Madela Wa- Madilu
JF-Expert Member
- Mar 24, 2007
- 3,063
- 743
1. Yaani mimi na mara ya kwanza kuona Mtanzania anakosa uzalendo na kusifu US au UK-a developed country kuliko home for whatever reasons!
Mkiona vinaelea basi vimeundwa!
Karibuni sana nyumbani ndugu zangu..bado ni nyumbani kwenu tu ni sehemu ya historia
yetu!
Karibuni Supu tam ya Kuku wa Kienyeji, Kongoro safi na mengine mengi tu mazuri tele!
2. Tz imebadilika sana na opportunities kibao tu! Wako wengi wameishi nje mda mrefu na kurudi Bongo na kuwa challenged na makubwa peers wao walioyafanya kwa mda mfupi bila hata kuiba!
3. Maendeleo ni popote tu duniani..sema uskae ukadharua nyumbani na wazee na mila
zetu! Wazee husema "Mpanda ngazi hushuka"!
Huku tuliko, yaani UESIEI, sema unataka nini unapata.
Hii nchi wenyenayo haswa ni Wahindi wekundu sisi wote ni wazamiaji.
Kuishi Tanzania au kuishi hapa ni sawa tu.
Kukosa uzalendo ni kuwasahau walionilea na kunilipia ada.
Lakinis kuishi Majuu si kuiponda nchi.
Mimi na mwizi wa fedha za miradi ya serikali aishie Tanzania nani mzalendo?
Mtu ajengae KUTA kwa fedha za kujengea DARAJA na mimi Mtz mbeba mabox hapa Marekani nani ni mzalendo?
Ukiwa huku majuu unajiju pia ukirudi hapo Tz unajiju, wapi zaidi?
Kam kuna mtu anataka turudi Tanzania ili tukajenge nchi mwulize vipi Bajeti ya TAnzania inategemea kodi za watu wa nchi nyingine kuliko wale waishio Tanzania??
Kam wako wanaoisadia Tanzania bila kukanyaga ardhi yake, ni kwa nini sisi tushindwe kuisadia nchi tuliyo zaliwa na kukulia hali tukiishi nje?
Aisifuye mvua imemnyea, asiye isifu je??