Duru za Siasa: Awamu ya 5 - Uongozi na Yanayojiri

Mkuu wewe bure kabisa upo hapa kuongea pumba zaidi, hii ni Forum unajaza matapishi ya watu wezi kama kina EL na aliyewauzia Mbuzi kwenye gunia. Unasema UK hawana Constitution. Usilete elimu za shule za kata, kukariri bila kufahamu kwa tarifa yako how does the UK is governed:

''Unlike most modern states, Britain does not have a codified constitution but an unwritten one formed of Acts of Parliament, court judgments and conventions. Professor Robert Blackburn explains this system, including Magna Carta’s place within it, and asks whether the UK should now have a written constitution.''

- See more at: Britain's unwritten constitution

Sasa angalia hiyo magna-carta ni ya lini? BTW nini maana ya Katiba? You can call it whatever you want Wacha kuwa gwiji la kujaza server wakati hakuna anayesoma mambo ya udaku. Badilika na andika vitu ambavyo vitasaidia nchi hii kwenda mbele. Uchaguzi umekwisha subiri 2020 kama mtabahatika lakini kwa mwendo wa JPM hamtaambulia kitu.
Katiba ikiwa unwritten inaeleweka vipi?

Nadhani anayepaswa ''kulalamika'' kuhusu server ni wamiliki wa JF,siyo wewe
Midhali wananipa fursa, hayo mengine hayakuhusu

Kama unasoma mambo yasiyokupendeza, kwanini unasoma? Si uache!

Nina ushahidi wapo wanasoma, mmoja wao ni wewe, ukisema hawapo unashangaza wakati unasoma kwa bidiii kabisa teh teh teh

Maandishi mekundu ni kukazia hoja zako, hata wewe unajua hazisimami zenyewe

Ahsante kwa mchango wako, tunashukuru sana tuache wapuuzi tuendelee wewe kaa pembeni soma kinachokufaa. Hulazimishwi kusoma hapa, nini hasa kinakukera?

Tena unasema watu hawasomi, sasa unakereka na nini? Si uache tu nipoteze muda wangu mwenyewe

Wana duru tutaendelea na wizara ya mambo ya ndani
 
Katiba ikiwa unwritten inaeleweka vipi?

Nadhani anayepaswa ''kulalamika'' kuhusu server ni wamiliki wa JF,siyo wewe
Midhali wananipa fursa, hayo mengine hayakuhusu

Kama unasoma mambo yasiyokupendeza, kwanini unasoma? Si uache!

Nina ushahidi wapo wanasoma, mmoja wao ni wewe, ukisema hawapo unashangaza wakati unasoma kwa bidiii kabisa teh teh teh

Maandishi mekundu ni kukazia hoja zako, hata wewe unajua hazisimami zenyewe

Ahsante kwa mchango wako, tunashukuru sana tuache wapuuzi tuendelee wewe kaa pembeni soma kinachokufaa. Hulazimishwi kusoma hapa, nini hasa kinakukera?

Tena unasema watu hawasomi, sasa unakereka na nini? Si uache tu nipoteze muda wangu mwenyewe

Wana duru tutaendelea na wizara ya mambo ya ndani


Haieleweki kwa waliosoma shule za kata. Waingereza wamekuwa wanaifuata hiyo tangu enzi hizo na wanatumia Acts tu (Viraka) kuiboresha wewe unafikiri waliyoandika hiyo ya kwetu wangekuwa na mawazo kama yako pengine usingekuwepo hapa ulipo leo.

Siwezi kupotezea kwa sababu unayoandika mengi ni upotoshaji ni sawa na kuwaacha ISIS wafanye wanavyotaka ati tu kwa sababu wana kasumba yao.

Kuhusu server usifikiri JF iliota kama uyoga, kuna watu ambao walijitolea kwa hali na mali, wewe imeiona ipo unafahamu chimbuko lake, unafahamu ilikuwa katika mikiki mikiki gani na kina nani ndio walikuwa hapa kuiwezesha. Wacha kuropoka kwa mambo ambayo hufahamu.
 
