Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

Akili za Lowassa ni tofauti na za malecela aliyekatwa jina na kuishia kulalamika tu huku akijifananisha na katapila,mkimfyeka El hawezi baki ccm haki yanani atajaribu kutupa karata yake upande wa pili!Anasema yeye ni mtu wa maamuzi magumu!What does he mean?A wiseman never act foolish!Jaribuni muone!
Mkuu,
Yale unadhani wewe/yeye ni maamuzi magumu kwa watu wengine yanaweza yakawa ni maamuzi rahisi sana.

Nimesema Lowassa anaweza kuondoka CCM kama atakuwa amejihakikishia kama CCM haichaguliki tena katika kiti cha Urais wa Tanzania. Kinyume cha hivyo, hawezi kuhama CCM.
 
Vaeni tisheti zenu tu muondoke hapo dodoma.tayari jina la fisadi limeondolewa .hafai hata kidogo.
 
wanafanya nini wote hao 3600 Dodoma hawana kazi za kufanya huko makwao

Hawana kazi ya kufanya na wamelipiwa kila kitu na mafisadi Kwa nini wasiwe Dodoma?nitawashangaa ccm kuchagua MTU kwa shinikizo la fedha.shame on you mafisadi.
 
Lowassa hawezi kupitishwa na kamati mkuu , turudi kwenye Huu Uzi , nitashangaa pia kama lowassa atahama ccm , kwanza hatashinda , upinzani kuchukua hivi nchi labda 2025 na kuendelea , pili hawa wafuasi wake wanaompa kiburi hawatamfuata upinzani , kwanini , kwa sababu wengi ni mafisadi , mafisadi wanataka kupiga hela na kujilinda kwenda upinzani ndio mwisho wao .
Mkuu,
Kwangu mimi sifahamu upinzani watachukua nchi lini lakini ninachofahamu kama ulivyosema, Lowassa hawezi kuhama CCM kama ana amini CCM bado inachagulika katika kiti cha Urais wa Tanzania.

Watu walio nyuma yake hawawezi kumruhusu kuhama CCM na CCM ya sasa haiwezi kumruhusu kuhama CCM kwa amani!
 
3600 duu,hapo inabidi timu eddo wavae tsheti mbilimbili,ili kama ikitokea jina lake likikatwa basi wanatoa ya juu,wanabaki na tisheti nyingine mbadala.
 
Tunachojua ni kwamba ukweli ndiyo huo na sisi vijana wengine yupo Iringa na sehemu nyingine za nchi huu ndiyo uwamuzi wetu vijana. Tupeni chaguo letu la siyo basi tusilaumiane mbele ya safari. Tuonaomba tutendewe haki tukashindwe kwenye kura!
Hata mimi ni kijana na wala simtaki hata kidogo. Aelezee kwanza ilikuwaje huko Richmond. Vinginevyo huna hoja
 
mkuu yote uliyoandika yanaukweli na logic ila hilo la kuwapa redet bil 35.5 bila shaka ume-exaggerate

Pamoja na nguvu kubwa ya mazingaombwe aliyokua nayo ya kucheza na media pamoja na fedha chafu hizi ndo sababu maalum hawezi kupita hata mchujo wa kwanza wa NEC(5 bora).

1. Ana tuhuma nzito za ufisadi wa richmond uliosababisha kujiuzulu na kutikisika kwa serikali 2008.Tuhuma hizi hakuweza kusafishwa mahakamani(walimbeba ) jambo linalopelekea tuhuma kusimama palepale kisheria.

2. Operation VUA GAMBA, target ya hii kauli mbiu ilikua ni lowassa,Mara baada ya kujeruhiwa bungeni 2008 chama chake kiliona ufisadi ni tatizo kikaanzisha operation ambayo ilipanga kumwangamiza kabisa kisiasa ndugu Ngoyayi alikwepaje tumuulize NAPE ,hapa maana yake chama chake chama chake HAKIMTAKI.
kumbuka kauli ambayo aliitoa katibu mkuu pale mwanza wakati anamaliza ziara za cha,a namnukuu "Tunairudisha misingi ya chama cha mapinduzi ,kiwe chama cha wakulima na wafanyakazi kama alama zinavyoonyesha, CCM sio chama cha wafanya biashara tena ,hawa wafanya biashara ndo wanatuletea ESCROW,RICHMOND,EPA ect" ni nani hajui kama manywele ni businesman?nani hajui kama hela anazogawa kama njugu kuna support kubwa ya business influence?

3. Amekiuka sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2011 kifungu Namba 14(1_2)mma kifungu namba 20(1-4) sambamba na kifungu namba 24 cha sheria hiyo ambayo inakataza mgombea yoyote wa nafasi ya urais,ubunge au udiwani .Ikumbukwe hadi sasa Lowassa ametumia zaidi ya billioni 50 kwa ajili ya kuwahonga waandishi wahabari,wenyeviti wa CCM wa mikoa,wabunge,waandesha bodaboda,maaskofu,mashekhe na hivi juzi ametumia zaidi ya shilingi billion 35.5 kuwahonga REDET.

