Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

Mkuu kuna vitu viwili umechanganya,naomba nikuwekee sawa ili ujadili bila kupoteza unguli wako unaoheshimika jamvini.

Kuhusu umeme, hakuna msaada wa nje unaotumiwa kulipa bili za Tanesco.
Tanesco inafanya kazi Tanganyika na inakusanya mapato yake huko.
Zanzibar wana Zesco, inauziwa umeme na Tanesco.
Kwamba Zesco wanakusanya kwa unit sh ngapi hilo ni juu yao.
Tunachojua kwa unit moja znz inalipa chini ya Mtanganyika.

Deni la Zesco kwa Tanesco ni baina ya mashirika mawili. Zesco wanakusanya mapesa na hayajulikani yanakwenda wapi.
Kuna scandal ya bilioni 20 kutoweka kiaina huko Zesco ambayo imefukiwa.

SMZ inachukua deni la Zesco na kuitupia serikali ya muungano. Sasa mznz analipa umeme jibu ni hapana.
Laiti wangekuwa wanalipa basi wasingegoma kulipa deni la bilioni zaidi ya 70. Deni linatoka wapi kama wznz wanalipa?

Hapo utakuja na hoja kuwa Zesco wanakula pesa. Well,walipojiondoa Tanesco ilikuwa ni kuwa na shirika lao.
Sisi tunawauzia umeme wao na ndiyo maana SMZ inatakiwa ilipe.
Mgomo wa kulipa,walitaka walipe kiwango cha chini cha unit za Tanganyika. Hiyo ndiyo akili ya ZNZ.

Pili, SMZ ilikuwa inatumia milioni 800 kwa mwezi kwa umeme wa Pemba.
Kwa mujibu wa waziri wao sasa hali itakuwa njema baada ya kuungwa na Tanesco kutokea Tanga.
Hali nzuri maana yake ni ile ile, watagoma kulipa na deni litapelekwa JMT. Wanaogoma ni znz kumbuka.

Tatu, kuhusu suala la misaada, umeme wa kwenda znz wa mwanzo ulikuwa mkopo na msaada uliolipiwa na JMT.
Mwezi Jan 2014 wamepeleka umeme kwa msaada wa nchi za nje ambzo zimetoa kiasi bilion 39? na SMZ bilioni 5. Kiaisi kilichotakiwa ambacho SMZ haikuweza kukilipia ni bilioni 11 walizoomba kutoka JMT.
Hadi hapo unaona jinsi gani mikopo na misaada inavyowafikia. Hivyo usichanganye kati ya bill na gharama za kupeleka umeme.

Unatakiwa ujiulize, kama mambo yote ni ya JMT, ZESCO imeundwa kumhudumia nani na kwanini.
Haya yote ni katika narcissism na nepotism, kwamba wanataka kutumia ubinafsi kujinufaisha kwa gharama za wengine.
Haiwezekani SMZ yenye kila chomba ipitishe matatizo yake kwa Mtanganyika kwa kisingizio cha jina.

Ili kuondoa kuvaa koti, tunataka Tanganyika yetu tushughulikie umasikini wa Watanganyika.
Znz wabaki huru waende kukopa na wapewe misaada kama Syechelles, Mauritius, Comoro, Haiti, Vnanuata, Fiji na Jamica.

Sijui mkuu kwanini hutaki tuweke equation sawa sawa.
Tunasema kama tumevaa koti basi tunaomba tulivue ili wenzetu nao wapate upande wa kujifunika. Hilo hutaki.

Usipoanza na kuwalaani wznz kwa ujahilia wao wa kudharau katiba yetu, na kuandika katiba yao ya kibaguzi ya 2010, unapoteza nguvu za hoja za kuwasemea.

Kwavile kuna dana dana za kuwapendeza, sisi tunasema they will pay the cost. Wana nafasi moja tu, kukubali uwepo wa Tanganyika. Wakiichezea hiyo tutawataka watusaidie kuizindua Tanganyika kwa gharama zao.
Mkuu wangu sijui unachokizungumza hapa zaidi ya kunichanganya zaidi.
Tanesco au Zeco yote ni mashirika ya Umma ambayo yanaendeshwa Kijamaa nikiwa na maana ya kwamba hayapati maipo halali kutoka kwa wateja wake. Na ukitazama miradi ya Mtera na Hydropower zote including za gas kina Richmond a.k.a Symbion yote ni mashirika mengine yanayofua Umeme kwa jina la Tanzania na kuwauzia Tanesco. Hivyo madeni yote ya Ufuaji umeme ni ya TAIFA hivyo bara tusipowalipa Tanesco, haina tofauti kabisa na Visiwani wasipowalipa Zeco. Swala hapa ni kwa nini wizara za serikali, nyumba za viongozi. bunge na taasisi mbali mbali za serikali ya JMT hazilipi madeni yao! huwezi kuchambua madeni ya zanzibar pekee pasipo mkutazama mlolongo wa list of shame toka serikali zote wasivyoweza kulipa madeni na kuwaweka wananchi na tanesco ktk hali ngumu.

Aidha nataka pia uelewe ya kwamba najua vizuri ya kwamba Zanzibar wanapata Umeme wao kupitia National grid, hivyo ingewezekana kabisa wao wakalipa mashirika ya ufuaji bila kupitia Tanesco kama Mambo yote yangekuwa ya Muungano.. Lakini tumechukua sisi jukumu la kuingia mikataba ya ufuaji kwa jina la tanzania lakini mikataba hiyo ni kwa ajili ya viongozi. Wewe na kundi lenu la mnashindwa kuutazama ukweli badala yake mnajiingiza ktk ukabila huku viongozi wa CCM wakiwacheka maana hata wao hawalipi kama unavyoitazama serikali ya Zanzibar. Kikulacho kii nguoni mwako hutaki kutazama!

Tazama mradi wa Rapid Transit wa Dar es Salaam, imekuwaje fedha za mkopo wa benki ya dunia kwa Tanzania nujenge barabara za dara kwa mabillioni halafu mradi huo uwe wa watu binafsi (Bakhresa na EL)?.. Deni hilo itadaiwa tanzania lakini watakao faidika na mradi mzima ni watu binafsi hii ni baada ya wananchi kupiga makelele kwa nini wananchi wazawa wasinufaike na miradi ya Taifa, sasa wajanja wamegundua njia ya kuchukua miradi ya taifa wao wenyewe.

Jiulize kwa nini mradi huu usiwe wa Manispaa ya Dar es salaam au mkoa wa Dar? kwa nini UDA usiwe mradi wa Dar, kwa nini usafishaji mji na majitaka usiwe mradi wa mkoa wa Dar ila unapewa watu binafsi ambao wameshindwa kuifanya kazi kutokana na uwezo wao mdogo ama ubakhiri wao ktk kununua vifaa vya kisasa. Ni kwa sababu mambo yote bado yapo mikononi mwa serikali ya CCM. Mawaziri ndio wenye kuendesha kila jambo la serikali ya Tanganyika au Tanzania, anayekumaliza wewe nani hapa?.

Sasa nini solution kwa mtazamo wangu. Unapofanya mambo yote kuwa ni ya Muungano, unazigawa kazi toka serikali kuu inakuwa na majukumu yake, serikali za nchi, serikali za mikoa, majimbo na hata wilaya na kata kote kila sehemu inafahamu majukumu yake ktk utekelezaji wa shughuli za selikari yao. Ufuaji umeme ni swala mla serikali kuu ambalo serikali hiyo inatakiwa kuwa na shirika lake kama Tanesco inayofua Umeme na sio kugawa umeme. Serikali kuu inaweza kuwa contract mashirika ya nje lakini chini ya shirika hilo na sio mashirika hayo kuwa independent na Tanesco shirika la Umma kuwa mteja wao!. Huu ni mfumo wa Kijamaa ambao bado tunaukumbatia kiasi kwamba tanesco inaendeshwa Kijamaa badala ya kuwa shirika Binafsi.

Na unapozidi kuzungumzia swala la Tanesco ni miujjiza mitupu kwani shirika hilo lilitakiwa lenyewe ndio chanzo cha ufuaji Umeme na kuwauzia mashirika binafsi ambayo ndio yatahusika na kusambaza umeme nchini. Huwezi kuliweka shirika la Umma (taifa) ktk hatua ya kufuatilia madeni ya wananchi, hii sio kazi ya serikal bali ni kazi ya mashirika binafsi ambayo yatauza umeme kutokana na Tanesco ku control bei za ufuaji, hivyo kuwa na sauti ktk bei ya usambazaji, serikali kujua kodi yao, profit and loss ya mashirika na kadhalika. Serikali kuu kazi yake ni kuweka miundombinu ambayo ufuaji wa umeme ni mojawapo! huwezi kuwapa mashirika binafsi kazi hiyo ilihali mikopo inachukuliwa na Taifa.. Huu ndio uhumi unaofanyika wewe unaitazama zanzibar wakati unaibiwa na viongozi wako wenyewe.
 
Mkuu
Kuhusu Tanesco na madeni, jinsi ilivyoshindwa na ubabaishaji wa serikali kuhusu ubinafsishaji, naafiki kabisa.
Hakuna shaka madeni ya Tanesco ni zao la kutolipa madeni ya ndani kwasababu haijiendeshi kibiashara bali huduma.

Katika mjadala wako hapo juu, umegusia kuwa kama tungekuwa na mambo yote ya muungano basi kusingekuwa na tatizo la kulipia znz deni lake kwasababu ni la Tanzania. Naafiki kabisa.

Lakini lazima uangalie baadhi ya mambo.
Madeni ya wizara tunayalipa wote Watanganyika kupitia ongezeko la bei ya umeme.
Kwa maana nyingine we stand or fall together. Hakuna shirika la umeme la Mtwara wala Tanga.
Hakuna Kigoma au Mbeya, tuna Tanesco moja.

Wazanzibar walijondoa Tanesco kwasababu wanataka ID yao. Wameanzisha shirika lao wakijua linaweza kutoa huduma nzuri kuliko Tanesco na kwamba, watakusanya mapato yao na kuyabakiza huko.
Mfano mzuri, Zeco waliwahi kugomea deni kwa niaba ya wateja wa znz wakisema hawakuambiwa bei imepanda na serikali ya JMT. Tena si Tanesco ni JMT kwakujua kuwa huko ndipo jalalani pa kutupa uchafu wao.

Kwa akili za kawaida, Zesco imetumika kukwepa kuwajibika kwa kutetea watu wa znz wasibebe mzigo waliobeba Watanganyika. Zesco haikulalamika kama taasisi ya Tanzania, bali ya nchi ya znz.
Kuunda shirika kulimaanisha kujitoa Tanzania, leo Mkandara anataka wawe Tanzania wakati wao hawataki!

Makusanyo yao hayatumiki kulipa deni Tanesco, yanaingia SMZ kwa shughuli za maendeleo ya huko. Tena wanaiba bilioni 20, SMZ haishughuliki kwasababu wanajua deni linatupwa kwa Mtanganyika.
Hivi kweli nje ya muungano, SMZ inaweza kuacha bilioni 20 ambazo ni sawa na 5% ya makausanyo ya ipotee tu!

Kwa mujibu wa katiba yao ya 2010 hawa ni nchi, taifa na serikali tofauti na sisi.
Kupitisha deni hilo kwetu ni kutuonea kwasababu wao si kama Mtwara au Mwanza wanaochangia hasara za shirika la Tanesco, wap wana ID na mambo yao kama Zeco

Mkuu, mfano wa Zesco unaeleza vizuri sana kuna sababu gani za msingi za kuanzisha Zeco.
Kama wanataka kufaidika na huduma za Tanzania kwanini Zesco.
Ni mkoa gani wa Tanzania una shirika lake na kwanini iwe znz.

Utaona yote yamefanyika kwa nguvu ya katiba ya 2010 inayowatambulisha kama si Watanzania.
Linapokuja suala la kulipa na gharama, wznz wanavaa vazi la Tanzania.

Huu ni uhuni, ni uhuni na ujahilia uliokithiri.
Wanatumia neno Tanzania kwa faida zao, lakini si wadau wa jina hilo. Huu ni wendawazimu kuendelea nao.

Laiti Tanganyika ingekuwepo, kusingekuwa na wizi wa namna hii.
Tanganyika ingesimama kudai wizara na mashirika yake na ingefanya biashara na SMZ. Period.

Na mwisho , kama wana haki ya kupitisha deni kwetu, haki ya kulalamika kuhusu misaada wanaipata wapi?
 
