Wanajukwaa!!!
Macho na masikio ya watanzania walio wengi yameelekezwa Dodoma ambapo CCM, Chama kikubwa na kikongwe kabisa hapa nchini na Afrika kwa ujumla kipo katika mchakato wa kumpata mtu wa kupeperusha bendera katika kumrithi Mhe Jakaya Kikwete.
Chambuzi nyingi za siasa kuelekea Magogoni 2015 zimekuwa zikiangaza nani atapitishwa na Chama, uimara wake na udhaifu wake.
Wapo wanaochambua kwa mapenzi, chuki, kutokujua na wengine kwa utaalamu wa hali ya juu.
Mimi kama mchambuzi wa siasa hesabu zangu zinanielekeza kuwa Mhe Edward Lowassa ana nafasi kubwa ya kuibuka mshindi akiwa ndani ya CCM na hata akiwa nje ya CCM.
Matokeo ya uchambuzi wangu hadi kufikia hitimisho kuwa Lowassa ana nafasi kubwa ni baada ya tafakuri ya kina ya mwenendo wa kisiasa tangu mwaka 2005 hadi sasa.
Mwaka 2005, Mhe Kikwete wa CCM alipata zaidi ya 80% ya kura zote na hivyo kuonesha namna gani wananchi walivyokuwa na kiu na imani kubwa kwa Kikwete binafsi na hata CCM kwa ujumla.
Miaka mitano (05) baadaye Mhe Kikwete aliporomoka kwa karibu 20% na hivyo kuambulia kura 5,276,827 sasa na 61.17% ya kura zote. Wapinzani kwa upande wao tunaona Chadema walipata kura 2,271,941; CUF kura 695,667 na NCCR kura 26,388 (hawa ndio UKAWA)
Sasa, tuangalie hesabu za Sayansi ya Siasa vipi zinambeba Lowassa ikiwa atakatwa jina lake na kuamua kuhamia katika mwamvuli wa UKAWA na wenye UKAWA wakampokea??
Kwanza, wakati wakiwa katika zoezi la kutafuta wadhamini Lowassa alijipatia jumla ya wadhamini 874,297 ambao tunaamini kuwa wapo tayari kumpigia kura popote atakapokuwa. Na iwapo kila mdhamini atashawishi watu watatu (03) ni kwamba Lowassa atakuwa na mtaji wa watu 2,532,891.
Sasa (wadhamini x 3)+(mtaji wa UKAWA 2010) =Kura kibindoni
2,532,297 + 2,993,996 = 5,526,293
Kwa hiyo, kama ataingia na mtaji huo katika uchaguzi mkuu atakuwa amebakiza kazi ndogo tu ya kushawishi undecided group na kwa kuzingatia kundi kubwa la vijana ambao hawakuweza kupiga kura 2010 kutokana na kuwa na umri chini ya miaka 18, ambao hakuna ubishi kuwa wengi ni wafuasi wa vyama vya upinzani na hivyo watampa kura mgombea wa Upinzani, ni dhahiri kuwa Lowassa ana nafasi kubwa ya kushinda ikiwa atagombea kupitia CCM au atapitia Muungano wa UKAWA.
Hizo ni hesabu zangu nikiwa mchambuzi huru.
Nimeweka kura za UKAWA, iwapo jina lake litakatwa na CCM na iwapo ataamua kukimbilia katika mwavuli wa UKAWAHongera kwa kufanya utafiti wazi wa kisayansi. Kuna sehemu inahitaji kuniwekea sawa. Mantiki ya kujumlisha na kura za ukawa
awe rais wa kuzimu labda zitambeba,
Nimeuona uchambuzi wako. Nauheshimu sanaHesabu zingine hizi hapa,
Lowassa naurais
Ndani ya CCMkuna udicteta ndani ya democrasi ya kwao,kuna chombo kinaitwa kamati kuu(CC)chombo hiki kina maamuzi mkubwa ambayo hayaruhusiwi kukatiwa rufaamahakamani,Lowassa alilaaniwa na Nyerere kila mtu anajua kwamba hafai kuwa Raiswa Tanzania kwa ajili alijilimpikizia mali,Mangula aliitwa kwenye chama tokakijijini kwake Mtwango alikokuwa analima viazi akawa makamo wa mwenyekiti nakuwa mjumbe wa CC kwa mjibu wa wadhifa wake, aliitwa aingie kwenye chombo hichokwa kazi moja tu, KULIPIGA LULA JINA LA LOWASSA PINDI WAKIANZA KUWAJADILIWAGOMBEA WATAOCHUKUA FORM KWA TIKITI YA CCM, hiyo ni moja.
Pili raismwenyewe majuzi alisema atapenda amwachie urais kijana,siyo mzee kama yeye
Kwa mantikihiyo Lowassa hawezi kuwa rais wa inchi hii
Mwisho Lowassaanautaka urais kwa udi na uvumba hivi anataka afanye nao nini?
Hizi Hesabu za wapi tena?Wanajukwaa!!!
Macho na masikio ya watanzania walio wengi yameelekezwa Dodoma ambapo CCM, Chama kikubwa na kikongwe kabisa hapa nchini na Afrika kwa ujumla kipo katika mchakato wa kumpata mtu wa kupeperusha bendera katika kumrithi Mhe Jakaya Kikwete.
