Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

Mkandara,

Mimi naona kuna mjadala mpana sana kuhusu hiyo mifumo unayojadili au kupendekeza hapa. Kwani unaposema kuwa kila jambo liwe la muungano kuna mengi sana ya kujadili katika kuchambua faida zake na khasara zake kwa nchi hizo mbili huru zilizoamua kuungana.

Mjadala huo utajikita zaidi katika nyanja hizi:
1. Kiuchumi
2. Kijamii
3. Kisiasa
4. Kiutawala

Sasa mimi ushauri wangu kwako NI KUWA TUWEKE UZI MAALUM WA KUJADILI HOJA YAKO YA KILA KITU KIWE MAMBO YA MUUNGANO ili tupate muda na nafasi pana katika kujadili katika mada husika kuliko hapa katika uzi huu.
Kwani kwa kufanya hivyo nafikiri wengi sana watanufaika na kufaidia na mada hiyo. Na nataraji itakuwa ni moja ya mada bora sana katika barza hii kuhusu muungano kama watu wote watakaochangia watapunguza jazba, chuki na kuweka kando ushabiki na kujikita katika kutengeneza FACTS na hoja zenye mashiko
.

Upande wangu insh'Allah japo nipo Ziara ya ibada hapa Madinat munawar lakin nitatafuta muda kuweka uzoefu na maoni yangu kuhusu utaratibu huo insh'Allah.

hayo ni maoni na ushauri wangu kuhusu hilo kwa nia ile ile ya kuilimishana na kuhabarishana ikiwemo kupeana mawazo na uzoefu mbalimbali kwa faida yetu sote.

Nikutakia siku njema.

Shukran ningekuomba wewe anzisha mada hiyo maana sielewi haswa unapokwazwa ama wanapokwazwa wengine. Maana ieleweke tu ya kwamba unapofanya mambo yote ya Muungano ina maana kila kitu kinaelezwa kwa ufasaha wake ktk Katiba ya nchi hivyo sheria za nchi zinapotungwa haziathiri sheria mama. Kuacha mambo mengine sio ya Muungano inaleta nchi moja inaweza kuandika na kupanga masharti wapendavyo ktk katiba yao maadam jambo hilo sio la Muungano.
 
Kuacha mambo mengine sio ya Muungano inaleta nchi moja inaweza kuandika na kupanga masharti wapendavyo ktk katiba yao maadam jambo hilo sio la Muungano.
Mkuu wangu hakuna athari zozote zinazoweza kutokea.

Kwasasa Zanzibar ina katiba yake na inaweka, kuondoa, kuvunja, kubagua n.k. hakuna kilichoharibika, vipi uone ujio wa Tanganyika ndio tatizo? Kwani huoni masharti ya katiba ya znz ya 2010 ilivyoandikwa 'wapendavyo' na tukiuliza tunaambiwa si jambo la muungano.

Tukiuliza, wewe Mkandara unasema ni haki yao. Tukiuliza unasema wao ni wachache n.k.
Hujaweza kukemea wlichofanya wznz unaanza kukemea kisichokuwepo! mkuu wangu !

Tanganyika ikizinduka, sheria zitawiana, ya upande mmoja sawa na mwingine. Hakutakuwa na mgogoro wa aina yoyote ile!
 
Shukran ningekuomba wewe anzisha mada hiyo maana sielewi haswa unapokwazwa ama wanapokwazwa wengine. Maana ieleweke tu ya kwamba unapofanya mambo yote ya Muungano ina maana kila kitu kinaelezwa kwa ufasaha wake ktk Katiba ya nchi hivyo sheria za nchi zinapotungwa haziathiri sheria mama. Kuacha mambo mengine sio ya Muungano inaleta nchi moja inaweza kuandika na kupanga masharti wapendavyo ktk katiba yao maadam jambo hilo sio la Muungano.

Mkandara,

Mimi nilishauri kwa nia njema sana kuwe na uzi maalum wa hoja yako hiyo na TITLE maalum yenye kuuliza au kuelezea kwanini mambo yote yasiwe ya muungano katika Muungano wa TGK na Znz?

Na hapo ungejenga hoja zako kutushawishi na sisi vile vile tungejazia nyama na hata kutoa ufafanuzi mbalimbali katika mambo mbali mbali katika nyanja ya kiuchumi, kisiasa, kiutawala na kijamii.

Kwani kifupi kuna mambo mengi a kuzingatia kutokana na historia kwa nchi zote zilizoungana zilikuwa ni nchi huru. Lakin ukiangalia Znz ina eneo la SQ Km 2000 na TGK ina Sq Km 885,800 na vile vile Population ya TGK ni zaidi ya 45 Mil na Znz ni chini ya 1.5 Mil.

Kwa vigezo hivyo tunaweza kuichambua hoja yako katika mambo makuu manne. Utawala, kisiasa, kiuchumi na kijamii.

nafikiri ukiweka uzi maalum utakuwa uzi mzuri sana na mengi tutajifunza kwayo na nafikiri unaweza kuwa uzi wa Mwaka katika JF katika nyanja ya Muungano wa Tz kama watu watakuwa serious katika kuchangia na kuacha chuki, jazba na ushabiki.

Kazi njema

 
Mkandara,

Mimi nilishauri kwa nia njema sana kuwe na uzi maalum wa hoja yako hiyo na TITLE maalum yenye kuuliza au kuelezea kwanini mambo yote yasiwe ya muungano katika Muungano wa TGK na Znz?

Na hapo ungejenga hoja zako kutushawishi na sisi vile vile tungejazia nyama na hata kutoa ufafanuzi mbalimbali katika mambo mbali mbali katika nyanja ya kiuchumi, kisiasa, kiutawala na kijamii.

Kwani kifupi kuna mambo mengi a kuzingatia kutokana na historia kwa nchi zote zilizoungana zilikuwa ni nchi huru. Lakin ukiangalia Znz ina eneo la SQ Km 2000 na TGK ina Sq Km 885,800 na vile vile Population ya TGK ni zaidi ya 45 Mil na Znz ni chini ya 1.5 Mil.

Kwa vigezo hivyo tunaweza kuichambua hoja yako katika mambo makuu manne. Utawala, kisiasa, kiuchumi na kijamii.

nafikiri ukiweka uzi maalum utakuwa uzi mzuri sana na mengi tutajifunza kwayo na nafikiri unaweza kuwa uzi wa Mwaka katika JF katika nyanja ya Muungano wa Tz kama watu watakuwa serious katika kuchangia na kuacha chuki, jazba na ushabiki.

Kazi njema

Shukran, nitaifanyia kazi japo mimi sii mwandishi mzuri lakini nitajihidi kadri ya uwezo wangu. Ila nakuomba sana iwe baada ya Ramadhan maana hii kitu inabidi niikalie kwa muda kuiandika.

Labda kwa kukuondoa hofu tu ya Zanzibar kumezwa inatakiwa leo hii tufahamu nini hasa waasisi wetu walimaanisha kumezwa huko, maana wapo wanaodhani ni ku protect Identity ya Zanzibar isife wakati wanajua kwamba hiyo Tanganyika ndio haipo kabisa na Zanzibar ipo, hivo ni yupi alomezwa! Muhimu sana kuelewa sababu hizo kisha tunajenga mfumo bora zaidi unaolinda mapungufu ama hofu hizi.

Kifupi, Franch - Quebec ni sehemu ndogo sana kwa mapana na population ukilinganisha na British - Canada, hivyo japo wao wanalilia Identity yao kwa miaka mingi ili jina la Quebec na mila na tamaduni za kama kifaransa (lugha) yao isipotee, wamekuwa wakitishia sana kujitoa ili kujitenga na Waingereza na haikuanza jana toka vita kuu ya Marekani.

Lakini sisi tuna hofu tofauti na hiyo yao maana, hivyo vigezo vyao ktk muungano tunaweza kuvitumia ktk kupata mfumo bora zaidi na wenye kutatzama mapungufu yetu ili tupate mfumo bora kulingana na mazingira yetu. hatuna haja wala sababu ya kuiga kila kitu bali tunajifunza kutoka kwao katika yale mazuri yanayoweza kuijenga nchi yetu.
 
MADAI YA WAZANIZBAR
MUUNGANO WA HAKI NA USAWA
MUUNGANO WA KUHESHIMIANA

Wazanzibar wamekuwa wanajenga hoja zao dhidi ya muungano wa sasa pengine kwa jazba au upungufu wa kuelewa.
Moja ya madai hayo ni kuwa na muungano wenye haki na usawa, ikiwa ni pamoja na kuheshimiana.

Wznz wanasema nchi hizi ziliungana kama nchi huru na hivyo kuwe na uswa na haki katika muungano.
Haki na usawa ni kweli vinahitajika, lakini kauli zao zishie hapo tu. Ni lazima watambue kuwa haki na usawa vina ambatana na wajibu.

Kauli ya haki na usawa ina aoungufu mengi. Wazanzibar hawapaswi kusema usawa, bali wanapaswa kusema usawa kwa kulingana. Ukishasema usawa na kutumia nchi mbili huru basi usawa huo unakwenda hadi katika wajibu.

Linapofika suala la wajibu wznz ni wazuri wa kukimbilia sababu ambazo hazina mashiko.Wakishadai haki na usawa inapaswa waende mbele zaidi kwa kudai kuwajibika. Haki na usawa haishii katika madai ya kugawa vyeo au nafasi.

Haki na usawa ni pamoja na kuhakikisha znz ina wajibu katibu muungano. Wanapodai haki na usawa wa vyeo wakikimbia haki na usawa wa kuendesha muungano, hapo hakuna haki wala usawa. Haki gani na usawa upi ikiwa hataki kuwajibika hata kwa udogo na uchache wao?

Kuna kukimbia wajibu kwa kutumia faida za haki na usawa. Na wajibu mkubwa walio nao ni pamoja na kuangalia gharama za muungano, na wala si udogo au uchache wa watu. Si haki kuwa na haki na usawa bila kungalia usawa huo upo pande zote?

Njia rahisi ya kupata haki na usawa ni kuwa na mshirika. Hivyo ni wajibu wao kuhakikisha kuwa Tanganyika inazinduka ili znz iweze kukaa meza moja na mshirika wake wajadili uwiano wa haki na usawa na wala si haki na usawa tu.

Tunategemea wazanzibar wabadili aina ya kufikiri. Si kila mara wadhani muungano umelenga kutoa nafasi za viongozi sawa, kupokezana uongozi au vitu vya namna hiyo.

Ni wajibu mkubwa kwao kudai haki wakizungumzia wajibu.
Wajibu ni pamoja na jinsi gani wanagharamia muungano huo ili waweze kujenga hoja ya uwiano wa haki na usawa.

Leo hoja zote za wazanzibar ni madai ya vyeo, mengine yakisikitisha.
Wanadai nafasi sawa za mabalozi, wakuu wa vyombo vya usalama na kupokezana nafasi za juu za uongozi wa taifa.
Hiyo ni haki na usawa, lakini pia wanapaswa kuieleza haki na usawa huo kwa kuangalia gharama zinazoambatana na hayo.

Wazanzibar watambue uchache na udogo wao wa eneo hata siku moja hawawezi kuwa sawa na Tanganyika na wala si sababu ya kujificha katika wajibu. Vipi ikifika kuwajibika hawasemi lolote lakini ni wazuri wa kudai mafao?

Hiyo haiondoi haki yao kama taifa, inaeleza tu jinsi madai yao yanavyopaswa kujengwa kwa weledi na ufahamu na si masuala ya madai tu yasiyoweza kusimama yenyewe.

Kuheshimiana
Wazanzibar wanadai kuwepo kuheshimiana kama nchi mbili huru.
Kwa muda mrefu waznz wameheshimiwa ndania ya muungano huu.

Kila mara wamesikilizwa na hata kupata wasichostahili.
Ni wazanzibar hao hao ambao hawana heshima kwa muungano.

Huwezi kuvunja katiba ya nchi ukadai kuheshimiana. Unaheshimiwa vipi ikiwa wewe hukuheshimu wenzako?

Mathalani, kuondoa masuala ya muungano bila kujadiliana na wenzao, kubadilisha katiba bila kuwafahamisha Watanganyika na kuchukua maamuzi bila kujali upande wa pili.

Leo watadai haki gani na usawa upi ikiwa wana baraza lao la mitihani? Hii maana ni kuwa baraza la mitihani si chombo chao. Wamefanya hivyo kwa kutoheshimiana. Wamechukua maamuzi tu bila kuheshimiana.

