Dunia inazungukaje?

Kaka naanzia hapa,kwani kutembea kwa mawingu ndio kunaonyesha mbingu inatembea ?

Pili,ili kitu kisiyumbe lazima kiwe kinatembea ?
nimekuuliza maswali kwenye comment yangu kabla hujayajibu unataka uanze kuniuliza mimi na hapo unataka nikujibu wakati weye hujajibu.

nimekuuliza milima kama imeshikana n ardhi vipi itembee milima alafu ardhi iwe haitembei..?

nmekuuliza unasemaje juu ya tafsiri ya shekhe abdallah saleh kuhusu hiyo aya..?

kwakuongezea

unafikiri mawingu na mbingu vimeshikanaka kama ilivyoshikana milima na ardhi..?
 
Kaka naanzia hapa,kwani kutembea kwa mawingu ndio kunaonyesha mbingu inatembea ?

Pili,ili kitu kisiyumbe lazima kiwe kinatembea ?
kitu ili kisiyumbe lazima kiwe hakijatulia eidha kiwe kinakwenda, au kinacheza cheza au kina vibrate.

ukisemanimeweka jiwe kwenye datfari ili lisiyumbe yumbe maana yake mwanzo halikutulia.

soma kwa umakini.

Allah anasema milima inakwenda kwa maana ya kuwa ipo katika motion, na Milima imeambatana na ardhi kwa maana kam milima inatembea na ardhi nayo inatembea

kwa hyo hapo ardhi na milima vypte vinatrmbea, na dunia huwezi kuitoa ardhi na milimaukasema sio sehemu ya dunia.au unaweza ?

kwahyo dunia nayo inakwenda (inatembea) kwa sabbu imeshikana na milima naardhi.
 
sijui inaelekea wapi.

kutokujua kwangu mimi na wewe haikanushi kuwa haizunguki.

na wala sijui yangu haikanushi Aya inayosema kuwa Milima inskwenda.


unas3maje juu ya tafsiri ya shekhe abdallah saleh kuhusu iyo haya...?
Wanazuoni wamekwenda na kauli mbili,katika aya hiyo,moja wanasema ya kuwa kutembea kwa milima kunatokana na kuzunguka kwa dunia lakini mtazamo huu sio sahihi kutokana na aya iliyokuja kabla ya aya ya 88, kwani aya hizo zinazungumzia siku ya kiyama na zikapewa nguvu na aya :

9. Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso, 9
10. Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa. ( at Tur : 9 - 10 )

Kadhalika kuonyesha aya hiyo inaongelea siku ya kiyama,anasema tena Allah aliye juu :
105. Na wanakuuliza khabari za milima. Waambie: Mola wangu Mlezi ataivuruga vuruga.
106. Na ataiacha tambarare, uwanda.
107. Hutaona humo mdidimio wala muinuko. (Ta'ha : 105 - 107 )

Akasema tena Allah aliye juu :

47. Na siku tutapo iondoa milima na ukaiona ardhi iwazi, na tukawafufua - wala hatutamwacha hata mmoja kati yao ( al Kahf : 47 )

Rejea Tafsir Ibn Kathiir.

Mtazamo wangu kuhusu tarjama ya Shaykh Abdullah Saleh al Farsiy Allah amrehemu naipinga kutokana na yale yaliyosemwa na wanazuoni wakubwa wa Tafsiri juu ya aya hiyo,ya kuwa inazungumzia siku ya KIYAMA.

Allah anajua zaidi.
 
nimekuuliza maswali kwenye comment yangu kabla hujayajibu unataka uanze kuniuliza mimi na hapo unataka nikujibu wakati weye hujajibu.

nimekuuliza milima kama imeshikana n ardhi vipi itembee milima alafu ardhi iwe haitembei..?

nmekuuliza unasemaje juu ya tafsiri ya shekhe abdallah saleh kuhusu hiyo aya..?

kwakuongezea

unafikiri mawingu na mbingu vimeshikanaka kama ilivyoshikana milima na ardhi..?

Hilo nimekujibu tayari hivi punde.

Soma post yangu # 63 kuna majibu ya maswali yako.
 
kitu ili kisiyumbe lazima kiwe hakijatulia eidha kiwe kinakwenda, au kinacheza cheza au kina vibrate.

ukisemanimeweka jiwe kwenye datfari ili lisiyumbe yumbe maana yake mwanzo halikutulia.

soma kwa umakini.

Allah anasema milima inakwenda kwa maana ya kuwa ipo katika motion, na Milima imeambatana na ardhi kwa maana kam milima inatembea na ardhi nayo inatembea

kwa hyo hapo ardhi na milima vypte vinatrmbea, na dunia huwezi kuitoa ardhi na milimaukasema sio sehemu ya dunia.au unaweza ?

kwahyo dunia nayo inakwenda (inatembea) kwa sabbu imeshikana na milima naardhi.
Naona unatumia mitindo dhaifu ya kimantiki kuhitimisha,leta dalili usiendeshwe na nadharia.

Hizo aya zinazungumzia siku ya Kiyama,na hii ndi kauli yenye nguvu mbele ya wanazuoni wa Tafsiri akiwemo Abul Fidah.
 
sababu haitabadilisha kitu.


Sasa unataka nihangaike juu yako, wakati unakiri huwezi kubadilika.

Kwakweli si amini kama wewe ni yule Zurri uliyekuwa mzuri wa hoja, umekumbwa na nini kaka??!!---.


Haya na mimi naomba maelezo ya hao wafasirina unaowaamini ambao wamenukuu maelezo (hadithi) ya mtume (saw) kuhusu hiyo aya (21:33), ili na mimi nijifunze, kwani mtume (saw) alisema kutafuta elimu ni faradhi kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke.

Karibu.
 
nimekuuliza maswali kwenye comment yangu kabla hujayajibu unataka uanze kuniuliza mimi na hapo unataka nikujibu wakati weye hujajibu.

nimekuuliza milima kama imeshikana n ardhi vipi itembee milima alafu ardhi iwe haitembei..?

nmekuuliza unasemaje juu ya tafsiri ya shekhe abdallah saleh kuhusu hiyo aya..?

kwakuongezea

unafikiri mawingu na mbingu vimeshikanaka kama ilivyoshikana milima na ardhi..?
Naongezea tena hapa,na Imaam Muhammad al Amiin ash Shanqitiy anasema ya kuwa aya zote zinazozungumzia kutembea kwa Milima katika Qur'aan zinazungumzia siku ya Kiyama rejea kitabu chake cha Tafsiri "Adh'wau al Bayani" juzuu ya 6 ukurasa wa 490 na katika Tafsir Ibn Kathii juzuu ya 6 ukirasa wa 217 na shaykh Muhammad al Amiin akamalizia kwa kunukuu aya ya 20 katika surat an Nabaai(78) na surat at-Takweer(81) aya ya 3.
 
Sasa unataka nihangaike juu yako, wakati unakiri huwezi kubadilika.

Kwakweli si amini kama wewe ni yule Zurri uliyekuwa mzuri wa hoja, umekumbwa na nini kaka??!!---.


Haya na mimi naomba maelezo ya hao wafasirina unaowaamini ambao wamenukuu maelezo (hadithi) ya mtume (saw) kuhusu hiyo aya (21:33), ili na mimi nijifunze, kwani mtume (saw) alisema kutafuta elimu ni faradhi kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke.

Karibu.

Rejea Tafsir Ibn Kathiir.

Kaka hivi ndivyo nilivyo mimi. Tunatakiwa turudi kwenye asili ili kuepuka kukosea. Kila kitu kipo wazi,leo ulinishangaza sana uliposema ya kuwa Qur'aan imezungumzia "The Big Bang Theory" nikaona ya kuwa kumbe hata hiyo nadharia huijui bali unaisikia.

Kwa kukutoa tu wasi wasi japo hili sio lengo na halisaidii chochote,mimi ninaishi katika ulimwengu wa Sayansi kama elimu katika "Secular" ,O level nimesoma Sayansi, A'level kadhalika Sayansi na Chuo nikasoma mambo hayo na nina endelea kuyasoma ila Sayansi ya anga niliikataa zamani sana,nilipo ona watu mpaka muda huu bado wanaamini kuna mtu alifika Mwezini.

Almuhimu Sayansi naijua hasa misingi yake na nina uwezo wa kuikosoa.
 
Naona unatumia mitindo dhaifu ya kimantiki kuhitimisha,leta dalili usiendeshwe na nadharia.

Hizo aya zinazungumzia siku ya Kiyama,na hii ndi kauli yenye nguvu mbele ya wanazuoni wa Tafsiri akiwemo Abul Fidah.
nimeweka ile comment ili kukukumbudha kwamba sio Mimi tu ndio nasema dunia inazunguka kwa mujibu aya bali hatashekhe abdallah sheikh alfarsiy naye kaona hivyo.

lakini tukija katika ayayenyewe namna ilivyokuja naomba kuuliza.

iko wapi kauli ya Mtume juu yaufafanuzi wa aya hiyo ?

au ha ulamaa waliosema ya kuwa kutembea huko ni siku ya kiama wameegemea dalili ipi ilhali aya inataja wakati uluopo "USIIONE IMETULIA, INAKWENDA "

vipi iwe siku ya kiama wakati aya inaleta habari hizi kwa lafdhi ya sasa hivi kjuu yakitendo hicho..?

lakini pia hata hizo kauli za ulamaa wanaokataa kuzunguka dunia badi ni dhaifu kwa sababu hazina munasaba wa kueleweka wa kuonesha kwamb aya ile inazungumzia siku ya kiama.

bali zinaendana kinyume,labda waliona aya zingine zimetaja milima wakaunganiha na hii aya ndi0o ikaonekana 8nazungumzia kiama.

tena aya zenyewe zinakwenda tofauti na ile aya ya 88.Aya ya 88 inasema ya kuwa USIONE milima imetulia HIYO INAKWENDA. kwa maana ina move..

sasa aya unazozitoa zinaenda kinyume na aya hiyo ati mfano

وَإِذَا الْجِبَالُ سُيِّرَتْ

(ATTAKWIR - 3)
Na milima ikaondolewa,

hii haizungumzii kwenda kwa milima bali inazungumzia kuondolewa kwa milima milima ikiondolewa haiwezi kutembea.hivyo haina munasaba wa wazi hata kidogo..

na pia

وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا

(ANNABAA - 20)
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.

na hii pia hvyp hivyo inazungumziwa kuondolewa kwa milima haina mafungamano na ile aya kule hii ni kama hyo ya attakwiyr

sasa hapa aya inaeleza SIKU ZITAKAPO..kwa maana wakati ujao sio leo hiyo

يَوْمَ تَمُورُ السَّمَاءُ مَوْرًا

(ATT'UR - 9)
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,

umeona aya inaonesha wakati unaokuja sio leo na wakati huu. ile aya ya milima kutembea inaelzea wakati huu hapa tuliopo.

ikaenda tena ikasema..

وَتَسِيرُ الْجِبَالُ سَيْرًا

(ATT'UR - 10)
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.

hii aya inasema milima itakwenda kwa mwendo mkubwa kinyume chake milima haitokwenda kwa mwendo mdogo.

aya hii inaelezea kiama ndio maaa ikasema itakuwa inakweda KWA MWENDO mkubwaa

na aya yetu ile imesema tu kwamba milima inakwenda kwa ufundi wa mweyezi Mungu. wala aya haikusema kama inakwenda kwa mwendo mkubwa au mdogo.

sasa aya hii ya 10 nxo inaelezea kiama ya kuwa milima itakuwa inakwenda kwa mwendo mkubwa tofauti na mwendo wake wa kawaida katika aya ya 88 ya annaml.

sasa sioni mafungamao ya hizo aya na ile aya ati kuwa ina, ungumzia kiama.


kama ni hivyo ipi maana ya Allah kusema kuwa milia inakwenda kama mawingu yanavyokwenda..?

hayo mawingu yanakwenda siku ya kiama au yanakwenda hapa nyaksti hizi kabla ya kiama..?
 