Kwa muda wa miezi 3 tangu hoja ya S3 iwekwe wazi, hatujasikia utetezi wa kwanini ziwe mbili kwa mantiki na akili. Kinachoendelea ni vitisho na sababu zisizo na msingi.

Hoja ya gharama za S3 imekufa, watetezi wa S2 wameshindwa kushawishi umma S2 na gharama zinakuwaje.
Tatizo linalowakumba ni ukweli kuwa huwezi kuwa na Tanzania ambayo znz ipo ukasema ni apande mmoja.

S2 maana yake ni 1.5 (Yaani moja ya znz na nusu nusu ya Tanganyika na ZNZ).
Katika mazingira hayo huwezi kuweka gharama za kuendesha muungano katika hesabu, utawala au maamuzi.

Hoja kubwa iliyobaki ni kuhusu misaada na mikopo.
Hoja hii nayo haina nguvu kwasababu ukiongelea misaada na mikopo ni lazima uwe na pande mbili

  1. Misaada na mikopo ya nje
  2. Misaada na mikopo ya ndani

Watetezi wa hoja wanajitia upofu wa kutoangalia pande zote.
Hata upande mmoja wanaouangalia kwa jicho la kengeza bado nao unawashtaki.

1.Unagawaje misaada na mikopo kwa sehemu moja ya Taifa la Tanzania ukiacha nyingine
2.Unagawaje misaada na mikopokwa kutumia vigezo gani, watu, eneo, utaifa au hesababu za namna gani.

Kinachoendelea kwa upande wa CCM ni kutoa zawadi kwa znz.
Mfano, ni kuongeza nafasi za ajira ambazo hazijulikani zimepatikana kwa uwiano au hesabu gani.
Hakuna anayeweza kueleza 21% imepatikanaje, hesabu gani zimetumika kuendesha muungano.

Mbinu ya CCM ni mbovu. Inaweza kufanikiwa kwa muda, siku itakapotibuka,mbinu hii itakuwa ni balaa.

Watanganyika kwa miaka mingi wamekuwa kimya, wanahoji kuhusu rasilimali zao zinavyotumika katika muungano

Ni wazi ni kuwa rasilimali za Mtanganyika ni za wote, za mzanzibar ni za zaznibar. Hili linaamsha hamasa na hasira na ipo siku muungano utakufa kama glass ya kioo inavyovunjika mara moja.

Njia muafaka kwa sasa si kugawa pipi na peremende kwa wznz,bali kusikiliza pande zote na kutafuta muafaka wa kati na kati kama muungano unatakiwa kuendelea.

Kinyume cha hapo, ni suala la muda tu, nchi itafikia mahali watu wanakimbizana mitaani, maofisini na kwenye taasisi nyingine kwasababu hawatakuwa tayari kusikia jingine bali kuona haki inatendeka.

Haki inayopaswa kutendwa ni kuwasikiliza pande zote na kutafuta suluhu.
Njia za kuficha matatizo kwa hoja za kilaghai, kama kuvunja utaifa, gharama n.k. hazitakuwa na nafasi.

Watanganyika wamechoka na dharau za wznz.
Kitendo cha kukiuka katiba na kuchukua maamuzi bila kuwasikiliza kinatia hasira.

Ndipo tunasema ipo siku Watanganyika watafuata kanuni ya mwiba unapoingilia ndipo unapotokea. Wafaransa wanasema tete a tete, kwa maana moja tu,watachukua hatua unilaterally kama wznz wanavofanya

Tofauti na wznz, watanganyika hawana chombo chao cha kuwatetea, watasimama na kujitetea.
Ikifika muda huo, hali itakuwa tofauti na mzaha unaoendelea.
Wznz watajikuta wanalipa gharama zinazoweza kuepukwa kama Watanganyika watasikilizwa.

Tusemezane
 
Mkuu
Kuhusu Tanesco na madeni, jinsi ilivyoshindwa na ubabaishaji wa serikali kuhusu ubinafsishaji, naafiki kabisa.
Hakuna shaka madeni ya Tanesco ni zao la kutolipa madeni ya ndani kwasababu haijiendeshi kibiashara bali huduma.

Katika mjadala wako hapo juu, umegusia kuwa kama tungekuwa na mambo yote ya muungano basi kusingekuwa na tatizo la kulipia znz deni lake kwasababu ni la Tanzania. Naafiki kabisa.

Lakini lazima uangalie baadhi ya mambo.
Madeni ya wizara tunayalipa wote Watanganyika kupitia ongezeko la bei ya umeme.
Kwa maana nyingine we stand or fall together. Hakuna shirika la umeme la Mtwara wala Tanga.
Hakuna Kigoma au Mbeya, tuna Tanesco moja.

Wazanzibar walijondoa Tanesco kwasababu wanataka ID yao. Wameanzisha shirika lao wakijua linaweza kutoa huduma nzuri kuliko Tanesco na kwamba, watakusanya mapato yao na kuyabakiza huko.
Mfano mzuri, Zeco waliwahi kugomea deni kwa niaba ya wateja wa znz wakisema hawakuambiwa bei imepanda na serikali ya JMT. Tena si Tanesco ni JMT kwakujua kuwa huko ndipo jalalani pa kutupa uchafu wao.

Kwa akili za kawaida, Zesco imetumika kukwepa kuwajibika kwa kutetea watu wa znz wasibebe mzigo waliobeba Watanganyika. Zesco haikulalamika kama taasisi ya Tanzania, bali ya nchi ya znz.
Kuunda shirika kulimaanisha kujitoa Tanzania, leo Mkandara anataka wawe Tanzania wakati wao hawataki!

Makusanyo yao hayatumiki kulipa deni Tanesco, yanaingia SMZ kwa shughuli za maendeleo ya huko. Tena wanaiba bilioni 20, SMZ haishughuliki kwasababu wanajua deni linatupwa kwa Mtanganyika.
Hivi kweli nje ya muungano, SMZ inaweza kuacha bilioni 20 ambazo ni sawa na 5% ya makausanyo ya ipotee tu!

Kwa mujibu wa katiba yao ya 2010 hawa ni nchi, taifa na serikali tofauti na sisi.
Kupitisha deni hilo kwetu ni kutuonea kwasababu wao si kama Mtwara au Mwanza wanaochangia hasara za shirika la Tanesco, wap wana ID na mambo yao kama Zeco

Mkuu, mfano wa Zesco unaeleza vizuri sana kuna sababu gani za msingi za kuanzisha Zeco.
Kama wanataka kufaidika na huduma za Tanzania kwanini Zesco.
Ni mkoa gani wa Tanzania una shirika lake na kwanini iwe znz.

Utaona yote yamefanyika kwa nguvu ya katiba ya 2010 inayowatambulisha kama si Watanzania.
Linapokuja suala la kulipa na gharama, wznz wanavaa vazi la Tanzania.

Huu ni uhuni, ni uhuni na ujahilia uliokithiri.
Wanatumia neno Tanzania kwa faida zao, lakini si wadau wa jina hilo. Huu ni wendawazimu kuendelea nao.

Laiti Tanganyika ingekuwepo, kusingekuwa na wizi wa namna hii.
Tanganyika ingesimama kudai wizara na mashirika yake na ingefanya biashara na SMZ. Period.

Na mwisho , kama wana haki ya kupitisha deni kwetu, haki ya kulalamika kuhusu misaada wanaipata wapi?
Mkuu nakuponfeza kwa kuanza kunielewa isipokuwa unapotunmia neno Wazanizbar hapo ndipo napokataa hoja zako kwa sababu Gonjwa hili lipo ktk mfumo mzima wa Utawala ambao bado kabisa unatumia fikra za Kijamaa pasipo kuimarisha nguzo kuu za uchumi wetu.

Swala la Zanzibar kujitoa sii ukweli bali ni lazima Zanzibar iwe na shirika lake hata huku majuu kila nchi inaendeshwa ya mashirka yake sii lazima shirika moja liendeshe shughuli zote za Taifa. Hivyo Zanzibar kuwa na Zeco ni utaratibu murwa kabisa wa kugawana mamlaka ya uendeshaji serikali na mashirika yake tena basi hata mikoani ilitakiwa mashirika binafsi yapewe tender ya kusambaza umeme kwa wananchi kupitia halmashauri zake na sii swala la Tanesco kusambaza umeme bali Tanesco wanatakiwa ku deal na mashirka yanayofua umeme.

Swala lako ni ulipaji wa madeni ya Tanesco, na ndio maana nimekwambia tatizo hili linatokana na utawala! serikali ya CCM kwa jina la JMT hawalipi madeni ya Tanesco, na vile vile serikali ya CCM Zanzibar hawalipi madeni hivyo hakuna kitu Uzanzibar wala Ubara!. Kilichopo hapa kati ni serikali ya CCM ambayo ndio hawalipi madeni yao iwe bara ama Zanzibar na mashirika hayo yanashindwa kujiendesha hivyo kuetegemea wananchi maskini wasiokuwa na uwezo kuendesha mashirika haya. Hivyo tusimchinje jogoo kwa sababu anawika saa tisa usiku wakati tunajua fika kwamba matumizi ya saa sasa hivi yapo hadi kwenye simu za mkononi (cellphone)! Jogoo wako anaweza kuwa alarm ya simu na sii kutafuta mchawi kuwa jogoo, mwisho wa siku ni wewe utakaye poteza ongezeko la vifaranga ama shamba la kuku!

Kwa hiyo basi usipende kulaumu kila kitu na kutafuta mchawi wakati mchawi ni hii serikali ya CCM ambayo inatawala pande zote mbili na hawalipi madeni. Ni serikali ambayo imetuingiza ktk janga la IPTL, Richmond (Symbion) na majanga mengine ya Meremeta, Rada na kadhalika bila kujali alokuwa rais ni Mwinyi, Mkapa au JK. Kuwatenga zanzibar ktk hali halisi ambayo hata sisi Bara tulitakiwa tugangamae kama wao kwa kutaka serikali za majimbo au madaraka mikoani ili kuviwezesha vyama vingine vya kisiasa kuendesha shughuli za serikali pale waliposhinda uchaguzi.

Zanzbar kwa upande mwigine wanafanya hivi kama njia ya Kupingana na CCM na sii Tanganyika au Watanganyika. CUF wanajua fika ya kwamba wameweza kushinda chaguzi za Zanzibar na wanapigana na utawala wa CCM ambao kwao nguvu yake ipo Bara. Wamejaribu kila njia, kila hila wameshindwa hivyo wanachokitaka sasa ni kuzitenganisha nchi ii wapate kutawala kama CCM ya Zanzibar.. Ni uroho wa Ukuubw atu badala ya kutafuta njia mbadala za kuisambaratisha CCM na serikali yake ya Ujima (Ujamaa na Kujitegemea kuwa mwongozo wa TAIFA).

Ni wale wajinga wachache wanaoongozwa na Ukabila, Udini na Uzoba wanaoshabikia vitu kwa sababu kasema Jussa ama Maalim Seif ambao wote wanatumia nafais hii kujikuza kisiasa ili wapate kupigiwa kura kila wanapogombea maana wananchi wamechoka na CCM hivyo wapo tayari kumsikiliza mtu yeyote anayetukana mfumo huu ambao kwao uliasisiwa na Nyerere hivyo, kwao ni BARA inayowaweka CCM ktk uongozi wa nchi hii na hivyo marafiki wa maadui zao ni maadui zao pia!.

Kama sisi tungekuwa kama wao, tukapigania mabadiliko (#changeTanzania) basi swala la kwanza ni kuitaka Katiba mpya ambayo itaondoa mfumo wa Ujima (Winner takes all). ni mfumo wa Kijamaa (chama kimoja) ambao hautakiwi kuwepo leo ktk utekelezaji wa shughuli za serikali laa sivyo nini maana ya kuwa na vyama vingi na demokrasia?. Uwazi na Uwajibikaji hawezi kuwepo ktk mfumo huu ambao ni sawa na tumechanganya mafuta na maji ili tupate mwongozo mbadala. Tazama ukweli ni upi, huu mfumo umewafanya viojngozi wetu kuwa na jeuri kubwa, wamekuwa watawala ambao wapo radhi kutumia nguvu ya dora kulinda maslahi yao ama ya chama.

