Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

SEHEMU YA 79

“Inawezekana mkawa mmemchanganya. Si mnajua duniani wawiliwawili!” alisema mwandishi huyo.
“Mtafuteni. Ila alikuwa akilia kama mtoto!”
“Kweli?”
“Habari ndiyo hiyo!” alijibu mtoa taarifa, waandishi wa habari wakaondoka na kuanza kuelekea nyumbani kwa Rosemary huku wakiwa na kiu ya kutaka kufahamu ukweli juu ya kitu kilichokuwa kikimliza mahakamani?

“Hii ishu inaweza kuwa habari kubwa sana,” alisema mwandishi mmoja.
“Ndiyo hivyo! Halafu siku nyingi hajasikika, kama tukiiandika, inaweza ikawa kiki kubwa ya kutupatia wasomaji wengi,” alisema mwandishi mwingine.
“Kweli kabisa. Hebu tuwahi nyumbani kwake kabla ya waandishi wengine hawajajua kuhusu hii taarifa,” alisema mwandishi mmoja, safari ikaanza.

*** “Ni kweli?” aliuliza mmoja wa waandishi wa habari waliokwenda kuonana naye.
“Kuhusu nini?”
“Kuhusu benki kuitaka nyumba yako kwa deni la milioni mia tano unalodaiwa?”
“Naomba mniache kwanza.”
Rosemary hakutaka kulizungumzia hilo, alitaka kuachwa kwani kwa kipindi hicho akili yake haikuwa sawa kabisa. Alijua fika kwamba mumewe hakuchukua huo mkopo, mumewe hakuwahi kufanya jambo kimyakimya pasipo kumtaarifu lakini hakujua mambo hayo yalisababishwa na nini kwani kama kufariki, alifariki na alichokijua ni kwamba kila kitu kilianza upya.

Akawasiliana na Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania National Party, Elibariki Edward na kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea. Mwenyekiti huyo hakuamini, alichomwambia ni kwamba angeonana naye na kulizungumza hilo kwani naye kwa jinsi alivyomfahamu Mapoto, asingeweza kufanya jambo kama hilo.

“Nakuja!”
Ndani ya nusu saa, mwanaume huyo alikuwa nyumbani kwa Mapoto kwa ajili ya kuzungumza na Rosemary. Alikuwa mwanamke mjane aliyehitaji msaada kwa hali na mali. Alizungumza naye, akamwambia jinsi alivyoletewa barua ile na mwanasheria wake kufuatilia kila kitu mahakamani na kuambiwa kwamba kile alichokiona ndicho kilivyokuwa.

“Inawezekana vipi?” aliuliza Edward huku akishangaa.
“Sijajua! Nimechanganyikiwa, sijajua ni kitu gani natakiwa kufanya. Huu ni uonevu, kwa nini jambo hili wasingelisema wakati mume wangu akiwa hai? Kwa nini wamesubiri mpaka afe?” aliuliza Rosemary.
 
SEHEMU YA 80

Hakukuwa na kitu kilichobadilika, bado msimamo wa Benki ya Watu ulimwambia kuwa alitakiwa kulipa kiasi cha pesa alichokuwa akidaiwa mume wake vinginevyo nyumba yake ambayo iliwekwa dhamana ingechukuliwa na benki hiyo kisha kupigwa mnada.

Hakuwa na kiasi hicho cha fedha, alikuwa tayari kwa kila kitu. Waandishi wa habari ambao walikwenda kufanya naye mahojiano wakaitoa habari ile katika magazeti. Kila mtu aliyeiona, alishtuka, hawakuamini kama Mapoto angeweza kufanya kitu cha kipumbavu kama kile.

Maneno yakaibuka, wengi wakasema kwamba serikali iliingiza mkono katika jambo hilo kwa ajili ya kumfilisi mwanamke huyo kwa kuhisi kwamba naye angeweza kuingia katika Chama cha Tanzania National Party na kuleta upinzani mkali.

“Serikali inajihami tu! Nina uhakika Mapoto hajawahi kufanya jambo kama hili,” alisema mwanaume mmoja.
“Wewe ni kama mimi! Yule ni mtu makini sana, nahisi kuna kitu ila siku si nyingi tutakijua tu,” alisema jamaa mwingine.
Rosemary alipewa muda wa kulipa deni alilotakiwa kulilipa. Hakuwa na furaha tena, ile kidogo ambayo ilianza kurudi moyoni mwake ikapotea, majonzi yakautawala moyo wake, kila alipokuwa alionekana kuwa na mawazo mno kitu kilichowafanya hata watu wengine waliokuwa wakimwangalia kumuonea huruma.

“Mom! What is going on?” (mama! Nini kinaendelea?) aliuliza Irene huku akiwa amemsogelea mama yake.
“Nothing my daughter!” (hakuna kitu binti yangu)
“But you look so upset!” (unaonekana huna furaha!)
“Me? No! I am happy Irene. Have you already eaten?” (mimi? Hapana! Nina furaha Irene. Tayari umekula?) aliuliza Rosemary kwa lengo la kumtoa Irene katika mambo aliyokuwa akimuuliza.

“Yes!” (ndiyo)
“Where is your brother?” (kaka yako yupo wapi?)
“He is already sleeping” (amelala)
Akamchukua Irene na kumpeleka chumbani kwake na kumlaza kisha na yeye kuelekea chumbani kwake. Hakupata usingizi, hakukuwa na kipindi kilichokuwa kigumu kwake kulala kama kipindi hicho.
 
Huyo Rosemary kafanyaje Shunie
Dada angu umeanza jamani yaan kwa ninavyokujua utakuwa umesoma kwa rosemary tu ni alikuwa mke wa marehemu mgombea uraisi wa upinzani sasa bada ya mumewe kufa ghafla tu imekuja bank ghafla inataka kumfirisi kuwa mumewe alikopa mill 500
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom