Umeeleweka.
Kwenye utamaduni wa kukariri na kulazimisha kukubaliana hapo kuna tabu sana.
One more story and then I am done for the day.
Nilipoanza chuo mwaka wa kwanza nilikuwa na kozi moja ya falsafa, elective.
Professor mzungu conservative anatoka upstate New York. Supporter wa George Bush. Republican. Judge. Mimi liberal, immigrant fresh off the plane from Bongo.
Darasa la introductory level philosophy, Western Philosophy, mainly pre-Socratic philosophy.
Basi nikataka kulianzisha siku ya kwanza kwa nini hawajaweka falsafa za sehemu nyingine. Lakini nikajirudi. Ukiwa mbishi kanuni ya kwanza ni kuusoma mchezo kabla ya kubisha.
Basi kutoka hapo, nikawa nabishana sana na Professor. Kila darasa ni ubishi. Halafu ubishi wa logic, arguments zangu Professor anazifahamu. Sibishi vitu ambavyo sijavisoma. Nabisha kwa kutumia hoja za wasomibwa falsafa ambazo hata Professor anazijua. Kwa hiyo nikibisha kwa point hii, Professor anajua hapo Locke, hapo John Stuart Mill, hapo Nietzche, hapo Aquinas, etc. Kuna wakati nikawa na dominate darasa mpaka nikaona imepita kiasi. Hususan topic za uwepo wa Mungu. Mpaka dada mmoja akaniuliza, vile unavyobisha unaamini kabisa au unafanya uzushi tu? Nikamwambia naamini hivyo.
Nikasema huyu Profesa atakuja kunifelisha. Kwa sababu nabishana naye sana, mtu mwingine anaweza kuona namvunjia heshima.
To cut a long story short, mwisho wa semester, professor aliniandikia email anasema usije kwenye mtihani wa mwisho wa semester. Nikaona tayari, Professor kashanifelisha kwa sababu ya ubishi wangu darasani. Nikamuuliza imekuwaje tena? Akaniambua hili darasa umeshapasi, umelionea sana. Zile arguments zako za darasani ni za graduate school level. Ni arguments za darasa la masters la falsafa. Hili darasa hata hukutakiwa kuwemo umelionea sana. Nakupa A+. Usije kwenye mtihani.
Nikasema mfumo wa elimu wa Marekani ni tofauti sana na Tanzania.
Nina hakika kama ingekuwa vyuo vyetu Profesa angenifelisha kwa kukosa nidhamu.
Wakati wenzetu Profesa anakubishia anaangalia umesoma na unaelewa nini. Akikuona unaweza kutetea arguments zako anakupitisha.
Kwa kweli yule Profesa alinitafuta sana urafiki akawa anataka niwe naenda kwenye mikutano yao ku network. Ila na mimi nikawa nina kazi zangu nyingi nikawa sina muda naye.
Kama unataka habari za kugezeana wote mseme sawa sehemu kama hiyo, hata kama una kipaji chako kiko tofauti, hakiwezi kuonekana.