Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

watu wajinga kweli. Wagombea wako 41, na wanataka watano, sasa hao vijana nini kinawasukuma kuwa lazima awe tano bora? ina maana wengine hawahitajiki kuwa hapo zaidi ya yeye? Akili za viroba bhana. But poa tu, sisi tunapeta ngoja muumizane
 
Nimekuelewa...kwamba ni analzimisha kuwe na deal...yaani aendelee kula mema hata kama amekatwa na kukubali kuisupport ccm.it is a wise but not intellectual game!
 
mkuu vipi nimeona uzi wa mtu wako kuchafuliwa ni kweli au majungu?

Ni majungu tu yale mkuu, timu fisadi wanaangaika kumchafua. Ujue anapingwa na timu fisadi lakini pia anapingwa na ukawa, wanajua akisimama hawana chao, ukawa wanataka asimame fisadi ili wamshambulie vizuri kwenye kampeni au asimame mtu mwingine dhaifu asiyejulikana kwa wananchi kama vile jaji ramadhani
 
Akili za Lowassa ni tofauti na za malecela aliyekatwa jina na kuishia kulalamika tu huku akijifananisha na katapila,mkimfyeka El hawezi baki ccm haki yanani atajaribu kutupa karata yake upande wa pili!Anasema yeye ni mtu wa maamuzi magumu!What does he mean?A wiseman never act foolish!Jaribuni muone!
 
Lowassa hawezi kupitishwa na kamati mkuu , turudi kwenye Huu Uzi , nitashangaa pia kama lowassa atahama ccm , kwanza hatashinda , upinzani kuchukua hivi nchi labda 2025 na kuendelea , pili hawa wafuasi wake wanaompa kiburi hawatamfuata upinzani , kwanini , kwa sababu wengi ni mafisadi , mafisadi wanataka kupiga hela na kujilinda kwenda upinzani ndio mwisho wao .
 
Lowassa, Ngereja, Muhongo wote wana madoa ya ufisadi. Walijiuzuru nafasi zao za uwaziri. Kwa nini basi umsakame Lowassa tu.
 
lala huna jipya
Mkuu,
Wewe ambaye unataka mimi nilale kwa kutokuwa na jipya, la kwako jipya ni lipi?.

Nani alikuambia wale wasio na jipya lazima walale?

Kwanza kama ungekuwa na jipya lazima ungefahamu Jamiiforums ni global ambapo wachangiaji na wasomaji wanatoka pande zote nne za dunia.

Pande moja ya dunia wakienda kulala, pande nyingine ndiyo wanaamuka halafu lazima uelewe kuna wengine wanalala mchana na wanaamka usiku, and vice versa.

Jikite kwenye hoja na kama unadhani hakuna hoja, soma na uende zako kwenye thread zenye hoja!
 
Na sisi UKAWA hatumtaki.mkimkata mpelekeni akachunge n'gombe zake.
Mkuu,
Kwa CCM ya sasa, anything is possible!

Anaweza asikatwe na akateuliwa na kupelekwa mpaka kwenye Mkutano Mkuu na hata kufikia kuteuliwa kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM.

Ninachofahamu kwa mazingira ya kisiasa ya watu wa timu wanaounda timu yake, hawawezi kumruhusu kuhama CCM na kwenda kupambana kwenye uwanja ambao hawana uhakika kama atashinda.
 
Back
Top Bottom