WIZARA YA MAMBO YA NDANI

Kwa haraka inaonekana kama wizara nyepesi,kiuhalisi imebeba dhamana kubwa ya usalama wa wananchi.

Vyombo vya usalama kama Polisi, Magereza , uhamiaji ni sehemu yake

Changamoto zinazoikbaili wizara hii ni kuzorota kwa hali ya usalama kutokana na ongezeko la vitendo vya uhalifu ikiwemo ujambazi.

Kuna idara ya uhamiaji inayohusika na Uraia, makazi na wageni
Kumekuwepo na ongezeko la wakazi haramu katika maeneo ya nchi.

Hilo linaweza kuwa tishio siku za usoni kama halitaangaliwa kwa jicho pevu

Hati za kusafiria ni tatizo la muda mrefu linalohitaji kudhibitiwa pia
Pamoja na matumizi ya teknolijia ya kisasa, bado kughushiwa hakujulikani chanzo halisi.

Lipo tatizo la msongamano katika magereza na ule utaratibu wa parole uliobuniwa miaka michache hauonekani kuzaa matunda.

Waziri wake ni Mbunge Mh Charles Kitwanga wa Misungwi.

Hii ni moja ya wizara za muungano. Kwa kuelewa hilo, naibu wake ni Mh Hamad Y Masauni. Huyu ni mbunge wa Kikwajuni kutokea Zanzibar

Uteuzi wa Masauni unakumbusha sakata la umri wake.

Katika chaguzi za CCM vijana, jina lake lilleta mtafaruaku ikisemwa amedanganya umri.
Alivuliwa uenyekiti wa UV-CCM 2010- Iringa

Mwenyekiti wa CCM akiwahi kuseama kilichomponza Masauni ni kughushi umri

Hakuna taarifa zingne endapo Mh Masauni aliwahi kutoa maelezo tofauti au kuthibitishwa hakuwa na tatizo kuhusu umri wake na tuhuma za kughushi zilizomkabili.

Mh Masauni kijana msomi katika uhandisi ndye naibu waziri wa mambo ya ndani akimsaidia waziri katika changamoto nyingi na nzito zinazoikabili wizara zikiwemo uhalifu wa nguvu na silaha, wahamiaji haramu,magereza na uhalifu wa kughushi hati na nyaraka nyingine za serikali

Inaendelea... Wizara ya sharia na katiba
 
WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Ni wizara iliyokuwa na majukumu makubwa mwishoni mwa awamu ya nne

Iliongozwa na Mh Asha Rose Migiro, mwanasheria mbobevu katika fani

Wizara ilishirikiana na serikali kuandaa miswada ikiwemo ule wa kuanzisha mchakato wa katiba mpya

Baadhi ya sheria zilipingwa na kuzua mitafaruku. Wapinzani wakisusia na kutoka nje ya bunge.

Hali haikuwa nzuri katika bunge la katiba lililozaa kile kinachojulikana -UKAWA

Mchakato uliacha 'wahanga' wa kisiasa. CCM iliyoendeleza ilikumbana na chuki kutoka katika jamii.

Kama yapo mambo yaliyoudhi wananchi bila kujali itikadi za kisiasa ni katiba

Kupitia mchakato ulioshindwa kufuata kanuni za kidemokrasia na za utungaji wa katiba, watu maarufu wamepoteza nafasi au heshima katika jamii. Kwa sasa wanaonekana kudhalilika

CCM ilisitisha mchakato baada ya kubaini wengi hawaafiki na ingeiondoa CCM madarakani

Wapo wahanga wa kisiasa ndani ya CCM yenyewe na wengine katika jamii

Jambo moja linaloshtua jamii sasa hivi ni kuona baadhi ya walioshiriki kuandaa katiba pendekezwa majina yao yamesomeka katika taasisi zilizo na matatizo wakiwa wajumbe wa bodi zilizovunjwa

Jambo hilo linatia shaka si uteuzi tu wa wajumbe bali umakini wao.
linazidi kushadidia hoja, mchakato ulitekwa na kuwa wa vyama kukiwa na ombwe la kuongoza.

Katiba ilishindikana na kubaki donda kwa uongozi wa awamu ya nne. Ni moja ya felia za awamu hiyo

Katiba pendekezwa kama itaendelea, lipo tatizo. Kwamba, kabla ya kura ya maoni ni lazima sheria zirudishwe bungeni, zilizokuwepo muda wake umeisha. Hilo linaweza kuzua kizaa zaa kingine tena

Mabadiliko ya hali ya kisiasa visiwani yatachangia hatma ya katiba. Hali ikibaki kama inavyosemwa, nguvu ya CCM kupitisha miswada kibabe itakumbana na upinzani kutoka upande wa pili wa nchi

Waziri ni Mh Mwakyembe aliyetumikia awamu ya nne katika wizara kadhaa.
Ni mwanasheria aliyebobea na mtajwa katika nafasi ya uwaziri mkuu.

Mh alijizolea umaarufu kupitia kamati ya bunge iliyochunguza suala la Richmond

Mh waziri amekaririwa akisema, moja ya kazi alizopewa ni kumalizia mchakato wa katiba,kuendeleza ulipoishia-katiba pendekezwa

Tunasisitiza kuwa mchakato uliopo na hali ya kisiasa unaweza kupoteza agenda zote zilizopo mezani.

Suala la katiba ni zito na lenye umuhimu kwa wananchi. Limeligawa Taifa na tusingependa ijirudie

Serikali ya awamu ya tano ikitaka kupoteza kuungwa mkono, ijaribu kulipeleka suala hilo kinguvu

Suala la katiba ni changamoto kubwa sana na linahitaji umakini wa hali ya juu

Inaendelea....
 
Last edited:
WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA

Ofisi ya makamu wa Rais imepewa jukumu la kawaida la muungano na mazingira. Ndivyo serikali zilizopita zilivyojihusisha na masuala hayo.

Katika hali iliyopo ya changamoto za muungano, hii ni 'wizara' muhimu sana
Makamu wa Rais alitumikia nafasi ya waziri wa nchi muungano awamu ya 4

Busara zinahitajika kwani changamoto ya muungano ipo na huenda mambo ya Zanzibar yakifikia muafaka agenda itarudi ikisaidiwa na wapinzani

Waziri wa nchi ni Mh Makamba aliyekuwa kiongozi wa timu ya kampeni .m Pia Mh aligombea Urais hatua za awali.Mh alikuwa naibu waziri awamu ya 4

Kumbu kumbu zinaonyesha, mijadala mingi iliyohusisha mambo ya muungano, waziri alisimama na chama chake. Uzoefu wake kidogo katika mambo ya muungano uta weza kuzibwa na uzoefu wa makamu wa Rais.

Kwa mtazamo wetu, mambo ya muungano huongozwa na ukomavu wa kisiasa na busara. Ni mambo tete yanayohitaji kuangaliwa kwa masilahi mapana ya nchi na busara zikitawala.

Hii ni ''wizara'' moja inayohusu mambo ya muungano

Itaendelea
Nguruvi3 naomba kwenye bandiko hili, nielekeze mjadala wangu kwenye maswala ya mazingira.
kwa kiwango kikubwa sana katika nchi hii swala hili la mazingira limekuwa likipewa uwanja mdogo sana. yaani hiki kitengo cha mazingira kipo kana kwamba sio kitu muhimu kwenye hii dunia.

kiukweli mie nilipenda sana maswala ya mazingira yawe linked na wizara ya afya moja kwa moja. Kiukweli huwez kuseparate hizi sekta mbili. na kwasabb ya kuzitenganisha ndio mana hata kitengo cha wizara ya afya kinachohusika na usafi kipo kama hakipo ndani ya wizara ya afya. yaani ofisi zake tu ni uchafu achilia mbali kazi yake ya kuratibu uteketezaj taka.

kwa mtazamo wangu niliona kutenga wizara ya mazingira kutoka wizara ya afya ndiko kunako changia maswala ya mazingira kuwa yanayumbayumba sana.

ikumbukwe kwamba changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi, yana athari kubwa sana za kiafya.
 