nimeweka ile comment ili kukukumbudha kwamba sio Mimi tu ndio nasema dunia inazunguka kwa mujibu aya bali hatashekhe abdallah sheikh alfarsiy naye kaona hivyo.
Pili,kaka Shaykh Abdullah Saleh al Farsy Allah amrehemu tunaijua nafasi yake hasa kwetu sisi watu wa Afrika Mashariki na kati,na amefanya juhudi kubwa sana katika kuihudumia dini na sunnah,Allah amrehemu,lakini hatumfanyi kuwa ni hoja katika hili,sababu yeye hakuwa mwanachuoni wa Tafsiri na ameenda kinyume na wanazuoni wa kubwa katika hili,bali ameenda kinyume aya kwa dhati yake.
lakini tukija katika ayayenyewe namna ilivyokuja naomba kuuliza.

iko wapi kauli ya Mtume juu yaufafanuzi wa aya hiyo ?
Ukisoma elimu ya Tafsiri ya Qur'aan yaani Usul Tafsiri,wameeleza sana namna ya aya inavyofasiriwa na aina ya Tafsiri.

Aya ya Qur'aan hutafsiriwa kwa aya Qur'aan pia,na hili ndilo alilolifanya mwanachuoni huyu mkubwa wa zama zetu,Imaam Muhammad al Amiin ash Shanqitiy katika Tafsiri yake iitwayo "Adhwa' al Bayaan fii idhwah Qur'aan bil Qur'aan", shaykh huko ametafsiri Qur'aan kwa Qur'aan.

Rejea mtiririko wa aya na zile aya nilizokunukulia kwa munasaba wa milima kutembea,alichokifanya Shaykh hapo ni kutafsiri aya moja kwa kutumia aya nyingine,na hii ni aina ya kutafsiri Qur'aan.

Ama kuhusu kauli ya mtume juu ya aya hii mpaka niitafute,na mtume hawezi kuoingana na aya,maadamu aya hiyo imetafsiriwa na aya nyingine hakuna maana ya zaidi itakayo kweda kinyume na aya hizo.
au ha ulamaa waliosema ya kuwa kutembea huko ni siku ya kiama wameegemea dalili ipi ilhali aya inataja wakati uluopo "USIIONE IMETULIA, INAKWENDA "
Soma tena huko nyuma nimeweka wazi ya kuwa aya hiyo imepew nguvu na aya hizo nilizo kunukulia kuhusu kutembea kwa milima na kusambaratishwa kwake,ndio maana wanazuoni wakubwa wa Tafsiri wakahitimisha ya kuwa aya hiyo inakusudia siku ya Kiyama na si kinyume chake.
vipi iwe siku ya kiama wakati aya inaleta habari hizi kwa lafdhi ya sasa hivi kjuu yakitendo hicho..?
Soma mtiririko wa aya na rejea aya nilizo kunukulia,n pia Qur'aan ni fasaha sana,ndio maana tunatakiwa kurejea katika asili ili kujua maana ya aya. Mara ngapi yamekuja matamko ya sasa kumaanisha wkati ujao,au dhamiri ya wingi kumaanisha umoja au dhamiri ya mbali kumaanisha karibu ?
 
Rejea Tafsir Ibn Kathiir.

Kaka hivi ndivyo nilivyo mimi. Tunatakiwa turudi kwenye asili ili kuepuka kukosea. Kila kitu kipo wazi,leo ulinishangaza sana uliposema ya kuwa Qur'aan imezungumzia "The Big Bang Theory" nikaona ya kuwa kumbe hata hiyo nadharia huijui bali unaisikia.

Kwa kukutoa tu wasi wasi japo hili sio lengo na halisaidii chochote,mimi ninaishi katika ulimwengu wa Sayansi kama elimu katika "Secular" ,O level nimesoma Sayansi, A'level kadhalika Sayansi na Chuo nikasoma mambo hayo na nina endelea kuyasoma ila Sayansi ya anga niliikataa zamani sana,nilipo ona watu mpaka muda huu bado wanaamini kuna mtu alifika Mwezini.

Almuhimu Sayansi naijua hasa misingi yake na nina uwezo wa kuikosoa.


