Edward Lowassa hukukidhi kiu ya wanawake!

Edward Lowassa hukukidhi kiu ya wanawake!

mimi sijaelewa alichoongea zaidi ya kuomba kura yani akina dada mmepoteza muda kwa ajili ya huo ujinga. Eti mgombea wa urais yeye hana cha kusema zaidi ya kumuonesha mahaba tu. Wakati hapo kulikuwa na madada poa, walemavu wa ngozi, mama ntilie, baamedi, nk.

Lakini sijasikia jambo la msingi ambalo ameongea kuhusu hayo makundizaidi ya kuomba mmtafutie kura. Akina mama wa dar es salaam jitambueni na si kufuata mkumbo.

nyie wadada wa dar mnaenda kufanya nini? Atawaeleza nini shahada yenyewe ya maigizo aliyonayo lowasa, ni aibu kama mumeenda shule,
nyie msubilini tu kwenye maingizo ya kupanda daladala ndo mtafaidi alichonacho

 
Shemeji yangu alikuwa amehudhuria mkutano wa Lowassa. Amesema kwamba awali walitangaziwa Lowassa ndie mgeni rasmi na atakuwepo mama Regina Lowassa. Lakini wameshangaa kukuta mgeni na msemaji mkuu ni mke wa Lowassa

Amesema ndio maana wanawake wengi walikuwa wanapiga story zao wakati bi. Regina alipokuwa akiongea.


..
 
ha ha ha haaaa naona mnakata tamaa mapema bado hajakimbia mdahalo, kwan ameomba urais si anajua n kaz ya kisiasa au alijua ukatibu mkuu kiongoz?

Hivi umemsikia magufuli akiongea??Je ile si ni hotuba ya JK ya mwaka 2010.Unajua badala ya kumjadili Lowassa au Magufuli tungejadili TanzNia kumetokea nini??Kwanini watnzania pamoja na maovu yake bado wanamtaka huyo muovu!Hivi tumeweza kujua ni kwanini??Ni mapenzi tu kw Lowassa??

Tumejiuliza serikali yetu imeshughulikiaje maswala muhimu ya Taifa,je tuliyekuwa naye ametufikisha wapi??Ametumia kiasi gani kwa kwenda nje kila leo na faida yake kwa taifa ni kweli value for money hizo safafri zote??Tumeshajiuliza huyu aliyeanza kunadi kuongeza wawekezaji na kuwapa unafuu wa kuwekeza je haturudi kjle tusikokutaka.

Pole huwanzipendi kumjadili mtu napenda tujadili hoja.Kwanini watanzaniantumefika tulipofika.

Rafiki Chuki ya marafiki wawili inaisambaratisha Taifa kama hujui fungua macho yako uone.
 
Wewe utakuwa ni mvivu wa kusoma. Pitia tena MDG's, Vienna Declaration, Human Rights etc na campaign ya 50% by 50%.

Wakati tunahangaika na mabadiliko ya katiba; kati ya maeneo wanawake tulilalamikia ni Haki ya kumiliki Ardhi kwa mwanamke, mirathi na kumiliki mali nk

Hayo kwa uchache wake yana portray ukombozi wa mwanamke.

Queen Esther

Kwa nini unadhani wanawake wanahitaji kukombolewa sasa mkuu...?

Miaka yote ya tawala zilizopita kipi kilichoshindikana kama kweli kuna ukombozi wa mwanamke?
 
Hata Mbowe hakuwa na raha kabisa.....kiufupi inaonesha anajutia moyoni kumtosa Dr Slaa.
 
hotuba ya katibu mkuu wa bawacha ilikuwa inataja ndugu mgeni rasmi. Mgeni rasmi alikuwa ni nani? Kwanza wakati wa hotuba ya katibu mkuu lowasa alikuwa hajaingia ukumbini.ameingia baada ya hotuba ya katibu mkuu. Hii ina maana kuwa regina ndiye alikuwa mgeni rasmi na sio lowasa.

mkuu hakuna shida na bado midahalo watamkumbua slaa,na hii dhabi ya kumsaliti slaa kwa kazi aliyoifanya inawatafuna mwaka huu,
 
Hayo ni MAHABA mpendwa.

Queen Esther

Hotuba ya katibu mkuu wa BAWACHA ilikuwa inataja ndugu mgeni rasmi. Mgeni rasmi alikuwa ni nani? Kwanza wakati wa hotuba ya katibu mkuu Lowasa alikuwa hajaingia ukumbini.Ameingia baada ya hotuba ya katibu mkuu. Hii ina maana kuwa Regina ndiye alikuwa mgeni rasmi na sio Lowasa.
 
