Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,410
- 31,395
- Thread starter
- #41
MGOGORO WA IRAN NA US
Hali katika mashariki bado ni tete na hainekani kuimarika katika siku za usoni
Mazishi ya Qassem, Kamanda wa kikosi cha mapinduzi yamefanyika nchini Irani
Umati uliojitokeza ni mkubwa kuwahi kuonekana katika miaka ya karibuni ukiachilia wakati wa kurejea kwa kiongozi wa kiislam Ayatollah Khomeni. Umati ulijawa na jazba ya kisasi
Kama tulivyowahi kusema si rahisi Iran kujibu mapigo kwa wakati huu wa mshtuko mkubwa.
Iran wanafahamu Marekani watakuwa wamejiandaa kukabiliana na kisasi chochote
Kwingine mashariki ya kati kama Lebanon, kauli za kisasi ndizo zilizotanda kumuadhimisha Qassem. Viongozi kama Nasrallah wa Hezbollah na makundi mengine wameapa kisasi
Hasira za watu zimeelekezwa kwa Israel pia ambayo nayo imesifu mauaji hayo
Inaeleweka shambulizi hilo limechagizwa pia na Israel inayotaka kuona Iran inapunguzwa nguvu
Israel inahofia kuwa nguvu za Iran katika mashariki ya kati zitaiweka katika wakati mgumu
Kwamba, makundi kama Hezbollah na Hamas yatapata nguvu licha ya Iran yenyewe
Nchini Iraq Bunge limeatoa azimio kwa majeshi yaMarekani kuondoka nchini humo
Marekani inajikuta katika wakati mgumu kimkakati.
Kuondoka Iraq kunapunguza nguvu za Marekani kimkakati (strategic position) kwasababu Iran na Iraq ni majirani, hivyo uwepo wa majeshi yake Iraq unafanya kazi kuwa rahisi .
Hofu ya Marekani ni kuwa kuondoka Iraq kutatoa nafasi kwa Shia wa Iraq kuungana na wenzao wa Iran, wale wa Qatar na kwingineko katika mashambulio dhidi ya Marekani kama ikitokea.
Rais Trump anatishia kuweka vikwazo Iraq, wachunguzi wanasema hilo litaileta mashariki ya kati karibu zaidi kwa kuwa na ''adui'' mmoja kwa wote
Marekani isingependa kwenda vitani na Iran kutokana na funzo la Iraq.
Hofu kubwa ni kuhusu mihemuko ya Rais Trump anayeweza kuamua jambo bila kufikiri
Iran sasa imejitoa katika nuclear deal na nchi za Ulaya ingawa inasema ipo tayari kuzungumza
Shambulio la Qassem limewapa nafasi (upper hand) katika majadiliano na nchi za Ulaya
Lengo na mkakati wa Marekani ni upi? Je, leo baada ya Qassem ipo salama kuliko jana?
Tusemezane
Hali katika mashariki bado ni tete na hainekani kuimarika katika siku za usoni
Mazishi ya Qassem, Kamanda wa kikosi cha mapinduzi yamefanyika nchini Irani
Umati uliojitokeza ni mkubwa kuwahi kuonekana katika miaka ya karibuni ukiachilia wakati wa kurejea kwa kiongozi wa kiislam Ayatollah Khomeni. Umati ulijawa na jazba ya kisasi
Kama tulivyowahi kusema si rahisi Iran kujibu mapigo kwa wakati huu wa mshtuko mkubwa.
Iran wanafahamu Marekani watakuwa wamejiandaa kukabiliana na kisasi chochote
Kwingine mashariki ya kati kama Lebanon, kauli za kisasi ndizo zilizotanda kumuadhimisha Qassem. Viongozi kama Nasrallah wa Hezbollah na makundi mengine wameapa kisasi
Hasira za watu zimeelekezwa kwa Israel pia ambayo nayo imesifu mauaji hayo
Inaeleweka shambulizi hilo limechagizwa pia na Israel inayotaka kuona Iran inapunguzwa nguvu
Israel inahofia kuwa nguvu za Iran katika mashariki ya kati zitaiweka katika wakati mgumu
Kwamba, makundi kama Hezbollah na Hamas yatapata nguvu licha ya Iran yenyewe
Nchini Iraq Bunge limeatoa azimio kwa majeshi yaMarekani kuondoka nchini humo
Marekani inajikuta katika wakati mgumu kimkakati.
Kuondoka Iraq kunapunguza nguvu za Marekani kimkakati (strategic position) kwasababu Iran na Iraq ni majirani, hivyo uwepo wa majeshi yake Iraq unafanya kazi kuwa rahisi .
Hofu ya Marekani ni kuwa kuondoka Iraq kutatoa nafasi kwa Shia wa Iraq kuungana na wenzao wa Iran, wale wa Qatar na kwingineko katika mashambulio dhidi ya Marekani kama ikitokea.
Rais Trump anatishia kuweka vikwazo Iraq, wachunguzi wanasema hilo litaileta mashariki ya kati karibu zaidi kwa kuwa na ''adui'' mmoja kwa wote
Marekani isingependa kwenda vitani na Iran kutokana na funzo la Iraq.
Hofu kubwa ni kuhusu mihemuko ya Rais Trump anayeweza kuamua jambo bila kufikiri
Iran sasa imejitoa katika nuclear deal na nchi za Ulaya ingawa inasema ipo tayari kuzungumza
Shambulio la Qassem limewapa nafasi (upper hand) katika majadiliano na nchi za Ulaya
Lengo na mkakati wa Marekani ni upi? Je, leo baada ya Qassem ipo salama kuliko jana?
Tusemezane