Nna ndio maana toka Ikulu, mawaziri, wakuu wa mkoa, wakuu wa wilaya, na hata makatibu wakuu ktk utekelezaji wa shughuli za serikali zote nchini ni viongozi toka chama tawala! hivyo unategemea vipi Mbunge au Meya aloshinda uchaguzi toka chama cha upinzani ataweza kuwa na nguvu ya kutimiza wajibu ama ahadi zake ktk utawlaa bora? Haiwezekani na hapa ndipo tunapokwama na sii serikali ngani! Tukiacha ushabiki, malumbano na Utanganyika nasi tukafikiri nje ya Box kutazama ni wapi tunapokwamishwa basi bila shaka nasi Wabara tutaihitaji katiba Mpya kwanza kabla ya muundo wa serikali kwa sababu hadi sasa Tanganyika yetu Ipo ikiitwa BARA ndani ya JMT na inatumiwa vibaya sana dhidi ya WaZanzibar na Watanganyika.

Kwa uhakika serikali ya CCM imevaa koti la Uheshimiwa, imekuwa kosa kubwa kuwaita viongozi wetu waheshimiwa na imekuwa muhari kwetu..Wamelivaa koti la Uheshimiwa kiasi kwamba miradi yote nchini inaendeshwa kwa majina ya watu bandia lakini ukweli ni kwamba hii ni miradi yao wenyewe. Toka viwanda vya Umma vilivyouzwa,, mashirika ya Umma hadi tender zote za serikali wanazichukua wao kwa kutumia majina ya wajinga wengine wanaotuzwa Utajiri ili mradi wapo karibu na Wakubwa. Tazama undani wa shirika la UDA, Majitaka, Bomba la gas toka Mtwara, ATC, TRA, Meremeta, Kiwila, mashirika ya simu, vyombo vya habari na kadhalika haya yote ni matokeo ya watu kuvaa koti la uheshimiwa! hakuna kitu confict of interest na ndio maana dollarisation ($) inaendelea kupitishwa na serikali ya CCM japo ukweli ni kwamba inaua nguvu ya Tsh.

Nilikwenda Botswana mwaka 1983, na dollar zangu nilipokwenda kiwandani kununua mali niliambiwa niende benki nikabadilishe wao wanachukua Pula, sikuamini nikaenda madukani hivyo hivyo Botswana walikataa matumizi ya Dollar toka miaka hiyo leo tunawashangaa jinsi gani uchumi wao umeendelea kuwa na nguvu kubwa Afrika. Sisis ndio kwanza hatuitaki Tsh, hatukitaki kuwasiliana kwa kiswahili ama kiwe lugha ya kufundishia kwa imani kwamba haifai, hatuzitaki mila na tamaduni zetu kwa sababu Udhungu umetuingia, nenda wasome viongozi wetu wa leo na kesho Face book na Twitter, utashangaa. Hii kama sio akili ya Kitumwa ni nini haswa?
 
Mkuu Mkandara

Wakati unakataa matumizi ya neno uzanzibar, kwa chini chini una hubiri uzanzibar kwa nguvu sana.
Nimekuuliza swali huko hujawahi kunijibu. Je, aliyeleta uzanzibar ni nani?
Je, katiba ya znz ya 2010 inayoitambua znz kama taifa, nchi yenye serikali na vyombo vyake ililenga nini kama si utambulisho wa uzanzibar.Kama hutakubali wznz ndio wanaoeneza uzanzibar, basi utakuwa katika state of denial kubwa sana.

Wazanzibar hawataki kuitwa Watanzania. Ndio wameamsha hisia za Utanganyika.
Ni mara ngapi umesikia watu wakijiita Watanganyika.
Baada ya wazanzibar kuonyesha chuki dhidi ya Watanganyika kwa kuwachoma moto, Watanganyika hawana option

Pili, Wazanzibar wanatumia Utanzania wanapohitaji mafao,hutumia uzanzibar wanapotaka kuwatenga Watanganyika.
Mfano, ili uweze kufanya kazi znz lazima uwe na kitambulisho cha uzanzibar.
Lakini, mzanzibar anapotaka kunufuaika na Tanganyika hutumia jina la Tanzania.

Mfano wa pili, wazanzibar wana sheria za ajira, ardhi n.k. ili kuwalinda wao kama wazanzibar kwa kutumia uzanzibar.
Wanapotaka mambo hayo hayo huja kwa kutumia Utanzania. Leo wanapewa 21% ya ajira za Tanganyika kwa kutumia neno Tanzania. Huko kwao kuna sheria mahususi za kuwagua na kwanyanyasa Watanganyika.

Leo, wanataka kupata ardhi hata kugombea ubunge, udiwani n.k. kwa kutumia neno Tanzania.
Huko kwao kuna sheria zianzopiga marufuku Watanganyika kupata fursa kama hizo.
Sheria hizo zinawalenga Watanganyika na si Waitaliano au Wa oman. Hiki unakiona ni sawa kabisa, Mkanadara!

Ubaguzi huo huo ndio wa kuanzisha Zeco ili wznz watumie umeme buree, na gharama zipitishwe kwa Watanganyika kwa jina la Tanzania. Zeco unayoitetea imeiba sh bilioni 20 kupitia SMZ halafu deni wanaleta Tanganyika. Mkuu, huu upuuzi unaouona ni jambo la maana sana. Mkuu huu uzezeta na uzembe unasimama hapa jukwaani kuutetea! serious! Haiwezekani deni lifikie bilioni zaidi ya 90 useme ni sawa. Huwezi kuchukua deni la SMZ ukalifanya la JMT! Hawa Watanganyika lini watafanya madeni yao sehemu ya SMZ?

Wewe unayesema mambo yote ni ya muungano. Nimekuuliza, kwanini kuwe na Zeco wakati tuna jambo moja la muungano ambalo ni Tanesco. Huna jibu !

Kwa ufupi hatuwezi kuendelea ku entertain uzanzibar ambao basically ni utegemezi.
Kwanini znz iwe na special preference over others.

Kwanini udhani kuwa wznz wana haki ya kupata hawana haki ya kuchangia.
Kwanini mkuu unafikia mahali unatetea hadi ujinga wa ZEco.

Kwamba, ni haki ZECO kwa kushirikiana na SMZ waibe bilioni 20 na ni haki Mtanganyika alipe umeme wa juu kufidia wizi wa wazanzibar! unaona haki kabisa, mkuu

Hili za ZECO tuliache huna jibu la maana. Kuhusu ubaguzi wa kizanzibar tuache huna hoja ya mashiko.
Hivi ina maana hata katiba ya znz hujaisoma? na kama umeisoma, umeielewa!!!


Tunataka Tanganyika ili tuhangaike na umasikini wetu.
Hatuhitaji kuwa na mzigo wa watu kila siku wanataka, wanaomba lakini hawana msaada wa aina yoyote kwa maendeleo yetu.
Eleza hapa, msaada wa znz ni kitu au jambo gani kwa Mtanganyika!

Hatuhitaji misaada au mikopo kwa kutumia jina la znz.
Na wala hatuhitaji kuwashikilia wao kupata misaada na mikopo.
In short, Mkandara hatuwahitaji wao! Hatuwahitaji kwasababu hakuna tunachonufaika kutoka kwao.

Tuwaache na fiscal autonomy yao nasi tupate yetu. Kama kuna ulazima tuwe na 7, kama hayawezekani wana hiari ya kwenda watakako kwasababu tunawasaidia wao, hawana msaada kwetu Mkandara!

Tusione haya tuwaambie wazazniabr ukweli, hatuwahitaji kwa lolote kwa chochote na wala hatuna sababu za kuwaibia kwasababu ni ujinga kumkamua ndama asiye na kiwele ukitegemea maziwa.
 
Nguruvi3
Wakati unakataa matumizi ya neno uzanzibar, kwa chini chini una hubiri uzanzibar kwa nguvu sana.
Nimekuuliza swali huko hujawahi kunijibu. Je, aliyeleta uzanzibar ni nani?
Je, katiba ya znz ya 2010 inayoitambua znz kama taifa, nchi yenye serikali na vyombo vyake ililenga nini kama si utambulisho wa uzanzibar.Kama hutakubali wznz ndio wanaoeneza uzanzibar, basi utakuwa katika state of denial kubwa sana.
Mkuu katibaa ya mwaka 1977 ina sema tuna serikali 2, moja ni ya Zanzibar na ya JMT. Hivyo unaposema serikali ni lazima ukubali kwamba serikali hiyo ya Zanzibar ina semi sovereignty as a republic. Hatuna republic of Tanganyika japo artical of Union ilianza na muundo huo wa kuzitambua nchi 2 ndani ya Muungano.

Madai yako yote na hao wenzako wote wa UKAWA ni kuondoa mfumo huu, hivyo sijui unachouliza maana mimi naposema zanzibar ni nchi ni kutokana na kwamba wao wana serikali ambayo inatakiwa iwe na mamlaka ya kuendesha shughuli zake, hivyo wanaunda vyombo vya kuwawezesha kuendesha mambo yao hapo ndipo nyie mnaona makosa dhidi ya katiba iliyopo.

Kumbuka tu ya kwamba katiba ile iliundwa mwaka 1977 na baada ya mabadiliko ya kisiasa na Uchumi, ilitakiwa LAZIMA katiba nayo ibadilishe muundo wake ili kutoa fursa pande zote 2 ziweze kuendesha shughuli zake. haikutokea na Wazanzibar waliendelea kukwamishwa ktk fursa zinazojitokeza kama nchi. Sisi bara na sio JMT tuliwapinga kwa kila ombi waloliweka na tukawatenga kama sii wamoja, hivyo Uzanzibar ukazaliwa.

Hata Chadema mwanzoni walikuwa chama tu cha upinzani kwa mtazamo wa demokrasia lakinmi kwa jinsi wanavyokandamizwa na CCM wametokea kuwa maadui wa CCM. Chadema walisusia bunge, walitoka bungeni wakati rais JK akija kutambulishwa bungeni, walifanya maandamano na kadhalika. Hivi leo Chadema wakizsusia Uchaguzi ujao sintowalaumu ya kuwa ni wao walojitenga. Ila nitawapongeza zaidi ikiwa mfumo mzima wa uchaguzi hautafanyiwa marekebisho ili kuvipa vyama vyote nafasi sawa ya kugombea majimbo na urais. Chadema wakichukua hatua yoyote dhidi ya katiba iliyopo sintowalaumu pia kwa sababu katiba hii inatakiwa kufanyiwa marekebisho na sii kuandika upya Artical of Union kwa sababu haihusu!..

Bila shaka umenielewa!...Tazama kwanza chanzo cha mapungufu yalosababiusha kero zote hizi..
 
Last edited by a moderator:
Mkandara;9894803]Nguruvi3Mkuu katibaa ya mwaka 1977 ina sema tuna serikali 2, moja ni ya Zanzibar na ya JMT. Hivyo unaposema serikali ni lazima ukubali kwamba serikali hiyo ya Zanzibar ina semi sovereignty as a republic. Hatuna republic of Tanganyika japo artical of Union ilianza na muundo huo wa kuzitambua nchi 2 ndani ya Muungano.
Hapa unaruka historia ili kukidhi haja. Hata hivyo nimekuuliza mara saba sabini, hii serikali ya JMT inaundwaje ikiwa na serikali moja ni ya Zanzibar? Hiyo ya pili ni ipi na kwanini imefichwa.
Makandara, huwezi kuwa na serikali ya znz halafu ukwa na serikali inayoundwa na znz na Tanganyika.Ndipo tatizo lilipo kwa mantiki na kwa hesabu. Laiti tungekuwa tunachangia muungano kwa usawa, wazanzibar wasingekubali. Wangekataa kuwa na mzigo wa serikali yao halafu wabebe wa muungano. Kwavile hawana msaada, ila wapo kwa ajili ya kuchota, kwao Tanzania ni muafaka. Wanakosa nini ikiwa wamewekeza herufi za ZAN katika jina?
Madai yako yote na hao wenzako wote wa UKAWA ni kuondoa mfumo huu, hivyo sijui unachouliza maana mimi naposema zanzibar ni nchi ni kutokana na kwamba wao wana serikali ambayo inatakiwa iwe na mamlaka ya kuendesha shughuli zake, hivyo wanaunda vyombo vya kuwawezesha kuendesha mambo yao hapo ndipo nyie mnaona makosa dhidi ya katiba iliyopo.
Mkuu , tunaomba ututendee haki.
Hivi kilio cha mamlaka kamili kimeanza kwa nani? Hivi serikali 3 na Mkataba ni debe la nani?
Hivi nani alichoma moto rasimu iliyopelekwa na Sitta kule zanzibar na kwasababu gani?