Jaman mwanzo kabisa MC alisema mama lowasa ataongea kwaniaba ya lowasa hapo hata lowasa alikuwa hajaingia ukumbin kwa hyo hotuba ya mzee ni ile iliyowakilishwa na mama Regina coz ulikuwa mkutano wa wanawake kiprotocal
 
Hata Mbowe hakuwa na raha kabisa.....kiufupi inaonesha anajutia moyoni kumtosa Dr Slaa.
Ukweli ni kuwa lowasa jukwaani ni zero. Sijui kama ndivyo alivyo ama ni madhara yaliyosababishwa na gonjwa lake, lakini bila shaka kampeni zikianza tutapata fursa ya kumfahamu vyema.
 
Lowassa pumba kabisa, cjategemea alichokifanya. Nilitegemea kwel atakuja na hizo hoja za ukomboz lkn kafanya mambo ya kitoto kabisa, theme na alichokifanya ni upuuzi mtupu.

Naona unatuonyesha jinsi ulivyo na akiri za ngiri
 
hata mbowe hakuwa na raha kabisa.....kiufupi inaonesha anajutia moyoni kumtosa dr slaa.

dhambi ya usaliti itamtafuna alimsaliti slaa akajiona ni bingwa,namkubusha usaliti wa zitto,
 
Lowassa sio mwongeaji,hata anapokua anaomba kura monduli,ndivyo alivyo.

hatutaki waongeaji sana ila inshu ni kwamba hata kicho kidogo anachoongea muheshimiwa huwa si mikakati bali kurudirudia ahadi, inatakiwa hata akiongea kidogo ila aseme MIKAKATI kwa mfano angeweza kusema kupanua benki ya wanawake,kupunguza interest za bank kwa wamama wajane, kutoa ruzuku kwa saccos bora za akina mama, kuunda mahakama maalum ya jinsia..hii ni mifano ya mikakati si kuimba imba na kutoa ahadi zile zile
 
kila mtu na maumbile yake.kuna waongeaji wazuri na kuna wengine si waongeaji.ni hulka ya.watu kuwa.tofauti.lowassa aonekanavyo si muongeaji sana.sijawahi msikia akiongea kama mwanasiasa hata alivhokuwa ccm so siwezi kumuhukumu kwa maumbile yake.[/quote queen esther
naona ume_like hii comment!! Kutokana na lawama zako juu ya enl hukupaswa ku_like hii.

kama umeenda shule inawezekana ukatenda bila kujua unatenda nini?
 
Heshima kwenu wana JF.

Nimefatilia kwa karibu sana sana hotuba ya Mhe. Mgombea u Rais kupitia UKAWA aliyoitoa hapa LAPF kwenye kongamano la wanawake BAWACHA na kubaini jambo moja kubwa sana.

Kauli mbiu ya kongamano ni "LOWASA NA HATMA ZA CHANGAMOTO ZA WANAWAKE TANZANIA"

Nimesikitika kuwa nilitegemea kwenye hotuba Yake ataweza kuelezea mikakati ya ukombozi huo wa mwanamke. Nasikitika kuwa sikuona mahali popote akiongelea changamoto hizo na jinsi ya kuzitatua.

Ameishia kuimba Wimbo wa Mhe. Magufuli "Alinselema Hadija, mchaka mchaka chinja" na kuzungumza mambo ya MAHABA!!!!!!!!

Nasikitika kusema mimi kama mwanamke nimeondoka na kiu yanguuuu!!!!!!!!!! Ngoja nimsubiri mzee original wa Alinselema. I hope atatuondolea kiu hii!!!!!! Tunataka kuona SERA za ukweli za kumkomboa mwanamke, sio MAIGIZO.

Naomba kuwasilisha.

Queen Esther

Huna hadhi ya kuitwa queen subiri uitwe kijivika vilemba vya ukoka kwetu cc ukawa no au subiri akupendae au akitokea akuite hivyo ila sizanii kama utakuwa na hadhii hiyo ila subiri upepo mbaya upite waweza kujitambua karibu ukawa karibu jangwani njoo uone garika hata hiyo kiu yako ya wanawake na vipaumbele utavipata chadema oyeeeee bawacha oyeeeeee....ushindi unakuja. que le votre nou.
 
Nimepoteza muda wangu kufatilia kwa makini Mkutano wa Edward Lowassa na wanawake wa DSM kutoka Ukumbi wa Millenium, ili nisikie Mhe Lowassa amewaandalia nini Wake na Mademu zetu.
Ila nimeshangazwa na hutuba yake, ambayo haikubabadua chochote cha kuwabadilishia awa viumbe!
Aisee UKAWA jipangeni, mgombea wenu hawezi kumiliki jukwaa, kusema ukweli!!

Kumiliki Jukwaa kwani umeambiwa Bongo flava ile mtaweweseka sana safari hii hamna mpya..
 
Watu mmezoea porojo za uongo za wanasiasa wa chama dola mpaka mkiambiwa kweli hamuamini. Mimi sipigii kura mtu anayekariri ilani na kuongea utadhani kawekewa redio mdomoni.
 
Dr Slaa asingerudia rudia maneno vile na kutoa hotuba dhaifu vile.
 
Back
Top Bottom