Sasa kutakuwepo na bodi ya mitihani isiyowahusisha, wznz wana haki gani ya kulalamika?
Watataka uteuzi wa bodi hiyo na nyingine kama bandari na TBS kwa utumia hoja ipi?

Wao hawaheshimu katika muungano huu, wapi na kwavipi wategemee kuheshimiwa?

Wznz wanadai hakuna haki katika uteuzi wa balozi zetu(jambo la kusikitisha ), swali la kuwauliza ni kuwa lini walidai haki na usawa wa kugharamia hata balozi moja tu kati ya hizo wanazodai.

Hoja kubwa hapa ni kuwa wznz wasiwe wazuri wa kudai haki na usawa katika sehemu zenya ulaini.
Wana wajibu wakudai haki na usawa kwa uwiano katika kuwajibika.

Endapo hawatakuwa na weledi wa kudai kuwajibika, basi haki na usawa au kuheshimiana wanakodai hakutapatikana.

Tunarudia kuwaasa wajenge hoja zenye weledi na mantiki na waache kulinganisha vitu visivyolingana.
Hatujengi muungano wa kupokezana marais au kupeana nafasi za ulaji.
Tunajenga muungano wa faida za wananchi.

Hoja zao lazima ziambatane na ukweli. Ukweli unapatikana kwa haki, usawa na kuwajibika na wala si udogo, uchache au historia.


Tusemezane
 
Mkuu wangu hakuna athari zozote zinazoweza kutokea.

Kwasasa Zanzibar ina katiba yake na inaweka, kuondoa, kuvunja, kubagua n.k. hakuna kilichoharibika, vipi uone ujio wa Tanganyika ndio tatizo? Kwani huoni masharti ya katiba ya znz ya 2010 ilivyoandikwa 'wapendavyo' na tukiuliza tunaambiwa si jambo la muungano.

Tukiuliza, wewe Mkandara unasema ni haki yao. Tukiuliza unasema wao ni wachache n.k.
Hujaweza kukemea wlichofanya wznz unaanza kukemea kisichokuwepo! mkuu wangu !

Tanganyika ikizinduka, sheria zitawiana, ya upande mmoja sawa na mwingine. Hakutakuwa na mgogoro wa aina yoyote ile!
hata sikuelewi kabisa, kwani Zanzibar hawakuwa na katiba yao kabla ya mwaka 2010, na hiyo katiba tuliandika pamoja au? Tunacholaumu wengi wetu ni yale makubaliano baina ya Utawala wa CCM na CUF pasipo kuwashirikisha wadau wengine ktk jambo muhimu kama hili kupelekea kuandikwa kwa katiba mpya ya Zanzibar ambayo ilitokana na makubaliano hayo.

Hivyo chama cha CCM wanakubaliana na mabadilliko hayo ambayo yanapelekea kuongeza zaidi mambo yasokuwa ya Muungano. Kwa hiyo usiseme wameandika katiba mpya wapendavyo, sio kweli kwani walipata ridhaa ya rais na baraza kuu la chama cha Mapinduzi wakiwemo wajumbe kutoka bara. haya ndio mapungufu ya katiba ya mwaka 1977 ambayo bado inawapa nguvu zote za kiutawala wa dola kuamua wayatakayo wao na ndio sababu ya kuitaka katiba mpya.

Na bado haitoshi kwao wana CUF ambao wanataka mambo yote yasiwe ya muungano ili Zanzibar ijitenge kama nchi huru ili tusiwe na muungano wetu bali tuwe na Shrikisho. Haya yote yametokana na sisi kushindwa kuwapa mamlaka kamili ktk utekelezaji wa shughuli zao pamoja na Uvaaji wa koti a Muungano. Ni muhimu kuwasoma watu wanataka nini kabla hujatoa maamuzi ama majibu. Kipi kinawezekana ama hakiwezekani badala ya ku react maana ndivyo wanavyotaka. Zipo njia sahihi zinazoweza kuondoa mgogoro huu na ndicho nimekuwa nikiandika muda wote lakini wewe una react kama vile huelewi gharama za kuunda Muungano na yapi yataathiri Umoja huu.
 
hata sikuelewi kabisa, kwani Zanzibar hawakuwa na katiba yao kabla ya mwaka 2010, na hiyo katiba tuliandika pamoja au? Tunacholaumu wengi wetu ni yale makubaliano baina ya Utawala wa CCM na CUF pasipo kuwashirikisha wadau wengine ktk jambo muhimu kama hili kupelekea kuandikwa kwa katiba mpya ya Zanzibar ambayo ilitokana na makubaliano hayo.

Hivyo chama cha CCM wanakubaliana na mabadilliko hayo ambayo yanapelekea kuongeza zaidi mambo yasokuwa ya Muungano. Kwa hiyo usiseme wameandika katiba mpya wapendavyo, sio kweli kwani walipata ridhaa ya rais na baraza kuu la chama cha Mapinduzi wakiwemo wajumbe kutoka bara. haya ndio mapungufu ya katiba ya mwaka 1977 ambayo bado inawapa nguvu zote za kiutawala wa dola kuamua wayatakayo wao na ndio sababu ya kuitaka katiba mpya.

Na bado haitoshi kwao wana CUF ambao wanataka mambo yote yasiwe ya muungano ili Zanzibar ijitenge kama nchi huru ili tusiwe na muungano wetu bali tuwe na Shrikisho. Haya yote yametokana na sisi kushindwa kuwapa mamlaka kamili ktk utekelezaji wa shughuli zao pamoja na Uvaaji wa koti a Muungano. Ni muhimu kuwasoma watu wanataka nini kabla hujatoa maamuzi ama majibu. Kipi kinawezekana ama hakiwezekani badala ya ku react maana ndivyo wanavyotaka. Zipo njia sahihi zinazoweza kuondoa mgogoro huu na ndicho nimekuwa nikiandika muda wote lakini wewe una react kama vile huelewi gharama za kuunda Muungano na yapi yataathiri Umoja huu.
Mkuu Mkandara , makubaliano ya vyama hayo hayana uhalali wa kuathiri katiba ya nchi.
Hakuna mahali bunge letu lilitaarifiwa mbadiliko ya katiba ya zanzibar ya mwaka 2010. Hakuna! Kama wameongea katika vikao vya CCM hayo ni maongezi ya mke na mumewe chumbani hayana nguvu za kisheria achilia mbali mantiki.

Hakuna mahali penye kumbu kumbu za kuonyesha Wananchi wa Tanganyika walitaarifiwa kuhusu ajira,bandari, TBS,ardhi n.k kuondolewa katika muungano.

Leo Mkandara unaingia hofu kusikia Tanganyika inakuja eti kwa kuogopa kila nchi itaweka mambo yake.
Yes, ndivyo itakavyokuwa na wala hakuna tatizo. Hiyo ndiyo njia ya kuvua koti la muungano.
Wazanzibar wameshaonyesha njia nini cha kuogopa sisi kama Watanganyika.

Yes, tutakuwa na sheria zetu zinazoambatana na mambo yatu kama ambavyo zanzibar itakuwa na sheria zake.
Kama upo umuhimu wa znz itawalazimu warekebishe sheria zao na siyo sisi turekebishe zetu.Hatuwezi kurekebisha sheria zetu ku-accomodate znz, ili wao wana uwezo huo ili tuwafanyie accomodation.

Kwa mfano, kama wataendelea na ugumu wa suala la ardhi, hatutakuwa na ardhi ya Tanzania.
Itakuwepo ya Tanganyika.Kama watazuia ajira au kuzitoa kwa upendeleo, well haki hiyo watakuwa nayo na tutakuwa nayo.

Tunachotaka ni kuvua koti la muungano. Habari ya nani ataumia hilo ni suala la nchi husika.
Wameanza wao miaka 4 iliyopita, Mkandara ulikuwa kimyaa, leo unataka kila jambo liwe la muungano.

Wazanzibar ambao unataka wawe na mamlaka kamili hawataki mambo ya muungano. Wasikilize video zao. Nitajie mzanzibar mmoja tu anayetaka kila jambo la muungano katika maarufu wa CCM na CUF

Tena ulivyo bias unasema wapewe mamlaka kamili, ama! halafu yale mambo ya Tanganyika ndiyo yawe ya Tanzania.
Sisi wengine hutuwezi kuuza nchi yetu Tanganyika kilaini na kizembe namna hiyo. Wazanzibar wameukana Utanzania.
Hawatutambui kama Watanzania, hatuna sababu za kuwatambua kama Watanzania, Ni wazanzibar tu

Tanganyika itazinduka na znz watapata mamlaka kamili. Hatuhitaji kuwanyonya wala kuwaonea.
We don't need znz, Mkandara. Nusu yao wanaishi kwetu na ndio taifa lililobeba wznz wengi duniani. Hivyo Tanganyika ni muhimu kwao, znz si muhimu kwetu, na wala haitakuwa muhimu kwa roho zao za kutaka Tanganyika ishinde(Ali Salehe)

Gharama za kuunda muungano ni zetu, na ukivunjika hakuna athari kwetu! Hakuna kichumi au kijamii.
Hatutegemei znz kwa lolote lile Mkandara, usiufanye ulimwengu kama wajinga, na kama wanataka kesho waondoke.

Ndio maana nakuuliza lile swali linalokukera, Tanganyika itaathirika na kitu gani muungano ukivunjika?

Huna jibu ila kutisha watu kuwa kuna athari. Zipi hizo unazozijua wewe mwenywe na ambazo hutaki kuzitaja.

Tunakueleza kwa jibu moja, hatutegemei znz kwa lolote, hatuna shida na uwepo wao na wala hatufaidiki zaidi ya kubeba zigo miaka 50 likielea mgongoni. Ndio maana tunakuambia hatuwahitaji na wala usiuchanganye umma eti kuna athari.
 
SITTA AENDELEZA UPOTOSHAJI
MBINU ZAMWISHIA, SASA ANATAMANI UBABE

HAKUNA KATIBA ISIYO NA MARIDHIANO


Kikao cha kamati aiyoiteua Sitta kimemalizika .
Wajumbe wa UKAWA hawakuhudhuria licha ya vitisho vya Sitta kuhusu kile alichokisema kama vichwa ngumu.

Hakika wamekuwa vichwa ngumu na kichwa kinamuuma Sitta wala si wao.
Anguko lake na uwezo wake kwa mambo ya kitaifa sasa hakuna shaka vimefika mwisho.

Katika taarifa yake, Sitta ametoa mapendekezo kadhaa ili kukidhi haja zake na CCM katika kuandika katiba yao

1.Kikao cha bunge maalumu kiendelee kama kilivyopangwa.
Hoja yake ni kuwa kuna mambo kama uvuvi, kilimo ambayo ni muhimu kuliko muundo wa serikali.
Sitta haelewi kuwa hakuna nyumba inayokamilika ikiwa na furniture tu bila jengo.

2.Kwamba, kikao hicho kimefanyika kwasababu akidi ya theluthi mbili ilitimia.
Sitta anafahamu yeye ndiye alichagua kamati hiyo na kujiwekea wajumbe anaojua watakidhi akidi
Kusema akidi imetimia ni kujidanganya mwenyewe, hakuna akidi inayotengenezwa na mtu na kutimia.

3.Kwamba, kuwe na mabadiliko ya kanuni ili kudhibiti utoro na ukosefu wa nidhamu
Sitta alikuwepo wakati bunge la JMT linapitisha sheria ya kuundwa bunge la katiba kwa akidi ya watu 100.
Kwa unafiki hakukemea, leo anapata wapi nguvu za kukemea uzembe alioshiriki kuutengeneza kutoka bunge la JMT

Lakini pia, kudhibiti nidhamu anakokutaka ni ili wajumbe wakubaliane naye.
Wale watakaokataa maoni yake wafukuzwe ili abaki na kundi la ‘ndiyo' mzee.

Sitta hatambui kuwa katiba inayoandikwa si yake wala watoto wake ni ya taifa na kwamba, lazima kuwe na mawazo mbadala hata kama hayapendi.

Udikteta kama wa kufukiwa Richmond, Meremeta haukubaliki zama hizi na hilo Sitta aelewe bila kumuonea aibu.
Sitta alifunika uzembe uliolitia taifa aibu na sasa anataka kurudia tena.

4. Kwamba, UKAWA wameombwa warudi na makundi ya jamii nay ale ya dini.
Sitta anapotosha kwasababu makundi ya dini yalitaka matakwa ya wananchi yasikilizwe.

Huko nyuma tuliwaonya UKAWA kuwa lazima wajibu tuhuma za viongozi wa dini wanaotumiwa.
Leo kina Sitta wanatumia viongozi wa dini katika mambo ya kisiasa.

