Elimu ya darasani haina faida zaidi ya kutengeneza vijana tegemezi

Hemedy Jr Junior

JF-Expert Member
Feb 17, 2023
908
1,064
Kuna watu tunawafahamu kabisa hawana hii elimu ila wako vizuri na unaweza shangaa wao ndio waliotusomesha mpaka leo tuko na degree na ma PhD ila wao hata hawakunusa karatasi.

Elimu ya darasani hii imerudisha maenndeleo ya wananchi nyuma kabisa. Mtu anauza shamba eti mwanae asome mwisho wa siku negative anaenda kupata. Hasara tupu

Bora kukosa elimu hii ya shule ukawa na akili maana elimu ya shule ni upigaji mtu kulemeza vijana, vijana wamekuwa wazembe. Shule unafundishwa mambo 40 kwa wakati mmoja.

Serikali inabidi ibadilishe mfumo mzima wa elimu (India mtoto mdogo anajua kupasua chura na kumurudisha kwenye hali yake ya kawaida ila bongo doctor ni mzee ashazeeka. Huku bongo tunasoma tukiwa wazee sana.

Ni nini tatizo?
 
Elimu ifumuliwe iendane na uhalisia wa maisha ya sasa, tatizo ni pesa za wahisani hawataki tujikomboe wataendelea kufadhili kama tutaendelea kufundishwa hii mitaala iliyopitwa na wakati ila mitaala ya kisasa na yenye tija hawaweki hata thumni
 
Elimu ifumuliwe iendane na uhalisia wa maisha ya sasa, tatizo ni pesa za wahisani hawataki tujikomboe wataendelea kufadhili kama tutaendelea kufundishwa hii mataala iliyopitwa na wakati ila mitaala ya kisasa na yenye tija hawaweki hata thumni
Hakika
 
Mbona kuna wenye elimu na mafanikio makubwa kama Dr. Mwigulu Nchemba🐒
 
Lete mfano wa ndugu yako mwenye hii elimu aliyefanikiwa .. ushawai kupata historia ya mwigulu
Wapo wengi tu wanajitegemea na wamefanikiwa.....historia ya Mwigulu hii hapa👇

 
Kuna watu tunawafahamu kabisa hawana hii elimu ila wako vizuri na unaweza shangaa wao ndo waliotusomesha mpaka leo tuko na degree na ma PhD ila wao hata hawakunusa karatasi.

Elimu ya darasani hii imerudisha maenendeleo ya wananchi nyuma kabisa. Mtu anauza shamba eti mwanae asome mwisho wa siku negative anaenda kupata. Hasara tupu

Bora kukosa elimu hii ya shule ukawa na akili maana elimu ya shule ni upigaji mtu kulemeza vijana, vijana wamekuwa wazembe. Shule unafundishwa mambo 40 kwa wakati mmoja.

Serikali inabidi ibadilishe mfumo mzima wa elimu (India mtoto mdogo anajua kupasua chura na kumurudisha kweny3 hali yake ya kawaida ila bongo doctor ni mzee ashazeeka. Uku bongo tunasoma tukiwa wazee sana.

Ni nini tatizo.....
Hemedi utaingia kwenye ignirant list ya watu wengi mnoo. Huwezi jaji ubora wa elimu Kwa kigezo cha ajira. Ya Ajira ni mengine kabisa na yanasababishwa na kitu kingine kabisa sio kinachofundiahwa darasani
 
Hapa nahitaji kufahamu maana halisi ya Elimu. Elimu ni nini? Mimi najua unapopata elimu means unaweza tatua changamoto zinazokabili jamii yako na kuleta maono mapya ndio maana ya elimu. Hata jamii inasema sisi tuna msomi..
 
Hemedi utaingia kwenye ignirant list ya watu wengi mnoo. Huwez jaji ubora wa elimu Kwa kigezo cha ajira. Ya Ajira ni mengine kabisa na yanasababishwa na kitu kingine kabisa sio kinachofundiahwa darasani
Umeelezea au umefafanunua... wasomi kingereza hamjui ila mnapenda kukitumia huo ni ujinga wa kwanza.
 
Wapo wengi tu wanajitegemea na wamefanikiwa.....historia ya Mwigulu hii hapa👇

Nimekuuliza wewe kwenye familia yako msomi nani? Au Mwingulu ndugu yako
 
Back
Top Bottom