JF katika ubora wake yaani mtu anauliza swala kwa hoehae ambaye ndio anaonekana ati ni mfahamu wa mambo, kama kweli huu ndio ugwiji kwa mambo ambayo yapo kwenye website za Tanzania tuna kazi kubwa ya kuliokoa hili Taifa na ukiritimba wa magwiji wa kutoka kwenye shule za kata. Wakiingia JF wanakuwa mabigwa baada ya kuandika mara mbili tatu. That said ndio sababu kuna wengi ambao ndio mabingwa haswa wa mambo wamekaa pembeni wanachungulia jinsi Watanzania wanavyolishwa matapishi. Tufike mahali tukemee upimbi. JF haikuanzishwa kuwapumbaza Watanzania.
 
That said ndio sababu kuna wengi ambao ndio mabingwa haswa wa mambo wamekaa pembeni wanachungulia jinsi Watanzania wanavyolishwa matapishi.

Tufike mahali tukemee upimbi. JF haikuanzishwa kuwapumbaza Watanzania.
Hakuna Watanzania wanaolishwa matapishi au kupumbazwa! Nakuhakikishia hakuna. Thibitisha kama wapo na nani anawalisha matapisha
 
Hakuna Watanzania wanaolishwa matapishi au kupumbazwa! Nakuhakikishia hakuna. Thibitisha kama wapo na nani anawalisha matapisha

Soma ulichoandika tangu uanzishe hii thread kuna mambo mengi ambayo sio kweli. Nilitoa viambatanisho mwanzo ambavyo ulishindwa kujibu ukaamua kujibu hoja chache nilizoibua. Nikafahamu uwezo wako wa kujibu hoja ni zero, kama huwezi kujibu hoja ni sawa na kuwalisha watu matapishi (soma #16 nilikuuliza nini?) wakiamini kwamba unayosema ni kweli.
 
Soma ulichoandika tangu uanzishe hii thread kuna mambo mengi ambayo sio kweli. Nilitoa viambatanisho mwanzo ambavyo ulishindwa kujibu ukaamua kujibu hoja chache nilizoibua. Nikafahamu uwezo wako wa kujibu hoja ni zero, kama huwezi kujibu hoja ni sawa na kuwalisha watu matapishi (soma #16 nilikuuliza nini?) wakiamini kwamba unayosema ni kweli.
Swali ni kuwa Watanzania gani wanapumbuzwa au kulishwa matapishi?
Hili ndilo swali unalotakiwa kujibu. Nina uhakika hawalishwi, prove kwamba wapo Watanzania wanaosoma na kulishwa matapishwi.

Kama hakuna basi huna sababu ya kuhangaika!

Pili, kuna kujibu hoja na kujibu matusi. Ukisoma mabandiko yako asilimia 99.99 ni matusi.
Mtu mwenye akili hajibu matusi kwa matusi, anapuuza, huo ndio uungwana na ukomavu wa akili

Lengo lako ni kupoteza maana ya thread ili tuingie katika majadiliano yasiyo na mantiki na hoja
Inaonyesha unakereka sana lakini ukweli utasemwa, unachotakiwa ni kupinga kwa hoja, kama huna hoja, unatulia misumari iingie. Tunasimama katika Utaifa na hilo hatuna mjadala nalo

Kwenye matusi tulishafeli mtihani, hatuwezi kurudia tena

Hatuondoki kwenye hoja tutapita kila mahali kwa kuangalia bila kuonea au kuhurumia. Ukweli tu

wizara ya ujenzi inafuata
 
Last edited:
WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO

Wizara hii imezichukua wizara za ujeniz, mawasiliano na mawasiliano kwa pamoja na kuwa moja.
Ni wizara inayosimama shughuli za ujenzi hasa miundo mbinu, uchukuzi wa njia zote na mawasiliano

Wizara ina majukumu mazito. Kusimamia miradi yote ya miundo mbinu

Changamoto kubwa ni ufufuaji wa relI kupunguza gharama za uchukuzi na kuimarisha barabara.

Jambo zuri, Rais amefanya kazi katika wizara ya ujenzi na kufahamu mengi.

Eneo lenye changamoto ni mawasiliano. Kuna makampuni ya simu yaliyohodhi biashara inayokadiriwa katika Trilion,imchango wa kodi uukiwa haonekani wazi.

Katika orodha ya Walipa kodi wakubwa, kampuni za vinywaji zingekaribiana na za simu, ni tofauti

Kuna tatizo gani makampuni haya hayafanyi vizuri katika mchango wa kodi?

Waziri ni Prof Mbarawa wa Zanzibar na mbunge wa kuteuliwa.
Awamu ya nne alikuwa waziri wa sayansi, mawasiliano na teknolojia

Mh Mbarawa alishiriki uanzishwaji wa sheria ya mitandao

Mh alikumbana na sakata la kodi za 'simcard' akiwa waziri liloleta sintofahamu kubwa

NI wakati wa sakata hilo, Mh alisaidiwa na Naibu wake Mh Makamba, waziri wa nchi ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira

Mh Mbarawa aliteuliwa waziri wa maji na umwagiliaji kwa siku kadhaa kabla ya kuhamishiwa.
Wizara ya maji na umwailiaji si kati ya mambo ya muungano.

Wizara ya uchukuzi , mawasiliano na ujenzi haieleweki vema.
Kwa kuwa na mamlaka tofauti za viwanja vya ndege, bandari na usafiri wa majini, wizara hii inapoteza sura ya muungano

Mh Makame ni msomi aliyebobea na mzoefu katika nafasi ya uwaziri.
Hana doa la kashfa zozote, lakini pia haeleweki sana katika utendaji wake

Swali ni je, ataweza kwenda kwa kasi ya mtangulizi wake hasa katika masuala ya ujenzi?

Ataweza kupambana na changmoto za uchukuzi?

Atafanya kipi tofauti katika sekta ya mawasiliano aliyowahi kuongoza?
Ataimudu sekta hiyo itoe huduma bora na ikachangia pato la Taifa?

Inaendelea....
 
Last edited:
Katiba ikiwa unwritten inaeleweka vipi?

Nadhani anayepaswa ''kulalamika'' kuhusu server ni wamiliki wa JF,siyo wewe
Midhali wananipa fursa, hayo mengine hayakuhusu

Kama unasoma mambo yasiyokupendeza, kwanini unasoma? Si uache!

Nina ushahidi wapo wanasoma, mmoja wao ni wewe, ukisema hawapo unashangaza wakati unasoma kwa bidiii kabisa teh teh teh

Maandishi mekundu ni kukazia hoja zako, hata wewe unajua hazisimami zenyewe

Ahsante kwa mchango wako, tunashukuru sana tuache wapuuzi tuendelee wewe kaa pembeni soma kinachokufaa. Hulazimishwi kusoma hapa, nini hasa kinakukera?

Tena unasema watu hawasomi, sasa unakereka na nini? Si uache tu nipoteze muda wangu mwenyewe

Wana duru tutaendelea na wizara ya mambo ya ndani


Sasa hapo ndio umesema nini? Ndio U-bogus wenyewe, yaani ni upimbi kwa kwenda mbele. Nilikwambia nchi yetu haiwezi kuendelea kama watu bogus kama wewe ni wengi, wamekalia majungu jungu tu. Wadanganye waliosomea shule za kata hapa umegonga mwamba, what a loser!
 
Sasa hapo ndio umesema nini?

Ndio U-bogus wenyewe, yaani ni upimbi kwa kwenda mbele.

Nilikwambia nchi yetu haiwezi kuendelea kama watu bogus kama wewe ni wengi, wamekalia majungu jungu tu. Wadanganye waliosomea shule za kata hapa umegonga mwamba, what a loser!
Bandiko 30 nimekuuliza, una ushahidi wa watu kupumbazwa au kulishwa matapishi? Watu hao ni akina nani kama wapo? Haya mengine unayonukuu si ulishatukana1 mbona unarudia tena.

Unacghopaswa kufanya ni kuonyesha majungu na kisha kuweka ukweli. Kama huonyeshi basi unachoandika ni majungu kuliko unayosoma

Nia yako ni kutuondoa katika mjadala ili twende kwenye matusi. Mtihani wa matusi tulifeli wengine na hatuhitaji suplementary
Njia ya busara ya kujibu tusi si kutoa tusi

Wanaduru inayofuata ni Wizara ya Habari na maelezo

Itaendelea
 
Bandiko 30 nimekuuliza, una ushahidi wa watu kupumbazwa au kulishwa matapishi? Watu hao ni akina nani kama wapo? Haya mengine unayonukuu si ulishatukana1 mbona unarudia tena.

Unacghopaswa kufanya ni kuonyesha majungu na kisha kuweka ukweli. Kama huonyeshi basi unachoandika ni majungu kuliko unayosoma

Nia yako ni kutuondoa katika mjadala ili twende kwenye matusi. Mtihani wa matusi tulifeli wengine na hatuhitaji suplementary
Njia ya busara ya kujibu tusi si kutoa tusi

Wanaduru inayofuata ni Wizara ya Habari na maelezo

Itaendelea

Sasa ulikuwa unajikomba komba kwangu ili iwe nini? Nikuonee huruma? Uliuliza swali nikakujibu ukaamua kukwepa maswali ya msingi ndio tunaita huo ni U-pimbi .. Grow up!
 
Sasa ulikuwa unajikomba komba kwangu ili iwe nini? Nikuonee huruma? Uliuliza swali nikakujibu ukaamua kukwepa maswali ya msingi ndio tunaita huo ni U-pimbi .. Grow up!
Swali, watanzania wapi wanapumbazwa maana upo kwenye rekodi ukisema watu hawasomi haya mabandiko na wala hatuwasiliani nao. Siku mbili baadaye unasema watu wanapumbazwa! mkuu hizi flip flop zinatokana na nini?

Mabandiko yapo na yantokana kila asubuhi hakuna namna unaweza kutupindisha turudi katika matusi aukujadili uanchotaka.

Sikukukualika umekuja mwenyewe, nijikombe kwa lipi? Huna unachoandika bali kutukana kinachoanidikwa !

Dawa ni chungu lakini lazima tunywe! misumari itaingia tu mkuu, hakuna kuonea au kuhurumiana

Inafuata wizara ya habari na Maelezo
 
WIZARA YA HABARI ,UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

Michezo imebaki na umuhimu tokea Enzi,inatumika kuwaunganisha wananchi nakutoa burudani, kuwasahaulisha wananchi katika maisha ya kila siku

Siku za karibuni, Sanaa imepewa kipaumbele kwa mchango wa ajira kwa na kutumiwa na wanasiasa. Ujumbe kupitia wasanii una nguvu zisizoweza kubezwa

Utamduni, ni eneo tusilolifahamu. Wengi wanadhani ni kucheza ngoma . Wanasahau maana halisi ya utamaduni kama mjumuisho wa tabia, desturi, mila ,vitu ,Sanaa na jamii nzima ilivyo

Chombo kinachobeba utamaduni ni lugha ikiwa yenyewe ni sehemu ya utamaduni husika. Ni eneo tusilolijua na tusilolipa kipaumbele stahili

Habari: Ni eneo linalotumika kwa mawasiliano ya jamii, mtu, watu, taasisi, vyama au serikali. Napo kuna tatizo, wengi wanadhani idara ya habari kazi yake ni kueleza tu au kutoa maelezo tu

Idara inahusisha mawasiliano ya njia mbili (two ways) ya kupata na kutoa habari. Katika hilo ni pamoja na kueleza, kutafasiri maelezo, kuyafafanua katika kiwango kinachoeleweka na rahisi

Wizara hii ni muhimu katika maeneo yote.. Kwa upande wa serikali, ni chombo kinachoIunganisha wananchii, taasisi za ndani au nje, na serikali na serikali

Kuna nyakati Idara inatumika kama chombo cha 'propaganda' cha serikali., zinazoweza kutetewa kimanti, busara na hoja

Tofauti na propaganda za siasa, habari za serikali zinahitaji umakini.
Tamko la wizara ni tamko la serikali na nchi kwa ujumla.

Ni taarifa zinazoweza kuleta mitafaraku au neema kutegemea zinazvyotolewa

Waziri ni Mh Nape Nanuye(MB) wa Mtama aliyekuwa katibu mwenezi wa idara ya itikadi na uenezaji ya CCM wa serikali ya awamu ya nne.

Akiwa mwanahabari, mh ana uzoefu wa kuongea na vyombo hivyo

Hata hivyo, uzoefu katika siasa za chama ni tofauti na za serikali.
Taarifa au maelezo ya vyama hayana uzito kwa kwavile ni sehemu ya propaganda za kisiasa

Taarifa za serikali au maelezo yake ni habari za nchi bila kujali itikadi za kisiasa.
Ni msimamo wa nchi na Taifa inayoweza kujenga au kubomoa

Kwa mfano, Mh Nape aliwahi kusema CCM itashinda hata kwa bao la mkono.

Kauli ni ya kisiasa na kichama imeendelea kuweka doa juu demokrasia nchini. Katibu mwenezi anapotoa kauli hiyo inaleta hisia mbaya katika jamiii

Majuzi Mh Nnauye alikaririwa akisema 'hali ya nchi ilifikia pabaya' kwa kuangalia mambo yaliyoibuliwa na serikali ya leo.

Tofauti ya kauli hizo mbili ni kubwa

Kauli ya chama inachukuliwa na alieleweka anatetea chama licha ya walakini.
Kwa mfano, hajawahi kueleza vita yake na mafisadi kwanini ilikwama

Kwasasa Mh ni waziri,kuelewa tofauti ya kauli za kichama na serikali ni muhimu.

Wizara ni kiungo katika habari na wizara au taasisi nyingine za ndani na nje. Maelezo yanapaswa kupimwa na kuelezwa kwa ufasaha, linahitaji umakini na mtu makini

Kwa ukubwa wa wizara hii na changamoto zilizopo kazi iliyopo mbele zito
Je, heshima katika maichezo hasa ya riadha itarudi kama miaka ya 70 na 80?
Je, Taifa litaweza kujitambua kwa kuthamini na kuenzi tamaduni zake?
Je, tutakuwa na chombo cha uhakika cha habari au ni mwendelezo wa propaganda kama tulizoona awamu ya nne?

Inaendelea
 
Kama unataka habari za uhakika huwezi kusoma wikipedia kwa sababu wataandika habari moja sahihi lakini zilizobaki ni za kumagumashi gumashi tu na hapa JF tuna wale wakongwe wa Wikipedia, wanatafuna peremende za Mafisadi.
 
Jukwaa la siasa umeshambulia wengine kwa kusema haya
JF katika ubora wake, hii nayo ni topic ya kujadili. Bure kabisa, imekaa kinafiki tu kutoka kwa wanaokula na kurambaramba peremende. You guys you need to grow up!
Hakuna kipya unachoandika , kila mahali umekuwa na kihoro hasa serikali ikitajwa

Wanaduru Inaendelea Wizara ya madini na nishati
 
Jukwaa la siasa umeshambulia wengine kwa kusema haya

Hakuna kipya unachoandika , kila mahali umekuwa na kihoro hasa serikali ikitajwa

Wanaduru Inaendelea Wizara ya madini na nishati

Napenda serikali ya JPM maana inasafisha wanaokula peremende kama wewe na watoaji wake, unasemaje?
 
Napenda serikali ya JPM maana inasafisha wanaokula peremende kama wewe na watoaji wake, unasemaje?
Hizi zote ni jithada za kuvuruga mjada

Wiara ya nishati inafuata, tukimaliza tutajadili picha nzima ya baraza kisha kupitia kila hatua zilizochukuliwa tukiangalia mafanikio, faida, kukwama na maamuzi mengine

inaendelea
 
Back
Top Bottom