Halafu kwa unafiki wanarudi kusema watu wasichanganye dini na siasa.
BMK ni la kisiasa na hivyo maoni ya viongozi wa dini ni sawa na yale ya wakulima na wavuvi na BMK halichagui Askofu au Sheikh kama Sitta anavyopotosha.

5.Sitta anasema makundi yanayoleta tatizo ni UKAWA na Tanzania kwanza.
Hili la Tanzania kwanza ni la chama chake cha CCM.

Wakati linaundwa Sitta alikuwa kimya leo anawezaje kusema ni tatizo wakati yeye alikuwa mshiriki wa kundi hilo.
Ushiriki wa Sitta ni pale alipotumwa na Tanzania kwanza kuhakikisha JK anahutubia na kumvuruga Warioba.

Samwel alishiriki vema na ni mwanachama wa Tanzania kwanza.
Hana moral authority ya kunyooshea kidole kundi hilo

7. Sitta anasema, makundi halali ni yale ya wajumbe wa Tanzania bara na wajumbe wa Zanzibar
Tazama mzee Sitta anavyojidhalilisha.

Kwanza, hakuna kundi la Tanzania bara. Sheria ya kuunda bunge hilo la katiba haitaji wajumbe wa Tanzania bara.

Hivyo mzee Sitta atambue kuwa sheria haimruhusu kusema achilia mbali kufikiri.
Tuna kundi la Zanzibar dhidi ya JMT. Wabunge wa bunge la JMT ni kutoka Dodoma wakiwemo wa CUF.

Vipi aseme wabunge wa bunge la JMT ni kutoka Tanzania bara.
Huu ni uongo usiopaswa kufanya na mzee wa umri wake tena akiwa mwanasheria.
Hilo lazima aambiwe ili asiendelee kutengeneza mazingira ya machafuko nchini .

Sitta amepewa nafasi ya kuendelea na bunge lake mwenyewe.
Kitu anachopaswa kukumbuka ni kuwa katiba haipatikani bila muafaka.

UKAWA wanawakilisha sehemu ya jamii.
Ni vipi Sitta anaweza kuipuuza sehemu hiyo akijivunia kuwa katiba inayoandaliwa ina mema kwa wananchi.

Samwel Sitta, CCM na wewe mtaandika katiba yenu. Muda si mrefu wananchi wa Tanzania wataandika katiba yao.
Wakati huo utakuwa nje ya system na tutakuwa na uwezo wa kukuita popote ueleze upotevu wa pesa unaoendelea kuufanya na wenzako.

Kenya walijaribu lakini nguvu ya umma ikatamalaki.
Watanzania wa leo si wa mwaka 1973 .

Sitta atafakari kama analitakia mema taifa hili siku zijazo.
Tunajua hawezi kuwa rais wan nchi hii tena, je, kinga aliyonayo JK yeye anayo?

Tusemezane
 
Nguruvi3
Mkuu Mkandara , makubaliano ya vyama hayo hayana uhalali wa kuathiri katiba ya nchi.
Hakuna mahali bunge letu lilitaarifiwa mbadiliko ya katiba ya zanzibar ya mwaka 2010. Hakuna! Kama wameongea katika vikao vya CCM hayo ni maongezi ya mke na mumewe chumbani hayana nguvu za kisheria achilia mbali mantiki.

Hakuna mahali penye kumbu kumbu za kuonyesha Wananchi wa Tanganyika walitaarifiwa kuhusu ajira,bandari, TBS,ardhi n.k kuondolewa katika muungano.
Unajua mkuu wangu wakati mwingine acha hata kuandika ama kujibu maana unapojibu ndio unatupoteza kabisa. sasa ikiwa wewe unaona makubaliano hayo hayana uhalali wa kuathiri katiba inakuwaje tena wewe unamtaka mume amtarakie mkewe? Wewe Mtanganyika ni sawa na mtoto alozaliwa ktk ndoa hiyo unataka vipi maswala walokubaliana mume na mke uyatolee wewe maamuzi kwa sababu tu unaathirika na ndoa yao.

Sii kinachotakiwa haswa ni wewe mtoto kutoka ktk nyumba hiyo ukaanze maisha yako? - Now utakwenda wapi ndio majibu yangu kwa hao kina Jussa watoto wa kufikia ila yanisikitisha hata nyie ndugu zangu mmejiunga nao kwa sababu ya mazoea. Na tutakapo gawana mabo sii bado utabakia na CCM au unadhani hiyo CCM itaondoka na Zanzibar maana humjui adui yako ni kunguni uliyemvaa na nguo zako. Na kibaya zaidi hao Wazanzibar usowataka na wanaopiga kelele ni samaki wadogo sana kwani mipapa yao yote yenye kuzua mgogoro huu makazi yao yapo Tanganyika na wamewekeza Tanganyika, Zanzibar ni kwenda kununua ardhi beach, mashamba ya karafuu na minazi. Hawa ndio wasotaka wewe ukanunue ardhi Zanzibar ili wao wakaiuze kwa Muuza unga wa Kitaliani au Mjarumani. Hawa watu hawanisumbui miye kwa sababu nawajua hila zao!

Tuache kurudi nyuma kuendeleza Ubishani juu ya mambo tulokwisha yatolea maelezo, isipokuwa nakuomba wewe, Barubaru, UKAWA na wengine wote wanaosoma mada hii waniambie wanachokifahamu wao kwa nini tume zote walojaribu kuandaa muundo mpya wa JMT walikwama ilipofikia ' Tanganyika itaimeza Zanzibar' ikiwa zitaundwa serikali 1 au serikali 3 ni gharama kubwa.
1..Je kuimeza huko walikuwa na maana gani? itamezwa vipi, na utafiti wao ulionyesha nini huko kumezwa ama kudhihirika kwa hizo gharama kubwa za serikali 3 ktk uchunguzi wao.
2. Je, Mnaweza kutoa mifano kusherehesha majibu, kisha
3. Naomba pia mnambie leo hii huu ushirika wa Shirikisho na serikali 3 leo hiii zinatoa majibu gani tofauti ambayo miaka ya nyuma isingewezekana!.

Tafadhali tusirudishene nyuma ktk mjadala tulokwisha utolea maelezo, twende mbele na kwa kituo. Naomba maelezo ya swali langu kenu nyote halafu tuendelee maana haitakuwa akili kutoa maelezo kibao wakati swala lilotukwaza kwa miaka yote hatufahamu hata ilikuwa ikimaanisha nini..
 
Nguruvi3
Tuache kurudi nyuma kuendeleza Ubishani juu ya mambo tulokwisha yatolea maelezo, isipokuwa nakuomba wewe, UKAWA na wengine wote wanaosoma mada hii waniambie wanachokifahamu wao kwa nini tume zote walojaribu kuandaa muundo mpya wa JMT walikwama ilipofikia ' Tanganyika itaimeza Zanzibar' ikiwa zitaundwa serikali 1 au serikali 3 ni gharama kubwa.
1..Je kuimeza huko walikuwa na maana gani? itamezwa vipi, na utafiti wao ulionyesha nini huko kumezwa ama kudhihirika kwa hizo gharama kubwa za serikali 3 ktk uchunguzi wao.
2. Je, Mnaweza kutoa mifano kusherehesha majibu, kisha
3. Naomba pia mnambie leo hii huu ushirika wa Shirikisho na serikali 3 leo hiii zinatoa majibu gani tofauti ambayo miaka ya nyuma isingewezekana!.

Tafadhali tusirudishene nyuma ktk mjadala tulokwisha utolea maelezo, twende mbele na kwa kituo. Naomba maelezo ya swali langu kenu nyote halafu tuendelee maana haitakuwa akili kutoa maelezo kibao wakati swala lilotukwaza kwa miaka yote hatufahamu hata ilikuwa ikimaanisha nini..
Kama unavyoona ilivyo ndivyo tume ziliyokutana nayo. Muungano ulilenga S1, nchi moja na taifa moja. Hilo halitawezekana kwasababu ya Narcissism ya Wazanzibar hata leo.

Kumeza kulimaanisha historia ya znz isifutike mapema nyakati hizo wakati tunajenga taifa.
Ilikuwa ni symbolic gesture ya historia tu, si kicuhumi wala kijamii.

Ililenga ku-preserve historia ya znz . Makosa yalifanyika pale ilipodhaniwa Tanganyika inaweza kufutika tu.
Hivyo kumezwa uelewe ni symbolic kwa ajili ya historia wakati huo tunaanza muungano. Haina maana kwa sasa.
Kama iakuwa na maana, basi maana hiyo ndiyo inatusukuma tuidai Tanganyika. Tanganyika ilikuwa na historia pia.

Ukumbuke kuwa tume zilikuwa zinakumbana na vikwazo kwavile wazanzibar wanadhani uzanzibar ni bora kuliko Utanzani. Of course wanaweza kuwa right, si kama wewe unayedhani Utanganyika ni hafifu kuliko Utanzania

Hili la S3 na gharama nadhani tusilijadili. Umeshindwa mara zaidi ya 7 kuonyesha unafuu wa S2 na gharama zake ukilinganisha na S3.

Pitia video hizi

Dakika 3-4.36
KAMATI YA MARIDHIANO SIX KAMISHNA ALLY SALEH COCONUT RADIO PART 2/3 - YouTube

Profesa Sheriff

Gharama za muungano amezibeba Mtanganyika. Kusema S3 kutaongeza gharama kuna maana moja tu, kwamba uwepo wa S3 utagawa gharama.

Na kama anayosema Ali Saleh na Salimin Awad katika video, kwasasa znz haina haichangii muungano.
Mkandara unachotaka kusema ni kuwa Watanganyika waendelee kubeba gharama za muungano huku znz wasichangie hata kidogo walicho nacho. Hoja ya gharama haina mashiko hadi utuonyeshe kwa namba gharama za S2 zipoje.

Serikali 3 zinatoa majibu yapi?Swali lako linajibika kama ifuatavyo

1. Kutakuwa na shughuli za kidola tu katika muungano. Malalamiko ya Zanzibar kuwa Tangayika imevaa koti yataondoka. Mfano, waziri wa kilimo wa muungano hatakuwepo. Kutakuwa na waziri wa kilimo wan chi husika. Koti limevuliwa. Dakika 10-14 KAMATI YA MARIDHIANO SIX KAMISHNA ALLY SALEH COCONUT RADIO PART 1/3 - YouTube

Zanzibar itawajibika kuchangia muungano na kutoa unafuu kwa Tanganyika.
Dakika 3-4.36 KAMATI YA MARIDHIANO SIX KAMISHNA ALLY SALEH COCONUT RADIO PART 2/3 - YouTube

2.Itapunguza mzigo kwa Tanganyika. Wizara za muungano zitachangia no matter how kidogo itakavyokuwa na kupunguza malalamiko. Mfano, gharama ambazo znz ingechukua kwa ulinzi na usalama ikiwa nje ya muungano sasa zitaingizwa katika mfuko wa muungano.Tofauti na sasa ambapo gharama hizo ni za Tanganyika.

3.Ubaguzi utafikia mwisho. Sheria zinazotawala znz pia zitatawala Tanganyika.
Kama wznz hawataki ajira ziwe za wote, Tanganyika itakuwa na haki ya kuwa na ajira zake.
Hilo litaondoa lawama kuwa wafanyakazi wa muungano wengi hawahudumii znz.

4. Sheria za kulinda ardhi kule znz zitatekelezwa bila kikwazo. Tanganyika itakuwa na sheria zake pia.

6. Znz itakuwa na uwezo wa kwenda kukopa popote na kuondokana na dhana ya kudhulumiwa na Tanganyika.

7. Znz itakuwa na uhuru wa kujiunga na taasisi na mashirika ya kimataifa bila kuingiliwa au kuomba ruhusu Tgk

8. Tanganyika itakuwa na uwezo wa kupanga mipango yake ya maendeleo bila kubeba mzigo wa Zanzibar

9. Zanzibar itakuwa na udhibiti wa uchumi wake usioingiliwa na Tanganyika(Fiscal autonomy kama ambavyo Tanganyika itakuwa na fiscal autonomy yake

10. Znz itakuwa na uwezo wa kusimamia rasilimali zake kama gesi na mafuta bila kuingiliwa na Tanganyika.

11. Znz itakuwa na uwezo wa kuwa na taasisi zake za kifedha, hivyo kukidhi bajeti yake kwa kutumia taasisi hizo.


Endapo S3 hazina jibu, je tuendelee na matatizo yaliyopo bila kutafuta ufumbuzi. Katika bunge la katiba, Rais alisema '' tuondoe mambo yenye mgogoro'' akimaanisha kuwa tutenge kati ya mambo ya muungano na yasiyo.

Hadi hapo anataka S3 kwasababu huwezi kuwa na pande 3 zisizo na usimamizi.
Labda wewe utueleze, unawezaje kuwa na JMT ambayo znz ipo halafu ukawa na Zanzibar bila kuwa na malalamiko ima kutoka Tanganyika au kutoka Zanzibar.

Na mwisho, wznz wanataka S3 au Mkataba. Wewe Mkandara unaona kitu gani kitawaridhisha zaidi ya hayo?
Kwanini unawang'angania wazanzibar tukifahamu kwa upande wa Tanganyika ni taabu tu maana hakuna tunachopata zaidi ya kupoteza.

Ndipo namalizia kwa lile swali linalokuudhi sana na kuamsha hisia za kauli za karaha.
Mkandara, Tanganyika itapoteza kitu gani kwa kuwa na S3 au kutokuwa na muungano.
 
Nguruvi3 Unajua mkuu wangu wakati mwingine acha hata kuandi

sasa ikiwa wewe unaona makubaliano hayo hayana uhalali wa kuathiri katiba inakuwaje tena wewe unamtaka mume amtarakie mkewe?

Wewe Mtanganyika ni sawa na mtoto alozaliwa ktk ndoa hiyo unataka vipi maswala walokubaliana mume na mke uyatolee wewe maamuzi kwa sababu tu unaathirika na ndoa yao.
Mfano huu ni irrelevant na usiwadanganye vijana wanaotusoma. Unawachanganya mkuu. Onea huruma viumbe vya mungu! Usitumie elimu yako kupotosha.

Mkandara, Tanganyika si mtoto wa muungano hata siku moja. Tanganyika ilikuwepo kabla ya muungano.
Tanganyika iliungana na Zanzibar mwaka 1964 na kuendelea kuwepo hadi 1967 ilipozaliwa Tanzania kutoka ubavuni kwa Tanganyika.

Wazazi walikuwa wawili, Tanganyika na Zanibar. Mkataba wa muungano haukuwahi kuitaja Tanzania hata sehemu moja.
Katiba iliyopo ni ya Tanzania ambayo Tanganyika ndiye ''yaya''. Sasa znz wanapofanya makubaliano na mtoto Tanzania, mzazi Tanganyika yupo wapi?

Tanganyika si mtoto hata siku moja, ni mzazi wa muungano.

Hili limekwisha halina mjadala.
 
Nguruvi3,
Mkuu #469 nimewauliza vizuri tu maswali matatu lakini umerudi hukujibu hata moja, isipokuwa umerudi na yako yale yale ya toka ukurasa wa kwanza unazunguka tu kama pia. Hili ndio tatizo lako yaani ni kama yule mtu asiyetaka kusikiliza wengine anaongea yeye tuu wala hajui kinachoongelewa ni nini ili mradi mfomo unamuasha akikaa kimya!
 
Mfano huu ni irrelevant na usiwadanganye vijana wanaotusoma. Unawachanganya mkuu. Onea huruma viumbe vya mungu! Usitumie elimu yako kupotosha.

Mkandara, Tanganyika si mtoto wa muungano hata siku moja. Tanganyika ilikuwepo kabla ya muungano.
Tanganyika iliungana na Zanzibar mwaka 1964 na kuendelea kuwepo hadi 1967 ilipozaliwa Tanzania kutoka ubavuni kwa Tanganyika.

Wazazi walikuwa wawili, Tanganyika na Zanibar. Mkataba wa muungano haukuwahi kuitaja Tanzania hata sehemu moja.
Katiba iliyopo ni ya Tanzania ambayo Tanganyika ndiye ''yaya''. Sasa znz wanapofanya makubaliano na mtoto Tanzania, mzazi Tanganyika yupo wapi?

Tanganyika si mtoto hata siku moja, ni mzazi wa muungano.Hili limekwisha halina mjadala.
Majibu yako yapo bandiko #470 . Sina namna ya kukupendeza na majibu isipokuwa kukueleza kile ninchotaka kukueleza na si kile unachotaka kusikia.

Msimamo wangu ni consistent tangu naingia JF 2010 nikitokea forums nyingine kuhusu muungano.
Niliwaambia akina Mdondoaji takashi GHIBUU Kake n.k kuwa walikuwa wanadai kitu wasichokijua.

Unakumbuka nimekuwekea bandiko la 2011, kabla ya wazo au tume kufikiriwa.
Bandiko hilo na mengine yaliwaweleza wazanzibar nini hatari ya kudai kisicho chao tena wakiwa hawna mchango.

Wote niliowataja waliniita Nyerereist likianzishwa na Mdondoaji.

Leo wote wamefutika JF forums kwa haya, soni na fedheha wengine wakigeuza njia na kurudi nilikowaeleza miaka 3 iliypita.

Hivyo mfumo wa wznz haunisumbui hata kidogo. Kinachonisumbua ni Watanganyika kutoelewa maana ya muungano, faida na hasara zake na jinsi wanavyoumia wakitesa familia zao kulea familia za watu walioukataa Utanzania ambao ni wazanzibar.

Mkandara, wazanzibar wote kwa pamoja wanasema hawachangii muungano.
Nasi tunasema hatuna sababu za kuwazuia wasikope nje ya nchi maana kukopa kwao ni fahari zaidi ya kupewa.

Na kwa vile hatuna manufaa na muungano , tupo tayari kushirikiana na si kutuweka mateka katika kuandika katiba ya Tanganyika.

Hatuhitaji kuwa wakoloni znz, hatuwalazimishi wafuate mfumo wa Nyerere laanatullah. Wana uhuru wa kuungana na Seychelles n.k.

Njia ni mbili
1.Wakubali tunawaambia nini, kwamba ni wadogo, wachanga
2. Njia nyeupee waende zao. Hatuna mahitaji nao nawe Mkandara unalijua hilo. Tunawasaidia hatuwahitaji

Kama hutakubali hilo, waaambie Watanganyika, nini watakosa znz ikiwa haipo.

Tunaendelea na elimu ya umma, msikilize Duni Haji anavyoshindwa kuelewa kama wznz wengine. Inafuata
 
WAZIRI WA AFYA ZANZIBAR APOTOSHA UMMA
NI MWENDELEZO WA WZNZ KUTOJUA WANADAI NINI

ADAI GESI YA TANGANYIKA NI YA MUUNGANO, YA ZNZ NI YAO PEKE YAO

Wengi wanasema wazanzibar wana mwamko wa muungano kuliko Watanganyika, kuna tatizo katika hilo.
Wazanzibar ni wazuri sana wa kujaa na kujazwa hamaki. Si wazuri wa kupembua, kutambua na kuchambua.
Ni bandera fuata upepo wenye 'courage' hata mbele ya mabomu. Wanahitaji tu kuambiwa watende,watalipuka

Kutokana na hali hiyo, wajanja na viongozi wa znz wamewatumia wazanzibar.Mfano, tume zote zilizoundwa, Nyalali, Kisanga, Warioba 1 na Rais wao Jumbe kwa pamoja walishauri uwepo wa S3.

Baraza la wawailishi na la Mapinduzi kwa nyakati mbali mbali wametaka uwepo wa S3.
Viongozi bila kujali CCM au CUF walikuwa mstari wa mbele kumzogoa na kumzomea Nyerere tena kwa laanatullah.
Hakuna kiongozi yoyote wa znz aliyekemea kauli hizo za kibaguzi na kipuuzi.

Leo tuna Wazanzibar nusu wanaotaka muundo wa ''Nyerere lanatullah'' wa S2.
Mfumo ambao wameuita wa kikoloni na kwamba Tanganyika ni wakoloni weusi.

Tuna makundi mawili, S3 na S2. Tena kuna waliotaka muungano wa mkataba ingawa hawajui unatetea nini.
Ukishakuwa maarufu unaweza ku-fool wznz kiasi unachotaka.

Tatizo linaanza pale wznz wanapokabidhi fikra zao kwa viongozi waongo na wadanganyifu.

Tazama video hii kuanzia dakika 10-12.

KAMATI YA MARIDHIANO SIX PART 2/3 MDAHALO ITV BUNGE KATIBA NA TANZANIA TUITAKAYO 4/05/2014 - YouTube

Waziri wa SMZ Duni Haji, anasema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.
Kwa miaka 7 Zanzibar haijapata pesa za gesi hiyo kutoka Muungano.
Duni kama walivyo wazanzibar wengie wana matatizo ya kusahau, kudanya au kupotosha na inawezekana ufahamu

Gesi si suala la muungano. Waliokataa suala hilo ni wazanzibar kwa kupitia katiba yao.
Waziri aliyeondoa gesi na mafuta katika muungano ni Mansour wakati huo akiwa CCM na kuungwa mkono na Duni Haji wa CUF.

Hivyo Tanganyika inatumia gesi yake na wala haina ulazima wa kuipa znz hata senti tano.

Alichokiongea Duni ni kuamsha hisia za audience yake ya wazanzibar kuwa wanaonewa akifahamu hawawezi kuchambua au kutafakari .

Gesi ya Tanganyika wazanzibar wanataka iwe ya muungano. Ile ya kwao iwe ya kwao.

Ndivyo walivyofanya kwa kujikusanya Dar es Salaa, makamu wa Rais JMT, makamu wa Rais SMZ, waziri ofisi ya Rais Muungano, waziri wa fedha wa JMT wakajipangia nafasi asilimia 21 ya ajira ambazo ni za Tanganyika.
Hakuna sababu mzanzibar ajiriwe wizara ya afya, elimu au kilimo n.k. kwasababu si za muungano kwa mujibu wao.

Uhalali wa wao kuja na kujipangia silimia 21 ndio huo anaotaka Duni wa kuchukua pesa za geshi Mtwara iende Zanzibar wakati yao hawataki iwe ya muungano.

Ni uongo huo huo aliousema Kamishana wa tume Ali Swalehe alipohojiwa na coconut FM. Alisema Wazaznibar wana uwezo mkubwa wa kulipa kodi kuliko Mtanganyika. Alichukua pato la znz kugawa kwa wznz milioni 1.3 na kupata wastani wa 138,000 kama kipato cha Mzanzibar. Akasema kwa Mtanganyika ni 38,000 hivyo mzanzibar anauwezo wa kuchangia muungano zaidi kuliko Mtanganyika.

Huu niuongo wa wazanzibar. Huwezi kugawa pato la taifa tukijua kuwa znz haina bajeti ya ulinzi na usalama, mambo ya ndani, mambo ya nje, mashirika ya kimataifa, balozi n.k.

Hivyo kuchukua pato na kuligawa kwa idadi ya watu ni kuwadanganya.
Znz ingekuwa na uwezo huo nusu yao wapatao 500,000 wasingekuja kuhemea njaa Tanganyika.

Ukienda znz, hali ya maisha ya watu ni duni. Ali Saleh anapowaambia wana uwezo anawadanganya tu.

Uchumi wa znz ni bilioni 400 ambazo asilimia 80 ni mishahara bila kuwa na gharama za ulinzi na usalama.
Bajeti ya ulinzi na usalama ya znz ni lazima iwe katika bilio 80-100. Ukitoa katika bilion 400 sijui nini kinabaki

Kwa Watanganyika hili ni funzo kubwa. Mnaona wanavyokuja na kujipangia nafasi za ajira.
Wanakuja na kusomesha watoto wao bure wenu wanalipa mikopo.

Wanakuja sasa wanataka kudai hata gesi na mafuta, yao wakiwa wamesaiondoa katika muungano.
Wanataka ulinzi na usalama na gharama nyingine. Hawachangii muungano na kubwa zaidi wao ndio tatizo katika muungano kwa malalamiko yasiyoisha na yasiyo na na mantiki.

Watanganyika, waulizeni akina @Hkigwangalla @Dr F .Ndugulile Nape Nnauye John Mnyika Mwigulu Nchemba Anna Tibaijuka n.k. kuwa Kwanini wapo tayari kuiuza Tanganyika ?Kwanini Watanganyika wabebe zigo hili la muungano wenyewe?

Kwanini wznz wawe na yao na yale yetu yawe ya muungano?
Kuna kitu gani tunapata kwa kuumiza wanachi wetu kwa kodi za kuihumia znz na muungano?

Kwanini tunadhani sisi ni Tanzania ikiwa wazanzaibar hawataki Utanzania.