4. Lowassa amezungukwa na wapambe ambao wana criminal records za kifisadi baadhi ni Rostam,Andrew chenge,Nazir Karamagi,Anna Tibaijuka,Kingunge etc.

5. Ugonjwa wake ,mzee ana mgogoro wa Afya si vizuri kuweka details zote hapa lakini hata nyie wenyewe mmeshajionea ameanguka mara kadhaa katika safari tu za kutafuta wazamini kutkana na power ya media manipulation hamkutangaziwa.

6. Alianza kampeni kabla ya wakati ,hamna asiyetambua yeye na wenzake walianza kampeni mapema hadi ikasababishia adhabu ,hata hivyo kipindo cha adhabu alikua bado anaendelea na kampeni hii tafsiri yake ni UTOVU WA NIDHAMU .

7.Visasi hapa nadhani mnanisoma mnakijua akina mwakyembe kiliwapata nini na wengine wakakoswakoswa

8.Makundi -Huyu ndo muasisi wa ccm ya walikua nacho na have nots ,NEC hawawezi wakafanya kosa la ku hype matabaka

9.Kashfa ya tuhuma ya kutaka kuutenganisha uenyekiti wa chama na urais hii siyo ndogo ipo bado kwenye records

Ni hayo tu
 
Mungu tuepushe mbali na huyu fisadi lowassa asije akawa Rais JMT,Mungu tunakuomba sana huyu mwizi asie na aibu,mtoa rushwa mkubwa huyu tuepushie mbali
 
Sema kabisa utagawa kabaang... ubet na watu... uone utafanyiwa nn...!!!!

Lowassa anapita iwe mchana au ucku...!!!

Huu ndio wakati wake...mmanina...!!!
 
kwanini unishangae kwa kutoifahamu ccm vizuri? what the hell is ccm?

umeharibu mada yako kwa kipengele hicho tu. byeee
Mkuu,
Kuharibu mada siyo tatizo, tatizo ni kutokuikarabati mada unayodhani imeharibika!

Kama huifahamu vizuri CCM hata uwezo wako katika kutoa maamuzi ya kisiasa katika sanduku la kura utakuwa umekosa mwelekeo unaofahamika.

Watu wenye fikra pana huwa hawapigi kura kwa kutumia msukumo wa ushabiki bali kwa kutumia sera, Ilani za Vyama na ahadi binafsi za wagombea.

Kama ungefahamu CCM ni chama kikongwe barani Africa kuongoza nchi kwa kipindi kirefu mfululizo nadhani usingepata hata nguvu za kuandika what the hell is CCM!
 
TAARIFA KWA 4U MOVEMENT DODOMA.

Habari, Wana 4u movement mliopo Dodoma na Watanzania wote wenye mapenzi mema na Edward Lowassa tunawaasa kutovaa T-shirt zozote za 4u movement au zenye jina la Edward Lowassa katika kipindi chote cha mikutano ya Chama.

Najua na kutambua hadi jana tarehe 07/07/2015 zaidi ya wana 4u movement 3600+ plus wamewasili Dodoma lakini wingi wetu usiwe sehemu ya kuwa chanzo cha vurugu ya Aina yeyote.

Tuna Taarifa za kuaminika kuna watu wenye mpango wa kutumia T-shirt zetu za 4u movement kufanya vurugu ndani ya Mji wa Dodoma kwa makusudi ili kuiondelea sifa ya utulivu na umakini wa Movement yetu. Yeyote atakae husika kufanya fujo au vurugu zozote kwa Makusudi huku akitumia jina letu tutakuwa msatari wa Mbele kumshughulikia.

Tunawaasa na kuwaomba wana 4umvt na Watanzania wote kuwa watulivu na wavumilivu na kuwapa nafasi Wajumbe wote wa vikao vya Maamuzi kwa kutii na kufuata kanuni za chama kufanya maamuzi kwa Utulivu maana ule wakati mabadiliko uliotabiriwa na Baba wa Taifa kuwa ukifika Basi mabadiliko tutayapata ndani ya CCM na tukikosa tutayapata nje ya ccm lakini ipo nafasi kubwa sana ya kuyapata Mabadiliko haya ndani ya CCM chini ya Balozi wetu wa 4u movement Mh Edward Lowassa.

Ahsanteni

Hemedy Ally
Mratibu Taifa (National Coordinator)
@4u movement
# UTUMISHI
# UWAJIBIKAJI
# UMOJA
# UZALENDO
YAH.TAMKO LA KUPONGEZA KAULI YA MKUU WA MKOA WA MWANZ NDUGU STANSLAUS MAGESA MULONGO.