Halafu unakata kona ghafala bila indicator. Umeshasahau kuwa umehubiri sana mambo yote kuwa ya muungano.
Arguably utasema kuwa na vyombo vyao si tatizo. Bado tuna swali, unawezaje kuwa na mambo ya pamoja ya muungano ikiwa jambo kama bandari wameliondoa. Hayo ya bandari ya pamoja yanatoka wapi na kwasababu gani?
Quebec, Ontario, Alberta n.k. kila mmoja ana mambo yake, halafu wana mambo ya pamoja. California, Minnesota, Washington state, Florida, kila mmoja ana mambo yake halafu wana ya pamoja.

Mkandara anasema, znz wawe na yao, halafu znz hiyo hiyo iwe na ya pamoja. Pamoja ya pili haijulikani ni ipi.
Kwani kuna tatizo gani tukiwa na znz na Tanganyika halafu ya pamoja Tanzania, kama ilivyo kwa US au CANADA?

Unawezaje kuwa na mambo ya pamoja ikiwa wana mambo yanayokinzana na katiba ya pamoja.
Ni katiba ipi iliyo juu, ile ya JMT ambayo wamo au ile ya 2010 inayowapa mamlaka ya kuunda vyombo vyao bila kujali uwepo wa ile ya JMT? Mambo ya pamoja unayozungumzia kila siku yamefia wapi hadi unaleta sovereignty mkuu.

Lakini basi, sisi kama ni taifa moja, unadhani ni kwanini znz ipewe 'preference' wakati Tanganyika si kuwa inanyimwa bali pia haitajwi. Kuna kitu gani unachodhani ni muhimu wazanzibar kupewa priority katika taifa moja.

Je huoni kufanya hivyo ni kuanza kupanda mbegu za ubaguzi katika taifa moja.
Nitajie mkoa mmoja unaopewa kipaumbele kwasababu ya umuhimu wake
Kumbuka tu ya kwamba katiba ile iliundwa mwaka 1977 na baada ya mabadiliko ya kisiasa na Uchumi, ilitakiwa LAZIMA katiba nayo ibadilishe muundo wake ili kutoa fursa pande zote 2 ziweze kuendesha shughuli zake. haikutokea na Wazanzibar waliendelea kukwamishwa ktk fursa zinazojitokeza kama nchi. Sisi bara na sio JMT tuliwapinga kwa kila ombi waloliweka na tukawatenga kama sii wamoja, hivyo Uzanzibar ukazaliwa.
Hapa ndipo nasema hesabu za JMT na Zanzibar hazina mantiki wala mashiko achilia mbali weledi.

Umeona! tayari umesharudi'kutoa fursa pande zote''. Upande wa pili ni Tanganyika.
JMT haiwezi kuwa upande wa pili kwasababu ndani yake ipo znz.

Unless useme referee kaamua kucheza timu nyingine, na hiyo sio soccer ni kitu cha aina yake.
Hesababu zinakurudisha katika mstari bila wewe kutambua.

Ni kanuni tu za hesabu wala huhitaji kufikiria au kusononeka. Unahitaji kuzitambua kanuni, mambo yananyooka.
Mkuu ni hesabu tu

Na mwisho, chanzo na mapungufu yanayosababisha kero ni haya
1. Zanzibar kukwepa wajibu na nafasi yake katika muungano kwa kuogopa wajibu
2. Zanzibar kudhani muungano upo kwa ajili ya kuwahudumia na wala si wao kuuhudumia
3. Uchoyo, ubinafsi, majivuno ya wazanzibar
4. Kudai, kuomba hata kisicho chake
5. Uelewa wa muungano na maana ya muungano.
6. Kudani wao ni raia bora kuliko raia wengine na kwamba wanahitaji kuhudumiwa kwa ubora wao.
 
TAZAMENI WZNZ WALIVYO VIGEUGEU NA WASIVYOFAHAMU WANATAKA NINI?

Mjadala huu endelevu umemhusisha Mkandara kama mchangiaji na mtetezi mkubwa wa Zanzibar. Tunakumbuka anavyobadili position zake katika suala hili. Mkandara hana tofauti na wazanzibar wengi na mmojwapo ni Mohamed Raza

Soma kipande hiki : Raza awapaka mawaziri wa SMT | Zanzibar Yetu

Kwa ufupi bunge la JMT lipo katika hatua za kuridhia mkataba wa sarafu moja. Bunge la JMT lina wajumbe 81 wanaowakilisha Zanzibar. Kama anavyosema Mknadara fedha ni jambo la muungano na mambo ''yote ni ya muungano ''
Tulitarajia kuwa ratification ya Dodoma inatosha kwasababu imefanywa na wabunge wa Pande zote mbili.

Kama inayosema katiba ya Zanzibar, jambo linalojadiliwa na Bunge la JMT. Profesa Shivji kama Mknadara walitudanganya kuwa hiyo ni 'formality' kwamba haina impact katika mswada wowote. Majuzi, waziri wa wizara ya muungano Samia Suluhu akiwa na naibu wa fedha Adam Malima, walikwenda kwenye BLW kutoa taarifa ya haatua za ku-ratify suala la feadha.

Kinyume na 'formality' ya Mkandara na Prof Shivji wanayohubiri, BLW likaja juu kwa Adam Malima likimtaka aombe radhi kwa kauli aliyotoa. Hiyo ilikuwa chuki kwanini waziri wa Tanganyika anakwenda kuwapa taarifa, hawakumshambulia Samia au kumtaka aombe radh. Masikini Adamu Malima akaomba radhi kwasababu ya udhaifu wake kwa znz kama ule wa Mkandara, wakiamini znz ni nchi bora sana na wao ni dhalili tu.

Katika watu waliopinga taarifa ni Mohamed Raza. Mjumbe Raza ambaye katika bunge la katiba alitaka serikali 2, ameshangaza kwa kulaumu kuwa masuala ya EAC znz ni nchi na inapaswa kushirikishwa. Hapa unaweza kuona upeo na akili ndogo za wenzetu. Wakati tunataka S3 tunakusudia wao wawe na mamlaka kama tume ya Warioba inavyosema.
Wakija Dodoma ni viumbe wangine, wakirudi minazini utadhani sio wale, kelele na kufungua vinywa hata mamba ana nafuu.

Tunasema hivi si kwa dharau, ni kwa ukweli. Waziri wa fedha ni mzanzibar, makamu wa Rais ni mzanzibar, waziri wa muungano ni mznz wote hawa wnaingia katika Cabinet. Hivi wznz wanataka wataarifiwe nini tena.
Tunapowaambia kuwa S3 ni jambo zuri wznz wantaka S2.

Leo wanapiga kelele eti suala la fedha lijadiliwe na pande mbili kwasababu linahusu nchi mbili. Wazanzibar hawajui kuwa hakuna nchi inayoitwa Tanzania peke yake. Tanzania ni nchi mbili tayari. Endapo wanataka kuwa znz ni lazima kwanza Tanganyika iwepo ili wake kama nchi mbili sawa kuzungumzia masuala ya fedha.

Huwezi kuwa na usawa kati ya JMT na Zanzibar. Hapa ndipo suala la elimu linapokuja, kwamba hawa wazanzibar hawajui nini hasa wanataka na kwa njia gani. Wao wanadai hata haki waliyo nayo mkononi.

Wazazanibar wamepewa fursa ya kuamua hatima ao. Wte bila kujali chama ni waoga wakubwa. Hakuna anayetaka mamlaka kamili. Wanapokuja Dar ni watanzania, wakirudi kwenye minazi kazi kubwa ni kufungua vinywa hata kama nzi wanaingia. Huu ni mfano mzuri wa Raza na akina Shivji wanavyopotosha umma.

Wtanganyika, nanyi pia mna matatizo sana. Mnaona aina ya watu tulioungana nao. Usawa wanautaka katika kujadili si katika kue ndesha muungano. Ukizungumzia gharam, wazanzibar wanakimbilia udogo na uchache. Baada ya hapo wanadai kila jambo kwa usawa, Tutaendelea kuishi na watu wa aina hii hadi lini?

Tunasema hadi lini kwasababu hawana imapact ya aina ya iana yoyote katika maisha ya Mtanganyika. Huo ni ukweli.
Siku hizi tunawaambi wznz kama hawataki muungani njia nyeupoe. Hakuna anayejaribu aua kuthubutu kwa sababu wanatuhitaji! Sisi hatuhitaji znz hata kwa bahati mbaya, ni wao wanatuhitaji na hivyo lazima wawe nna adabu!

Tunawabeba miaka 50, sasa wanaendele akuwa kero. Kila siku wanadai jambo jipya. Lazima Watanganyika msimame na kutetea nchi yenu. Hawa wznz wanaishi kwenu, wanachukua kodi zenu na maisha yao yanawategemea! hawana sababu za kutunga sheria juu yenu. Mtanedelea kuwa mazezeta hadi lini?
 
Last edited by a moderator:
TAZAMENI WZNZ WALIVYO VIGEUGEU NA WASIVYOFAHAMU WANATAKA NINI?

Mjadala huu endelevu umemhusisha Mkandara kama mchangiaji na mtetezi mkubwa wa Zanzibar. Tunakumbuka anavyobadili position zake katika suala hili. Mkandara hana tofauti na wazanzibar wengi na mmojwapo ni Mohamed Raza

Soma kipande hiki : Raza awapaka mawaziri wa SMT | Zanzibar Yetu

Kwa ufupi bunge la JMT lipo katika hatua za kuridhia mkataba wa sarafu moja. Bunge la JMT lina wajumbe 81 wanaowakilisha Zanzibar. Kama anavyosema Mkandara fedha ni jambo la muungano na mambo ''yote ni ya muungano ''
Tulitarajia kuwa ratification ya Dodoma inatosha kwasababu imefanywa na wabunge wa Pande zote mbili.

Kama inayosema katiba ya Zanzibar, jambo linalojadiliwa na Bunge la JMT lazima lifike BLW.
Profesa Shivji alitudanganya kuwa hiyo ni 'formality' kwamba haina impact katika mswada wowote.

Majuzi, waziri wa wizara ya muungano Samia Suluhu akiwa na naibu wa fedha Adam Malima, walikwenda kwenye BLW kutoa taarifa ya hatua za ku-ratify suala la feadha.BLW limekataa kwasababu znz haikushirikishwa. Sijui znz ilitaka ishirikishwe vipi wakati waziri wa fedha, muungano, naibu gavana, makamu wa Rais n.k. ni wznz na wapo si kwa sifa zao bali sifa ya uzanzibar tu. kwamba nafasi zao hazihitaji elimu, ukiwa mznz inatosha, na wapo wamepewa.

Kinyume na 'formality' ya Prof Shivji anayohubiri, BLW likaja juu kwa Adam Malima likimtaka aombe radhi kwa kauli aliyotoa isyo husiana na mambo ya fedha, just stupid arrogance ya kizanzibar.

Hiyo ilikuwa chuki kwanini waziri wa Tanganyika anakwenda kuwapa taarifa, hawakumshambulia Samia Suluhu.
Masikini Adamu Malima akaomba radhi kwasababu ya udhaifu wake kwa znz kama ule wa Mkandara, wakiamini znz ni nchi bora sana na wao ni dhalili kwa wazazibar. Hyaa mazwazo hya kudhani kuwa znz ni eneo takatifu na bora yanayopandikizwa kwa umma na akina Prof Shivji na Mkandara ni ya kulaani sana.

Ni ya kulaani kwasababu inawafanya wznz wasiwe werevu hata siku moja. Wanadhani kuwa uznz ni tiketi ya ubora na sasa hawajishughulishi isipokuwa kudai upendeleo wa kila kitu hata kisicho chao. Akilini mwao kumejengekea hisia kuwa wao ni bora, na wao wanadhani ni hivyo. Ndio hawa akina Raza atunaowasowasikia. Leo anataka S2 esho anataka ZNZ huru n.k. Ndivyo alivyowadanganya Shivji wakati wa mbaraza ya kata.

Katika watu waliopinga taarifa ni Mohamed Raza. Mjumbe Raza ambaye katika bunge la katiba alitaka serikali 2, ameshangaza kwa kulaumu kuwa masuala ya EAC znz ni nchi na inapaswa kushirikishwa. Hapa unaweza kuona upeo na akili ndogo za wenzetu. Wakati tunataka S3 tunakusudia wao wawe na mamlaka kama tume ya Warioba inavyosema.
Wakija Dodoma ni viumbe wangine, wakirudi minazini utadhani sio wale, kelele na kufungua vinywa hata mamba ana nafuu.

