Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,580
- 23,915
Queen Esther, kwanza pole sana. Pili vuta subira, kiu yako ya matumaini karibu itatulizwa. Tatu nianze kwa kukupongeza kwamba pamoja na umeme kukatwa bado uliweza kufuatilia mkutano ulioitishwa na Baraza la Wanawake Chadema. Tukubali tusikubali UKAWA, Chadema na Lowassa ndio habari ya mjini na anayejaribu kuzima sauti ya mabadiliko asije akashangaa kusikia hata mawe yakinguruma.Heshima kwenu wana JF.
Nimefatilia kwa karibu sana sana hotuba ya Mhe. Mgombea u Rais kupitia UKAWA aliyoitoa hapa LAPF kwenye kongamano la wanawake BAWACHA na kubaini jambo moja kubwa sana.
Kauli mbiu ya kongamano ni "LOWASA NA HATMA ZA CHANGAMOTO ZA WANAWAKE TANZANIA"
Nimesikitika kuwa nilitegemea kwenye hotuba Yake ataweza kuelezea mikakati ya ukombozi huo wa mwanamke. Nasikitika kuwa sikuona mahali popote akiongelea changamoto hizo na jinsi ya kuzitatua.
Ameishia kuimba Wimbo wa Mhe. Magufuli "Alinselema Hadija, mchaka mchaka chinja" na kuzungumza mambo ya MAHABA!!!!!!!!
Nasikitika kusema mimi kama mwanamke nimeondoka na kiu yanguuuu!!!!!!!!!! Ngoja nimsubiri mzee original wa Alinselema. I hope atatuondolea kiu hii!!!!!! Tunataka kuona SERA za ukweli za kumkomboa mwanamke, sio MAIGIZO.
Naomba kuwasilisha.
Queen Esther
Lowassa hakualikwa kutoa hotuba, hapana, hiyo shughuli bado...huo ulikuwa ni muendelezo tu katika ratiba ya kukutana na kuwasikiliza wananchi. UKAWA, kama huna habari, hawajazindua hata hiyo kampeni yao, kazi hiyo itafanyika Uwanja wa Jangwani Dar es Salaam siku ya Jumamosi tarehe 29 mwezi huu na kwa sasa bado tu saa 30. Hakikisha unawahi uwanjani na eneo maalum kwako limetengwa tayari.
Kwa sasa Lowassa hakutani na vikundi mbalimbali katika jamii kuwatatulia matatizo yao, hapana, hilo wakati wake bado; anakutana nao kusikiliza wanavyonyanyasika kila siku chini ya utawala uliochoka na kupoteza dira. Anawakumbusha kwamba hatua ya kwanza ya kuondokana na kero za miaka 50, ni kufanya mabadiliko...mabadiliko ambayo hayawezi kuletwa na chama kile kile kilicho chanzo cha kero hizo.
Akiendelea anawaomba wampe fursa ya kuwatumikia kwa kuyaongoza, kuyasimamia na kufanikisha hayo mabadiliko na kazi hiyo hawezi kuifanya mpaka hapo tarehe 25 Oktoba 2015 atakapopewa idhini kwa njia ya kura. Kama sehemu ya jamii, wanawake wanayo turufu kubwa katika mustakabali wa taifa hili na asante sana kwa kuacha shughuli zako na kukaa karibu na redio uweze kuwa sehemu ya matumaini.