Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

SEHEMU YA 76

Matokeo ya darasa la saba yalipotoka, walifaulu vizuri na hivyo kutakiwa kujiunga katika shule za sekondari, Godwin alichaguliwa kujiunga na Shule ya Wavulana ya Azania huku dada yake, Irene alitakiwa kujiunga na Shule ya Wasichana ya Jangwani alipokuwa akifundisha mama yake.

Bado walikuwa na fedha, Rosemary hakuona kama shule hizo zilikuwa sahihi kwa watoto wake, kama alivyokubaliana na mumewe kwamba Godwin na Irene walitakiwa kupata elimu bora, akaamua kuwapeleka katika shule nyingine ya watoto wa matajiri na viongozi serikalini iliyoitwa Kingston iliyokuwa Mikocheni B jijini Dar es Salaam.

Huko, masomo yalianza, hawakubadilika, bado walikuwa na uwezo mkubwa darasani, walijua kuzungumza Kiingereza kizuri, walipendwa shuleni hapo, walifanana na hata uwezo wao darasani ulikuwa mkubwa kiasi kwamba hata walimu wa shule hiyo walitamani sana kuona watoto wale wakiwa watoto wao.
“Hawa ndiyo watoto wa Balozi Mapoto?” aliuliza mwalimu mmoja.

“Ndiyo!”
“Mmh! Hawa watoto wana uwezo wa ajabu sana. Ni magenius, wana akili kupita kawaida,” alisema mwalimu huyo huku akionekana kushangaa.
Huo ulikuwa mwaka wao wa kwanza katika shule hiyo, walisoma bila tatizo lolote lile na hata mwaka ulipokwisha, walifanya vizuri na kuongoza kwa wanafunzi wote wa kidato cha kwanza.

Kufaulu kwao vizuri ilikuwa ni kama zawadi kwa baba yao ambaye kila siku aliwaambia kuwa walitakiwa kusoma kwa bidii kwani kusingekuwa na kitu chochote ambacho kingewatoa pale walipokuwa mbali na elimu. Mwaka huo ukamalizika, ulipoingia mwaka wa pili na kuendelea na masomo yao ndipo matatizo yalipoanza rasmi.

“Mama! Kuna karatasi imetoka Benki ya Watu,” alisema mwanaume mmoja aliyekuwa amemfuata Rosemary shuleni alipokuwa akifundisha.
“Kutoka benki?”
“Ndiyo!”
“Inasemaje?”
“Sijajua!”
“Na wewe nani?”

“Mleta barua kutoka hapohapo benki!” alijibu kijana huyo, hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, akaondoka zake.
Rosemary akawa na hofu, hakujua ni kitu gani kilichokuwa kimetokea, hakujua sababu iliyomfanya kupokea barua hiyo, hakujua ilikuwa ni barua ya nini, akaifungua bahasha ile na kuanza kuisoma.
 
SEHEMU YA 77

Ilikuwa ni barua fupi iliyompa taarifa kwamba alitakiwa kunyang’anywa nyumba aliyokuwa akiishi kwa kuwa mume wake aliiweka kama dhamana alipokwenda kuchukua mkopo wa shilingi milioni mia tano benki.

“Mkopo? Mume wangu alichukua mkopo? Lini?” alijiuliza swali hilo bila kupata jibu.
Alichanganyikiwa, hakuamini kama huo ulikuwa ukweli, alimfahamu mume wake, walipanga mipango pamoja, waliambiana kila kitu kilichokuwa kikiendelea, ilikuwa vigumu kwa mume wake kuchukua mkopo benki pasipo kumwambia, akahisi kwamba kulikuwa na kitu, alichokifanya ni kuwasiliana na mwanasheria wake.

“Umepokea barua kutoka Benki ya Watu?” aliuliza mwanasheria huyo aliyeitwa kwa jina la Emmanuel Makange.
“Ndiyo!”
“Inasema kwamba mumeo alichukua mkopo wa milioni mia tano kwa kuiweka dhamana nyumba yenu?” aliuliza Makange.

“Ndiyo!”
“Hebu niione!”
Akapewa barua hiyo na kuanza kuiangalia, ni kweli ilitoka katika benki hiyo, kulikuwa na sahini ya mkurugenzi wa benki hiyo na muhuri, ilionekana kuwa barua halisi iliyotoka katika benki hiyo.

Alichokifanya mwanasheria huyo ni kuondoka na kuelekea huko benki, alitaka kupata ukweli juu ya barua hiyo, alipofika, akaomba kuonana na mkurugenzi na kumwambia kile kilichokuwa kimetokea na mkurugenzi huyo kuthibitisha kwamba kweli Bwana Mapoto alichukua mkopo na aliahidi kurudisha mwezi huo.

