Kwa mtazamo wangu!.
Watanzania inabidi tubadilike, tuache kulalamika lalamika, tuache uvivu, tuchape kazi kwa pamoja tujenge nchi yetu, tuige mifano mizuri ya Malaysia, China, Phillipines, korea, Singapore nk. nchi ambazo miaka ya 1960's tulikuwa karibu sawa katika hatua za kimaendeleo, tujifunze kwa wenzetu hawa.
Wananchi wamepata maono ya mtu anayewafaa katika mapambano dhidi ya majanga makubwa ya kitaifa, Maradhi, Umasikini, Ujinga na Uongozi bora. Mh. Lowasa ni kiongozi bora, na hayo yalijidhihirisha wazi pindi alipokuwa waziri mkuu (2005). Kwani aliweza kupambana na viongozi wavivu katika idara mbalimbali za serikali, tuliona uwajibishwaji wa wazi wazi kwa viongozi wasio kuwa na uzalendo wa dhati katika kusimamia rasilimali na miradi mbali mbali ya kimaendeleo kwa jamii. Pia kiongozi huyu alikuwa mstari wa mbele katika kuipa ELIMU kipaumbele, maana pasipo ELIMU BORA maendeleo katika jamii yeyote, huwa duni sana.Maana Elimu Bora huleta maarifa, na Maarifa ndiyo humkomboa mwanadamu aweze kupambana na changamoto za kimazingira kufikia hali bora ya kimaisha.Mh. Lowasa, alisimamia kikamilifu ujenzi wa shule za kata, pia chuo kikuu cha Dodoma nk. Nchi yetu inahitaji kiongozi mwenye Uthubutu wa kufanya maamuzi magumu, ya kimaendeleo katika muda mfupi. Huo ni mtazamo wangu binafsi.