BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Nyumbani ni nyumbani kweli, lakini maisha siyo lazima uishi nyumbani. Dunia ya leo ya utandawazi nyumbani panaweza kuwa kokote pale ambapo maisha yanakuendea vizuri. Tusilemae Watanzania kwamba kwa kuwa sisi ni Watanzania basi ni lazima tuishi Tanzania. Uchumi wetu ni mdogo sana na viongozi ni mafisadi hawafanyi lolote la kuinua uchumi wa Tanzania ili uweze kucreate kazi nyingi. Kama wewe ni msomi na unaweza kupata ajira popote pale duniani inayolipa mshahara hata mara 10 au zaidi ya ule ambao ungepata Tanzania, kwa nini ung'ang;anie kuishi Tanzania? Kwa sababu tu "nyumbani ni nyumbani"?
Kuna Watanzania wengi wanapata mishahara ya $100,000 kwa mwaka au hata zaidi, sasa Watanzania kama hawa tutasema wanasua sua na inabidi warudi nyumbani kwa kuwa 'nyumbani ni nyumbani'? Mwajiri gani Tanzania anaweza kuwapa Watanzania kama hawa mishahara hata nusu ya huo, jibu....HAKUNA. Ndiyo maana nikasema aliwahoji Watanzani wangapi, lini na wapi ili kufikia tamati ya hayo aliyoandika? vinginevyo ni hadithi tu ambayo haina ushahidi wowote wa kusupport kilichoandikwa
Watanzania wengi waliosoma wanafanya vizuri, msikutane na Watanzania wachache ambao elimu yao ni ya kubabatiza na kuwaona wanasuasua mkadhani Watanzania walio wengi wako katika hali kama hiyo kimaisha
Kuna Watanzania wengi wanapata mishahara ya $100,000 kwa mwaka au hata zaidi, sasa Watanzania kama hawa tutasema wanasua sua na inabidi warudi nyumbani kwa kuwa 'nyumbani ni nyumbani'? Mwajiri gani Tanzania anaweza kuwapa Watanzania kama hawa mishahara hata nusu ya huo, jibu....HAKUNA. Ndiyo maana nikasema aliwahoji Watanzani wangapi, lini na wapi ili kufikia tamati ya hayo aliyoandika? vinginevyo ni hadithi tu ambayo haina ushahidi wowote wa kusupport kilichoandikwa
Watanzania wengi waliosoma wanafanya vizuri, msikutane na Watanzania wachache ambao elimu yao ni ya kubabatiza na kuwaona wanasuasua mkadhani Watanzania walio wengi wako katika hali kama hiyo kimaisha