Ni kwanini wabunge hao wa CCM wameamua makusudi kuitoa kafara Tanganyika na kuwaumiza Watanganyika?

Hatuna sababu za kulalamikiwa na znz kwa wema na ukarimu. Tunajitosheleza kama Tanganyika na hatuhitaji Znz.

Tunataka Tanganyika yetu izunduke ili tuhangaike na matatizo ya wanananchi wa Tanganyika na si wa nchi jirani ya zanzibar.

Tusemezane
 
Nguruvi3 Unajua mkuu wangu wakati mwingine acha hata kuandika ama kujibu maana unapojibu ndio unatupoteza kabisa. sasa ikiwa wewe unaona makubaliano hayo hayana uhalali wa kuathiri katiba inakuwaje tena wewe unamtaka mume amtarakie mkewe? Wewe Mtanganyika ni sawa na mtoto alozaliwa ktk ndoa hiyo unataka vipi maswala walokubaliana mume na mke uyatolee wewe maamuzi kwa sababu tu unaathirika na ndoa yao.

Sii kinachotakiwa haswa ni wewe mtoto kutoka ktk nyumba hiyo ukaanze maisha yako? - Now utakwenda wapi ndio majibu yangu kwa hao kina Jussa watoto wa kufikia ila yanisikitisha hata nyie ndugu zangu mmejiunga nao kwa sababu ya mazoea. Na tutakapo gawana mabo sii bado utabakia na CCM au unadhani hiyo CCM itaondoka na Zanzibar maana humjui adui yako ni kunguni uliyemvaa na nguo zako. Na kibaya zaidi hao Wazanzibar usowataka na wanaopiga kelele ni samaki wadogo sana kwani mipapa yao yote yenye kuzua mgogoro huu makazi yao yapo Tanganyika na wamewekeza Tanganyika, Zanzibar ni kwenda kununua ardhi beach, mashamba ya karafuu na minazi. Hawa ndio wasotaka wewe ukanunue ardhi Zanzibar ili wao wakaiuze kwa Muuza unga wa Kitaliani au Mjarumani. Hawa watu hawanisumbui miye kwa sababu nawajua hila zao!

Tuache kurudi nyuma kuendeleza Ubishani juu ya mambo tulokwisha yatolea maelezo, isipokuwa nakuomba wewe, Barubaru, UKAWA na wengine wote wanaosoma mada hii waniambie wanachokifahamu wao kwa nini tume zote walojaribu kuandaa muundo mpya wa JMT walikwama ilipofikia ' Tanganyika itaimeza Zanzibar' ikiwa zitaundwa serikali 1 au serikali 3 ni gharama kubwa.
1..Je kuimeza huko walikuwa na maana gani? itamezwa vipi, na utafiti wao ulionyesha nini huko kumezwa ama kudhihirika kwa hizo gharama kubwa za serikali 3 ktk uchunguzi wao.
2. Je, Mnaweza kutoa mifano kusherehesha majibu, kisha
3. Naomba pia mnambie leo hii huu ushirika wa Shirikisho na serikali 3 leo hiii zinatoa majibu gani tofauti ambayo miaka ya nyuma isingewezekana!.

Tafadhali tusirudishene nyuma ktk mjadala tulokwisha utolea maelezo, twende mbele na kwa kituo. Naomba maelezo ya swali langu kenu nyote halafu tuendelee maana haitakuwa akili kutoa maelezo kibao wakati swala lilotukwaza kwa miaka yote hatufahamu hata ilikuwa ikimaanisha nini..

Mkandara,

Ahali yangu kuna mengi sana ya kuyaongelea katika huo muundo wa sasa wa muungano kwani kuna ukakasi mwingi sana na haiwezekani abadan, asilan kuuondoa ukakasi huo.

Kumbuka Muungano wa Tanzania una sura mbili kwa wakti mmoja. Kama ukibahatika kuutazama ukitokea Znz utauoana tofauti kabisa na ukiutazama ukitokea Tanganyika. Hilo ni tatizo kubwa kitu kimoja kuonekana tofauti kutokana na upande utakaotazama dubwana hilo muungano.

Lakin kubwa Znz ni nchi huru yenye mila, sirka utamaduni wake toka dahli na dahali na wana Historia yao . Vile vile Tanganyika ni nchi huru na wakaazi wake wana mila na desturi zao na historia zao. Je itawezekana kuzificha au kuzipoteza historia hizo na mila na desturi hizo.

Mfano mzuri ni mimi mwenyewe baba na mama yangu wote asili yao Oman na mimi nimezaliwa Znz na kubwa zaidi kuanzia darsa la nne mpaka chuo kikuu nimesomea Tanganyika na hata kazi miaka 8 nimefanya Serikali ya JMTz kwa upande wa Tanganyika. Lakin tunarudi pale pale sijaweza kusahau asili yangu lakin pia kupaenzi na kupatetea pale nilipo zaliwa Znz.

Lakin Kubwa Mkandara, pamoja na mambo ya kijiografia ya TGK na Znz lakin pia tazama population ya nchi hizo yaani Znz ni 1.5 Mil na TGK ni zaidi ya 45 Mil. Lakin lingine TGK ina eneo la zaidi ya 450,000 Sq Km na Znz eneo lisilozidi 2,000 Sq Km.
Hizo zilikuwa ni dondoo tu za kukuelekeza katika kujadili nchi hizi mbili
.

Lakin kubwa mimi siamini kabisa kama kuna Gharama kubwa. Kwani kama mimi kama mchumi naona ni upotoshaji tu na hadaa kwa wananchi. Wachumi wanasema kila jambo zuri ni Gharama.. Unaona hata Bunge lenu la Katiba mpya si linatumia gharama katika kutaka kupata katiba mpya.. Hakuna kizuri bila gharama.

Mimi naamini NI BORA MPATE GHARAMA KATIKA KUUNDA CHOMBO BORA KULIKO KUKWEPA GHARAMA NA KUISHI KWA MAISHA YA MASHAKA , KUTUHUMIANA NA KUTOAMINIANA kama mlivyo sasa.

Kumbukeni maneno yanakua na yakishakomaa hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasilete mush'kira.

 
Mkandara,

Ahali yangu kuna mengi sana ya kuyaongelea katika huo muundo wa sasa wa muungano kwani kuna ukakasi mwingi sana na haiwezekani abadan, asilan kuuondoa ukakasi huo.

Kumbuka Muungano wa Tanzania una sura mbili kwa wakti mmoja. Kama ukibahatika kuutazama ukitokea Znz utauoana tofauti kabisa na ukiutazama ukitokea Tanganyika. Hilo ni tatizo kubwa kitu kimoja kuonekana tofauti kutokana na upande utakaotazama dubwana hilo muungano.

Lakin kubwa Znz ni nchi huru yenye mila, sirka utamaduni wake toka dahli na dahali na wana Historia yao . Vile vile Tanganyika ni nchi huru na wakaazi wake wana mila na desturi zao na historia zao. Je itawezekana kuzificha au kuzipoteza historia hizo na mila na desturi hizo.

Mfano mzuri ni mimi mwenyewe baba na mama yangu wote asili yao Oman na mimi nimezaliwa Znz na kubwa zaidi kuanzia darsa la nne mpaka chuo kikuu nimesomea Tanganyika na hata kazi miaka 8 nimefanya Serikali ya JMTz kwa upande wa Tanganyika. Lakin tunarudi pale pale sijaweza kusahau asili yangu lakin pia kupaenzi na kupatetea pale nilipo zaliwa Znz.

Lakin Kubwa Mkandara, pamoja na mambo ya kijiografia ya TGK na Znz lakin pia tazama population ya nchi hizo yaani Znz ni 1.5 Mil na TGK ni zaidi ya 45 Mil. Lakin lingine TGK ina eneo la zaidi ya 450,000 Sq Km na Znz eneo lisilozidi 2,000 Sq Km.
Hizo zilikuwa ni dondoo tu za kukuelekeza katika kujadili nchi hizi mbili
.

Lakin kubwa mimi siamini kabisa kama kuna Gharama kubwa. Kwani kama mimi kama mchumi naona ni upotoshaji tu na hadaa kwa wananchi. Wachumi wanasema kila jambo zuri ni Gharama.. Unaona hata Bunge lenu la Katiba mpya si linatumia gharama katika kutaka kupata katiba mpya.. Hakuna kizuri bila gharama.

Mimi naamini NI BORA MPATE GHARAMA KATIKA KUUNDA CHOMBO BORA KULIKO KUKWEPA GHARAMA NA KUISHI KWA MAISHA YA MASHAKA , KUTUHUMIANA NA KUTOAMINIANA kama mlivyo sasa.

Kumbukeni maneno yanakua na yakishakomaa hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasilete mush'kira.

Mkuu wangu alhan Wasahlan, Kwanza Eid Mubarak,

Mimi nitakwamba ukweli wangu juu ya Historia yako na ile ya Zanzibar na wapi tunatofautiana. Uzawa wako na asili yako kwangu sii hoja bali fikra zako ndizo nazipinga kwa sababu hu represent Uzanzibar bali Asili na nasaba yako na fikra zako zinalenga kuhalalisha kisichowezekana.

Kwanza, nikwambie tu ya kwamba Zanzibar haikuwa huru ila baada ya Mapinduzi! hii kubali usikubali na ndipo tunaposhindana. Na sababu haswa ni kwamba huu uhuru wa Zanzibar ulitoka kwa mtawala gani? maana alokuwa akitawala miaka yote ni Sultan ambaye aliomba hifadhi ya Muingereza kama kinga kuepuka Uvamizi wa Mreno, hivyo swala la Muingereza kuruhusu uchaguzi na kumpa mwanya Sultan kugombea uongozi ulitokana na kutokuwepo na hofu ama Mreno. hivyo aliwajibika kutrudisha utawala ule kwa wenyewe. Utanisamehe lakini kusema kwamba Uhuru wa mwaka 1963 wa Zanzibar hiyo ni sawa kabisa na Uhuru wa Rhodesia November 11 1963 hivi ndivyo inavyoonekana kwa waafrika wote regardless of their race or colour. Na sidhani kama wewe umesimama hapa kutetea Utawala wa Jamheed toka kwa Muingereza alowapa hifadhi, bali Uhuru wa Wazanizbar toka utawala wa kisultan.

Unaweza kuwa Mwarabu mwenye asili ya Oman lakini hukubaliania na utawala wa Sultan na labda nikukumbushe tu ya kwamba wapo makaburu waliokataa Uhuru wa mwaka 1963 wakashirikiana na wenyeji hadi Uhuru kamili wa Zimbabwe ulipopatikana mwaka 1980. yalofuata Allahu Yaalam na wanapigana kumwondoa Mugabe sio tena kaburu maana limeshapita wala hakuna anayezungumzia Uhuru wa mwaka 1963. Hivyo sitokushauri utumie sana asili yako kuhalalisha Uhuru wa Zanzibar kwani Sultan ndiye alikuwa mtawala kabla ya Uhuru na ndiye alokuja kupata ushindi ktk uchaguzi wa mwaka 1963 kwa mchezo mchafu wa kisiasa kama aloufanya Ian Smith.

Tuyaache hayo, ila nakuomba unapozungumzia Zanzibar izungumzie kama mzawa mwenye haki ya kushiriki sawa na Wazanzibar wengine ktk Zanzibar hii huru ambayo inatakiwa kuheshimu haki ya Uraia wako kama mzawa na mwenye historia kubwa na nchi hiyo. Na sii asili yako maana asili yako iko Oman ambako unapa enzi hadi leo hii kama mimi navyo paenzi Ukerewe hata kama ingekuwa chini ya Utawala wa Uganda ama Kenya bado haitaondoa asili yangu maana hii mipaka imewekwa na binaadam.

Swala la Population,
hapa mimi nakubaliana na wewe sana tu lakini nisichokubalianana wewe ni kipimo mnachotumia kwa sababu Zanzibar yenye watu 1.3 Mil wanaweza kufaidika na soko la Tanganyika na zaidi ya fursa na hapo ajira zinazopatikana Tanganyika kama ulivyosema wewe ulisomea Tanganyika na ukafanya azi miaka 8. Pia kumbuka kuna zaidi ya watu mil 3 wenye asili ya Zanzibar waishio Tanganyika leo hii hivyo hesabu hii sio ndogo kama unavyofikiria acha mbali wale waloenda kuishi nje.