Ndugu wanahabari na watanzania wote.

Kwanza nitumie fursa hii kuwashukuru kwa kuitikia wito na kukubari kuja kuungana nasi kwa lengo la kuwajuza watanzania kwa kile kinachoendelea katika mkoa wetu Wa mwanza kwa faida na manufaa ya watanzania wote.






Siku ya 6/7/2015, mkuu wetu wa mkoa Wa mwanza alitoa maelekezo kwa makamanda wa polisi kuzuia watu wasio kua na malengo mazuri kwa nchi yetu na taifa letu. Wanao kwenda Dodoma kwa lengo la uvunjifu wa amani,katika kipindi hiki cha mchakato
wa vikao vinavyoendelea vya kuchuja na kupata kiongozi atakae peperusha bendera ya chama cha mapinduzi,Huo ni wajibu wake akiwa ni mwenyekiti Wa kamati ya ulinzi na usalama
wa mkoa, na ndio muwakirishi Wa rais kwa ngazi ya mkoa anawajibu na kila sababu ya kukemea,kuonya,kushauri na kuelekeza mambo yote yanayohusu raia
na Mali zao hivyo sisi wana mwanza na watanzania kwa ujumla hatukuona ubaya Wa aina yeyote kwa kauli ya mkuu wetu wa mkoa.



Cha kusikitish Jana 7/7/2015. Kuona katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari mtu

anae jiita mtemi Sylvester yared. ambae ndio mratibu Wa genge la vijana wahuni wanaojiita 4U movement. Akidhihaki na kupinga tamko la mkuu wetu Wa mkoa wa mwanza. Binafsi nilishitushwa sana


Katika Katiba yetu ya chama cha mapinduzi na kanuni zake tuna jumuiya tatu
1.Jumuiya ya wanawake(UWT)
2.Jumuiya ya wazazi
3.Jumuiya ya vijana (UVCCM)
Ndani ya cham cha mapinduzi hatuna taasisi wala jumuiya inayoitwa 4Umovement.
Swali la kujiuliza jeuri, kiburi na mamlaka ya kuunda chombo kisicho rasmi chenye lengo la kuvuruga,kuhatarisha mustakabari wa chama chetu na Taifa letu kwa maslahi ya mtu binafsi,anaetumia kundi la vijana wasio jitambua kwa gharama yeyote ili aingie ikulu,na huyu si mwingime bali ni ndugu Edward Lowasa.




Ninayaongea haya kwa ushahidi, ninao hapa viongozi wawili kutoka kundi la mabaunsa na machinga,wa mkoa wa mwanza ambao walifatwa na kupewa kazi ya kuandaa na kukusanya vijana wasiojielewa kwa lengo la kwenda Dodoma. Kushinikiza viongozi Wa chama kumchagua mgombea wao, na kundi jingine la vijana na akina mama Wa CCM kusimama njiani kusimamisha misafara ya wajumbe Wa NEC, na mkutano mkuu wa chama Taifa kuwapa shinikizo na vitisho, kwamba lazima warudi na mgombea wao ndugu Edward Lowasa.Hayo yote yanafanywa kwa malipo, Na kila kijana atalipwa tsh 100,000.kwa kila siku ,kwa siku zote atakazo fanya kazi, mpaka kieleweke.






Ndugu wanahabari Mimi kijana mzalendo wa Tanzania ninapata wakati mgumu na Mashaka makubwa pindi ninapo ona mtu ambae hakubaliki katika jamii ya watanzania mwenye madoa na kashfa chungu nzima tena afya yake ikiwa ya kususua analazimisha kwa kutumia gharama kubwa ili afike Ikulu mtu huyu kwa kauli ya hayati baba Wa Taifa,namnukuu, Tumuogope kama ukoma hafai.mwisho wa kunukuu.





Nimalizie kwa kuwashukuru na kuwapongeza viongozi wetu wakuu wa chama na serikali kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kujenga na kuimarisha chama na serikali kwa kutatua na kusimamia maslah ya watanzania, Mwisho kwa nafasi ya kipekee niwashukuru wanahabari wote mlio hudhuria na watanzania wote mnao nisikiliza na kunitazama.Mungu kibariki chama chetu CCM, Mungu ibariki Tanzania.






Imeandaliwa na
Hussein.A.kimu
Mw/kiti UVCCM(W)nyamagana mwanza.
 
Inamaana kujaa huko kunaonesha wengine sio bora ila lowassa pekee? ?. Vipi kingu anawekwa position gani maana nasikia kwa lowassa mmeshajipa mpaka vyeo
 
Mtaji mkubwa wa El ni anawapata na kuwatumia wajinga na wapumbavu kama hawa wakina .. budget
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom