Vurugu za bunge ! Inaendelea...WIZARA YA HABARI ,UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
Habari: Ni eneo linalotumika kwa mawasiliano ya jamii, mtu, watu, taasisi, vyama au serikali. Napo kuna tatizo, wengi wanadhani idara ya habari kazi yake ni kueleza tu au kutoa maelezo tu
Idara inahusisha mawasiliano ya njia mbili (two ways) ya kupata na kutoa habari.
Katika hilo ni pamoja na kueleza, kutafasiri maelezo, kuyafafanua katika kiwango kinachoeleweka na rahisi
Wizara hii ni muhimu katika maeneo yote.. Kwa upande wa serikali, ni chombo kinachoIunganisha wananchii, taasisi za ndani au nje, na serikali na serikali
Kuna nyakati inatumika kama chombo cha 'propaganda' cha serikali., zinazoweza kutetewa kimanti, busara na hoja
Tofauti na propaganda za siasa, habari za serikali zinahitaji umakini.
Tamko la wizara ni tamko la serikali na nchi kwa ujumla.
Ni taarifa zinazoweza kuleta mitafaraku au neema kutegemea zinazvyotolewa
Waziri ni Mh Nape Nanuye(MB) wa Mtama aliyekuwa katibu mwenezi wa idara ya itikadi na uenezaji ya CCM wa serikali ya awamu ya nne.
Akiwa mwanahabari, mh ana uzoefu wa kuongea na vyombo hivyo
Hata hivyo, uzoefu katika siasa za chama ni tofauti na za serikali.
Taarifa au maelezo ya vyama hayana uzito kwa kwavile ni sehemu ya propaganda za kisiasa
Taarifa za serikali au maelezo yake ni habari za nchi bila kujali itikadi za kisiasa.
Ni msimamo wa nchi na Taifa inayoweza kujenga au kubomoa
Kwa mfano, Mh Nape aliwahi kusema CCM itashinda hata kwa bao la mkono.
Kauli ni ya kisiasa na kichama imeendelea kuweka doa juu demokrasia nchini.
Katibu mwenezi anapotoa kauli hiyo inaleta hisia mbaya katika jamiii
Majuzi Mh Nape alikaririwa 'hali ya nchi ilifikia pabaya' kwa kuangalia mambo yaliyoibuliwa na serikali ya leo.
Tofauti ya kauli hizo mbili ni kubwa
Kauli ya chama inachukuliwa na alieleweka anatetea chama licha ya walakini.
Kwa mfano, hajawahi kueleza vita yake na mafisadi kwanini ilikwama
Kwasasa Mh ni waziri,kuelewa tofauti ya kauli za kichama na serikali ni muhimu.
Wizara ni kiungo katika habari na wizara au taasisi nyingine za ndani na nje.
Maelezo yanapaswa kupimwa na kuelezwa kwa ufasaha, linahitaji umakini na mtu makini
Je, tutakuwa na chombo cha uhakika cha habari au ni mwendelezo wa propaganda kama tulizoona awamu ya nne?
Ahsante na wale wote wanaotutia moyoNguruvi3,
Naendelea kufuatilia kwa makini uchambuzi wako, hakika ni darasa kubwa na lamuhimu sana. Ukitaka kushangaa kizazi cha sasa hutaona wengi wakichangia maoni uzi huu, na baadhi kama rafiki yetu kuchangia kwake ni kejeli/matusi nk
Kwa idhini yako Mkuu,naomba nikusanye uchambuzi huu pamoja ili niweze kujisomea/kutafukuri zaidi siku zijazo.