Chambuzi nyingi za siasa kuelekea Magogoni 2015 zimekuwa zikiangaza nani atapitishwa na Chama, uimara wake na udhaifu wake.
Wapo wanaochambua kwa mapenzi, chuki, kutokujua na wengine kwa utaalamu wa hali ya juu.
Mimi kama mchambuzi wa siasa hesabu zangu zinanielekeza kuwa Mhe Edward Lowassa ana nafasi kubwa ya kuibuka mshindi akiwa ndani ya CCM na hata akiwa nje ya CCM.
Matokeo ya uchambuzi wangu hadi kufikia hitimisho kuwa Lowassa ana nafasi kubwa ni baada ya tafakuri ya kina ya mwenendo wa kisiasa tangu mwaka 2005 hadi sasa.
Mwaka 2005, Mhe Kikwete wa CCM alipata zaidi ya 80% ya kura zote na hivyo kuonesha namna gani wananchi walivyokuwa na kiu na imani kubwa kwa Kikwete binafsi na hata CCM kwa ujumla.
Miaka mitano (05) baadaye Mhe Kikwete aliporomoka kwa karibu 20% na hivyo kuambulia kura 5,276,827 sasa na 61.17% ya kura zote. Wapinzani kwa upande wao tunaona Chadema walipata kura 2,271,941; CUF kura 695,667 na NCCR kura 26,388 (hawa ndio UKAWA)
Sasa, tuangalie hesabu za Sayansi ya Siasa vipi zinambeba Lowassa ikiwa atakatwa jina lake na kuamua kuhamia katika mwamvuli wa UKAWA na wenye UKAWA wakampokea??
Kwanza, wakati wakiwa katika zoezi la kutafuta wadhamini Lowassa alijipatia jumla ya wadhamini 874,297 ambao tunaamini kuwa wapo tayari kumpigia kura popote atakapokuwa. Na iwapo kila mdhamini atashawishi watu watatu (03) ni kwamba Lowassa atakuwa na mtaji wa watu 2,532,891.
Sasa (wadhamini x 3)+(mtaji wa UKAWA 2010) =Kura kibindoni
2,532,297 + 2,993,996 = 5,526,293
Kwa hiyo, kama ataingia na mtaji huo katika uchaguzi mkuu atakuwa amebakiza kazi ndogo tu ya kushawishi undecided group na kwa kuzingatia kundi kubwa la vijana ambao hawakuweza kupiga kura 2010 kutokana na kuwa na umri chini ya miaka 18, ambao hakuna ubishi kuwa wengi ni wafuasi wa vyama vya upinzani na hivyo watampa kura mgombea wa Upinzani, ni dhahiri kuwa Lowassa ana nafasi kubwa ya kushinda ikiwa atagombea kupitia CCM au atapitia Muungano wa UKAWA.
Hizo ni hesabu zangu nikiwa mchambuzi huru.
EL alikuwa mwanajeshi piaAngalia hesabu hizi
Kigezo
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Jaji Agustino Ramadhani
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Edward Ngoyayi Lowassa
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Umri
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Miaka 70
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] 62
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Elimu
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Ni ya juu ngazi ya shahada ya sheria
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Elimu ya juu ngazi ya shahada
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Uzoefu wa kazi
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Amebobea kwenye mhimili wa dola upande wa mahakama
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Amebobea kwenye mhimili wa dola upande wa serikali na bunge
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Uadirifu
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Hakuna mashaka yoyote kuhusu uadirifu wake
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Kuna mashaka mengi sana kuhusu suala la uadirifu
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Kazi alizofanya
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Jaji, mwanajeshi, mchungaji
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Kichunga ng`ombe, katibu wa chama, mkurugenzi IACC, mbunge, waziri, waziri mkuu.
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Historia kazini
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Amefanya kazi serikalini hadi amestaafu kwa mjibu wa sheria
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Alijihudhuru uwaziri mkuu kwa tuhuma ya kuipa tenda ya kufua umeme na kuiuzia Tanesco kampuni ya richmond ambayo haikuwa na sifa
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Kugombea urais
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Hajawahi kugombea labda hii itakuwa ni mala ya kwanza
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Aligombea mwaka 1995 jina lilikatwa kwa kukosa sifa
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Hali ya kugombea urais iliyopo hivi sasa
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Ameombwa agombee tena ameombwa sana
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Alianza mda mrefu kuonyesha nia ya kugombea urais, kuna mashaka mengi anahonga, ananunua makundi ili yamuunge mkono
[/TD]
[TD="width: 186, bgcolor: transparent"] Afya
[/TD]
[TD="width: 327, bgcolor: transparent"] Afya yake ni imala sana
[/TD]
[TD="width: 257, bgcolor: transparent"] Afya ni mgogoro mala nyingi huendaUgermani kupima afya, mala kadhaa huwa na kitetemeshi hasa asubuhi, hana uwezo wa kuhimili mikikimikiki kwa mda mrefu
[/TD]
Hizi Hesabu za wapi tena?
(1.)Naona umechukulia hakuna mabadiriko ya wapiga kura(hakuna vifo hakuna wapiga kura wapya hakuna ambao hawatapiga kura kwa sababu moja au nyingine)
(2.)Kwa nn umejumlisha idadi ya kura za upinzani ina maana upinzani una msupport jamaa?
ILA HONGERENI KWA MATUMAINI.