Tunasema hivi si kwa dharau, ni kwa ukweli. Waziri wa fedha ni mzanzibar, makamu wa Rais ni mzanzibar, waziri wa muungano ni mznz wote hawa wnaingia katika Cabinet. Hivi wznz wanataka wataarifiwe nini tena.
Tunapowaambia kuwa S3 ni jambo zuri wznz wanataka S2 leo wanakimbia hovyo hatujui wanataka nini.
Shivji aliwaingiza Mkenge na baada ya kubaini rasimu ya kwanza ni moto kwao, leo anawaambia S2 ni muafaka, na hawa akina Raza wanaofuata upepop wanaadhirika sasa. Hawajui kipi ni chema kwao.

Leo wanapiga kelele eti suala la fedha lijadiliwe na pande mbili kwasababu linahusu nchi mbili.
Wazanzibar hawajui kuwa hakuna nchi inayoitwa Tanzania peke yake. Tanzania ni nchi mbili tayari.
Endapo wanataka kuwa znz ni lazima kwanza Tanganyika iwepo ili wakae kama nchi mbili sawa kuzungumzia masuala ya fedha.

Huwezi kuwa na usawa kati ya JMT na Zanzibar. Hapa ndipo suala la elimu linapokuja, kwamba hawa wazanzibar hawajui nini hasa wanataka na kwa njia gani. Wao wanadai hata haki waliyo nayo mkononi.

Wazanzibar wamepewa fursa ya kuamua hatima yao. Wote bila kujali chama ni waoga wakubwa.
Hakuna anayetaka mamlaka kamili. Wanapokuja Dar ni watanzania, wakirudi kwenye minazi kazi kubwa ni kufungua vinywa hata kama nzi wanaingia. Huu ni mfano mzuri wa Raza na akina Shivji wanavyopotosha umma.

Watanganyika, nanyi pia mna matatizo sana. Mnaona aina ya watu tulioungana nao.
Usawa wanautaka katika kujadili si katika kuendesha muungano. Ukizungumzia gharama, wazanzibar wanakimbilia udogo na uchache. Baada ya hapo wanadai kila jambo kwa usawa, Tutaendelea kuishi na watu wa aina hii hadi lini?

Tunasema hadi lini kwasababu hawana impact ya aina ya iana yoyote katika maisha ya Mtanganyika. Huo ni ukweli.

Siku hizi tunawaambi wznz kama hawataki muungani njia nyepee. Hakuna anayejaribu au kuthubutu kwa sababu wanatuhitaji! Sisi hatuhitaji znz hata kwa bahati mbaya, ni wao wanatuhitaji na hivyo lazima wawe na adabu!

Tunawabeba miaka 50, sasa wanaendele kuwa kero. Kila siku wanadai jambo jipya.
Lazima Watanganyika msimame na kutetea nchi yenu.

Hawa wznz wanaishi kwenu, wanachukua kodi zenu na maisha yao yanawategemea! hawana sababu za kutunga sheria juu yenu. Mtaendelea kuwa mazezeta hadi lini?

Hivi hamuoni walivyoingia baridi? Wakisikia Tanganyika matumbo yanawauma wote maliwato!
Hawana sababu za kutunga sheria au kuweka vikwazo kwa Tanganyika.
Mkiwasoma hawa akina Mkandara wanawaaminisha kuwa znz ni nchi kubwa kiuchumi. Bilioni 400 tu ndizo walizo nazo.
Hawawezi kuendesha JMT hata kwa wiki mbili kwa pato lao la mwaka bila kuondoa senti tano.

Leo Watanganyika wanakubali kupotezewa muda na nafasi za kujadili mambo muhimu na hawa wznz wasiona tija kwa lololote
 
HARAKATI ZA KUPUNGUZA MALALAMIKO YA MUUNGANO
JITIHADA ZA SERIKALI KUZIBA VIRAKA, NA SI KUPONYA KIDONDA


Wiki hii tumefikiwa na ugeni wa makamu wa Rais wa China na mtoto wa falme wa Japan
Wote wawili wametembelea Tanzania na Zanzibar!

Ujio wao kwa Tanzania ulimaanisha Tanganyika na Zanzibar. Kutokana na mantiki mbaya, wageni wamtembelea Tanzania na Zanzibar. Hapa kuna maana moja kuwa, kuna Tanzania ambayo ni Tanganyika na ipo Zanzibar.

Kwa bahati nzuri au mbaya Tanzania inaundwa na Tanganyika na Zanzibar. Hivyo wageni wametembelea Znz mara mbili ingawa haionekani. Anayekataa hili atuambie mantiki ya wageni kuja Tanzania na Zanzibar ni ipi?

Hili limefanyika ili kuondoa malalamiko ya wazanzibar kuwa wageni wa kitaifa huishia Tanganyika.
Halina tatizo kama wanakwenda huko pia. Tuliachie hapo

La pili ni makamu wa rais wa zanzibar kufungua maonyesho ya biashara ya Dar es Salaam.
Nalo pia limelenga katika kuwaonyesha wazanzibar kuwa nao ni sehemu ya Tanzania.
Hakuna tatizo pia kwasababu ukiacha katiba yao ya 2010 iliyopinga uwepo wa Tanzania, muungano unawatambua kama Watanzania.
Ukiacha wazanzibar kuvunja katiba ya JMT na kukana Utanzania, hakika wao ni sehemu ya nchi Tanzania.

Tatizo linalojitokeza ambalo wengi hawalioni ni hadhi ya makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar.
Katiba ya JMT haimtabui kwasababu walipofanya mabadiliko hakukuwa na mabadiliko katika katiba ya JMT

Ujio wa makamu wa pili kufungua maonyesho hauna tatizo.
Ni sawa tu na pale tunapowkaribisha wageni wengine kama wa Msumbiji au Botswana kufungua maonyesho hayo.
Tatizo linapokuja ni kuwa haya yanafanyika kwa ubandia'cosmetic'

Makamu wa pili wa Zanzibar hajulikani ni nani Tanzania kwa mujibu wa katiba ya JMT ya 1977.
Hata protocol hazikueleza makamu wa pili na waziri mkuu wa JMT nani mwenye hadhi kubwa.
Waziri mkuu alitembelea mabanda baada ya makamu wa pili kufungua maonyesho. Nani ni mkubwa hapo?

Unless tuambiwe alikuja kama waziri tu kutoka Kenya au Uganda ambao ni wa nchi jirani, hakuna namna suala hilo linaweza kutafsiriwa katika muungano wa sasa kikatiba, licha ya kuwa mgeni tu aliyetokea zanzibar

Katiba haimtambui na uwepo wake ni kama wa mgeni rasmi katika shughuli fulani na si katika hadhi ya makamu wa rais.

Hoja kubwa ni kuwa muungano hautadumishwa kwa pipi na peremende.
Kiini cha matatizo yaliyopo ni uchumi na siasa.Hapo ndipo viongozi wanapaswa kutilia mkazo.

Na katika kuangalia suala hilo lazima mambo yaangaliwe kwa haki bila jicho la kengeza.
Hizi hila za kuamini kuwa znz wanapaswa kupewa kila wanachodai ndizo zitavunja muungano.

Tumeona Rais Kikwete alivyokaa kimya katiba ya 2010 ya znz inayokiuka ya JMT ilipoandikwa na kupitishwa.
Leo Rais Kikwete ana changanoto kubwa ya kuwashawishi wznz wabadili katiba hiyo kama muungano unatakiwa udumu.

Watanganyika wamechachamaa kwamba kama katiba hiyo itabaki ilivyo, hakutakuwa na uwezekano wa kuwa na katiba ya pamoja ya JMT. Lazima kutatokea mgongano wa kikatiba utakaopelekea kuvunjika kwa muungano siku moja.

Rai yetu ni kuwa, tuache kufanya mambo kwa njia za bandia ''cosmetic'.
Ni lazima tuyakabili matatizo kama yanavyojitokeza na si kuwafurahisha wazanzibar.Huko ni kujidanganya.
Upo umuhimu wa ku-adress matatizo ya pande zote na kuyatafutia suluhu ya kudumu.

Kutafuta suluhu ya muda ni kuongeza matatizo.
Wiki mbili zilizopita wazanzibar wamezusha kero nyingine ndani ya BLW baada ya ile ya asilimia 21 kufanikiwa kwa 'bendeji'

Wanataka kodi ya kuingiza bidhaa Tanganyika ifutwe ili walete bidhaa zao sokoni bure.
Kwa Maana kuwa wana haki ya kutoza kodi bidhaa zinazoingia znz.
Lakini hawataki kutozwa kodi kwa bidhaa zinazoingizwa Tanganyika kutoka Zanzibar.

Kwa njia hizo,wanataka kukusanya kodi na kufanya Tanganyika uchochoro wa bidhaa zao kufika sokoni Tanganyika.
Kama tutaendelea kuwafurahisha ipo siku serikali haitakusanya hata senti tano kwavile znz itakuwa ni sehemu ya kukwepa kodi kwa kila mfanyabiashara.

Tanganyika itajikuta katika wakati mgumu sana kwasababu rahisi za kuwafurahisha wazanzibar wasioutambua huu muungano.

Kero za wazanzibar haziishi hadi pale watakapoweza kulipwa mishahara bila kufanya kazi.
Na wala hazitaisha kwa kupeleka wageni wa kitaifa au kuwaleta wafungue maonyesho na kongamano.

Suluhu inayotakiwa ni kutafuta ufumbuzi si kuweka kitambaa au bendeji katika kidonda.

Ufumbuzi ni mmoja tu, kila mtu apewe nafasi ya kuhudumia jamii yake kwa kuwa na serikali 3.
Huu ujanja wa kuita Tanganyika kama Tanzania ni kujidanganya na kuwanyima haki Watanganyika.

Tusemezane.
 
Mkuu Nguruvi
Hivi viongozi wa CCM wana maslahi gani na Zanzibar?
Ni kwanini wanaikumbatia znz kwa nguvu sana? Kuna nini nyuma ya pazia?
 
Mkuu Nguruvi
Hivi viongozi wa CCM wana maslahi gani na Zanzibar?
Ni kwanini wanaikumbatia znz kwa nguvu sana? Kuna nini nyuma ya pazia?
Zumbemkuu , viongozi wa CCM wengi hawajui kwanini wazanzibar wakumbatiwe.

Wanachojua ni pride tu ya kuwa na muungano uliodumu muda mrefu Afrika.
Wengi hawafahamu madhara na hasara za muundo wa sasa wa muungano kwa Watanganyika.

Hata miongoni mwa wana CCM wapo wachache wanaokereka na suala la muungano hasa kuwakumbatia wazanzibar.
Kanuni ya CCM ya kupiga kura za wazi ni ushahidi kuwa kuna rebellion ndani ya CCM.
Kauli ya mbunge kesi ya kuwaambia wznz njia nyeupe ni dalili nzuri kuwa wapo wanaokereka lakini wafanye nini

Nguvu ya kukumbatia ipo sehemu mbili
1. Kukumbatia kwa pride ambayo ni sehemu ya CCM bara
2. Kukumbatiwa ambayo ni sehemu ya CCM zanzibar

Mgawanyiko wa wazanzibar una ambatana na masuala ya kihistoria. Suala la mapinduzi ni miongoni mwao. Urangi na asili ni sehemu ya pili na wogani sehemu ya tatu.

CCM wanakumbatia muungano kwa maana ya kumuenzi Mwalimu. Wasichokijua kwasababu wengi hawasomi na hawashughulishi akili ni kuwa Mwalimu alikuwa 'Dynamic'. Leo angekuwa hai angeungalia muungano kwa jicho lingine.
Unafiki wa CCM ni kumuenzi kwa muungano huku mambo kama azimio la Arusha wakiwa wameyazika.

Sababu hasa zilizoplekea muungano kwasasa hazipo. Kulikuwa na hofu ya utawala wa zanzibar kuondolewa kutokana na udhaifu uliokuwepo. Kulikuwa na hofu ya znz kutumika katika kuhujumu Tanganyika.
Hizo ndizo sababu za wakati huo.

Kwasasa, kumeingia sababu nyingine ya kisiasa. CCM wanaitumia znz kufikia malengo yao ya kutawala na hata kifasadi.
Wazanzibar wa CCM nao wanaitumia hiyo kwa hofu ya madaraka na nafasi zao siku za baadaye.

