1milion inatosha kabisa kuanziajubilant kwa sasa gharama ya kufunga umeme wa kadiri yako ni shilingi ngapi kwa kununua solar
Last edited by a moderator:
1milion inatosha kabisa kuanziajubilant kwa sasa gharama ya kufunga umeme wa kadiri yako ni shilingi ngapi kwa kununua solar
Kontelo Unapozungumzia mfumo wa sola, fikiria vifaa ambavyo ni power sever (inch 32 flat ni chini ya 50w,taa zipo 1w,2w,3w....tofauti ya mwanga ni ndogo mno). Hata hivyo naomba tutambue kuwa jambo la betri ni mtambuka hatuhitaji ukubwa wa betri tu, pia fikiria betri yenye uwezo na sio kujaza madudu majumbani.
MIMI NAITUMIA FLAT 32 48W,TAA 6 @2W NA KING'AMUZI. >pamoja na familia kuangalia mchana, nimeonyesha kombe la dunia mpaka mechi za saa 7 bila kuhofia wateja.
{100ah+120w+ conveter300w} Chini ya M.
Naona bora kufunga change over kuliko kuweka mara 2.Hapa ongeza gharama ya wiring na hii hutegemeana na aina ya wiring.
Solar pekee na Tanesco kwa pamoja maana ya system mbili
Au
Tanesco na Solar lakin lazima ufunge "change over switch"
Weka budget ya 3-5m maana huwezi kutumia wiring ile ile kwa solar na tanesco, kila kimoja kinajitegemea
Hii si kweli. Naongea nikiwa Electrical and Electronics Engineer.
Naona bora kufunga change over kuliko kuweka mara 2.
Kwan nn madhara ya kuweka change over swich..?
Ni panel aina gani na nitaitambuaje kama ni halisi?MFUMO WA SOLA; Una sura mbili ya kwnza ni ya kitaalam, ambayo kwa sasa inawapa watu wengi wakati mgumu (waliofungiwa wengi wanalia, bei kubwa na matokeo hafifu-chukua tahadhari) source:walimu.
Yapili kutokana na uzoefu, hii inasaidia sana, yaani unapata kilichochujwa na unaruka vikwazo au badhi ya changamoto.
Mfano: Kwa wale wanaofikiria kuingia katika mfumo huu nakushauri yafuatayo-betri kavu ni mzuri kuliko ya maji{ah=kavu & N=ya maji}, na inafaa zaidi kuanzia 65ah na kuendelea, upande wa Sola ni kwamba sola inatakiwa izidi betri kwa ukubwa, mfano 65ah=sola 100w, 100ah=150w.+10A charge controller. Tupunguze jazba ili tubadilishane uzoefu,kama hatuko kimasilahi au kibiashara zaidi.
Ni kampuni gani nzuri ya sola ambyo panel yake haisumbui.
Ni panel aina gani na nitaitambuaje kama ni halisi?
Battery za 500Ah zipo ila nyingi ni 2volts, ambapo kupata 12v inabidi uunganishe battery katika series. Kumbuka ukiunga series unaongeza Vlts na Ah zinabaki zile zile za battery 1, na ukifunga parallel unaongeza Ah, V zinabaki zile zile za battery 1 hata kama umeunganisha Batt 10.
Panel zipo za kampuni tofauti.
1. Yingli
2. Suntech
3. Kyocera
4. BP
5. Sanyo
6. Schott
7. Photowatt
8. Sharp
9. Istar
10. Shell
Gharama hutegemeana na matumizi ila kwangu ni kama ifutavyo.
.Panel ya 160watt ...500,000/-
.Sealed battery 500N ..500,000/-
.Phoenix Auto Inveter 12V/350VA..400,000/-
.15A Controller 250,000/-
.Base ya panel 30,000 hili ni chuma (angleline ambalo halishiki kutu) linakatwa then linaungwa kwa umeme japo wengine huunga mbao.
Wireing inategemeana na ukubwa na matumizi yako, mf kwangu nimeweka system mbili tofaut na zinajitegemea Tanesco na Solar, maana yake ni kwamba nimefanya a complete wiring system zinazojitegemea na pia nilijiwekea standards kuwa sitaki extension cables ndani na nje ya nyumba so utakuta ukuta mzima umejaa socket za umeme maana kila kitu kinachukulia ukutani and mind u kuna socket za tanesco na za solar.
Bei ya bulb 5000/- kwa watts yoyote (1,2 au 3) kila moja so itatemeana na idadi
Huu ni mwaka wa tatu sasa na sijajuta na pia nataka niongeze tena walau panel moja na betri yake kwa ajiri ya fridge tu
Kwa mahesabu hayo nimewekeza zaidi ya 3m ila pia si lazima uanze kwa level hiyo hapana, unaweza kuanza kidogo kidogo hasa kwenye wiring lakin panel na battery lazima upate vitu geniune
Kuna kampun ya sunday... nayo vp ina bei chee aana huku
nimesoma coments za wachangiaji wengi naona zinapishana pishana coments nyingi hazimalizii utamu wengi wanabuni na kuvutia kwenye unafuu zaidi wa gharama. kinachokosekana ni utaalamu na hii ni kutokana na mfumo wa elimu katika vyuo vyetu vya ufundi yaani VTC na vya engineering katika nchi yetu ni jambo la kawaida kukuta electrical engineer ana bach or masters hana knowledge yoyote kuhusu solar labda awe amepata exposure ya solar au refresher course ya solar vinginevyo hakuna kwa sababu vyuo vingi havina mtaala wa solar. kuhusu solar iko hivi kwanza yenyewe ni mahususi kwa ajili ya maeneo ambayo kupata source nyingine ya umeme ni vigumu kwa hiyo kwa matumizi ya kawaida kama taa tv na kucharge simu cost sio kubwa ila ukihitaji zaidi kama jiko pasi na mengineyo gharma lazima iwe kubwa coz hiyo ni luxury. na ukitaka kuishi kijijini kama unaishi mjini lazima itakugharimu sana.
Huenda usingizi umempitia ngoja tufute subiraMkuu Mohamed Ngwasu, mbona hujanyoosha hayo maelezo yanayopishana?