“Hapana! Mzee asingeweza kufanya kitu pasipo kumshirikisha mama,” alisema Makange.
“Labda alifanya hivyo kwa ajili ya kimada wake, angemshirikishaje mama?” aliuliza mkurugenzi huyo.

“Hapana! Hakuwa mtu wa hivyo!”
“Wewe ni mwanaume! Hivi kweli inawezekana kuwa na mtu aliyekosa kimada? Usiusemee moyo,” alisema mkurugenzi huyo.

Hakuishia mahali hapo, ili kumuaminisha kwa kile alichokuwa amemwambia, akamtolea na nyaraka nyingine nyingi ambazo zilionyesha kwamba Bwana Mapoto alichukua mkopo huo ndani ya benki hiyo.

Hawakuishia katika nyaraka zilizokuwa kwenye makaratasi tu bali akamchukua na kumpeleka katika kompyuta na kumuonyeshea kila kitu ambacho alitakiwa kukiona.

Emmanuel alichanganyikiwa, aliangalia sahini, ilikuwa ni ya Bwana Mapoto. Akarudi nyumbani kwa Rosemary akiwa hana nguvu kabisa, alichoka, alichokiona kule benki kilimshtua sana.
 
SEHEMU YA 78

“Imekuwaje?”
“Mama! Hali ni ngumu sana!”
“Lakini si huwa kitu kama hiki kunakuwa na mwanasheria. Ningependa nionane na huyo mwanasheria ambaye alimsimamia katika hili,” alisema Rosemary huku akionekana kuchanganyikiwa hasa.
Hilo halikuwa tatizo, kwa sababu katika karatasi zile aliandikwa mwanasheria aliyemsimamia katika hilo, akatafutwa na alipoulizwa, alimwambia Rosemary kwamba kweli alikuwepo siku hiyo na yeye ndiye aliyemsimamia Mapoto kupata pesa hizo, na uzuri ni kwamba walikwenda kuandikisha mpaka mahakamani.

“Mpaka mahakamani?”
“Ndiyo!”
Rosemary hakutaka kukubali, alitaka kujua kila kitu kilichokuwa kimetokea, akaelekea mahakamani, kweli, alipofika akaonyeshewa nyaraka zote alizosaini mume wake kama kukamilisha kuuchukua mkopo huo mkubwa.

Miguu yake ikakosa nguvu, palepale mahakamani alipokuwa, akapiga magoti na kuuficha uso wake, akaanza kulia kama mtoto mdogo kwani alihisi akiwa amebeba dunia nzima, alijiona kuwa mtu mwenye mikosi kuliko watu wote duniani.

Hakujua angekimbilia wapi, hakujua angefanya nini kuzilipa fedha hizo, kilikuwa kiasi kikubwa sana ambacho asingeweza kulipa, na kama angeshindwa kulipa, inamaana kuwa angepokonywa nyumba aliyokuwa akiishi.

“Haiwezekani! Mungu! Mume wangu hawezi kufanya ujinga huu! Hapa kuna kitu, ninamuamini mume wangu, ni mtu makini, tulishirikiana kwa kila kitu, hawezi kufanya hivi,” alisema Rosemary huku akiwa amekiinamisha kichwa chake, alikuwa akilia kama mtoto.

Watu wote waliokuwa mahali hapo walimshangaa, walimfahamu, alikuwa mke wa mtu aliyekuwa na nguvu sana nchini Tanzania, hawakujua ni kitu gani kilitokea mpaka kumwaga machozi namna ile hapo mahakamani. Hawakukubali, wakawapigia simu waandishi wa habari na kuwapa taarifa kile kilichokuwa kinaendelea mahali hapo.

Ni kama Rosemary alijua, hakutaka kukaa sana mahakamani hapo, akaingia ndani ya gari lake na kuondoka huku akiendelea kulia kama kawaida. Baada ya dakika kadhaa, waandishi wakafika mahali hapo wakiwa na kamera zao, walitaka kuhakikisha kile walichokuwa wameambiwa.

“Yupo wapi?” aliuliza mwandishi mmoja.
“Ameondoka!”
“Mna uhakika kwamba ni yeye?”
“Sasa sisi tutakupa taarifa ya uongo bwana! Kwani hatumjui?” aliuliza jamaa mmoja.
 
Sio mm huyo mkuu huyo ni mdogo wangu
Ila kama ni wewe mzuri sana we Dada.shida yangu mimi sio wewe malizia story.baada ya barua nini kiliendelea? Walinyang'anywa nyumba? Baki na uzuri wako tu
 
Ila kama ni wewe mzuri sana we Dada.shida yangu mimi sio wewe malizia story.baada ya barua nini kiliendelea? Walinyang'anywa nyumba? Baki na uzuri wako tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom