Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,410
- 31,395
- Thread starter
- #381
KAMATA KAMATA, VUNJA VUNJA VINATUSAIDIAJE?
NINI KIPAUMBELE CHETU KATIKA UJENZI WA TAIFA
Rais Magufuli amenukuliwa mara nyingi akisema 'Maendeleo hayana chama'.
Kwamba, maendeleo iwe kubuni, kutatua matatizo au kuendeleza hakuna uchama
Kauli hii ina maana sisi ni wamoja, tunajenga taifa moja kama Taifa na Rais
Tofauti ya itikadi za kisiasa isiwe chanzo cha kuzorotesha nchi kimaendeleo
Kuna mwendelezo wa kukamata watu na nyakati nyingine kuwaachia bila kuwafungulia mashtaka. Jambo hili ni ukikwaji wa haki za Raia na matumizi mabaya ya madaraka
Siasa za vyama vingi zina robo karne nchini na ni jambo jema hakujawahi kutokea matatizo yanayosababishwa na wanasiasa.
Yametokea matatizo kutokana na kukiuka haki za msingi za wananchi hasa za kukutana
Majuzi viongozi wa Chadema wamekamatwa Ubungo kwa amri ya DC.
Hakuna sababu zozote za kutishia usalama isipokuwa tu ni hoja za taratibu kutofuatwa
Hatudhani wapinzani wanaoongoza sehemu ya jamii yetu hawana haki ya kujadili maendeleo ya wananchi kama alivyosema Rais.
Kama maendeleo hayana chama kuna tatizo gani kila mmoja kuchagiza maendeleo?
Madiwani wamekamatwa Arusha. Hakuna maelezo ya kuridhisha bali uwepo wao chini ya vyombo vya dola. Kama kuna tukio lenye kutishia amani kwanini haisemwi?
Hiyo ni mifano michache tukilinganisha na matukio ya kamata kamata na mengine ya kuvunja maeneo kama mashamba au uwekezaji kwasababu tu wahusika ni Wapinzani
Kuvurugwa kwa shamba la M/kiti wa Chadema imeelezwa ni kulinda vyanzo vya maji. Ulinzi wa vyanzo vya maji ni muhimu sana na ni tatizo kubwa nchini.
Kushughulikia tatizo ni jambo jema, namna gani linashughulikiwa ni jambo jingine
Hatuamini kama viongozi wanAotenda hayo wamemwelewa mh Rais na kauli mbiu ya Maendeleo. Imefika mahali wananchi wanahisi kuna 'maagizo' zaidi kutoka kwingine
Viongozi wanaotenda hayo kwa utaratibu usiofaa wanachonganisha serikali na wananchi, wanapanda chuki katika jamii, wanakiuka desturi na taratibu zinazozingatia utawala wa sheria.
Kinachoshangaza viongozi hawalioni hilo kama tatizo kana kwamba kuna ''baraka zao''
Wakati huo huo viongozi wa CCM wakiendelea kutenda bila kuguswa na vyombo dola
Tuna matatizo makubwa kama ujambazi kule Rufiji unaotishia amani na usalama wa wananchi na vyombo vya dola.
Ujambazi umesababisha vifo vingi kuliko matatizo yanayotokana na siasa kwa muda mrefu sana. Haya ndiyo kipaumbele chetu
Katika miezi sita tumepoteza Askari wetu zaidi ya 10 kwa matukio ya ujambazi
Katika kipindi hicho hakuna askari hata mmoja aliyepata tatizo kutokana na siasa
Hivi tunawawezaje kuamini kuwa siasa na wanasiasa wanaotembea mitaani , wanaoishi nasi na tunaowajua wamekuwa tatizo kubwa kuliko majambazi yanayoumiza Raia na Askari kule Rufiji! Je, tunatumia rationale gani kutoa vipaumbele kwa matatizo yetu!
Tusitumie muda na akili kwa mambo yasiyosaidia Taifa bali kujenga chuki na uhasama
Mambo ya siasa yasifike mahali yanavuruga nchi ,hayaruhusu shughuli za maendeleo, yanakiuka haki za binadamu na yanachagiza matumizi mabaya ya madaraka
Tatizo lililopo mbele yetu ni usalama hasa Rufiji, si wanasiasa wanaokutana kujadiliana tu
Tusemezane
NINI KIPAUMBELE CHETU KATIKA UJENZI WA TAIFA
Rais Magufuli amenukuliwa mara nyingi akisema 'Maendeleo hayana chama'.