Tatu, Udogo wa Zanzibar

Udogo sio sababu kabisa kumezwa na Tanganyika ikiwa hatutakuwa tumeungana na kuunda serikali 1. Sidhani kama New York ama Hawaii hazikufaidika kutokana na udogo wao tena katika nchi 50. Itawezekana tu ikiwa tutaunda serikali moja maana serikali moja naweza kuimeza Znz ikawa kama Mkoa tu kwani Zanzibar haitakuwa na seirkali yake tena bali serikali moja ya Muungano. Hivyo Muungano wa serikali 2 au 3 unaondoa swala la kumezwa na ndio maana Zanzibar ina serikali yake leo hii ambayo kwa madai yenu inapewa asilimia 4.5 tu wakati mnasahau kwamba kwenye serikali ya Jamhuri Zanzibar bado ipo katika mambo ya Muungano ambayo bajeti yake huwashirikisha wabunge wa Zanzibar.

Na matumizi na wizara zote hizi za JMT, toka viongozi wake, watumishi hadi ofisi zake kote bara na Zanzibar hulipwa na serikali ya JMT sio serikali ya Znz. Kwa hiyo tusiwasikilize sana wanasiasa uchwara ambao hupotosha aidha makusudi ama kwa kutofahamu ya kwamba JMT ina mfuko wake tofauti na mfuko wa serikali ya Zanzibar na ndio maana tuna JMT kuhudumia nchi 2 na sii Tanganyika. Kwa maana ya kwamba ktk fungu la 10 ukitoa 2 za Serikali ya Znz, JMT inabakiwabakliwa na 8, hizi 8 sii za bara bali za serikali ya JMT ambayo matumizi yake hujadiliwa ktk bunge la JMT na huduma zake hufanyika pande zote mbili.

Na wala isifahamike kwa watu kwamba hizo 8 zilitakiwa kuwa za Tangayika (bara) kama wanavyofikiria kina Nguruvi3 kwa sababu tu ya mchango mdogo wa Zanzibar ktk mfuko wa taifa wakati wanashindwa kuelewa kwamba Wazanzibar mil 1.3 waishio zanzibar ni asilimia 2.9 ya watu mil.45 wa bara, hivyo Zanzibar ikichangia asilimia 3 tu ya mfuko wa Taifa wametuzidi bara (mathlan JMT imekusanya bil.10 - bil.9.7 wanatakiwa kutoka bara na Zanzibar .3) hapa huwezi kusema ati Zanzibar wananufaika. Hawa wanaosema haya nao ni wapotoshaji wengine ambao somo la uchumi limewapiga magoli kama Brazil na Ujarumani.

Kuhusu Gharama.
Watu wengi wanachukulia swala hili juu juu tu kwa kwa sababu imependekezwa serikali ya JMT kuwa na mambo ya muungano 7 tu. Hii haiwezekani mkuu wangu wa sababu serikali ya JMT hutegemea fungu kutoka serikali zake kwa ajili ya matumizi ya nchi husika. Sasa ikiwa wizara zote zilizowekwa ktk mambo 7 ya Muungano hazizalishi ila ni matumizi matupu unafikiri hiyo serikali kuu itapata wapi fedha za kujiendesha? Na kama haina mamlaka kabisa ktk mambo mengine hiyo serikali itaweza vipi kuweka dhamana juu ya maswala la maendeleo ya nchi hizo ikiwa nchi hizo hazitambuliwi kimataifa? Nani atakaye ikopesha Tanganyika ama Zanzibar pasipo mhuri wa TAIFA maana msidhani kujiunga na UN ni kutambuliwa Uhuru wa nchi na mtawala bali hupata ridhaa ya mataifa hivyo unaweza kukopeshwa ktk miradi ya maendeleo na ukafuata masharti ya kimataifa. Tangayika na zanzbar ni sawa na mtoto wa chini ya Miaka 18 na mzazi ni JMT nani atakaye kubali kumkoposha mtoto ilihali mzazi hayupo labda awe molester!

Nani atakaye ipeleka Zanzibar au Tanganyika mahakama ya Dunia ikiwa nchi hizo zitagoma kulipa mikopo yake ambayo JMT imewawekea dhamana. Je, rais wa JMT akikataa kudhaminia kitu ambacho anakiona hakina umuhimu kwa taifa itakuwaje? Na hata nchi husika wakiamua kuzitumia vibaya fedha hizo huyo rais atakuwa na mamlaka gani ya kusimamisha matumizi hayo maana hayamhusu!. haya ndio maswali tunayotakiwa kujiuliza kwanza kabla ya kuvamia kupendekeza mambo 7 ya Muungano.
Kwa hiyo haiwezekani wala haitawezekana hadi serikali kuu ihusike kikamilifu na maswala ya maendeleo ya nchi hizi japo mipango ya utekelezaji wa shughuli hizo zitapitishwa na kutekelezwa na nchi husika. Na sheria zitakuwepo za JMT na zile za kila nchi ambazo serikali ya JMT haiwezi kupindua.

Halafu, kumbuka lile swala la 10-2 ikabakia 8 ya JMT hili haitakuwepo tena kwa sababu JMT haitakuwa na 10 tena bali Tanganyika na 7.7 kwa sababu Zanzibar hawatachangiza .3 zao, hivyo wao watasubiri kipenga. Na wizara za visiwani/bara hazitapungua ila kutakuwa na ongezeko la matumizi kwa mambo yote isipokuwa hayo 7 ya muungano ni sawa na kusema kati ya 22 za mambo ya muungano toa 7 kuna mambo 14 yatakuwa mzigo mpya kwa bara na visiwani ambao ni maskini. Ni rahisi sana kusema kwani asilimia .3 kitu gani, ila nakuhakikishia hiyo asilimia inaweza kuvunja muungano kwa sababu haitaonekana faida ya kuwa na mambo 7 yanayo wagharimu pande zote pasipo kuwepo vyanzo vya mapato yake yenyewe. Itakuwa swala la mtu una deep ndani ya mfuko wako kugharamia mambo 7 wakati kuna mambo 14 muhimu kwa wananchi wako ambayo yanahitaji fedha,huu utakuwa wendawazimu!. Ni sawa na Mapenzi ukanyimwa Unyumbashughuli yake kubwa sana, japo wanasayansi wanasema huo unyumba ni asilimia 1 tu mambo muhimu ktk ndoa.... I wonder!.

Kuna usemi huku Canada na Marekani watu husema hivi, inakuwaje Marekani au Canada wana madeni ya Trillioni za dollar wakidaiwa na nchi za nje, hawalipi madeni hayo bali wao ndio hutoa mikopo na misaada kwa nchi maskini kwa mabillioni? kwa nini wasitumie fedha hizo kulipa madeni yao?.. Jibu lake ni kwamba mikopo na misaada hiyo ndiyo biashara yenyewe ya Utandawazi, ni sawa na benki inayokupa mkopo wewe mkopo, wao hawana fedha mkononi bali wewe unayeweka akiba ya fedha zako benki ndizo huzunguka kwa kukopesha wengine na wao huvuta interest na mikataba ambayo huwanufaisha benki sio wewe. Hivyo Marekani wanapotupa sisi mikopo wao hufaidika na masharti yenye interest na mikataba mibovu kama tunayowapa hivyo hutengeneza mara 10 ya msaada walioutoa. Sisi woote ni wateja wa nchi matajiri na hivyo hawataisha kutukopesha ili wao watajirike.

Sasa wewe nambie hizi serikali kugharamia hayo mambo 7 ya Muungano watafaidika vipi kiuchumi wakati wangekuwa na nguvu zaidi kama yangekuwa yao, na kwa nini wasichukue mzigo mzima wenyewe? yaani kuua Muungano kabisa hata kama ni wa Shirikisho. Lini maskini wakashirikiana ktk matatizo ya ikadumu kama sio ndugu?
 
Mkuu Mkandara
Naomba nipitie hoja zako kwa majibu haya nitakayoyagawanya katika vifungu kwa urahisi wa wasomaji kufuatilia. Yote yanatoka katika bandiko lako hapo juu

Sehemu ya I
Mkandara;10185722]Kwanza, nikwambie tu ya kwamba Zanzibar haikuwa huru ila baada ya Mapinduzi! hii kubali maana al Utanisamehe lakini kusema kwamba Uhuru wa mwaka 1963 wa Zanzibar hiyo ni sawa kabisa na Uhuru wa Rhodesia November 11 1963 hivi ndivyo inavyoonekana kwa waafrika wote regardless of their race or colour
Awali ya yote Eid Mubarak.

Kwa kuongezea ni sawa na uhuru wa Africa kusini ulivyokuwa, kutoka kwa mwingereza kwenda kwa kaburu.
The bottom-line mwafrika hakuwa huru, ilikuwa kubadilisha kati ya Mwingereza na Mwarabu. Hilo ndilo chimbuko la Mapinduzi ya 1964.
Mkandara;10185722Hivyo sitokushauri utumie sana asili yako kuhalalisha Uhuru wa Zanzibar kwani Sultan ndiye alikuwa mtawala kabla ya Uhuru na ndiye alokuja kupata ushindi ktk uchaguzi wa mwaka 1963 kwa mchezo mchafu wa kisiasa kama aloufanya Ian Smith
Ndivyo Ian Smith alivyotawala akimtumia Askofu Abel Muzorewa.M
kandara;10185722 Swala la Population,hapa mimi nakubaliana na wewe sana tu lakini nisichokubalianana wewe ni kipimo mnachotumia kwa sababu Zanzibar yenye watu 1.3 Mil wanaweza kufaidika na soko la Tanganyika na zaidi ya fursa na hapo ajira zinazopatikana
Huu ni ukweli usioweza kupingika. Laiti wazanzibar wasingekuwa na faida na muungano wangeshaondoka.Kijiografia, kibiashara, kijamii na kiusalama Zanzibar inategemea Tanganyika.Ushahidi wa kufadika ni nusu yao kuishi Tanganyika kuliko sehemu nyingine duniani

kama si kweli hakuna sababu za kuwalazimisha, waha hiari ya kutafuta partner mwingine.
Mkandara;10185722 Udogo wa Zanzibar .Udogo sio sababu kabisa kumezwa na Tanganyika ikiwa hatutakuwa tumeungana na kuunda serikali 1. Sidhani kama New York ama Hawaii hazikufaidika kutokana na udogo wao tena katika nchi 50.

Itawezekana tu ikiwa tutaunda serikali moja maana serikali moja naweza kuimeza Znz ikawa kama Mkoa tu kwani Zanzibar haitakuwa na seirkali yake tena bali serikali moja ya Muungano.

Hivyo Muungano wa serikali 2 au 3 unaondoa swala la kumezwa na ndio maana Zanzibar ina serikali yake leo hii ambayo kwa madai yenu inapewa asilimia 4.5 tu wakati mnasahau kwamba kwenye serikali ya Jamhuri Zanzibar bado ipo katika mambo ya Muungano ambayo bajeti yake huwashirikisha wabunge wa Zanzibar.

Na matumizi na wizara zote hizi za JMT, toka viongozi wake, watumishi hadi ofisi zake kote bara na Zanzibar hulipwa na serikali ya JMT sio serikali ya Znz. Kwa hiyo tusiwasikilize sana wanasiasa uchwara ambao hupotosha aidha makusudi ama kwa kutofahamu ya kwamba JMT ina mfuko wake tofauti na mfuko wa serikali ya Zanzibar na ndio maana tuna JMT kuhudumia nchi 2 na sii Tanganyika. Kwa maana ya kwamba ktk fungu la 10 ukitoa 2 za Serikali ya Znz, JMT inabakiwabakliwa na 8, hizi 8 sii za bara bali za serikali ya JMT ambayo matumizi yake hujadiliwa ktk bunge la JMT na huduma zake hufanyika pande zote mbili.
Kuungana kuwa serikali 1 hakuwezekani.

Unaposema znz iwe na serikali yake unazungumzia dhana ile ile ya kuwa serikali moja ni impossible.
Katika muungano ukishatoa unjustifiable preference hupati muungano mmoja tena.

Wabunge kuwashirikisha si tatizo. Hakuna sababu za mbunge aliyekuja kama wazanzibar kuongelea mambo ya Tanganyika.

Mbunge wa kigoma anaweza kuongelea mambo ya Kilimanjaro kwasababu ni wawakilishi wa maeneo tofauti ya sehemu moja inayoitwa Tanganyika.

Unaposema wabunge wa Zanzibar na huko juu umetoa uhalali wa wao kuwa na serikali yao, tayari umewatofutisha na wale wa Kigoma na Kilimanjaro. Kuwabagua huko kwa nia njema ndiko kunawa wafanya wawe useless katika bunge la JMT.

Laiti wangelikuja kama wabunge wa Kiembe samaki na kwamtipura, ingeeleweka japo kidogo.
Wao wanakuja kama wabunge wa Zanzibar yenye serikali yake.

Tena kuna wanaotoka BLW la SMZ kuja bunge la JMT.
Hakuna mbunge wa JMT anayeingia BLW. Kwanini kuwe na one way na siyo two way traffic kama tu nchi moja.

Kuhusu mfuko wa 10, hapo unakosea. Huwezi kutoa 2 za Zanzibar zikabaki 8.

Katika 8 ambazo ni za Tanganyika ukasema znz imo.
Hapo ndipo hatukubaliani kama ambavyo Duni haji amesema, gesi ya Mtwara ni ya muungano.
Gesi ya Zanzibar ni ya Zanzibar. Hiyo ndiyo 2,8 na 10 unayoongelea. Hapo mkuu haikubaliki.

Hoja yako kuhusu 8 katika fungu la 10 ni kuwa kuna misaada na mikopo.
Kufikiria kuwa muungano upo kutokana na misaada na mikopo is a very primitive way of thinking.

Misaada na mikopo ni dhalili na umesema interest zake hapo juu zinavyotumiwa na Canada na Marekani.
Kwamba, muungano unategemea hilo inasikitisha.

Kwanini tusiangalie kuwa mapato ya Tanganyika net ni 12Trilioni. Mapato ya Zanzibar ni 400 Bilioni.
Halafu tujiulize katika fungu la 8, Zanzibar inachangia asilimia ngapi. Hata kama ni 0.0001, je inachangia?

Haji Duni(Waziri wa Afya), Ali Salehe( Mwakilishi wa CUF na adui wa Tanganyika, Salmin Awad(Katibu mkuu wa CCM Zanzibar) ambao ni Key opinion leaders visiwani na ellite so as to speak, wamethibitisha kutochangia hata senti.

Hoja inayojengwa ni kuwa wachangie wapi kama hakuna mfuko wa pamoja.
Well, wanawezaje kuchukua 4.5% na pesa za kufidia bajeti, huduma n.k. kutoka JMT bila kujua zinatoka wapi na kwa utaratibu gani.

Wanawezaje kukubali huduma za ulinzi na usalama, mambo ya ndani, nje na nyinginezo kutoka JMT ambayo wao wenyewe wamekiri hawachangii, halafu wakakataa kuchangia kwa kukosa mfuko. Hivi huoni kuna uhayawani hapo.

Ni sawa na Mkandara na Nguruvi kuwa na duka la pamoja.
Duka hilo ni mtaji wangu ila mkandara yupo kwasababu tuliamua kulianzisha pamoja.

Mkandara hataki kuongeza mtaji wa duka letu, lakini yupo tayari kuona namnunulia mkewe khanga, nanunulia vibinti vyake Ipod, Yule kijana wake namnunulia k-ku dengriz, Mkandara haulizi pesa zinatoaka akautnti gani ya duka, kaka kimyaaa.
Anachosema, mkewe anahitaji vitenge, gold n.k.
 
Sehemu ya II

Mkandara;10185722 Na wala isifahamike kwa watu kwamba hizo 8 zilitakiwa kuwa za Tangayika (bara) kama wanavyofikiria kina Nguruvi3 kwa sababu tu ya mchango mdogo wa Zanzibar ktk mfuko wa taifa wakati wanashindwa kuelewa kwamba Wazanzibar mil 1.3 waishio zanzibar ni asilimia 2.9 ya watu mil.45 wa bara, hivyo Zanzibar ikichangia asilimia 3 tu ya mfuko wa Taifa wametuzidi bara (mathlan JMT imekusanya bil.10 - bil.7.7 ni a bara na Zanzibar .3) hapa huwezi kusema ati Zanzibar wananufaika.

Hawa wanaosema haya nao ni wapotoshaji wengine ambao somo la uchumi limewapiga magoli kama Brazil na Ujarumani.
Ndipo usipotuelewa, tunasema hivi hata kama ni 0.00001 lazima wachangie. Kwa sasa ni sifuri.

Pili, lazima uelewe nani ameanza kufungua Pandora box.

Hawa wazanzibar unaosema mchango wao wa 03% mkubwa, wanapata wapi uhalali wa kudai mambo kwa usawa?

Fikiria kuwa tume ya Warioba wazanzibar waligoma hadi wapewe 50%.
Matumizi ya tume ni takribani bilioni 60. Kama wznz wangelipa 3% unayosema kutokana na population yao, wangechangia 3% ya bilioni 60, hiyo ni sawa na 1.8 Bilioni.

Walichokisema ni kuwa pesa zinatoka JMT. Well,kama zinatoka JMT ambako kuna znz na Tanganyika, wale wajumbe 15 sawa wanalipiwaje na JMT huku Tanganyika ikiwa haina wajumbe?

Usichanganyikiwe hapa. Tunaposema Tanganyika haina wajumbe, ni kwasababu wabunge wa JMT wakiwemo wznz ndio waliokwenda BML kwa kofia ya JMT na si Tanganyika.

Hivyo SMZ ililazimika kulipia 50% ya wajumbe wake waliokwenda kwa masilahi ya Zanzibar na si JMT.

Je, hili nalo lilihitaji account? Kwamba bill ya bilioni 60 haijulikani hadi account. Ni afadhali sikusoma uchumi.

Madai ya znz kuhusu usawa ndiyo yanachagiza Watanganyika wajiulize, inakuwaje Wazanzibar ni wazuri sana wa kudai vyeo, fursa kwa usawa, tunapofikia kuwajibika wao hukimbilia udogo na uchache?

Arguably kuna suala la siasa na uchumi. Kwamba, nafasi kama za utawala ni za kisiasa.
Ni wapi tunaweza kutenga siasa na uchumi kama separate entity tukabaki kuwa salama?

Unatakiwa ujiulize, kwanini kumekuwa na kelele za wazanzibar kutochangia. Nini mkimebadilika siku hizi.

Ni lazima kuwe na balance, huwezi kulalamika eti upewe nafasi za utawala ikiwa huna wajibu wala wa kile unachoenda kusimamia.

Hebu niambie , kwa mwendo huu ambao znz wamegoma kuchangia muungano hata kwa 0.001, unawezaje kuwa na rais wa JMT kutoka znz akaheshimika

Pili, kama znz kwa 3% ina mchango mkubwa, je kwa fursa kama ajira nini mchango wao?
Na kama ni 3% yenye maana, ni hesabu gani zinawapa 21% ya ajira?
Mkandara;10185722 Kuhusu Gharama.
Watu wengi wanachukulia swala hili juu juu tu kwa kwa sababu imependekezwa serikali ya JMT kuwa na mambo ya muungano 7 tu. Hii haiwezekani mkuu wangu wa sababu serikali ya JMT hutegemea fungu kutoka serikali zake kwa ajili ya matumizi ya nchi husika. Sasa ikiwa wizara zote zilizowekwa ktk mambo 7 ya Muungano hazizalishi ila ni matumizi matupu unafikiri hiyo serikali kuu itapata wapi fedha za kujiendesha?
Na hapa ndipo hueleweki. Kwani sasa hivi inapata wapi?
Mkandara;10185722 Na kama serikali ya shirikisho haina mamlaka kabisa ktk mambo mengine hiyo serikali itaweza vipi kuweka dhamana juu ya maswala la maendeleo ya nchi hizo ikiwa nchi hizo hazitambuliwi kimataifa?
Si kweli, sasa hivi Tanzania inadhamini asilimia 88 ya madeni ya Zanzibar ambayo haitambuliki kimataifa.

Iweje kuwe na tatizo kukiwa na Tanganyika? Nadhani uanze kwanza kupinga udhamini wa Zanzibar kutoka JMT.
Kinyume chake, ni kiwewe tu cha uwepo wa Tanzania ndicho kinakusukuma kuandika majibu na si maswali
Mkandara;10185722 Nani atakaye ikopesha Tanganyika ama Zanzibar pasipo mhuri wa TAIFA maana msidhani kujiunga na UN ni kutambuliwa Uhuru wa nchi na mtawala bali hupata ridhaa ya mataifa hivyo unaweza kukopeshwa ktk miradi ya maendeleo na ukafuata masharti ya kimataifa. Tangayika na zanzbar ni sawa na mtoto wa chini ya Miaka 18 na mzazi ni JMT nani atakaye kubali kumkoposha mtoto ilihali mzazi hayupo labda awe molester!
Si kweli, na wewe kupitia uzi wako umethibitisha kuwa inawezekana.Katika uzi huo umesema ili kuondoa matatizo ya muungano, Zanzibar iruhusiwe kukopa nje(Ushahidi upo wa maneno yako)

Leo uwepo wa Tanganyika tayari unafuta hoja yako uliyosema ya Zanzibar ipewe fursa za kukopa.
Hapa kuna tatizo gani mkuu?

Kwanini uwepo wa Tanganyika uwe kikwazo lakini status quo unaipa upper hand tena ukisema Zanzibar iruhusiwe kukopa.

Kinachofanyika hapa ni Tanganyika ijivue koti(umesema sana) ili nayo iende kukopa kama Zanzibar ilivyopewa fursa hizo sasa hivi ikidhaminiwa na JMT bila kuwepo kikwazo cha UN.

Hakuna suala la UN wala nini, kama ulikubali kuwa znz ikope na ipewe fursa za kujiunga na mashirika, leo tunaposema Tanganyika ipewe fursa hiyo ili ijivue koti, tayari unageukia UN n.k. Mkuu double standards haifai.

Stick to the point, siyo kuyumba yumba . Nina evidence za maneno yako, kinachonishangaza ni kuabadilika kila siku.
Mkandara;10185722 Nani atakaye ipeleka Zanzibar au Tanganyika mahakama ya Dunia ikiwa nchi hizo zitagoma kulipa mikopo yake ambayo JMT imewawekea dhamana. Je, rais wa JMT akikataa kudhaminia kitu ambacho anakiona hakina umuhimu kwa taifa itakuwaje?
Na hata nchi husika wakiamua kuzitumia vibaya fedha hizo huyo rais atakuwa na mamlaka gani ya kusimamisha matumizi hayo maana hayamhusu!. haya ndio maswali tunayotakiwa kujiuliza kwanza kabla ya kuvamia kupendekeza mambo 7 ya Muungano.
Mkuu rudi kasome rasimu uielewe kwanza.

Pili, wewe umesema mara nyingi kwamba znz ipewe fursa zake pekee za kukopa. Fursa hizo imepewa.
Je, ikikataa kulipa nani atapelekwa mahakama ya Dunia? Kama itakayopelekwa mahakamani ni JMT iliyodhamini 88% ya madeni ya znz, kwanini uwepo wa Tanganyika ubadilishe equation nzima.

Ndicho kilichopo sasa hivi, tunachotaka kufanya ni kuongeza Tanganyika katika utaratibu unaotumika sasa hivi.

Rais wa JMT kwa mujibu wa rasimu hana kazi ya kuomba misaada na mikopo.

Rasimu imesema ‘endapo' kutakuwa na ulazima, JMT itawajibika kuwadhamini washirika.

Siyo suala la Rais kukubali tu, ni suala la vyombo vya rais kutathmini kuwa znz au Tanganyika zitakuwa na uwezo wa kulipa.
Ndiyo maana kuna bunge la JMT na vyombo vingine muhimu.

Kama nchi washirika zitatumia vibaya hiyo ni shauri yao. Hata sasa hivi zinatumia vibaya kama radar n.k.
Mbona huoni tatizo, bali S3 ndilo tatizo kubwa kwako? Kwa mfano, JMT imedhamini asilimia 88 ya deni la znz.
Nani anajua zinalipia nini.

Si kazi ya rais kujua SMZ imeafanyia nini, ni wajibu wake kujua kama znz inalipa deni husika. Period.
Na ndivyo itakavyokuwa kwa Tanganyika.Kwanini Tanganyika inakupa kiwewe mkuu.

Mkandara;10185722 Halafu, kumbuka lile swala la 10-2 ikabakia 8 ya JMT hili haitakuwepo tena kwa sababu JMT haitakuwa na 10 tena bali Tanganyika na 7.7 kwa sababu Zanzibar hawatachangiza .3 zao, hivyo wao watasubiri kipenga. Na wizara za visiwani/bara hazitapungua ila kutakuwa na ongezeko la matumizi kwa mabo yote isipokuwa hayo 7 ya muungano ni sawa na kusema kati ya 22 za mambo ya muungano toa 7 kuna mambo 14 yatakuwa mzigo mpya kwa bara na visiwani ambao ni maskini.
Mkuu usizunguke mbuyu. Kuna mambo 14 ambayo kila mshirika atabeba.

