EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,093
Wengi wetu humu wakati tukiwa watoto tumekuwa katika mfumo tofauti kabisa wa maisha tofauti na yalivyo sasa kwa mfano mi nikiwa mtoto karibu kila sikukuu tulikuwa lazima tule pilau haijalishi ni xmas au eid na ikiwezekana na nguo mpya. Cine Clubndio yalikuwa maeneo yetu ya kutembelea na mashindano ya kudance nyimbo kama OPP, Ice Ice baby, Nzawisa na kadhalika.
Chakula favaourite kwa watoto enzi hizo kilikuwa ni wali maharage, mchezo mkubwa ukiwa mpira, kutengeneza magari, kuendesha baiskeli na kwenda kuogelea beach. Nakumbuka pale Cine Club ndipo tulikuwa tunapita kuoga tukitoka kuogelea enzi hizo pakiwa panamalizikia kuwa Tanzania Film Cooperation (TFC) nakumbuka tulikuwa tunaokota ile mikanda ya filamu za zamani inafanana na negative za picha za analojia hivi.
Dah Kombolela na kidali po........
Nini unakikumbuka enzi zako za utoto ambacho kwa watoto wa sasa hakipo?
Chakula favaourite kwa watoto enzi hizo kilikuwa ni wali maharage, mchezo mkubwa ukiwa mpira, kutengeneza magari, kuendesha baiskeli na kwenda kuogelea beach. Nakumbuka pale Cine Club ndipo tulikuwa tunapita kuoga tukitoka kuogelea enzi hizo pakiwa panamalizikia kuwa Tanzania Film Cooperation (TFC) nakumbuka tulikuwa tunaokota ile mikanda ya filamu za zamani inafanana na negative za picha za analojia hivi.
Dah Kombolela na kidali po........
Nini unakikumbuka enzi zako za utoto ambacho kwa watoto wa sasa hakipo?