Muungano ulilenga katika Pan Americanism. Sina tatizo na muungano kwasababu hata wakubwa wanaungana.
Hilo ni wazo zuri kabisa. Nina tatizo na muundo wa muungano wa sasa.

Kwa mfano, tuna wasomi na watu wenye exposure kama Mkuu Mkandara ambao tumejadiliana nao hapa.
Katika kila tulilowauliza hakuna jibu isipokuwa kuwa tu tuendelee kwa mazoea.
Ndivyo CCM walivyoshindwa kwenda mikoani kuwashawishi watu kwanini muundo wa sasa ni mzuri.

Muundo uliopo unatoa nafasi kwa Zanzibar kama sehemu ndogo kuitumia Tanganyika. Na kwavile wanajua hilo kila mara wamekuwa wazuri sana wa kudai na kutaka hata kisicho chao. Wanaelewa Watanganyika wengi hawaoni madhara ya sehemu ndogo sana kuchukua sehemu kubwa sana ya uchumi wa taifa.

Utashangaa nikikumabia kuwa wabunge 81 wa znz wanatumia kiasi kikubwa kuliko halamshauri moja ya Tanganyika kwa mwaka. Wabunge 81 kwa sh milioni 10 kwa miezi 12 ni sawa na bilioni 9.6.
Ofisi ya waziri mkuu imepewa biilioni 500 kwa halmashauri 54 katika wastani wa bilioni 10 kila moja. Think about it.

Muundo wa sasa unaongelewa na akina Mkandara, mwigulu na Nape hauna maelezo yanayojitosheleza na waka haujibu hoja iwe za Tanganyika au za ZNZ.

Wenzetu hao wanasema tuendelee na S2 kawasababu zina mafanikio. Tukiuliza mafanikio yapi katika lindi la migogoro, hawana majibu. Tunawauliza S2 zinatoka wapi ikiwa kuna ya Zanzibar na ile ya Tanganyika na Zanzibar? Hakuna jibu.
Tukiwauliza inakuwaje miaka 50 muungano una matatizo zaidi kuliko kuimarika? Hakuna jibu.

Tunachokitaka ni kuzinduka kwa Tanganyika kwa ajili ya Watanganyika. Kuna znz kwa ajili ya wazanzbar.
Kusema Tanganyika ndiyo Tanzania ni kuhalalisha wazanzibar watitumie Tanganyika bila kuwa na mafao kutoka kwao.

Hapa tulipofika ambapo znz sasa ni nchi na kila kitu, serikali, utaifa, vyombo vya dola na hata Amir jeshi, hakuna namna Watanganyika watakaa kimya tena. Katiba ya JMT inavunjwa na wazanzibar, bado tuamini kuwa tuna muungano.

CCM wataweza kuzuia kwa kutumia hila na mbinu, mabomu na magrenade. Kitu wasichokijua ni kuwa kuna grievance kuba sana ambayo ni chachu nzuri ya kuvunjika muungano siku yoyote. Hilo litatokea pale Watanganyika watakapochoka kutoa pipi na permende. Na kwa sasa linaonekana wazi.

Njia muafaka ilikuwa kukaa pamoja na kuondoa kasoro husika. Kasoro hizo si kupeleka viongozi na kwaaalika wafunge maonyesho. Ni tofauti za kiuchumi ambazo hugusa maisha ya kila mmoja wetu.

Leo kwanini Watanganyika wakae kimya Wazanzibar wakaitumia mawaziri wao kujigawia nafasi za ajira ambazo kimsingi ni za Tanganyika? Wamekaa makamu wa rais wa JMT, makamu wa pili wa rais wa znz, waziri wa znz wa muungano, wznz wa fedha wa muungano ambao wote ni wazanzibar, wakiwa na waziri mkuu wa Tanzania ambayo znz ipo kujipangia asilimia 21 ya ajira. Hakuna kigezo kinachoelezwa ni kwanini iwe 21. Utashangaa katika zile aslimia 79 wznz wana haki kama Watanzania. Hadi hapo unaona chuki inavyopanda.

Haieleweki kwanini znz ipate asilimia 4.5 ya pato la Tanzania ambalo ni la Tanganyika. Kibaya zaidi haielezwi wazanzibar wanatakiwa kuchangia nini katika muungano. Hakuna asilimia yoyote ya wao kuchangia ila kuna asilimia za wao kuchota

Kule znz kuna ZHSLB ambayo mwanafunzi wa Tanganyika ni marufuku kupata. Wznz hao hao wakija Tanganyika wanapata HESLB bila mikopo a.k.a zawadi. Kwanini sehemu moja iruhusiwe kkuendeleza ubaguzi huku ikijibanza kwa sehemu nyingine kwa kutumia jina.

Zumbe tupo hapa kuwaamsha Watanganyika. Laiti wangejua madhila, dhulma na uhuni wanaofanyiwa na kasehemu kadogo sana kasiko na impact yoyote kwa maisha yao, sidhani kama wangekubali hata mambo 7 ya tume.

Tatizo ni Watanganyika siyo CCM. Inabidi waamke na kutetea utaifa na taifa lao.
Hatuwezi kuwa na muungano uliokwishavunjika.

Waliovunja ni wznz, hivyo tunatakiwa tukusanye mbao ili tujenge jahazi la Tanganyika.
Tuwaache na mamlka kamili, uhuru wa kukopa washington n.k. Sisi tuhangaike na yetu.

Tusemezane
 
WASIKILIZE AKINA ZAMBI
WANATOBOA SIRI ZA MWENYEKITI NA RAIS WA NCHI BILA AIBU WALA HAYA

Kwa hisani ya gazeti la mwananchi.

Mbeya. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya, Godfrey Zambi amefichua sababu za chama hicho kushikilia msimamo wa muundo wa serikali mbili katika mjadala wa Katiba Mpya, akisema ni "maagizo ya mwenyekiti wa CCM".

Mjadala wa Katiba Mpya ulikumbwa na mtikisiko baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kitu alichokiita maoni yake binafsi wakati akizindua Bunge la Katiba kwa kueleza kuwa angependa muundo wa Muungano wa serikali mbili tofauti na Rasimu ya Katiba iliyopendekeza serikali tatu.

Mjadala huo ulivurugika kabisa baada ya kundi la wajumbe kutoka vyama vya upinzani waliounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao likidai mjadala umepoteza mwelekeo kwa kuweka kando maoni ya wananchi ya kutaka muundo wa serikali tatu.

Akifungua mkutano wa Baraza la Utendaji la Umoja wa Vijana wa CCM wa Mkoa wa Mbeya juzi jioni, Zambi alisema mwenyekiti wa CCM alishawaambia kwamba msimamo wa chama ni kuhakikisha zinabaki serikali mbili kwenye Katiba Mpya.

''Vijana sasa lazima niwaeleze ukweli kuhusu muundo wa serikali, ni kwamba piga ua, CCM inataka kuimarisha muundo wa serikali mbili na hili ni agizo la mwenyekiti wetu Rais Jakaya Kikwete," alisema huku akishangiliwa.

Alisema suala la Muungano ni maelewano na kwamba baadhi ya shughuli muhimu za Zanzibar zimehamishiwa Bara wakati nyingine za Bara zimehamishiwa Zanzibar.

Hata hivyo, alisema kero iliyopo kwa sasa kwenye Muungano huo ni namna ya kugawana mapato makubwa ambayo alisema Serikali inaendelea kuyafanyia kazi.

"Rais Kikwete katika kutueleza msimamo wa chama, pia alifafanua vizuri suala la serikali tatu kuongeza gharama za uendeshaji, jambo ambalo hata mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba aliliona, ingawa alifafanua kwamba halina namna," alisema.

Zambi, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, alisema anamshangaa Mwenyekiti wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe anapotamka kwamba serikali tatu ni lazima.

"Vijana wote na wanaCCM mkoani Mbeya naomba muelewe kwamba sisi chini ya mwenyekiti wetu wa CCM, Rais Kikwete, tumeamua muundo wa serikali mbili tu," alisema.

Alisisitiza kwamba kama wachache hawataafiki msimamo huo kwa busara, Serikali ya CCM itaendelea na katiba iliyopo.

Akieleza sababu za msimamo wake wa serikali mbili wakati akizindua Bunge la Katiba, Rais Kikwete alizungumzia gharama za uendeshaji wa serikali tatu akisema katika muundo wa serikali tatu, Serikali ya Muungano haitakuwa na vyanzo vya uhakika vya fedha na kwamba hilo linaweza kusababisha kushindwa kulipa mishahara kama ya wanajeshi na hivyo kusababisha chombo hicho cha dola kuchukua serikali
zumbemkuu , katika bandiko lako uliuliza ni kwanini viongozi wanang'ang'ania S2.
Nilikujibu kuwa sehemu kubwa ya viongozi na wanachama wao hawajui bali wanaelekezwa tu kufuata mkumbo.
Unaweza kumsoma Mwenyekiti Zambi ambaye ni waziri akithibitisha maneno yangu.

Katika hoja za Zambi, moja ni ile anayosema kero iliyobaki ni kugawana mapato makubwa. Inasikitisha sana kuona huyu Mtanganyika yupo tayari kuona kodi za wakulima na wafanyakazi wa Mbeya zinaelekezwa Zanzibar ambako wamekataa muungano na hawautambui si kwa maneno bali hata kuvunja katiba anayoitete Zambi ya mwaka 1977.

Zambi haelewi kuwa unapokuwa na Tanganyika na Zanzibar hakuna kitu kinachoitwa kugawana mapato.
Takwimu zote zinaonyesha Zanzibar haijachangia na haichangii katika muungano kwa lolote lile.
Wapi Zambi anapata ushujaa wa kusema tunagawana mapato?

Tungemuelewa kama angesema tugawane mapato ya Tanganyika na Wazanzibar. Hakuna mahali katika muungano huu ambako Mtanganyika anaweza kusema anafaidika na lolote au chochote kutoka Zanzibar.Si kwa takwimu zozote zile.

Zambi anaendelea kuwadanganya vijana kwa kusema, shughuli zingine za bara zimehamishiwa Zanzibar na Zan zimehamishiwa bara. Hakueleza ni shughuli gani za bara zimehamishiwa Zanzibar. Hizi ndizo hoja za kudanganya vijana wasiokuwa na elimu nao bila aibu wanashangilia.

Vijana hao wanashangilia maumivu yao. Hawajui kuwa wadogo zao wamenyimwa fursa za nafasi na mikopo ili kupelekea znz ambako hawatambui Tanzania. Vijana hawajui kuwa wanalipa kodi katika mishahara na biashara zao ili ziende Zanzibar kufidia bajeti na kuwaletea neema wenzao wao wakiendelea kumenyeka.

Hoja nyingine ya Zambi ni ile ya gharama za S3. Hoja hii tumeijadili sana hapa kuwa kama S3 ni gharama tuonyeshwe unafuu wa S2. Si Mkandara au Nape, Kinana au Chiligati aliyeweza kutuonyesha ukweli wa nafuu za S2. Hakuna hata mmoja anyethiubutu hata kuweka namba. Leo Zambi anasema tu bila takwimu kwasababu katumwa na Kikwete.

Hoja ya gharama inasikitisha. Zambi hajui kuwa mfumo wa S3 si wa wapinzani au watu wengine. Ni mfumo ulioasisiwa na CCM yenyewe. Fikiria hivi:
Kuna Mwenyekiti wa CCM Tanzania
Kuna Makamu mwenyekiti wa CCM tanganyika
Makamu mwenyekiti wa CCM Zanzibar.

Kuna katibu mkuu Tanzania
Kuna naibu katibu mkuu Tanganyika(Migulu)
Naibu katibu mkuu Zaznibar (Vuai)

Hadi hapo CCM haijaona gharama za kuwa na utatu huo wa S3 za CCM.
CCM inaona gharama kwa S3 za Tanganyika, Zanzibar na Tanzania. Zambi hajui kuwa mfumo anaoutumikia ni S3.

Na hoja ya mwisho ni ile anayosema, kama katiba haitapakana basi mfumo uliopo utaendelea.
Zambi, mfumo huo utaendelea katika matatizo makubwa. Itakuwa ni sawa na kuvuta kamba kwa muda mrefu.
Ipo siku kamba itakatika bila taarifa.

Na kwa wenzetu wa Zanzibar, nafasi nyingi za kukidhi malalamiko yenu mumeziacha zikapita.
Hii ilikuwa ni nafasi ya mwisho na nzuri sana ya kupata Zanzibar yenye mamlaka kamili.

Kama mtaendelea kubabaika kama mlivyo sasa, basi mtaendelea kuwa kamkoa ka Tanganyika.
Hatutakubali tena kusikia mkibweka huko Zanzibar. Mtakaa mtulie msikilize wenye nchi wanasema nini.

Mtapewe pipi na peremende kama anavyosema Zambi.
Kama ndicho manahitaji,njooni Dodoma haraka mpewe zawadi kisha mrejee minazini kuendele kubweka na kulia lilia hovyo.

Sisi tunajipanga kuizindua Tanganyika. Tutafanya hivyo kwa gharama zenu na si zetu.
Tuna uwezo huo kwa kila kigezo. Msije kutulaumu maana mtalipa gharama kubwa sana.

Tusemezane

 
MSIKILIZENI ALI SALEHE

ATOA HOJA ZA KUJICHANGANYA


KAMATI YA MARIDHIANO SIX 5 APRIL 2014 UKAWA @ LANDMARK HOTEL PART 4/5 - YouTube

Ali Salehe kama tunavyomjua ndiye kinara wa kuvunja shirikisho la mpira Tanzania akishirikiana na Farook Karim.
Yeye ni mjumbe wa tume ya Warioba anayetetea Zanzibar huru.

Nimedokoa baadhi ya hoja zake muone jinsi Wazanzibar wanavyobabaika na ujio wa Tanganyika, wanavyojitahidi kujificha katika mgongo wa Tanganyika na wanavyoweka mirija yao kuinyonya Tanganyika.

Wanachokifanya wazanzibar ni kutaka kuendelea kuitumia Tanganyika wakiwa hawaitambui Tanzania.

1. Ali Salehe anasema mashirika ya muungano yana mapato ambayo znz inapewa 4.5 na si 50-50 kama washirika.
Well, asichokitambua Ali ni mapato ya mashirika hayo yanatoka Tanganyika.
Kwa mfano, mapato ya shirika la posta znz ni chini ya mara 20 ya mapato ya Tanganyika.
Hapa kugawana 50-50 kunatoka wapi?
Kodi za mashirika ya simu asilimia 99 ni za Tanganyika, 50% kugawana ni kitu gani kama si ukosefu wa weledi

Huwezi kuchukua mali za Tanganyika ukazigawa 50-50 kwa kisingizio cha muungano.

Hoja hii itajichanganya huko mbele kama tutakvyoeleza.

2. Ali Salehe anasema wafanyakazi wa Tanganyika ndio wa muungano, hufanya kazi huko Nyarugusu na kwingine kusikohusu Zanzibar. Anauliza kwanini waitwe wa muungano na si wa Tanganyika.

Well, Ali Salehe anatusaidia kujenga hoja kuwa wale wazanzibar wanaofanya kazi wizara zisizo za muungano na halmashauri zisizowahusu sasa ni muda warudi kwao kwasababu wanafanya kazi sehemu isiyowahusu.

3. Ali Salehe anasema Polisi lisiwe jambo la muungano. Hapa pia anatusaidia kujenga hoja kuwa Tanganyika inapaswa irudi ili znz wawe na askari wao na wale walioajairiwa bara kama sehemu ya utumishi asilimia 21 warudi kwao.
Tunamshukuru sana Ali Salehe kwa kutuonyesha hili.

4. Ali Salehe anasema kutakuwepo na ushirikiano wa mkataba wa sehemu mbili kwa muda fulani.
Akatoa mfano wa elimu ya juu.

Sisi tunasema hatuhitaji mkataba kwasasbabu hakuna sababu za Tanganyika kuhemea znz kwa ka uchumi kake.
Tutakutana EAC na huko tutakuwa na mkataba wa mambo mengi kama ulivyo na nchi nyingine.

5. Anasema znz ni ndogo haiwezi kuchangia 50-50. Angalia hoja namba moja hapo juu ambapo Ali Salehe anataka tugawane mapato ya mashirika 50-50.

Inapofika kugawana wazanzibar wanaijua sana 50%, wakati wa kuchangia wanakimbilia udogo na uchache wa watu.
Huu upuuzi hatutaki, tunasema kama wanataka hadhi na haki lazima wawe na haki na usawa wa kuchangia.
Kinyume chake hatutakubali kunyonywa kwa 50% bila sababu. Hayo Ali Salehe atambue sasa tunayajua

6. Ali Salehe anasema, mapato ya zanzibar yanabaki kule kwasababu kuna wafanyakazi wa Tanganyika kama askari wanaotegemea huduma za hospitali. Well, tazama akili hiyo.

Tanganyika imebeba nusu ya wznz wote duniani.
Wanapata kazi na wanatumia huduma kama elimu na afya na wala hatujalalamika.

Anachokisema Ali Salehe ni kuwa znz ina haki ya kulinda huduma zake, zile za Tanganyika ni zetu wote.
Huu nao ni upuuzi tunaoelekea kuukomesha muda si mrefu. Tanganyika ni kwa Watanganyika na znz ibaki na haki zake.

7. Ali Salehe anasema ardhi iwe ya pamoja. Angalia akili hii.
Hivi znz walioondoa ardhi na kuweka sheria za kumbagua Mtanganyika haikuona jambo hilo.

Hapa anataka kutetea znz kuja kupora ardhi kwa kigezo cha muungano.
Tena anasema eti ardhi ni ya Rais wa JMT hivyo ni ya wote. Kumbuka hapa ni ardhi ya Tanganyika.

8. Ali anasema Rais wa JMT hana haki ya kugawa znz.
Halafu hoja namba 7 anasema rais huyo huyo anamiliki ardhi ya Tanzania.
Ali Salehe ni ardhi ipi ya znz ambayo rais wa JMT hawezi kuigawa halafu ile ya Tanganyika, rais wa JMT aigawe kwa wznz?

Ukiwasikiliza wazanzibar ni kama wamechangikiwa. Hawana hoja za maana za kutushawishi kuwa ndani ya muungano huu kuna faida kwa Mtanganyika. Wanatumia ujanja ujanja na hoja dhaifu kuficha ukweli kama gharama za muungano.

Kama Ali Salehe anataka 50-50 ya mashirika ya mma, kwanini asidai 50% ya jeshi ambayo gharama zake ni bajeti ya znz ya mwaka mmoja na nusu bila kuondoa senti tano.

Ali Salehe anataka Polisi, well, si Polisi tu tunamtaka adai na wanajeshi wake.
Sisi tunatoa ajira kwa wznz na hivyo kuondoka kwao ni faraja kwetu kwetu kwasababu Ali Salehe ameshindwa, narudia ameshindwa kueleza mchango wa znz ni kiasi gani.

Kuna sehemu amesema mchango wa znz ni utakuwa kati ya asilimia 5-8 ya bajeti ya muungano.
Bajaeti yetu bila mikopo au misaada ni trilioni 12.
Kama shirikisho litakuwa na gharama za 1.5 Trilioni kiwango hicho ni kwa asilimia 8 takribani na Bilioni 96

Bilioni 96 wanazotaka kuchangia haziwezi kuendesha idara kama ya ulinzi kwao tu. Leo wanataka hicho ndicho waweke katika kapu la trilioni 1.5 halafu wadai 50%. Haya tunayaangalia na muda ukifika tutakabiliana nayo. Huu ni ukupe usiokubalika.

Bajeti ya znz mwaka 2014/15 ni bilioni 710. Hiyo ni pamoja na kutokuwa na gharama za mashirika ya kimatifa, wizara 4 kubwa n.k.
Na pia ni pamoja na kusaidiwa bajeti yake kwa takribani nusu na Tanganyika huku ikipewa 4.5 ya pato la Tanzania nzima, pato lake likiwa bilioni 400

Ukiondoa yote hayo ni wazi znz kwa bilioni 96 ni sehemu kubwa bajeti imeondoka
Kama hawawezi kulipa bilioni 50 ya umeme kwa miaka nenda rudi, sijui itakuwaje

Kama ni hivyo 50% ya kugawana inatoka wapi. Yaani wachangie 8% tugawane 50% kama si ujinga mtu anieleze n kitu gani
Kwa haraka haraka unaweza kuona ni jinsi gani muungano unavyoiumiza Tanganyika

Uwepo wa Tanganyika utawezesha kuwa na mipango yake bila kubeba zigo la znz.

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3 mimi haya masuala ya muungano yameshanichosha siku nyingi sana sana naomba Mungu atokee mwanasiasa makini auvunjilie mbali huu muungano uchwara.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 mimi haya masuala ya muungano yameshanichosha siku nyingi sana sana naomba Mungu atokee mwanasiasa makini auvunjilie mbali huu muungano uchwara.
Ngongo , usichoke kuuangalia huu muungano.
Ukichoka ni sawa na kuwakabidhi watoto mzigo tuliokabidhiwa miaka 50.

Tumeaminishwa kwa dhati muungano huu ni kwa Tanganyika kuionyonya Zanzibar kiuchumi.Siku hizi hawathubutu kusema.

Msikilize Ali Salehe, mahali pa kuchangia muungano hakuweza kusema jambo hata moja la maana.
Alichokisema ni kuwa kodi inabaki znz ili iwahudumie askari waliopo kule, huo ndio mchango wa znz!!!!
Hawana kingine cha kuseama.

Akizungumzia rasilimali alisema eti Tanganyika haina pia kama znz, hajui kuwa assets ni pamoja na ardhi.
Nani ana uhakika wa kuikopesha znz kwa uchumi wa bilioni 400, eneo na population yake!

Na Ali Salehe anasema lazima kuwe na kusaidiana katika kukopa.
Hapa anakubali ukweli kuwa znz yenyewe haiwezi kwenda kukopa, inachoweza ni kununuliwa.

Huo ndio ukweli ambao wznz hawataki kuusikia. Leo Tanganyika imebeba dhamana ya asilimia 88 madeni ya znz.
Tanganyika inabeba dhamana kwasababu ina assets. Na kwa ujinga wa Watanganyika, znz itakacha deni na kulipitisha kwa Watanganyika kama kawaida.

Ali Salehe ambaye ni key opinion leader kule Unguja, anasema znz inapaswa kuchangia asilimia 5-8 katika muungano.
Halafu kuna sehemu anasema tugawane 50-50. Huu ni uzezeta wa hali ya juu sana. Unaweka 5 unachukua 50.

Kwetu sisi hakuna namna tunaweza kukwepa kikombe hicho cha ukupe isipokuwa kuwa na Tanganyika.
Tunahitaji Tanganyika kwasababu nyingi.
1. Tuwape wznz nafasi ya kuendesha nchi yao kwa uhuru bila kuwaingilia.
2. Watupe nafasi ya kupanga mipango yetu bila vurugu zao
3. Kila mmoja atumie rasilimali zake kwa watu wake.

Huu muungano ambao mmoja amedandia akisubiri mgao ni ukupe, tuukatae.
Akina Nape wanafahamu wanachokifanya ni kutetea matumbo yao tu.
Wanapitisha matatizo kwa watoto wetu, wao wana uhakika kupitia propaganda wataendelea kunufaika.

Ni wajibu wetu kusimama na kuwaambi wabunge sasa tunataka Tanganyika.
Hatuhitaji kupoteza muda na fedha zaidi kujadili namna ya kuwasaidia wznz kama ilivyo sasa katika bunge la katiba.
Hatuhitaji ku-accomodate matatizo ya wznz kwa gharama zetu, tuna matatizo ya wananchi wetu.

Kama wanataka waje kwa nidhamu ana adabu tuwasaidie si suala la kuungana.znz haina uwezo wa kuendesha wizara moja ya muungano,tumeungana nini kama si kuwasadia?

Kuna video Ali Salehe anashukuru kwa miradi ya Tanganyika kufeli.
Huyu anayeshangilia anguko la Tanganyika tunaendelea kumsikiliza tu.

Tena bila haya anatetea uvunjifu wa katiba na kusema znz wamelazimisha.Y
aani wanalazimisha uvunja katiba yetu na bado tunawaangalia tu.

Hapa kuna jibu moja, Tanganyika izinduke, wakitaka yawepo mambo 7, ima hawataki wasije Dodoma August 5.

We don't need znz kwa lolote zaidi ya kubeba mzigo usio na manufaa kwetu. Hatuwahitaji kwa lolote huo ni ukweli.
Wametambua kuwa hatuwahitaji na sasa wanang'ang'ania muungano.

Hatuwahitaji kwasababu hakuna mafao ya aina yoyote tunayopata kutoka znz.
Huo ukweli wanautambua sasa na tuna jeuri ya kuwaambia njia nyeupee bila majibu.
 
nguruvi,
Mkuu inaposemwa 50 -50 ina maana tofauti na unavyofiiria wewe, Ni kwamba (mfamo) kama wewe unaingiza mil 200 ukatakiwa kutoa asilimia 10 ya mauzo hayo kama kodi basi na yule anayeingiza mil.100 atatakiwa pia kutoa asilimia 10 ya pato lake. Na hivyo huyo Saleh nadhani kasahihisha tu ukweli uliopo ya kwamba Zanzibar hupewa 4.5 na sio 50 -50 ya mapato ya mashirika maana wengi wanadhani ya kwamba kama zimekusanywa bil.100/ basi mgawanyo ni 50-50.

Sioni kigumu kipi kuelewa hapo..
 
nguruvi,
Mkuu inaposemwa 50 -50 ina maana tofauti na unavyofiiria wewe, Ni kwamba (mfamo) kama wewe unaingiza mil 200 ukatakiwa kutoa asilimia 10 ya mauzo hayo kama kodi basi na yule anayeingiza mil.100 atatakiwa pia kutoa asilimia 10 ya pato lake. Na hivyo huyo Saleh nadhani kasahihisha tu ukweli uliopo ya kwamba Zanzibar hupewa 4.5 na sio 50 -50 ya mapato ya mashirika maana wengi wanadhani ya kwamba kama zimekusanywa bil.100/ basi mgawanyo ni 50-50.

Sioni kigumu kipi kuelewa hapo..
Umesikiliza video yake vizuri lakini. Yeye alichosema ni kuwa mashirika ya umma yanapata mapato na ilipaswa kugawiwa 50-50. Kinyume chake ZNZ inapewa 4.5% uonevu.
Hakusema inapata 50%, alichosema ilipaswa ipate 50-50 lakini inafanyiwa hiana


Anachozungumzia Ali Salehe ni kugawana si kutoa kama ulivyoelewa.
Msikilize vizuri.
 
Umesikiliza video yake vizuri lakini. Yeye alichosema ni kuwa mashirika ya umma yanapata mapato na ilipaswa kugawiwa 50-50. Kinyume chake ZNZ inapewa 4.5% uonevu.
Hakusema inapata 50%, alichosema ilipaswa ipate 50-50 lakini inafanyiwa hiana


Anachozungumzia Ali Salehe ni kugawana si kutoa kama ulivyoelewa.
Msikilize vizuri.
Kama kasema hivyo ndiyo haya ya UKAWA ambao mnawashangilia kuundwa kwa serikali 3 wakati tatizo la mgawanyo litaendelea kuwepo kwa sababu wanavyo amini wao, ushirika lazima watu wagawane 50 kwa 50 ya mapato hata kama wamechangia asilimia 2 wakapewa mara 4.5 zaidi ya walichochangia bado kwao hazitoshi. Na ndio maana kila mara nakukumbusha ya kwamba hawa watu wa aina hii hawataridhika na lolote kwani serikali 3 bado haina jibu la hoja kama hii na hatuwezi kuwa na serikali kuu isokuwa na vyanzo vya mapato.

Mtu wa aina hii ni kumuelimisha kwanza maana hajui asomacho wala haelewi huu mfumo wa Kijamaa unafanya kazi vipi ktk dunia ya leo zaidi ya kufikirika. Na kinachosababisha yote haya ni mfumo mbovu wa utawala ambao yeye anashindwa kuelewa kwamba ile asilimia 95.5 anayoitolea macho ya serikali ya JMT bado Zanzibar inahusika ktk mambo ya Muungano ambayo Zanzibar ina wabunge wake na mawaziri wake ndani na wizara zake huko Zanzibar. Inayopewa asilimia 4.5 ni serikali ya Zanzibar yenye wabunge na mawaziri wake tofauti na wale wa JMT kwa mambo yao yasokuwa ya Muungano na ktk ile ya Muungano na miradi ya maendeleo Zanzibar bado inanufaika kutoka mfumo wa Taifa.

Kosa kubwa linalofanyika ni Zanzibar kutokuwa na mamlaka yake kamili ili kodi zinazokusanywa na mashirika haya ziingine moja kwa moja ktk mfumo wa serikali hiyo kwa asilimia tuseme 10, halafu zile zinazokusanywa bara pia asilimia 10 iwe ya bara na asilimia inayobakia ndio iwe ya Mfuko wa Taifa, na hii ndio itakayo jadiliwa ni miradi ktk gani ya maendeleo Kitaifa fedha hizo zitumike ambako hutakuwa na asilimia tena bali miradi gani inahitajika na kwa sehemu gani ili kuongeza pato la Taifa.

Hata mfanya biashara huwekeza pale penye kuzalisha akijua soko liko wapi. Huwezi kwenda kuuza samaki Pemba zinakuvuliwa, bali utawekeza Pemba ktk miradi ya Uvuvi kwa kuelewa soko liko Bara, hivyo Pemba lazima wafaidike na mazao yanayouzwa bara na sii kwamba maadam samaki wameuzwa bara basi hili ni pato mla Bara. Ndio hapa tunajikuta na matatizo ya Gas ya Mtwara maana hawafaidiki nayo! Tazama Nigeria Mafuta yanachimbwa kusini lakini wanaofaidika ni Kaskazini ilihali mauzo yanafanyika nje ya nchi hiyo! sio kweli kunakouzwa kitu ndio wanaokusanya mapato zaidi isipokuwa wanaozalisha ndio wanatakiwa kufaidika zaidi kwa kila kinachouzwa nje.

Mfumo huu unawezekana tu tukipata kaitba mpya ikiwa mambo yote yatakuwa ya Muungano.
 
Kama kasema hivyo ndiyo haya ya UKAWA ambao mnawashangilia kuundwa kwa serikali 3 wakati tatizo la mgawanyo litaendelea kuwepo kwa sababu wanavyo amini wao, ushirika lazima watu wagawane 50 kwa 50 ya mapato hata kama wamechangia asilimia 2 wakapewa mara 4.5 zaidi ya walichochangia bado kwao hazitoshi. Na ndio maana kila mara nakukumbusha ya kwamba hawa watu wa aina hii hawataridhika na lolote kwani serikali 3 bado haina jibu la hoja kama hii na hatuwezi kuwa na serikali kuu isokuwa na vyanzo vya mapato.

Mtu wa aina hii ni kumuelimisha kwanza maana hajui asomacho wala haelewi huu mfumo wa Kijamaa unafanya kazi vipi ktk dunia ya leo zaidi ya kufikirika. Na kinachosababisha yote haya ni mfumo mbovu wa utawala ambao yeye anashindwa kuelewa kwamba ile asilimia 95.5 anayoitolea macho ya serikali ya JMT bado Zanzibar inahusika ktk mambo ya Muungano ambayo Zanzibar ina wabunge wake na mawaziri wake ndani na wizara zake huko Zanzibar.

Inayopewa asilimia 4.5 ni serikali ya Zanzibar yenye wabunge na mawaziri wake tofauti na wale wa JMT kwa mambo yao yasokuwa ya Muungano na ktk ile ya Muungano na miradi ya maendeleo Zanzibar bado inanufaika kutoka mfumo wa Taifa.

Kosa kubwa linalofanyika ni Zanzibar kutokuwa na mamlaka yake kamili ili kodi zinazokusanywa na mashirika haya ziingine moja kwa moja ktk mfumo wa serikali hiyo kwa asilimia tuseme 10, halafu zile zinazokusanywa bara pia asilimia 10 iwe ya bara na asilimia inayobakia ndio iwe ya Mfuko wa Taifa, na hii ndio itakayo jadiliwa ni miradi ktk gani ya maendeleo Kitaifa fedha hizo zitumike ambako hutakuwa na asilimia tena bali miradi gani inahitajika na kwa sehemu gani ili kuongeza pato la Taifa.

Mfumo huu unawezekana tu tukipata kaitba mpya ikiwa mambo yote yatakuwa ya Muungano.
Mkuu kama umeangalia video za ZIRPP n.k. utabaini kuwa hakuna uwezekano wa kuwa na mambo ya pamoja. Umemsikia Ali Salehe akitamba kwamba wana ZBS, Baraza la mitihani n.k. Katika hali hiyo unawezaje kuwa na mambo ya muungano ya pamoja ukabaki salama? Si kila mara nakuambia kuwa tulifikia 22 ambayo ni 47, si hayo ndiyo yanaleta matatizo, je unataka turudi kule kule?

Pili,Kutoridhika ni upungufu wa weledi kwa wazanzibar. Umimi na ubinafsi ni sehemu ya utamaduni wao. Walipokimbiza mafuta na gesi ni umimi, leo unataka mambo yote yawe ya muungano! white elephant, si mzanzibar.

Tatu, S3 zina suluhu. Kwanza tunatenga mambo yote yanayotuhusu na kuwahusu wao. Kisha tunaangalia gharama za mambo hayo ambayo kwasasa ni 7. Baada ya hapo kila mmoja anakuwa na uhuru wa kufanya atakalo.

Nne, Kama unakubali kuwa znz inatakiwa iwe na mamlaka kamili, basi lazima Tanganyika izinduke. Huwezi kuwa na Zanzibar na JMT. Nitakuwekea video inayoonyesha wznz wanavyopigania jina la NIA.
Hivyo huwezi kuwa na Zanzibar halafu ukasema eti ichangie 10% na Tanganyika isiyokuwepo 10%

Kibaya zaidi unataka 90% ya Tanganyika uifanye 100% ya Tanzania. Tunajua kuwa 10% ya mapato ya znz ni bilioni 40.
10% ya mapato ya Tanganyika ni 1.2 Trilioni. Ukisema Znz ichangie 10 ya pato lake una maana bilioni 40 na Tanganyika Trilioni 1.5. Halafu unachukua 90% ya Tanganyika unaifanya Tanzania ili kugawana na znz isiyo na lolote katika 90%.

Mkuu hapa hapakubaliki, na yanaongeza chuki kubwa. Yakitendwa kiuhuni uhuni hakuna namna bali kuingia mitaani na kuondoa udhia na kadhia kwa namna yoyote. Watanganyika wameamka na wala usione wapo kimya ukadhani wameridhika.
Haya mambo yatakuja fumuka watu wakakimbizana mitaani hovyo. Ni fact tu wala usigope mkuu

Hatuwezi kuumiza watu wetu ili kuwafurahisha wzn Mkandara. Tunaweza kuishi bila wazanzibar na hakuna kitakachopungua kwetu. Hatuwahitaji hivyo hatuna sababu za kuumiza walipa kodi wetu kwa ajili yao.

Kama hawaridhiki na wanachoipata sasa ambacho ni msaada, wasije August 5 kwenye BML waone kama tutawabembeleza.
Mkandara zile zama za wazanzibar kutisha kuvunja muungano zimekwisha.
Sasa hivi tunawaambia wazi kuwa kama hawataki njia neyupee., we don't need them! period.

Nadhani umeona walivyoufyata. Hatuwezi kusimamisha maendeleo ya nchi yetu tukiwajadili kila siku.
Tunasisitiza kwa dhati kuwa hata leo wakaitaka waondoke, hatuna sababu nao wala nchi yao, hatuna kabisa.

Nimekuuliza mara nyingi sana,. tunafaidika nini na uwepo wa Zanzibar.
Na kwanini wao wanaotaka mamlaka kamili wasiondoke ikiwa kila mlango upo wazi kabis kwao

In fact S3 ni kuwasaidia tu, in worst case scenario muungano ufe tu, hatuna tatizo, wanalo tatizo na wala si kazi yetu kutatua matatizo yao.

Hatuna hofu ya aina yoyote wala hatuwahitaji kwa mkataba au jambo lolote.
Tutakutana EAC . Narudi Mkandara tuambie tunawahitaji wazanzibar kwa lipi, kwanini na kwa faida ipi.

Tueleze, kama hakuna basi waambie wawe na adabu maana tunawasiaida hatukuungana.

Wazanizbar wasiseme wanataka muungano wa haki na usawa. Tunawaambia kuwa hatukuungana, bali tunawasaidia.
Kama wanadhani hawana haki na hawapati usawa, njia nyeupee waondoke.
 
Back
Top Bottom