Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,410
- 31,395
- Thread starter
- #361
SAKATA LA MCHANGA NA BUNGE LETU
Mh SPIKA KWA HILI LA LUSINDE NA MNYIKA KUNA KUPOTOKA
Mjadala unaondelea nchini ni hatua za Serikali kupitia kamati ya Prof Mruma-'wizi' wa mchanga wa madini
Mjadala umegawanyika maeneo mawili, wanaounga mkono kwamba ni hatua nzuri za kuanzia
Hoja yao ikiwa yaliyopita si ndwele tugange yaliyopo na yajayo
Pili,wanaosema tumechelewa , tuanze na wahusika waliotufikisha hapa, kisha twende mbele
Hawa wana hoja, hatuwezi kutenda makosa yale yale, bila kuangalia tulipokosea na kwasababu gani
Katika kundi la pili, kuna kunyooshewa vidole kwa watu na taasisi.
Kwanza ni kwa CCM inayounda serikali na taasisi zinazosimamia sekta ya madini
Eneo jingine ni Bunge. CCM yenye idadi kubwa ya Wabunge ilishindwa kusimamia serikali ya CCM
Hoja ya Bunge inaeleza mchango wa Wapinzani uliozimwa kwa sauti 'ya ndiyoo', kukubali kwa wingi na si mantiki
Sakata limerudi tena bungeni. Ilitegemewa kungekuwa na kujifunza kwa namna makosa yasijirudie
Majibizano ya Mbunge Lusinde na Mnyika yamepelekea vurugu ambazo busara ingetumika zisingetokea
Spika alipoombwa 'taarifa' alisema '..unamchokoza Lusinde' akibariki kauli za Lusinde bila kujali athari zake
Mnyika aliomba kufutwa kwa kauli ya Mwizi, Spika hakumsikiliza akitaka Lusinde aendelee!!
Spika amesahau kauli ya H.Mdee ilisikika katika vipaza sauti na alichukuliwa hatua
Je, utaratibu umebadilika lini hadi kuita Askari na kumtoa Mnyika katika dhalili ya kiasi kile
Ni dhahiri Spika alitaka kusikia alichokita na si kile kinachosemwa. Kauli za 'Mwizi' hazikuwa na ladha
Spika angetumia busara kusikiliza hoja kwa utulivu yasingetokea yaliyotokea. Inasikitisha sana
Spika hakutaka kusikia jingine zaidi ya sifa alizokuwa anazimwaga Lusinde kwa Serikali
Ni utaratibu huo ndio umetufikisha hapa pa tatizo la Mchanga na madini kwa ujumla
Hoja ya Mnyika tunaibiwa dhahabu na si mchanga peke yake ina mantiki na uzito.
Ilipaswa kujadiliwa ili kutafuta majibu.
Hoja ilikuwa nzito kuliko amri ya kutumia askari ikionyesha udhaifu na mapungufu ya busara
Tusipobadilika na kujadili hoja za nchi tutaendelea kuibiwa.
Matumizi ya nguvu ya Spika hayakulisaidia Taifa kwa bahati mbaya.
Kwa hili Spika aliingia katika mtego wa kujadili viroja badala ya hoja.
Tutaendelea kuibiwa,inasikitisha inauma sana
Tusemezane
Mh SPIKA KWA HILI LA LUSINDE NA MNYIKA KUNA KUPOTOKA
Mjadala unaondelea nchini ni hatua za Serikali kupitia kamati ya Prof Mruma-'wizi' wa mchanga wa madini
Mjadala umegawanyika maeneo mawili, wanaounga mkono kwamba ni hatua nzuri za kuanzia
Hoja yao ikiwa yaliyopita si ndwele tugange yaliyopo na yajayo
Pili,wanaosema tumechelewa , tuanze na wahusika waliotufikisha hapa, kisha twende mbele
Hawa wana hoja, hatuwezi kutenda makosa yale yale, bila kuangalia tulipokosea na kwasababu gani
Katika kundi la pili, kuna kunyooshewa vidole kwa watu na taasisi.
Kwanza ni kwa CCM inayounda serikali na taasisi zinazosimamia sekta ya madini
Eneo jingine ni Bunge. CCM yenye idadi kubwa ya Wabunge ilishindwa kusimamia serikali ya CCM
Hoja ya Bunge inaeleza mchango wa Wapinzani uliozimwa kwa sauti 'ya ndiyoo', kukubali kwa wingi na si mantiki
Sakata limerudi tena bungeni. Ilitegemewa kungekuwa na kujifunza kwa namna makosa yasijirudie
Majibizano ya Mbunge Lusinde na Mnyika yamepelekea vurugu ambazo busara ingetumika zisingetokea
Spika alipoombwa 'taarifa' alisema '..unamchokoza Lusinde' akibariki kauli za Lusinde bila kujali athari zake
Mnyika aliomba kufutwa kwa kauli ya Mwizi, Spika hakumsikiliza akitaka Lusinde aendelee!!
Spika amesahau kauli ya H.Mdee ilisikika katika vipaza sauti na alichukuliwa hatua
Je, utaratibu umebadilika lini hadi kuita Askari na kumtoa Mnyika katika dhalili ya kiasi kile
Ni dhahiri Spika alitaka kusikia alichokita na si kile kinachosemwa. Kauli za 'Mwizi' hazikuwa na ladha
Spika angetumia busara kusikiliza hoja kwa utulivu yasingetokea yaliyotokea. Inasikitisha sana
Spika hakutaka kusikia jingine zaidi ya sifa alizokuwa anazimwaga Lusinde kwa Serikali
Ni utaratibu huo ndio umetufikisha hapa pa tatizo la Mchanga na madini kwa ujumla
Hoja ya Mnyika tunaibiwa dhahabu na si mchanga peke yake ina mantiki na uzito.
Ilipaswa kujadiliwa ili kutafuta majibu.
Hoja ilikuwa nzito kuliko amri ya kutumia askari ikionyesha udhaifu na mapungufu ya busara
Tusipobadilika na kujadili hoja za nchi tutaendelea kuibiwa.
Matumizi ya nguvu ya Spika hayakulisaidia Taifa kwa bahati mbaya.
Kwa hili Spika aliingia katika mtego wa kujadili viroja badala ya hoja.
Tutaendelea kuibiwa,inasikitisha inauma sana
Tusemezane