Kwamba, maendeleo iwe kubuni, kutatua matatizo au kuendeleza hakuna uchama
Kauli hii ina maana sisi ni wamoja, tunajenga taifa moja kama Taifa na Rais
Tofauti ya itikadi za kisiasa isiwe chanzo cha kuzorotesha nchi kimaendeleo
Kuna mwendelezo wa kukamata watu na nyakati nyingine kuwaachia bila kuwafungulia mashtaka. Jambo hili ni ukikwaji wa haki za Raia na matumizi mabaya ya madaraka
Siasa za vyama vingi zina robo karne nchini na ni jambo jema hakujawahi kutokea matatizo yanayosababishwa na wanasiasa.
Yametokea matatizo kutokana na kukiuka haki za msingi za wananchi hasa za kukutana
Majuzi viongozi wa Chadema wamekamatwa Ubungo kwa amri ya DC.
Hakuna sababu zozote za kutishia usalama isipokuwa tu ni hoja za taratibu kutofuatwa
Hatudhani wapinzani wanaoongoza sehemu ya jamii yetu hawana haki ya kujadili maendeleo ya wananchi kama alivyosema Rais.
Kama maendeleo hayana chama kuna tatizo gani kila mmoja kuchagiza maendeleo?
Madiwani wamekamatwa Arusha. Hakuna maelezo ya kuridhisha bali uwepo wao chini ya vyombo vya dola. Kama kuna tukio lenye kutishia amani kwanini haisemwi?
Hiyo ni mifano michache tukilinganisha na matukio ya kamata kamata na mengine ya kuvunja maeneo kama mashamba au uwekezaji kwasababu tu wahusika ni Wapinzani
Kuvurugwa kwa shamba la M/kiti wa Chadema imeelezwa ni kulinda vyanzo vya maji. Ulinzi wa vyanzo vya maji ni muhimu sana na ni tatizo kubwa nchini.
Kushughulikia tatizo ni jambo jema, namna gani linashughulikiwa ni jambo jingine
Hatuamini kama viongozi wanAotenda hayo wamemwelewa mh Rais na kauli mbiu ya Maendeleo. Imefika mahali wananchi wanahisi kuna 'maagizo' zaidi kutoka kwingine
Viongozi wanaotenda hayo kwa utaratibu usiofaa wanachonganisha serikali na wananchi, wanapanda chuki katika jamii, wanakiuka desturi na taratibu zinazozingatia utawala wa sheria.
Kinachoshangaza viongozi hawalioni hilo kama tatizo kana kwamba kuna ''baraka zao''
Wakati huo huo viongozi wa CCM wakiendelea kutenda bila kuguswa na vyombo dola
Tuna matatizo makubwa kama ujambazi kule Rufiji unaotishia amani na usalama wa wananchi na vyombo vya dola.
Ujambazi umesababisha vifo vingi kuliko matatizo yanayotokana na siasa kwa muda mrefu sana. Haya ndiyo kipaumbele chetu
Katika miezi sita tumepoteza Askari wetu zaidi ya 10 kwa matukio ya ujambazi
Katika kipindi hicho hakuna askari hata mmoja aliyepata tatizo kutokana na siasa
Hivi tunawawezaje kuamini kuwa siasa na wanasiasa wanaotembea mitaani , wanaoishi nasi na tunaowajua wamekuwa tatizo kubwa kuliko majambazi yanayoumiza Raia na Askari kule Rufiji! Je, tunatumia rationale gani kutoa vipaumbele kwa matatizo yetu!
Tusitumie muda na akili kwa mambo yasiyosaidia Taifa bali kujenga chuki na uhasama
Mambo ya siasa yasifike mahali yanavuruga nchi ,hayaruhusu shughuli za maendeleo, yanakiuka haki za binadamu na yanachagiza matumizi mabaya ya madaraka
Tatizo lililopo mbele yetu ni usalama hasa Rufiji, si wanasiasa wanaokutana kujadiliana tu
Tusemezane