Kaka, kuna watu humu nao wanafuatilia kwa faida yao naomba utuwekee hapa hiyo tafsir ya ibn kathir ambano amenukuu hadhithi ya (za) mtume (saw) zikitoa maelezo ya hiyo aya (21:33), lengo ni kujifunza na bora zaidi kujifunza kutoka kwa huyo mtukufu wa daraja mtume Muhammad (saw).

Umenukuu juu ya "Big bang"-- Qur'an imeeleza, halikadhakika imeeleza juu ya "the Black hole", tofauti ni hii kwamba Mungu katika Qur'an ameeleza mambo hayo kwa namna yake na wanasayansi wameeleza kwa namna yao, ni kwa akili zetu ndipo tunaweza kuoanisha na kuona kwamba Wanasayansi wamefanikiwa kugundua vitu vilivyokwisha elezwa na Qur'an, hapo sasa ndipo Utukufu wa Mungu na utukufu wa Qur'an unapoonekana na hakuna kitabu chochote cha dini zingine kinachoweza kuizidi Qur'an katika jambo hilo na mambo mengi mengine.

Kaka, lazima ujue kwamba kuna elimu za sayansi za uongo na zipo za kweli, mimi ninaunga mkono elimu za sayansi za kweli. Umenukuu kuhusu habari ya watu kutua mwezini suala hili liwe la uongo au kweli bado halibatilishi elimu zingine za kweli za sayansi,

Ukisoma historia misingi ya sayansi na mahesabu na fizikia, elimu za nyota (astrology) na elimu ya tiba za leo zimewekwa na Wanasayansi wa kiislamu katika "medieval era", na hili halipingiki.

Kaka, nasubiri nipate elimu ya Ibn kathir akitoa maelezo ya aya 21:33, kwa kunukuu kauli za Al Rasulullah (saw)., nitapenda kujua ili nibadilishe msimamo wangu juu ya kuzunguka kwa dunia.
 
Umenukuu juu ya "Big bang"-- Qur'an imeeleza, halikadhakika imeeleza juu ya "the Black hole", tofauti ni hii kwamba Mungu katika Qur'an ameeleza mambo hayo kwa namna yake na wanasayansi wameeleza kwa namna yao,

Kaka unatakiwa uelewe,maelezo ya Sayansi yanakuwa yapo katika misingi yao,na haya wezi kifanana na maelezo ya Allah,ndio masana tunasema hivi hakuna Big Bang wala Black Hole katika Qur'aan.

Labda kama hizi theory huzisomi vizuri na ukazielew unaishia kuzisikia au kuzisoma juu juu.

Ukizisoma thoery hizo kwa undani hutaona mfanano hata kidogo kulingana na yale aliyo yasema Allah mtukufu.
 
Kaka unatakiwa uelewe,maelezo ya Sayansi yanakuwa yapo katika misingi yao,na haya wezi kifanana na maelezo ya Allah,ndio masana tunasema hivi hakuna Big Bang wala Black Hole katika Qur'aan.

Labda kama hizi theory huzisomi vizuri na ukazielew unaishia kuzisikia



(1) Kaka, kwanza naomba maelezo ya Ibn kathir juu ya hiyo aya 21:33, yakinukuu maneno ya mtume. Ili nipate kujifunza elimu niliyokuwa siijui.

(2) Naomba unifafanulie jinsi ulivyozielewa kwa mujibu wa wanasayansi the Big bang na the black hole, kwani labda mimi sikuwaelewa hao wanasayansi.

Mimi, kaka nataka leo niwe mwanafunzi wako, nitafurahi sana wewe uwe mwalimu wangu.
 
