Dunia inazungukaje?

Kijana Jua halizunguki hili weka akilini....jua ndilo linalozungukwa na vilivyomo kwenye mfumo wake....mfumo wa jua una sayari kadhaa ikiwemo dunia miezi kadhaa ukiwemo huu wa kwetu vimondo na takataka zingine zote zinalizunguka jua ambalo lina nguvu kubwa ya uvutano hivyo hakuna kinachotoka nje ya msari wake

Dunia hujizungusha yenyewe wakati huo huo ikilizunguka jua....mwezi nao unajizungusha wenyewe huku unaizunguka dunia hapo hapo inalizunguka jua pamoja na dunia
Ndio maana wakati fulani kunakuwa na kupatwa kwa jua ama mwezi kutokana na mizunguko yao
Jua ni nyota iliyo karibu na sisi nyota zingine zipo mbali sana nazo zina mifumo yao nayo huzungukwa vilevile ila siku zote nyota hazizunguki bali sayari na maumbo mengine


Mkuu, ninakuomba unapotaka kutoa hoja au kujibu swali mbele ya hadhara unatakiwa ufanye tafiti au uulize kwanza au ujisomee kabla ya kuwasilisha.

Nikwamba kila kitu kilichomo angani hakijatulia, yaani ama kinajizungusha, kinazunguka kitu kingine au kinaenda katika mwendo wa kawaida ( linear motion) kutoka sehemu moja kwenda nyingine, jua nalo linajizungusha hapohapo lilipo.

Na hayo ni matokeo ya "the big bang".
 
Mkuu, ninakuomba unapotaka kutoa hoja au kujibu swali mbele ya hadhara unatakiwa ufanye tafiti au uulize kwanza au ujisomee kabla ya kuwasilisha.

Nikwamba kila kitu kilichomo angani hakijatulia, yaani ama kinajizungusha, kinazunguka kitu kingine au kinaenda katika mwendo wa kawaida ( linear motion) kutoka sehemu moja kwenda nyingine, jua nalo linajizungusha hapohapo lilipo.

Na hayo ni matokeo ya "the big bang".
Dah tatizo mkuu umekuja muda ambao nataka nilale...nashkuru kwa kutia maguu.

Naomba kama ukiwafikishwa pitia vijiswali vyangu juu uvidadavue kimoja na kingine بإذن الله

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeishia form four ila napenda kujua haya mambo,hivyo ukija na porojo ooh huna shule kasome utapoteza muda tu,tujadili hili suala.

Kuhusu jua na mwezi hivi bila shaka vinazunguka na nadharia yake iiko madhubuti kueleweka.lakini hii ya dunia kuzunguka imekaaje mbona inakanganya sana wadau?

Hii dunia kama inazunguka tena kwa spidi kubwa sana inakuwaje wale ambao wanatoka nje ya dunia wakirudi hurudia pale pale tu hata hawatui pengine?

Yaani muweke sisimizi kwenye tufe alafu jaalia pale alipo ndo anatoka duniani anaenda mbali katika sayari zinginee.jaalia umempaisha sasa alafu alipotoka katika anga ya dunia ile dunia(tufe)likawa linazunguka kwa spidi kali sana.umepata picha?.
Sasa je ili arudi na ile kasi ya dunia yenyewe kuzunguka naweza kutua pale pale kweli?

Hawa wanaopaa wannafanyaje mpaka wanaarudi pale pale walipotokea?

Naomba tueleweshane nipo hapa kujifunza wadau.sitaki kejelii

Mokaze
Shark

AL - ANBIYAA - 33
Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga vinaogelea.

YA-SIN - 39
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe

YA-SIN - 38
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.


Sent using Jamii Forums mobile app


Mkuu Safuher, Swali ulilouliza ni swali zuri, na wahandishi wa vyombo vya anga za juu na wanasayansi hushughulika na hiyo kadhia kabla hawajarusha chombo husika angani au kabla hawajatua na chombo kutoka anga za juu. Wanachoangalia ni kitu kinachoitwa "Timing" (kwa kiswahili ni kama kutegesha) kati ya mwendo wa dunia kujizungusha katika mhimili wake na kuzunguka jua kwa sababu jukwaa la kurushia hivyo vyombo ni juu ya uso wa dunia, mfano kama wanataka kurusha satellite angani basi hicho chombo kilichobeba hiyo satellite kitasafiri katika muelekeo wa mzunguko wa dunia katika mhimili wake kutoka magharibi kwenda mashariki ili chombo hicho kipate kasi ya kutosha kutokana kuzunguka kwa dunia katika mhimili wake na hivyo kupunguza gharama za mafuta na hata muda, halikadhalika hali kama hiyo hufanyika kwa safari ya kurudi duniani.

Kifupi ni timing ndiyo inayotumika katika kufanikisha safari hizo za kwenda na kurudi.

Nilijaribu kutafuta page fulani katika google ili uipitie utapata habari fulani ambayo itakupa mwanga kiasi gulani; google:- "Launch a rocket from a spinning planet".

🌎🌎
 
Dah tatizo mkuu umekuja muda ambao nataka nilale...nashkuru kwa kutia maguu.

Naomba kama ukiwafikishwa pitia vijiswali vyangu juu uvidadavue kimoja na kingine بإذن الله

Sent using Jamii Forums mobile app



Tayari nimeshaeleza kwa kifupi kwani hiyo ni elimu pana sana na inahitaji utaalamu mkubwa wa kiueledi, nadhani watakuja wajuzi zaidi kuifafanua.

إالله يعلم
 
Dunia ina Engine yake ya kujizungushia...ipo underground kabisa ya Dunia.. ni Petrol engine na bado ni ya kizamani inatumia calbulator kuna siku za mvua huwa inapatwa na miss jet zinaziba hivyo matokeo yake ndio matetemeko tetema kama kule bukoba
 
Dunia ina Engine yake ya kujizungushia...ipo underground kabisa ya Dunia.. ni Petrol engine na bado ni ya kizamani inatumia calbulator kuna siku za mvua huwa inapatwa name miss jet zinaziba hivyo matokeo yake ndio matetemeko tetema kama kule bukoba



🌎 👈🏻 Haya dunia hiyo hapo, onyesha hiyo petrol engine yako??!!


👁👃🏻👁
👄
 
Vile vifaa vina kas kubwa kuliko dunia. Vinaweza kuikimbiza na kuipata na kuipita kisha kuisubilia. kutua kina ingia kwenye anga ya dunia kisha kinajichagulia tu pa kutua. Ukumbuke kinapokuwa katika anga ya dunia kinakuwa chini ya sheria ya mvutano wa dunia. Hivyo kinatembea kama ndege kufika pale kinapotakiwa
 
Ngoja nitulie niendele kuuliza mana naona maswali yangu umedadavua vozuri sana mpaka inaingia akilini
Tayari nimeshaeleza kwa kifupi kwani hiyo ni elimu pana sana na inahitaji utaalamu mkubwa wa kiueledi, nadhani watakuja wajuzi zaidi kuifafanua.

إالله يعلم

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, ninakuomba unapotaka kutoa hoja au kujibu swali mbele ya hadhara unatakiwa ufanye tafiti au uulize kwanza au ujisomee kabla ya kuwasilisha.

Nikwamba kila kitu kilichomo angani hakijatulia, yaani ama kinajizungusha, kinazunguka kitu kingine au kinaenda katika mwendo wa kawaida ( linear motion) kutoka sehemu moja kwenda nyingine, jua nalo linajizungusha hapohapo lilipo.

Na hayo ni matokeo ya "the big bang".
mkuu ina maana jua halimove lipo hapo hapo...?

sasa kwa nini jua pekee ndo liwe halimove na bodies zingine liwe zinamove...?
 
mkuu ina maana jua halimove lipo hapo hapo...?

sasa kwa nini jua pekee ndo liwe halimove na bodies zingine liwe zinamove...?


Ndio, jua halisogei (move/revolve/orbiting) jinsi sayari zingine zinavyofanya kulizunguka Jua, Jua ndiyo "kiini cha rejea" (reference point) ya jinsi hizo sayari za mfumo wetu (our solar system ) zinavyozunguka jua.

Licha ya jua kuto- move/revolve/orbiting katika huu mfumo wetu wa jua, lakini jua linajizungusha (rotates) lenyewe hapo lilipo na linatumia takriban masaa (saa 27) kukamilisha mzunguko wake.

Juu ya yote, mfumo wetu wa jua (solar system) unao ndugu zake (wanafamilia wenzake/ Galaxy) na familia hiyo inaitwa "milk way galaxy" na katika ulimwengu kuna galaxy nyingi mno zinazofanya "Universe", sasa wataalamu wa Sayanswanasema wanafamilia wote wa milky way Galaxy (na solar system yetu ikiwemo) zote zinazunguka (revolve/orbiting) kwenye point moja ya rejea (reference point).

Hivyo licha ya jua kutozunguka (revolve) lakini zote sayari na jua kwa pamoja zinazunguka (revolve) kwenye point moja, zinazunguka kwenye point hiyo zikiwa pamoja na wana member wenziwe wa "milky way".

Umeuliza, kwanini jua lisimove na body zingine ziwe zina move (revolve), jibu ni hivi; Mungu amefanya hivyo ili hizo body ziendelee kuwepo kwenye njia yake (orbit) kwasababu kama zitaacha ku move basi zitavutwa na Jua na hapo ndipo "Kiyama" kitatokea na ujue hata dunia yetu pia itavutwa na na kumezwa na jua na kla kitu kitasambaratika.

Allah akbar.
 
mkuu kuna ishara kweye Qurani inasema milima inakwenda.

sasa kama milima inakwenda haiwezi kuwa ishara kuwa dunia nayo inakwenda mkuu ?

Unaweza kunipa hiyo ili tuangalie Wanachuoni wameitafsiri vipi aya hiyo ?

Unaposema Milima inakwenda,yaani inakwenda wapi ?

Allah aliye juu anasema :

6. Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
7. Na milima kama vigingi? ( an Nabaa : 6 - 7 )

Akasema tena :

15. Na kaweka katika ardhi milima ili ardhi isiyumbe yumbe nanyi.Na mito, na njia ili mpate kuongoka. ( an Nahl : 15 )
 
Ndio, jua halisogei (move/revolve/orbiting) jinsi sayari zingine zinavyofanya kulizunguka Jua, Jua ndiyo "kiini cha rejea" (reference point) ya jinsi hizo sayari za mfumo wetu (our solar system ) zinavyozunguka jua.
Kaka haya uliyo yaandika ni kwa mujibu wa Sayansi au Qur'aan ? Kama ni kwa mujibu wa kimoja kati ya viwili hivyo,unaweza kuthibitisha hilo ?

Allah aliye juu anasema :

5. Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Hufunika usiku juu ya mchana, na hufunika mchana juu ya usiku. Na amefanya jua na mwezi vitumike. Kila kimojapo kinakwenda kwa kipindi kilicho wekewa. Jueni mtanabahi! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe! ( az Zumar : 5 )
Licha ya jua kuto- move/revolve/orbiting katika huu mfumo wetu wa jua, lakini jua linajizungusha (rotates) lenyewe hapo lilipo na linatumia takriban masaa (saa 27) kukamilisha mzunguko wake.

Haya umeyapata wapi ? Je unaweza kututhibitishia ukweli wake ?
Juu ya yote, mfumo wetu wa jua (solar system) unao ndugu zake (wanafamilia wenzake/ Galaxy) na familia hiyo inaitwa "milk way galaxy" na katika ulimwengu kuna galaxy nyingi mno zinazofanya "Universe", sasa wataalamu wa Sayanswanasema wanafamilia wote wa milky way Galaxy (na solar system yetu ikiwemo) zote zinazunguka (revolve/orbiting) kwenye point moja ya rejea (reference point).
Hili walilithibitishaje ? Je walifika huko ? Kama hawakufika walijuaje hayo ?
Hivyo licha ya jua kutozunguka (revolve) lakini zote sayari na jua kwa pamoja zinazunguka (revolve) kwenye point moja, zinazunguka kwenye point hiyo zikiwa pamoja na wana member wenziwe wa "milky way".
Thibitisha hili.
Umeuliza, kwanini jua lisimove na body zingine ziwe zina move (revolve), jibu ni hivi; Mungu amefanya hivyo ili hizo body ziendelee kuwepo kwenye njia yake (orbit) kwasababu kama zitaacha ku move basi zitavutwa na Jua na hapo ndipo "Kiyama" kitatokea na ujue hata dunia yetu pia itavutwa na na kumezwa na jua na kla kitu kitasambaratika.
Naomba aya au hadithi juu ya maneno haya.
 
Kaka haya uliyo yaandika ni kwa mujibu wa Sayansi au Qur'aan ? Kama ni kwa mujibu wa kimoja kati ya viwili hivyo,unaweza kuthibitisha hilo ?

Allah aliye juu anasema :

5. Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Hufunika usiku juu ya mchana, na hufunika mchana juu ya usiku. Na amefanya jua na mwezi vitumike. Kila kimojapo kinakwenda kwa kipindi kilicho wekewa. Jueni mtanabahi! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe! ( az Zumar : 5 )


Haya umeyapata wapi ? Je unaweza kututhibitishia ukweli wake ?

Hili walilithibitishaje ? Je walifika huko ? Kama hawakufika walijuaje hayo ?

Thibitisha hili.

Naomba aya au hadithi juu ya maneno haya.


Inasikitisha sana sana kwa Muisilamu kama wewe kuhoji maswali kama hayo.

Ni wewe Zurri ninayekujua au ni Zurri mwingine???.


Sayansi ni elimu kutoka kwa Allah, ni elimu ambayo Allah kampatia Mwanadamu ili aweze kuyajua na kuyakabili mazingira yake na pia aweze kutambua utukufu wa Allah katika uumbaji wake.

Dini licha kwamba inazo definitions nyingi lakini kwa ufupi dini ni taratibu maalum aliyoiweka Allah kwa ajili ya watu kupitia Mitume wake ili watu wapate kujua maneno/ sheria za Allah na hasa kumjua Yeye.

Hivyo Sayansi ya KWELI na dini zote za KWELI zinatoka kwa Allah, hivyo basi kamwe huwezi kuona Sayansi ya kweli zikipingana na dini ya kweli, na hapa dini ya kweli ni Uislamu.
 
Hivyo Sayansi ya KWELI na dini zote za KWELI zinatoka kwa Allah, hivyo basi kamwe huwezi kuona Sayansi ya kweli zikipingana na dini ya kweli, na hapa dini ya kweli ni Uislamu.
Japo hujajibu maswali yangu zaidi ya kutetea jambo ambalo misingi yake iko wazi,labda uwe huijui Sayansi.

Nakuuliza swali,vipi Sayansi inapooingana na Qur'aan unachukua lipi ?

Usisahau kujibu maswali niliyo kuuliza.
Ni wewe Zurri ninayekujua au ni Zurri mwingine???.
Ndio mimi kaka. Kama kuna sehemu nimekosea naomba unikosoe kielimu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom