Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

WHATTSUP, FACEBOOK ZATUMIKA KUKAMILISHA UHUNI
BORA LIENDE, TUMALIZIE MAJENGO YETU, KATIBA SHAURI YAO

NCHI INAELEA KAMA BOYA,KILA MMOJA KIONGOZI.
WENYE MAJUKUMU WAJIFICHA, WASUBIRI MWANYA WAENDELEZE UNAFIKI

Katika mahoka nzuri ndani ya bunge la Sitta linalokamilisha rasimu ya CCM ni hili la kupiga kura.
Dunia ilijua muda wa kwenda Hija kwa Waislam katika kalenda na taratibu za Dini kwa yoyote anayeshughulisha akili
Hilo lilipaswa lidahamike ili ratiba isiingiliane nalo. Vipi walijua uwepo wa bunge la bajeti, wasijue kuna ibada ya Hija?

Ili kukamilisha uhuni mjini Dodoma, Sitta akaamua Mahujaji wapige kura kwa kutumia Whattsup na facebook.

Hakuna anayejua huko whattsup nani ana verify kura hizo, achilia mbali ukiuakwaji wa sheria za nchi.
Sitta kaagiza, Pinda waziri mkuu akishuhudia tena kwa vimemo, na Rais wa nchi yetu akiwa safarini kusaka misaada

Kanuni za asili zikagoma kukubaliana na Sitta. Mbinu mpya ikatangazwa kuwa wapo wabunge wa UKAWA waliotaka kupiga kura.
Hili lilitangazwa baada ya kugundua kura za facebook na whattsup hazikamilisha azma ya uovu.
Waovu ni wazuri na mahiri wa mbinu. Sitta awali alisema walitaka kupiga kura ni UKAWA 25.

Jana wakati wanajadili uhuni, Sitta akasema zimepatikana kura 2. Hakusema katika 25 ngapi zimesema hapana.

Wait a minute! hapa kuna jambo pia, Sitta na CCM walitumia zaidi ya wiki 2 kukataa kura ya siri.
Baada ya kubaini facebook na Whattsup hazitaleta matokeo mema ya uovu, ndipo likaja suala la kupiga kura kwa siri.

Suala lile lile CCM ililokataa tena chini ya waovu kama Sitta na Chenge.
Leo wamegeuka eti wanahifadhi majina ya hao UKAWA. Samwel hana sababu za kuhifadhi majina, yeye alitakiwa asimamie kanuni za chama chake za kura za wazi ili katiba yao ya CCM itimie. UKAWA hawapo sasa kura za siri za nini?

Tena kura hizo za siri ni 2 ili kukamilisha uovu. Mzee Sitta ameshindwa kuelewa hata mtoto wa kidato cha II C, asingeweza kufanya mbinu za kitoto, kipuuzi na kihuni kama alivyofanya.

Hivi leo ni mwendawazimu gani ataamini kuna watu 2 walipiga kura ya siri.

Ingefaa kama angesema 30 wamepiga kura, au 75 maana hakuna wa kuthibitisha hilo.
Ni suala la Sitta kuamua anataka nini kukamilisha uovu wake.

Mtu kama Sitta anapotuma vimemo vya kutumia pesa za umma kununu kura, inaeleza bila kificho jinsi taifa hili linavyojiongoza kwa kutumia nguvu za jua na mizimu na si zakili za watu. Kuna akili gani katika ujinga uliokamilika Dodoma hata kama ni katiba ya CCM.

Rais wa nchi yupo kimya akisubiri kutoa vyeti kwa wahuni waliomaliza kazi ya kihuni kwa sababu ya uhuni wa CCM

Yote hayo yamefanyika ili kuzuia muundo uliopenedekezwa na tume.

Hivi nani alitegemea mtu kama Andrew Chenge akubali maadili ya uongozi?
Yeye akikubali tutarajie atatumia mbinu gani kuhamisha fedha kwenda visiwa wa Jersy!!

Katika kundi linalotia simamzi ni la vijana. Nao wameungana na wazee wahuni kufanya uhuni katika katiba ya chama chao.

Wamekubali kukaa kimya, wakasokomezwa matambara midomo! yes, tunaambia taifa linahitaji vijana. Ni hawa tuliowaona Dodoma.

Kama tunahitaji vijana wazoefu hawa wa Dodoma ni muhimu sana.
Wamepata uzoefu wa kufanya uhuni, kutumia teknolojia katika uovu, na hata mizimu kupiga kura, isipokuwa baadhi ya mizimu iliyopuMzika kwa amani na sasa inahangaika kuliona taifa likitumbukia katika sintofahamu kubwa.

Wengi wanasema Nyerere alifeli katika baadhi ya mambo, sasa jiulizeni angeweza kufaulu vipi ikiwa wananchi wanagundua waliokuwa wamemzunguka mwalimu na akina Sitta.

Hawa waliomba Mwalimu atoweke ili watimize haja zao ovu.
Leo wanashangilia na mizimu ya Nyerere inabubujikwa na machozi.

Laana hiyo haitawaacha salama. Mbele ya safari tunaweza kumsikia Sitta katika vichwa vya habari.
Tutamsikia wakati anakwenda kuungana na Charles Tailor kule the Hague.

Tunaweza kumsikia Sitta akiwa Nairobi ili kuungana na Rauto na wenzao kwenda the Hague
.
Na safari ya the Hague ikitokea(Mungu apishilie mbali madhara yake kwa wananchi) taifa hili litakuwa la majuha kama Sitta hatapewa ticket ya first class.

Uhuni wa CCM umekamilika, na wala hakuna tatizo.
Tatizo litakuja pale watakapotaka kuingiza uhuni huo kama nyaraka ya taifa. Hapo kutakuwa na tatizo.

Tusemezane
 
With due respect, hakuna demokrasia Tanzania
Namsikitikia sana Raisi Kikwete kwa kuacha Legacy moja mbaya sana nyuma yake, ya Katiba ya "kuwalazimishia" Watanzania.

Bora Nyerere na wenzao waliotupa katiba ya mwaka 1977 kwa kuiandika wao na huku wakikiri hivyo. Kuliko huyu anayetusakamizia katiba ya "CCM" huku akijifanya eti imetokana na Wananchi!!.

Honestly binafsi siwezi kumpa Kikwete credit za katiba mpya, ambayo ni dhahiri 2/3 ya Wazanzibari imechakachuliwa!
Kibaya zaidi rekodi zipo, na ni uthibitisho wa kizazi kijacho kwamba muungano huu, na serikali mbili zinalindwa kwa hila!

BINAFSI NINAUNGA MKONO SERIKALI MBILI, LAKINI SI "BY ANY MEANS NECESSARY", NATAKA ZIPATIKANE KWA HAKI, NA KWA WATU KURIDHIA SI KWA KULAZIMISHA!!!
 
Last edited by a moderator:
Kwanini tunalazimisha kutetea ulaghai? 3 zitakazopatikana kwa mindset hii ya KUKOMOANA/TUONE SASA, na 2 zitakazopatikana kwa fikra hizihizi za mtawala na koloni lake, na hoja nyingi za kizembe kama kulinda identity yetu/yao, zitakuwa na masilahi gani kwa Mtanzania (si mtanganyika/mzanzibar), hivi ni kweli hatuoni Utanzania ukienea madoa machafu tena hata ya damu? Iwe 3 au 2, je hatuoni Utanzania ukijenga matatizo kwa Mtanganyika na Mzanzibar? Kwanini watu hawa wawili wagombane kisa Utanzania? Kama tumeamua ku-take risk ni kwanini isiwe kwa Moja (1) na si 2 wala 3?

Hivi ni kweli kuna watu hawaoni umuhimu wa serikali 1 over 2 na 3 ukitanguliza ustawi wa mtanzania? Kwanini kipaumbele chetu kiwe muungano badala ya maslahi ya umma? Je kuna mtu haoni umuhimu wa kuvunja muungano kama serikali 1 inashindikana? Hivi tumegundua ilivyo shida kumuelewa mtu anayetaka serikali 2? Je, tumegundua shida inayokupata unapotaka kumuelewesha mtu juu ya serikali 3? NI KWA VILE TUNAJARIBU KUTETEA UONGO KUWA UKWELI, na ili uongo uonekane ukweli hauna budi kukwepa baadhi ya mizani ya ukweli, huo ni UBATILI. Sasa kwanini tunalazimika kuishi ulaghai? Ni kwa faida ya nani? KWANINI TUSIISHI TUNACHOKIAMINI? Ili tuweze kusema HAPANA, basi hatuna budi kuishi facts. Ukweli ni kwamba, HAKUNA MUUNGANO/UMOJA BILA KUJIKATAA, kukataa individualism.

'1 AU UFE' tunapinga kwa hoja zipi? Je, ni kwakuwa tumezuiwa kujadili? Kama tunataka wananchi waseme HAPANA, aje watatuelewa wakati sisi tumeshindwa kusemea Hapana hilo dogo tu? Je, hapana tuitakayo ni selective kiasi hicho? TUISHI UKWELI SASA, SI KILE TUSICHOKIAMINI.
Anaita sasa!
 
UnaweZa kufafanua jinsi gani serikali Mbili zinaweza kupatikana kwa Haki na maridhiano?

Cc Mag3, JokaKuu, Nguruvi3, Bongolander, Dingswayo, chama, MwanaDiwani, JokaKuu

Sent from my iPhone using JamiiForums

Nadhani mchambuzi utakuwa unazungumzia usanii uliofanyika bungeni baada ya kuonekana kuwa serikali mbili haziwezi kupatikana kwa haki. Naona sasa tuangalie hatua zinazokuja.

Lakini uzuri ni kwamba hata ndani ya CCM sauti ya haki this time imesikika zaidi kuliko huko nyuma.
 
Kwanini tunalazimisha kutetea ulaghai? 3 zitakazopatikana kwa mindset hii ya KUKOMOANA/TUONE SASA, na 2 zitakazopatikana kwa fikra hizihizi za mtawala na koloni lake, na hoja nyingi za kizembe kama kulinda identity yetu/yao, zitakuwa na masilahi gani kwa Mtanzania (si mtanganyika/mzanzibar), hivi ni kweli hatuoni Utanzania ukienea madoa machafu tena hata ya damu? Iwe 3 au 2, je hatuoni Utanzania ukijenga matatizo kwa Mtanganyika na Mzanzibar? Kwanini watu hawa wawili wagombane kisa Utanzania? Kama tumeamua ku-take risk ni kwanini isiwe kwa Moja (1) na si 2 wala 3?

Hivi ni kweli kuna watu hawaoni umuhimu wa serikali 1 over 2 na 3 ukitanguliza ustawi wa mtanzania? Kwanini kipaumbele chetu kiwe muungano badala ya maslahi ya umma? Je kuna mtu haoni umuhimu wa kuvunja muungano kama serikali 1 inashindikana? Hivi tumegundua ilivyo shida kumuelewa mtu anayetaka serikali 2? Je, tumegundua shida inayokupata unapotaka kumuelewesha mtu juu ya serikali 3? NI KWA VILE TUNAJARIBU KUTETEA UONGO KUWA UKWELI, na ili uongo uonekane ukweli hauna budi kukwepa baadhi ya mizani ya ukweli, huo ni UBATILI. Sasa kwanini tunalazimika kuishi ulaghai? Ni kwa faida ya nani? KWANINI TUSIISHI TUNACHOKIAMINI? Ili tuweze kusema HAPANA, basi hatuna budi kuishi facts. Ukweli ni kwamba, HAKUNA MUUNGANO/UMOJA BILA KUJIKATAA, kukataa individualism.

'1 AU UFE' tunapinga kwa hoja zipi? Je, ni kwakuwa tumezuiwa kujadili? Kama tunataka wananchi waseme HAPANA, aje watatuelewa wakati sisi tumeshindwa kusemea Hapana hilo dogo tu? Je, hapana tuitakayo ni selective kiasi hicho? TUISHI UKWELI SASA, SI KILE TUSICHOKIAMINI.
Anaita sasa!
Nadhani suala la katiba ikiwemo muundo wa muungano ni muhimu sana.
Umesema lazima tuangalie masilahi ya wananchi. Ni kweli, lakini pia tuwe na muongozo wa kuangalia masilahi yao. Hatuwezi kusema S3,S2 bila kutaja masilahi ya wananchi.

Muundo wa muungano ni muhimu sana katika kutetea masilahi hayo.
Katika nyuzi nyingi tumeonyesha kwa uhakika namna muungano ulivyoshindwa kutetea masilahi ya wananchi, hivyo hatuwezi kutetea masilahi ya wananchi bila muundo na muongozo sahihi.

Umuhimu wa S1 unaonekana, kinachotawala ni ubinafsi na masilahi ya wananchi.
Na hapa nisema tatizo ni znz ambao wapo tayari kulinda masilahi yao kwa gharama za Mtanganyika.

Hapo hakuna haki, na haki ikikosekana hakuna upendo. Suala la S1 ni mfu na halijadiliki tena kwa msingi huo.
Pengine katika hoja zako ungeongeza hoja kuwa kama hatuwezi kuishi kwa kuaminiana kwanini tusivunje muungano?

Nasema hivyo kwasababu unapokuwa na kidonda kinachotishia uhai wako kuna nyakati inabidi ukubaliane na madaktari, mguu au mkono ukatwe. Ni radical solution lakini yenye matokeo mazuri.

Pengine znz na Tanganyika leo zinmgekuwa zinajadili namna ya kuwahudumia wananchi wao katika kuondoa ujinga, maradhi na umasikini. Kwanini tuhangaike na dude ambalo basically hatuoni umuhimu wake kama hatwezi kukubaliana

Mchambuzi kauliza, ni njia gani tunaweza kuwa na serikali mbili za haki?
Hapa naongeza kidogo, muungano upo miaka 50 na hakuna solution, haki hiyo inapatikanaje katika mazingira tuliyo nayo. Gamba la Nyoka tusaidie hili

Bongolander kwakweli hata CCM wanaona aibu kwa uhuni uliofanywa.
Hoja kubwa waliyo nayo ni kutumia ignorance ya wananchi hasa wa vijijini kupata uhalali wa uharamu huo.
Kwa CCM kikwazo kulikuwa BMK ambalo lilikufa llikabaki la CCM.

Ninachojua kwa uhakika tutaandika katiba nyingine soon.
Waliokuwa Dodoma wanajua ukweli kilichofanyika ni wao kukubaliana na uongo ili wapate allowance za kumalizia majengo yao.

Tutaandika katiba upya iwe kwa njia za amani au zenye gharama kubwa, katiba itaandikwa tena.

Hakuna utawala uliowahi kushinda hoja na nguvu za umma.
Si Shah wa Iran, Si Marcos, Pincot, Ceussicue wa Romani au awaye.
Wote walikuwa na nguvu za dola kama CCM wanavyotumia majeshi.

Nchi haiongozwi kwa maguvu inaongozwa kwa utangamano, na hapo ndipo CCM walipopotoka.

Gamba la Nyoka, Kikwete legacy yake inazidi kujieleza.
Na hakika kila jambo lina pande mbili, ubaya na uzuri.
Mchakato umetupa picha ambayo wengi walikuwa hawana uhakika nayo.

Picha hiyo ni ile ya kwanini sisi ni masikini, kwanini inasemwa uongozi uliopo ni dhaifu, kwanini majirani wanatutenga na kwanini tumepoteza nuru yetu kimataifa.

Tukiangalia uongozi wa Kikwete na jinsi alivyoshindwa management ya ''familia yake Tanzania'' hakuna shaka tumerudi nyuma miaka 30. JK hana legacy nyingine zaidi ya hii mbovu iliyoondoa hata ile ndogo aliyokuwa nayo.

Rais wa nchi anapokaa kimya uhuni ukifanyanyika, anapocheza doubel agent na anapokuwa ndumila kuwili, si kuwa ni tatizo la demokrasia tu bali lazima tulale macho maana hata usalama wetu unatia mashaka sana.

Hatua zinazokuja ni kuendelea kupinga uhuni.
Ninapendekeza haya

1. Kwanza kutojadili rasimu hiyo kabisa. Hiki ni kitu haramu na kuendelea kukijadili ni kutoa uhalali katika uharamu. Huwezi kujadili haramu. Hivyo wananchi waache kabisa kuijadili

2. Wananchi wajadili zaidi uhuni na namna ulivyotendeka ili kuwaambia akina Sitta kuwa hatupo tayari.
Pengine watatumia Polisi lakini nasisitiza, hakuna dola iliyowahi kushinda nguvu ya umma.

3. Madai ya katiba ya Tanzania yaendelee. Hatua za awali zilikamilika ikiwa ni pamoja na tume kuwasilisha maoni ya wananchi. Hapo ndipo wananchi wanapaswa kusisitiza na kujadili.

4. Vyama vya upinzani viache knee jerk reaction ya kuzungumzia rasimu ya CCM.
Vielekeze nguvu zao katika haya
a) Kwanini waliondoka na nini kiliwasukuma kuondoka.
b) Rasimu ya Warioba ilikuwa na nini ambacho wao wanakiona kilikuwa bora kutoka kwa wananchi
c) Kwanini CCM wamechakachua rasimu ya Warioba
d) Kwamba kilichofanyika Dodoma si maoni ya wananchi ni maoni ya wana CCM wengine kama Sitta na Chenge wakiwa katika mashaka ya uadilifu wao kwa kiasi kisichovumilika

e) Madai ya katiba mpya yaendelee kwa nguvu kuliko wakati mwingine
n.k.

Elimu ya umma itasaidia sana katika hili, na sote ni wadau wa elimu hiyo
 
Hakika Mkuu Nguruvi3, na hicho ndicho nilichomaanisha, ndio maana niliuliza JE KUNA MTU ASIYEONA UMUHIMU WA KUVUNJA MUUNGANO KAMA SERIKALI MOJA INASHINDIKANA? Pia nimesema kuwa ili kuunda umoja haina budi kwa pande zote kujikataa. Ni wazi Mzanzibari hayupo tayari kwa hilo, yaani mbali ya Utanzania bado anataka atumie Uzanzibari wake kudai maslahi ya Utanzania 'special care', ni upuuzi kiasi gani huu?

Mantiki hairuhusu mjadala wa muundo wa serikali kufikia masilahi ya umma, Mantiki inasema 1 au UFE, mjadala si wa muundo tena, ila aidha tunakubaliana KUJIKATAA pande zote au TUUVUNJE. Sasa kama nguvu tunazotumia kushawishiana juu ya S2 na S3 zingetumika katika Mantiki hii ya 'S1 AU UFE' tungefikia wapi hadi sasa?
Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom