Chakula favaourite kwa watoto enzi hizo kilikuwa ni wali maharage, mchezo mkubwa ukiwa mpira, kutengeneza magari, kuendesha baiskeli na kwenda kuogelea beach. Nakumbuka pale Cine Club ndipo tulikuwa tunapita kuoga tukitoka kuogelea enzi hizo pakiwa panamalizikia kuwa Tanzania Film Cooperation (TFC) nakumbuka tulikuwa tunaokota ile mikanda ya filamu za zamani inafanana na negative za picha za analojia hivi.

Dah Kombolela na kidali po........

Nini unakikumbuka enzi zako za utoto ambacho kwa watoto wa sasa hakipo?

Wewe kweli Jr! Mambo yote kidongo chekundu enzi ya utoto wangu! Wewe unaongelea cineclub! Ah! Nimejua, mimi nimekulia manzese kilima hewa nawe ni wa oysterbay. Inawezekana cine club ni ya zamani pia
 
nene noya kukangwa na homa
ukumija kung'ang'ala gwike
munh'ya one ombele jagwa
maduma gete lo mababayu
mino za gete lya seka iwa.

Repeat 100000 times
Dah leo umenifurahisha sana we nanihiii........ntafute nikupe zawadi
 
......OPP, Ice Ice baby, Nzawisa hivi ni vitu gani? Unaweza kuelezea kidogo.
 
Wewe kweli Jr! Mambo yote kidongo chekundu enzi ya utoto wangu! Wewe unaongelea cineclub! Ah! Nimejua, mimi nimekulia manzese kilima hewa nawe ni wa oysterbay. Inawezekana cine club ni ya zamani pia
Hahahahahaaa ilikuwa Mikocheni kaka, dah Cine Club nadhani ni ya zamani hii naongelea early 90s nilikuwa ndo naanza anza primary school enzi hizo ila ilikuwa kama club ya kawaida kabisa not the way ilivyo sasa
 
nene noya kukangwa na homa
ukumija kung'ang'ala gwikeo
munh'ya one ombele jagwa
maduma gete lo mababayu
mino za gete lya seka iwa.

Repeat 100000 times

Vavuda ene nafuma kapa henaho! Hamo uyombe mkinyamwezi. Kimba uveve ukuyomba kidama hamo!
 
......OPP, Ice Ice baby, Nzawisa hivi ni vitu gani? Unaweza kuelezea kidogo.


Nimemkamata Preta! Ajue mambo ya mzungu wa 47 kufukuzwa Tanganyika asijue nzawisa? We binti, rudisha shikamoo zangu nilizokupa haraka!
 
Back
Top Bottom