Kwa upande wa Tanganyika , kwasasa inayabeba yote 14. Hivyo hatutarajii kuna tofauti yoyote zaidi ya kupungua kwa mzigo.
Kwa upande wa znz itabidi wajifunze kuishi na mambo 14 waliokuwa hawana.

Hivyo hakuna suala la kugawana umasikini hapa. Lipo suala la kugawana majukumu na wajibu.
Tueleze kwa kupunguza mambo hadi 14, Tanganyika imepoteza nini kiasi cha kudhani tunagawana umasikini.

Znz haiwezi kujificha nyuma ya Tanganyika ikisema ''sisi''. Wakati wa kuwajibika inasema wao.
Hilo sasa linafikia mwisho.Hakuna kugawana umasiki mkuu. Kila mshirika atawajibika kwa watu wake.

Tena hapo juu umesema znz kwa idadi yake inachangia zaidi asilimia 3 kuliko Tanganyika.
Sisi tunasema hilo ni jambo jema, wapewe nafasi ya kutumia asilimia zao kwa maendeleo yao.

Na sisi Tanganyika hatuna kinyongo na wao kutumia kilicho chao.

Tunachukizwa wanapotumia chetu na kutulaumu kwa kuwasaidia. Hatupendi tunataka kuvua koti.
Kama wanataka tuwe wamoja, jibu ni S1.

Vinginevyo S2 ni njia ya kutaka wazanzibar waendele kunufaika katika mgongo wetu.

Sasa hivi hakuna kurudi nyuma, kila mtu aonje machungu ya muungano.
Hapo wznz wataheshimu muungano.

Kwasasa wanachukulia muungano ni haki yao, sisi tunasema ni haki yetu sote kuvuna na kuchomwa miiba.
Wazo lako la kuwa na JMT na SMZ linakataa kabisa logic zako.

Na wala Tanganyika haiwezi kuwa na nafuu kwa kuwa na znz. Ndio maana tunasema hakuna kugawana umasikini.
Mchango wao kwetu sisi ni negligible, tunagawana umasikini upi. Sisi ni masikini tu bila znz, na uwepo wao haupunguzi umasikini wetu zaidi ya kuongeza
Mkandara;10185722 Ni rahisi sana kusema kwani asilimia .3 kitu gani, ila nakuhakikishia hiyo asilimia inaweza kuvunja muungano kwa sababu haitaonekana faida ya kuwa na mambo 7 yanayo wagharimu pande zote pasipo kuwepo vyanzo vya mapato yake yenyewe. itakuja swala la mtu una deep ndani ya mfuko wako kugharamia mambo 7 wakati kuna mambo 14 muhimu kwa wananchi wako ambayo yanahitaji fedha! huu wenzdawazimu.!.
Mkandara, wewe umesema tumechukua mambo yote na kuyafanya muungano na hilo linawanyima wazanzibar fursa( bandiko lipo ukitaka kuliona).

Ukasema mambo yalikuwa 11 sasa ni 22 ambayo znz inaumia.
Ukatoa mifano mingi tu ikiwemo OIC bandari n.k. Leo tunapunguza kutoka 22 hadi 7 ikiwa ni pungufu ya yale 11 ya awali unageuza kibao.

Wazanzibar wanasema kwa ukubwa wan chi yao na watu wake hawahitaji mambo ya Tanganyika yawe ya muungano.

Wanalalamika kwanini kuwe na ujenzi wa reli ya muungano ikiwa kwao haihitajiki.
Solution ondoa hilo.
 
Sehemu ya III

Mkandara hataki Tanganyika izinduke kwa kujua kuwa muungano utakuwa na uzito kwa zanzibar.
Anachokisema, tuwe na JMT na SMZ kwasababu Zanzibar inapaswa kupewa preference katika muungano kwasababu asizoziweka wazi.

Hofu kubwa ya Mkandara ni uwepo wa Tanganyika utakaondoa utegemezi wa Zanzibar kwa jina la JMT.
Mkuu anajichanganya pale anapolaumu Tanganyika kuvaa koti la muungano huku ikigoma isilivue

Hoja kubwa ya wazanzibar ni Tanganyika kunufaika kwa kuwa katika kivuli cha Tanzania.
Faida wanazosisema Wznz na Mkandara ni mikopo na misaada.
Wao wanaamini muungano wetu umesimamimshwa na misaada na mikopo.

Katika hali ya kawaida ya kufikiri kitimamu, ni jambo la kushangaza pale baba mwenye nyumba atakapopanga bajeti ya nyumbani kwake na mkewe kwa kuangalia mikopo dukani kwa masawee au Mpemba.

Mantiki inasema, bajeti ni kile unachokipata na unachotarajia kutumia na si msaada au mkopo wa usio na uhakika nao.

Tanganyika wanasema, ili kuvua koti la muungano lazima izinduke na iwe kando kama zanzibar ilivyo.
Halafu, tuangalie bajeti zetu mikononi hata kama ni ndogo kiasi gani ili tuone tunaweza kufanya nini kwa pamoja.

Katika kuvua koti, Tanganyika tunataka tuwe na serikali yetu itakayopanga mipango yetu bila kuingiliwa au kuingilia SMZ.

Hakuna sababu za Tanganyika kubeba muungano huu wenyewe huku Wazanzibar wakitumia flimpsy argument za kutokuwepo kwa account.

SMZ haikuweza kulipa umeme na mishara kwa miaka zaidi ya 30, leo account hiyo ingechangiwa na nini.

Wabunge wa znz pale Dodoma wanalipwa kutoka account gani. Mona hilo hawahoji
Wafanyakazi wa muungano wanalipwa kutoka account gani. Mbona hilo hawahoji
Mishahara ya kwenda SMZ tangu zama za komandoo hadi sasa inatoka account gani Dar es salaam

Ile fidia ya bajeti yao inayotoka muungano, inatoka account gani
Gharama za kusomesha waoto wao bure zinatoka account gani
Gharama za usalama na ulinzi zinatoka account gani wanaoijua wao

Gharama za shirika la bandari znz zinazolipwa na Tanzania maritime zinatoka account gani

Linapofika suala la gharama wznz wanakimbilia hoja dhaifu na hafifu ya account ya pamoja.
Kinachoshangaza ni wepesi sana wa kudai vyeo, madaraka na nafasi za ubalozi.

Wakati umefika wa kuwaeleimisha kuwa ubalozi ni ofisi yenye gharama, si vacation centre au employement centre.
Wakiongelea ubalozi watangulize gharama kwanza. Kama hawajui gharama hawana uhalali wa kudai wasichogharamia.


Ali Salehe anayehoji account ya pamoja, hajawaambia wazanzibar mamilioni aliyovuna kutoka tume ya Warioba yanatoka katika account gani ya pamoja.

Gharama za usafiri wa Maalim Seif na Rais Shein kwa kutumia vyombo vya muungano zinatoka account gani ya pamoja

Hoja ya kwamba znz inaweza kuchangia ni ya ajabu sana. Kwasasa pato la znz kwa mwaka ni bilioni 400.
Pesa wanazopata kutoka katika pato la taifa ni 4.5%Kumbuka hii si ya muungano ni ya Tanganyika kutoka trilllioni 12.

Endapo wataweka hiyo mikopo na misaada, basi hakuna deni linalokwenda SMZ.

Kwa hesabu za kawaida hiyo ni karibia na sawa na pato la znz kwa mwaka. Ukweli huu upingwe kwa namba.

Mkuu Mkandara anataka Znz ibaki na madaraka yake, anganyika iwe Tanzania ili znz iweze kutumia jina kupata inachokitaka.

Kwa Watanganyika, hakuna kitu wanachopata ambacho nje ya muungano wataweza kukikosa.
Ni kweli kama tungeungana kama nchi moja hiyo ni dalili ya nguvu, lakini wasiotaka hilo ni wazanzibar.

Wazanzibar hawataki mambo yasiyo ya muungano yakawa ya pamoja.
Kwa uchache zanzibar inavizia kwenye gharama kubwa kama ulinzi na usalama, mambo ya ndani, nje n.k.
Nje ya hapo wao sio Watanzania. Hili la ukupe linatia kinyaa

Hakuna mjumbe au kiongozi yoyote wa zanzibar anayeongelea ulinzi na usalama kama wanavyoongelea sehemu nyingine.
Katika eneo hilo kinachozungumzwa ni kugawana vyeo baasi. Gharama haziongelewi ni za Mtanganyika.

Mkandara anaposema kupunguza mambo ya muungano kutoka 22 hadi 7 ni kugawana umasikini, si kweli.
Katika mambo 14 yaliyoondolewa hakuna hata moja linalomuathiri Mtanganyika zaidi ya kumpunguzia mzigo.
Hatuwezi kugawana umasikini na zanzibar kwa viwango vya aina yoyote.

Hoja hii anaijenga ili kuonyesha kuwa znz ni muhimu kiuchumi kwa Tanganyika na ina mchango katika uchumi huu.
Umuhimu wa znz katika dunia ya sasa ya uchumi ni namba na si siasa.

Mkandara anapaswa kutonyesha kwa namba ni wapi na kwavipi Watanganyika wananufaika na muungano huu.

Hoja ya mikopo na misaada ukiachilia mbali kuwa ni primitive, bado inabaki kuwa na ukweli kuwa nje ya muungano nchi hizi zitakopa tu. Sasa suala la kulipa ni dhima ya kila taifa.

Kuendelea kukopa au kupata misaada inayoambatana na manyanyaso na matusi ya wazanzibar ni kujivunjia heshima.
Hatuna sababu za kuvaa koti la muungano au kujificha ili kunyonya kisichokuwepo.
Tunataka Tanganyika ili tuamue hatima ya taifa letu kama wanavyofanya wazanzibar.

Endapo kuna eneo tunaweza kufanya kazi pamoja basi iwe ni kwa manufaa ya pande zote.
Wenyewe wanasema ndani ya EAC znz itakuwa na hadhi sawa na nchi nyingine bila muungano.
Kwa mantiki hiyo nje ya mambo 7 mengine tukutane huko EAC.

Suala asilokubali Mkandara ni kuwa zama za muungano wa kisiasa sasa zimekwisha.
Kilichopo mbele yetu ni muungano wa kiuchumi.

Hadi pale wazanzibar watakapopata uchungu wa gharama za muungano suluhu ipo mbali.

Haiwezekani rasilimali za Tanganyika zikawa za muungano halafu za znz zikawa zao tukasema tuna muungano.
 
ngurubi3,
Mimi sitaki kuendelea na mjadala na wewe kwa sababu kwanza hujui hata kwa nini kama tungekuwa na serikali moja Tanganyika ingeimeza Zanzibar, nikidhani utani umekuja na utunzi wa ngonjela kumbe hujui kweli ati - 'Kumeza kulimaanisha historia ya znz isifutike mapema nyakati hizo wakati tunajenga taifa. Ilikuwa ni symbolic gesture ya historia tu, si kicuhumi wala kijamii'.

Sasa nitaendelea vipi kujadili na mtu ambaye anayefikiri anajua kumbe hajui maswala ya muundo wa serikali?. ikiwa hujui kumezwa kwa Zanzibar ingetokanaje ati ilikuwa symbolic gesture ya historia tu inanipa picha yako kamili na sii uongo. Mkuu utanisamehe sana na samahani miye nakomea hapa labda nitajadiliana na Barubaru kama atapenda maana napoteza muda wangu kujadili usolijua.

Mtu asiyejua hata mikopo tunayozungumzia ina malengo gani kwani tungeweza vipi kuchimba mafuta pasipo mikopo, tungeweza vipi kuchimba dhahabu, makaa ya mawe kujenga viwanja vya ndege, reli, bandari na zana zake n.k pasipo mikopo. Ikiwa Marekani wenyewe wanakopeshwa itakuwaje ajabu kwa Tanzania kukopeshwa fedha kwa ajili ya maendeleo yake? Sisi tunatengeneza Matrekta? tunatengeneza Ndege? tunatengeneza vifaa vya jeshi? Swala ni mikopo gani tunayoihitaji na kwa manufaa yapi ya Taifa jambo ambalo CCM wanapwaya kwa ufisadi wao. Huyo baba mwenye kiwanja (kiwanja sii nyumba kabla hujakijenga) sio lazima awe na fedha za kujenga nyumba bali tatizo ni pale anapopoteza hadi kiwanja kwa tamaa ya fedha.
 
36 Reactions
Reply
Back
Top Bottom