Kaka, lazima ujue kwamba kuna elimu za sayansi za uongo na zipo za kweli, mimi ninaunga mkono elimu za sayansi za kweli. Umenukuu kuhusu habari ya watu kutua mwezini suala hili liwe la uongo au kweli bado halibatilishi elimu zingine za kweli za sayansi,

Sijasema ya kuwa hakuna ukweli kwenye Sayansi,ila kuitafsiri aya kisayansi hapa ndipo huwa mnakosea na mnakosea sana,na hawa kina Haruh Yahya,kina Abdul Majid Zindani na mfano wao ndio wamewapoteza wengi,kwanza si wasomi wa dini,kwahiyo wanatumia fikra zao kutafsiri Qur'aan wakati kia kitu kipo wazi.
Ukisoma historia misingi ya sayansi na mahesabu na fizikia, elimu za nyota (astrology) na elimu ya tiba za leo zimewekwa na Wanasayansi wa kiislamu katika "medieval era", na hili halipingiki.

Sasa swali la msingi,je wao walikuwa wanatafsiri aya za Qur'aan kama wanavyofanya hawa wa sasa ? Fatilia hili kwa mapana zaidi utaona wapi mnakosea.
 
Pili,kaka Shaykh Abdullah Saleh al Farsy Allah amrehemu tunaijua nafasi yake hasa kwetu sisi watu wa Afrika Mashariki na kati,na amefanya juhudi kubwa sana katika kuihudumia dini na sunnah,Allah amrehemu,lakini hatumfanyi kuwa ni hoja katika hili,sababu yeye hakuwa mwanachuoni wa Tafsiri na ameenda kinyume na wanazuoni wa kubwa katika hili,bali ameenda kinyume aya kwa dhati yake.

Ukisoma elimu ya Tafsiri ya Qur'aan yaani Usul Tafsiri,wameeleza sana namna ya aya inavyofasiriwa na aina ya Tafsiri.

Aya ya Qur'aan hutafsiriwa kwa aya Qur'aan pia,na hili ndilo alilolifanya mwanachuoni huyu mkubwa wa zama zetu,Imaam Muhammad al Amiin ash Shanqitiy katika Tafsiri yake iitwayo "Adhwa' al Bayaan fii idhwah Qur'aan bil Qur'aan", shaykh huko ametafsiri Qur'aan kwa Qur'aan.

Rejea mtiririko wa aya na zile aya nilizokunukulia kwa munasaba wa milima kutembea,alichokifanya Shaykh hapo ni kutafsiri aya moja kwa kutumia aya nyingine,na hii ni aina ya kutafsiri Qur'aan.

Ama kuhusu kauli ya mtume juu ya aya hii mpaka niitafute,na mtume hawezi kuoingana na aya,maadamu aya hiyo imetafsiriwa na aya nyingine hakuna maana ya zaidi itakayo kweda kinyume na aya hizo.

Soma tena huko nyuma nimeweka wazi ya kuwa aya hiyo imepew nguvu na aya hizo nilizo kunukulia kuhusu kutembea kwa milima na kusambaratishwa kwake,ndio maana wanazuoni wakubwa wa Tafsiri wakahitimisha ya kuwa aya hiyo inakusudia siku ya Kiyama na si kinyume chake.

Soma mtiririko wa aya na rejea aya nilizo kunukulia,n pia Qur'aan ni fasaha sana,ndio maana tunatakiwa kurejea katika asili ili kujua maana ya aya. Mara ngapi yamekuja matamko ya sasa kumaanisha wkati ujao,au dhamiri ya wingi kumaanisha umoja au dhamiri ya mbali kumaanisha karibu ?
aya ulizonukuu hazina mafungamano na aya hiyo ya 88 ni vitu tofauti kabisa.

aya yetu inasema..

وَتَرَى الْجِبَالَ تَحْسَبُهَا جَامِدَةً وَهِيَ تَمُرُّ مَرَّ السَّحَابِ ۚ صُنْعَ اللَّهِ الَّذِي أَتْقَنَ كُلَّ شَيْءٍ ۚ إِنَّهُ خَبِيرٌ بِمَا تَفْعَلُونَ

[ AN-NAML - 88 ]
Na unaiona milima unaidhunia imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu. Huo ndio ufundi wa Mwenyezi Mungu aliye tengeneza vilivyo kila kitu. Hakika Yeye anazo khabari za yote myatendayo.

aya inafafanua kwamba nyakati hizi kabla ya kiama hiyo milima inakwenda kama ambavyo mawingu yanakwenda.

sasa kama hapo kinachozungumziwa ni siku ya kiama je NA KUTEMBEA KWA MAWINGU AMBAYO YANATEMBEA KAMA MILIMA INA MAANA MAWINGU NAYO YATATEMBEA SIKU YA KIAMA ?

kama utasema mawingu yatatembea siku ya kiama basi unapingana na aya hii hapa chini..

إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ وَالْفُلْكِ الَّتِي تَجْرِي فِي الْبَحْرِ بِمَا يَنفَعُ النَّاسَ وَمَا أَنزَلَ اللَّهُ مِنَ السَّمَاءِ مِن مَّاءٍ فَأَحْيَا بِهِ الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا وَبَثَّ فِيهَا مِن كُلِّ دَابَّةٍ وَتَصْرِيفِ الرِّيَاحِ وَالسَّحَابِ الْمُسَخَّرِ بَيْنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَعْقِلُونَ

[ AL - BAQARA - 164 ]
Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana, na marikebu ambazo hupita baharini kwa viwafaavyo watu, na maji anayo yateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na katika mabadiliko ya pepo, na MAWINGU YANAYO AMRISHWA KUPITA BAINA YA MBINGU NA ARDHI. bila shaka zimo Ishara kwa watu wanao zingatia.

unaona hapo mawingu yanaamrishwa kupita baina yambingu na ardhi kwa maana ya kuwa mae
wingu yanatembea baina ya hivyo viwili.

Allah ataamrisha mawingu yapite siku ya kiama au nyakati hizi....?
aya ile imetolea mfano kwaba maeingu yakwenda kwa maana kabla ya kiama hivi sasa na kile kilichotolewa mfano ni vile vile kabla ya kiama kwa maana hivi sasa.

haiwezekni Allah atoe mfano wa Aya ya kiama ailete kabla ya kiama.huo sio usahihi.

na aya nyingi Allah husifia ufundi wake anaelezea kabla ya kiama na wala hazungumzii wakati wa kiama

eti aya Allah anasifia ufundi wake alafu wewe unasema siku ya kiama ?

aya gani Allah amejisifia juu ya ufundi wa uumbaji wake alafu akakusudia kuwa hiyo ni siku ya kiama..?
 
(1) Kaka, kwanza naomba maelezo ya Ibn kathir juu ya hiyo aya 21:33, yakinukuu maneno ya mtume. Ili nipate kujifunza elimu niliyokuwa siijui.
Sasa kwanini unataka maneno ya mtume tu ? Je kama kuna aya inayofafanua aya hiyo,utaikubali au ?

Na vioi kuhusu uhalisia ?
(2) Naomba unifafanulie jinsi ulivyozielewa kwa mujibu wa wanasayansi the Big bang na the black hole, kwani labda mimi sikuwaelewa hao wanasayansi.
Nilicho kielewa mimi ni kuwa hizo ni nadharia tu ambazo wao wenyewe hawawezi kuzithibitisha.
Mimi, kaka nataka leo niwe mwanafunzi wako, nitafurahi sana wewe uwe mwalimu wangu.
Ninacho kusihi kwanza uwe unasoma Tafsiri za Qur'aan kutoka kwa wanazuoni wakubwa wa kubwa ambaa wanategemewa.
 
sasa kama hapo kinachozungumziwa ni siku ya kiama je NA KUTEMBEA KWA MAWINGU AMBAYO YANATEMBEA KAMA MILIMA INA MAANA MAWINGU NAYO YATATEMBEA SIKU YA KIAMA ?
Jifunze kuhoji kielimu na usintumie mitindo ya kivivu ya ki logic kuhoji,sababu kadhia ya mawingu iko wazi hali kadhalika kadhia ya ardhi iko wazi,kwani hata hivyo mbingu zitakuja kukunjwa.
 
unaona hapo mawingu yanaamrishwa kupita baina yambingu na ardhi kwa maana ya kuwa mae
wingu yanatembea baina ya hivyo viwili.
Hivyo vyote vinafanya kazi kwa amri ya Allah,inaonekana hujazisoma aya nilizo kunukulia,kazisome kwanza kisha uje kujenga hoja upya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom