Alichosema Dr Sezibera ni kwamba:
Tukianza na suala la liberalization of current account - makubaliano ni kwamba barriers & restrictions zote on the movement, sale, investment & payments of capital inatakiwa viondolewe; Vile vile kuna makubaliano to remove all discrimination based on the nationality or on the place of residence of the persons or on the place where the capital is invested. Ni kweli kwamba wenzetu Kenya, Uganda na Rwanda wameshafungulia haya, imebakia Tanzania na Burundi; Lakini pamoja na hayo, makubaliano ilikuwa kwamba Tanzania na Burundi wawe wametekeleza haya katika kipindi cha 2010 2015, kwahiyo tusubri tuone nini kitajiri ndani ya miaka miwili ijayo;
Tukija kwenye suala la work permit fees makubaliano ni kwamba workers kutoka any partner state waruhusiwe kutafuta kazi katika nchi yoyote mwanachama wa EAC; Free movement of labour ni kwenye professions Fulani Fulani, sio professions zote, na professions hizi zipo listed wazi;
That said and done, lazima tuambiane ukweli kwamba pamoja na kwamba Tanzania ilikuwa mstari wa mbele baada ya uhuru kutafuta regional integration, katika kipindi cha hivi karibuni, tumejionyesha kuwa shy partners; kwa kweli hatujiamini, hivyo kufanya tusiwe na imani sana na EAC; Kuna vituko kadhaa tumevifanya in the past two years kuashiria kwamba hatuna genuine commitment mfano kufunga mpaka wetu na Kenya Taveta (2012), kuzuia kuvusha mazao/nafaka kwenda nchi jirani(2011), kupingana na political federation and mutual defense pact (2011), na mahakama kuu Tanzania kuikingia kifua kampuni ya kitanzania (blueline) iliyofisadi na kukaribia kuifilisi east african development bank (EADB);;
Mbali ya haya, pengine hali yetu ya kusua sua pia inachangiwa Zaidi na hoja ifuatayo aliyotoa Waziri Mwakyembe mwaka jana wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Tanzania to the EAC (Dodoma) ambapo alisema:
Maswali yanayofuatia ni je, ipi ni tafsiri sahihi kati ya hizi:
- Kusua sua kwetu kunatokana na ukweli kwamba suala la EAC integration tulikuwa tunaliendesha kisiasa Zaidi na sasa uchumi unapoanza kupewa prominence na kuanza kupambanishwa na wenzetu (hasa Kenya), tunagundua jinsi gani hatujajiandaa both on the micro/household level, na pia macro level, structure of the economy and how it affects the balance of trade kati yetu na wakenya?
- Ni woga wetu to share rasilimali na ardhi ambazo ni nyingi sana kuliko wenzetu?
- Ni ignorance juu ya compromise zinazokuja na regional integration?
Pengine kuna justification katika suala la ardhi, kwani makala moja inatusema kwamba:
Tanzania accounts for about 52% of East Africas total land area, na ingawa we have the largest population in the region, bado there is is significant land available. Suala hili is both a THREAT and an OPPORTUNITY kwetu sisi katika muktadha wa EAC, na ukweli utaendelea kubakia hivyo;
Mwisho ni suala la passport uraia hapa pia tuna sua sua linapokuja suala la common passport tofauti na wenzetu; Katika hili, given given ukweli kwamba almost 33% ya population ya EAC region ipo Tanzania, tunahitaji kuwa waangalifu sana hasa ikizingatiwa kwamba wenzetu wanasukumwa Zaidi na population pressure & shortage of land kuliko chochote kwa mfano population density Tanzania ipo chini sana ikilinganishwa na Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda; we have 47 people per square Kms, the lowest in the regions, huku Uganda na Kenya wakiwa juu Zaidi, na Rwanda na Burundu wakiongoza, 430 & 301, respectively;
Inawezekana sijapanga hoja katika mtiririko mzuri, lakini mniwie radhi, ilikuwa ni suala la haraka haraka tu katika kuchangia hoja; Nitarudi kwa hoja Zaidi
Mkuu
Mchambuzi, ahsante kwa maoni yako.
Hapo juu umeonyesha kuwa miaka miwili Tanzania imekuwa haijiamini. Napenda kukuhakikishia kuwa kutojiamini ni tofauti na kutoaminiana.
Katika miaka zaidi ya mitano Uganda imepiga debe sana kwa Rwanda na Burundi kupewa uanachama kamili. Lengo lilikuwa Rwanda ili kuongeza nguvu katika mambo ''yanayokusudiwa''.
Ushirika wa sasa wa KKK haukuanza leo. NI mkakati mkubwa na Tanzania iliposhtuka ndipo ikaonekana kama haijiamini, ukweli ni kuwa inachukua tahadhari.
Waziri wa ushirikiano wa EAC mh Sitta amefanya kazi na Nyerere, Kenyatta, Obote, Moi na hawa wa sasa.
Hakuna mwenye uzoefu katika integration ya sasa na iliyopita kama yeye.
Huyu Sezibera hana uzoefu wowote labda kama ni kuongoza Genocide.
Hivyo kuna sababu muhimu sana za Tanzania kuchukua tahadhari.
Magazeti ya IPP ya jana yametoa siri kubwa sana inayounga mkono hoja zangu.(Nina nakala nitaweka hapa).
Chanzo cha habari ni cha kauaminika.
Kulikuwa na mpango wa kuunda jeshi la pamoja la EAC.
Taarifa za kuundwa kwa jeshi hilo alikuwa nazo Sezibera bila kujadiliwa na nchi wanachama.
Alichokifanya Sezibera ni kuweka mkakati wa kiuchumi halafu akachomeka kipengele cha jeshi.
Haiwezekani jambo kubwa kama hili lifanyike kihuni kwa kusainiwa na mawaziri bila mjadala wa maana.
Kumbe nyuma ya kifungu hicho kilichofichwa na Sezibera kulikuwa na mkakati wa Kagame na Museveni wa kuunganisha majeshi ili kuzuia majeshi ya Tanzania kuingilia mgogoro wa Congo wenye manufaa kwao.
Tanzania ilipokataa suala hilo likaahirishwa kwasababu maana nzima ilishapotea.
Hoja ilikuwa kuiweka Tanzania on the spot na kuendelea na ajenda zao.
Sasa ninapokuja katika maswali yako,unaposema kusuasua kwetu ni kutojiamini, woga au ignorance si dhani ni sahihi. Vipi kama ni tahadhari inachukuliwa hasa tukizingatia usiri na mkakati wa KKK dhidi ya Tanzania.
Mpango wao wa kujenga vitu kama reli si suala la siku moja ni mpango waliokuwa nao siku nyingi ilipoonekana Tanzania inachukua tahadhari wakaamua kwenda wenyewe kama njia ya kushinikiza.
Nadhani
Zinedine #161 ameeleza mambo mengine yanayoshadidia hoja zangu
Kuhusu Tanzania kuchukukia integration kisiasa zaidi kuliko kiuchumi, mimi nadhani wengine ndio wanafanya hivyo.
Huwezi kuwa na nguvu ya kiuchumi bila kuwa na msingi imara wa kisiasa na kinyume chake.
Ni vitu visivyoweza kutengnishwa. Endapo wenzetu wangekuwa na fikra za kiuchumi zaidi kwanini basi wachomeke hoja za majeshi ya pamoja na wala si kuwa na benki kuu ya EAC kwanza?
Hivi hapa si siasa kweli na nani anafanya hivyo?
Leo wenzetu wapo makini kutuburuza tuamini kuwa hatujiamini huku wakiwa na ajenda za mambo kama ardhi, na jeshi ambayo hawayasemi bali wanampa Sezibira aandae vifungu vya siri na kuvichomeka kama sehemu tu ili tutakapokubali suala zima la uchumi basi na yale wanayokusudia tunayakubali.
Hebu tujiulize kwanini Kenya a Uganda walikataa suala la passport za EAC?
Jibu ni simple , passport zingezuia ajenda ya ardhi. Wakaja na ajenda ya vitambulisho kwa mlango wa nyuma.
Sasa Tanzania ikichukua hadhari kwanini ionekane inasuasua au ignorance.
Na hili la ardhi umekubali kuwa linahitaji hadhari ambayo wenzetu wanasema ni waoga wa ushindani.
Nadhani tuangalie nia za wenzetu na kinachoisumbua Tanzania sasa hivi ni kuwa na washirika wasioaminika na wenye nia za siri. Lazima hadhari ichukuliwe vinginevyo tunaweza kuunda EAC yaviongozi na si wananchi tukarudi kule kule kwa 1977.
cc
JokaKuu zidane